Wamiliki wa mabasi fursa mmetengenezewa hiyo hapo chukueni hela

Wamiliki wa mabasi fursa mmetengenezewa hiyo hapo chukueni hela

Ego is the Enemy

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2014
Posts
8,201
Reaction score
16,246
Habari zenu wanajukwaa!

Tupeane namna ya kukwepa kutuma hela kwa simu Mana jamaa wanadai wazalendo Ila hata Mia Yao mbovu haikatwi pia hatunziwi hela wake kupewa wakizeeka Ila wewe ndiye wa kutunziwa pia ndiye wa kulipa Kodi ya kizalendo.

Jamaa wamelewa Kodi zetu,kumbuka yeye hajui kuwa Kuna shida afrika yaani yeye anaishi life hata mzungu wa uk hampati.

Nisiwapotezee muda ishu Iko Ivi Kama mwenye umiliki wa mabasi ama mtu anaweza akaingia nao ubia wakafanya biashara hii.

Niko dar natoa hela kwa kampuni labda ni 50k afu wewe uko mbeya uko kwa iyo ofisi ya hapo mbeya wao wanahakiki aliyeko dar akatoa hela afu wa mbeya anapewa hapo baadaye wanajumlisha fresh Mambo yanaenda.

Mie Niko zangu Singida unayemtumia uko bukoba nenda ofisi Fulani wasiliana nao yaani ukiwapa tu wa bukoba namie Niko singida nachukua.

Pia kuweka hela benki Mana mawakala wamejaa kila Kona halafu nenda atm chukua hela makato ni 1200 kila unapochukua hela kuanzia 5k mpaka 400k.

Na kwa ATM waweza chukua mpaka 2M so makato jumla ni 1200*5=6k.

Aisee hii njia ya mabasi wakitokea wakiwa na akili itakuwa poa sana.

Yanai ofisi ya mabasi ya kisire iko mza kahama na Tarime ni mwendo tu Niko kahama nawapa hela afu wao wanampatia hela wa mwanza Mana wanahakiki kuwa huyu jamaa mwenye namba hii mpe 50k.

Ngoja niachie hapa nadhani nimeeleweka. Makato wanaweka nusu ya yaliyopo kutumaa na kutokea.

Yaani wameweka kutuma na kutoa pote pote jamani kweli.

Yaani Hawa jamaa sijui wanalewa sana.
 
Binafsi nilikuwa nishaaicha mitandao.

Hela ni mwendo wa kunitumia kwa akaunti nikipita palipo na ATM navuta zangu tulaki twangu twa matumizi basi kwishnei.
Aisee hela yangu ninavyoihangaikia usiku na mchana afu iende bure bure sikujaligi kabisa.

Afu usikute kampuni ya uchimbaji madini wamesamehewa Kodi miaka mitano ili waone Kama watapata faida. Pia kumbuka Airtel ilikuwa haijawahi kulipa gawio serikalini Mana hawakuwa wanapata faida mpaka jembe alivyokuja faida ikapatikana.

Yaani nchi kumamae Kuna wsngrema kadhaa Kama 300 ivi wanaendesha watu 60M.wanatunyonya na wanatumia masikini wenzetu Askari kututuliza tunapotaka kudai nchi yetu.

Masikini na umasikini ni kitu kibaya kisenge. Yaani askrai ni masikini Kama mie Ila anaamrishwa na jamaa Fulani kuwa mshughulikie huyu ili niwanyonye vizuri naye anakubali kisa anadanganywa vijisenti kidogo.

Ile TAL anadai watu waingie roads utafika muda tutaingia wenyewe tu. Mafuta yamepanda soko la dunia Ila Kodi Yao imeongezea pia.
 
Wakianza watafuatwa na kupigwa mkwara.lakini ndionjia tulizokua tunatumia miaka ya nyuma mfano kutuma pesa toka Muscat Oman ilikua unampa mtu kule oman Rial zenye thamani ya pesa inayotaka mtu apate tz then wanakuchaji ada yao basi fasta mtu huku tz anapigiwa simu afuate pesa very simple.

Njia za kutuma na kupokea pesa zipo nyingi tutaweza ikimbia hii mitandao yao.

Yaani tunarudishana nyuma aisee
 
Ngoja waliokuelewa waje, naamini Watanielewesha hasa uzi una Elezea nini? Nimesoma zaidi ya mara mbili ila sijaelewa
Acha kukaza fuvu ilo....

Shotly anamaanisha wamiliki wa mabus ya mkoa waanze kutoa huduma ya miamala. Mf. Wewe unakwenda pale Shekilango kwa Kilimanjaro express unawapa laki 1 huku babe wako anaenda Kilimanjaro express Arusha kuchukua hizo pesa.
 
Wewe tena, nakuaminia
Eeh ni kutengeneza Metropolitan Network tu na mawakala wengine ambao mnaaminiana!

