Wamiliki wa Mabasi ya Mikoani, kwanini mnatutesa na kutukomoa Abiria wenu katika dakika 20 za huduma mnazotupa mkisimama njiani?

Mabasi yote ya safari ndefu yawe na vyoo vya ndani, pia kisheria baada ya masaa manne matano kupumzika iwe lazima. Hiyo itamsaidia dereva kupumzika kidogo na kupunguza ajali zinazosababishwa na uchovu.
Kila baada ya masaa manne upumzike Dar Bukoba utafika baada ya siku ngapi?
 
Kwan Driver and Kondakta wao huwa hawashiriki hizo huduma ulizozitaja? Je wao huwa wanatumia dk ngapi?
 

Wenzetu vitu vituo vizuri kila baada ya 100km nchi nzima. Kuna huduma zote unakuta, kuna Migahawa misafi na fast food chain kama McDonald, KFC, Starbuck, vyoo kama 30 visafi kabisa.

Hata sisi tunaweza ni uamuzi tu.
 

Hili sipandi kabisa kuna siku niliwaambia waniache waende wakanisubiri maana nilikuwa nawaharibia wangeondoka
 
Yaan dk 20 unaona ndogo?alafu ww kama ni wa kiume unatia aibu futa hii post, watu wanaolalamika kwa mambo ya kijinga kama haya huwa ni wanawake..

Mwiso niseme kuna haja ya serikali kufanya iwe lazima kwa kila mtu mwenye miaka 17 kwenye JKT ili kuwa wakakamavu... taifa hili linapaswa kuwa na watu wakakamavu sio hawa wanaolilia kupewa dk 45 kwenda choon.. yaan ww ktk safari unawaza kunya na kula tu?

Unatia aibu mkuu
 
Kamwone Daktari mkuu yaan dakika kumi! i mean ten minutes haja ya kawaida(ukiacha la tumbo la kuhara) unakua hujamaliza???
 
We ni wale wanao ogopa hadi mende makabatini mkuu?
 
We ni wale wanao ogopa hadi mende makabatini mkuu?

Haha, standards, viwango, ustaarabu.

Mama, dada, bibi yako anachuchumaa hapa wewe uko pembeni unakojoa.

Kulinda utu, heshima ni muhimu kwa binadamu wote.

Usiwe mbinafsi, siku zote unajifikiria wewe. Look at big picture.Watu wote, wazee, walemavu, watoto, wanawake,wagonjwa.
 
Ila mabasi mengi hutoa dakika kumi tu kwa abiria kupata chakula na pia kwenda maliwato kujisaidia. Huu ni ukatili usiomithilika.
 
Nchi imejaa misukule mioga, inapelekeshwa kama nyumbu! Hivi hili nalo ni jambo la kulalamika? Kwa nini abiria kwa umoja wao wasiseme kuwa muda hautoshi? Hii nchi yetu ina laana gani watu wanapelekeshwa kila kona na kuhoji hawahoji?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…