Kwa Tabata unakuwa na mtu kila kituo kuanzia stand ya Kimanga pale to Bima to Segerea na kila muamala unachaji buku tu wala sio hela nyingi! Kupitia network hio nyie kama mawakala mtapiga hela hadi mchoke sababu hela zenu zinakuwa zinazunguka na commission ni cash money! Kadri mtandao wako wa trusted patners unavyoongezeka ndivyo ambavyo mnazidi kupiga hela!

Kikubwa unaji market tu kama wakala wa zone ya Tabata kwahio watu wote wenye shida za kutuma hela maeneo hayo wakutumie wewe tu network yako ya patners inakuwa wazi na ukomo wako wa huduma mwisho labda saa 10 jioni kwa sababu za kiusalama zaidi! Mnakutana mlimani City mnapeana kila mtu kibunda chake kulingana na records game over!

Hela mnakuwa hampitishi kwa hawa wanyonyaji wa mitandao na mwigulu! Wasifikiri ile system yao ni kitu cha ajabu sana mbinu zipo bado!
 
Acha kukaza fuvu ilo....

Shotly anamaanisha wamiliki wa mabus ya mkoa waanze kutoa huduma ya miamala. Mf. Wewe unakwenda pale Shekilango kwa Kilimanjaro express unawapa laki 1 huku babe wako anaenda Kilimanjaro express Arusha kuchukua hizo pesa.
Easy bro yani so easy na anaacha buku tu kwa mfano! Kwa wenye mitaji hili ni bonge la fursa
 
Acha kukaza fuvu ilo....

Shotly anamaanisha wamiliki wa mabus ya mkoa waanze kutoa huduma ya miamala. Mf. Wewe unakwenda pale Shekilango kwa Kilimanjaro express unawapa laki 1 huku babe wako anaenda Kilimanjaro express Arusha kuchukua hizo pesa.
Hapo ndo nimeelewa mkuu, Je, wenyewe wanafaidikaje na huduma hiyo
 
Hii kitu walifanyaga Scandnavia Express enzi hizo naona sasa tunarudishwa zama hizo kijanja!
Duu mkuu enzi hizo mie nikiwa Advance sikujua hela kwa emo ama ems.
Hii lazima ifanyike tu.

Yaani uko Arusha nawapa hapa Chato afu wanapiga simu huko Arusha ofisi zao kuwa mwenye namba hii akuonyeshe I'd mpe 20k Mambo Kwisha.

Namie hapa nimewapa buku mbili. Yaani Nina tumilioni twangu sijui nifanye hizo Mambo nikiwa na ubia kwa jina la kampuni.
Subirieni e wallet ziingie hapa nchini watu wazijue like Skrill ,PayPal, netteller n.k.

Enzi za mpj eti walipiga biti kusafirisha vifurushi eti vipitie posta. So mie Niko mbeya nishafiri once/twice kuja dar nikafahamiana na wafanyabiashara Kuna haja gani kila wakati kusafiri.

Natuma hela funga mzigo Kuna peleka kwa kampuni Fulani ya usafirishaji wape nitachukulia hapa ofisini kwao wakupe receipt piga picha nitumie.

Yaani Hawa kmmake life linarahishwa afu ndo wanataka watu tuumie huku watt wao wakisomea kanada USA uk Australia huku wa kwetu wamekalia tofali za udongo.

Na mikopo wanakaziwa hawapewi ili waendelee kuwa wanyonge. Wanatengeneza kitu ama bomu siku likilipuka tutakuwa Kama sauzi saivi.

Mie nitawahi kuvunja zangu ATM tu achana na yule msnge aliyekuwa anakula keki
 
Duu mkuu enzi hizo mie nikiwa Advance sikujua hela kwa emo ama ems.
Hii lazima ifanyike tu...
Kuna bank walikujaga na E-Wallet yao ilikuwa inaitwa SPENN ACCOUNT sema naona haikuwa successful! Ila ilikuwa bonge la tech. Haikuwa na makato kabisa ya kiduanzi
 
IDEA YAKO NI PERFECT SANA[emoji23][emoji23][emoji23]
Mfano unaongea na wenye basi unaweka mtu ofisini kwao kila mkoa so ndiye anayekuwa anafanya hii kazi Kama wao wanaogopa kufilisiwa.

Eti Kuna mkijani mmoja anadai eti lipa tozo afu uone matokeo yake Mana hazipendi mifukoni mwao hao jamaa waliozileta.
Na ilala mmekosa nini mpaka mkatuletea huyo mzalendo ambaye hata Mia yake haikatwi.

Yaani wao wangeanza wao kwanza wakatwe tuone Kama ni wazalendo. Afu eti kajamaa kalikorudia pr anadai ni tozo ya uzalendo mbona wao hawakatwi ama wao uzalendo hauwahusu kweli.

Tuwe wazalendo wote kwa mifano jamani na sio wachache wanajazwa kichwa eti uzalendo Mara wanyonge kumbe ni gia ya kuwakamua
 
Back
Top Bottom