Wana jamiiforum ambao hatujawahi kufika Dar es salaam toka tuzaliwe tukutane hapa

Wana jamiiforum ambao hatujawahi kufika Dar es salaam toka tuzaliwe tukutane hapa

Kwa sisi wanajamiiforum wa vijijini ambao toka tuzaliwe hatujawahi kukanyaga Hilo jiji hebu tukutane hapa na kufarijiana maana wanadarisalama wanatudharau Sana. Jambo moja kubwa ambalo naamini kwa asilimia Mia moja ni kwamba sisi wanaume wa vijijini tunawazidi nguvu wanaume wa dar.
Hehehehe
 
Tupo mkuu...Mimi zamani ndo nilikuwa natamani Sana kufika Dar , saiv umri umeenda acha nimalizie ujana huku Bonga,Itaswi,Yaeda ampa,Bashnet,Tlawi,Endasak,Mamire
 
Hapa Omurushaka, Kayanga, Kyerwa, Nkwenda, Mulongo
Kigoma, Kasulu, Kibondo, Buzebazeba, Gungu
Mpeta, Uvinza, Kazuramimba
Sengerema, Tabaruka, Ibisabageni
Ngudu Huku Kote JF Ipo Na Ina Members Tele
wale wa Masanza kona na Isunga ngwanda tupatane chemba
 
Karibu darcity mkuu...piga jembe laki mbili ,inakuwezesha kufika na kutalii angalau kwa siku mbili.

By the way....msalimie dada yako,mwambie kuna rafiki yako wa Dar amekusalimia kisha nipe mrejesho.
 
Ndugu kwanza ujue Dar ziko zaidi ya nne.
Kuna Ile Dar ya posta, Dar ya kisomi.
Kuna Dar ya kariakoo hii hata Kama huna elimu ya fomfoo ruksa kwenda.
Kuna Dar ya Oysterbay Hadi Masaki, hapa you need to have solid money.
Kuna hizi Dar wanazokaa noveau Richie yaani Dar za watu walioanza kupata hela juzi juzi Kama Goba, Mbezi beach, Bunju, Tegeta nk.
Then Kuna hizi Dar za waswahili huku hata Kama huna elimu ya Msingi ruksa kwenda hata ukitaka kujenga hakuna atakaye kuuliza.
 
Kwani nani anawadanganya hizi habari? Eti hatuna nguvu?
Mko lainilain maisha yenu hayana suruba ngozi zenu hata hazionyeshi mishipa ya damu mkienda hospital kwasababu ya ulainilain wenu na utipwatipwa. Mmekaa mifutafuta ya uzembe Wala bisi na chips weak society nyie.
 
Kwa sisi wana JamiiForums wa vijijini ambao toka tuzaliwe hatujawahi kukanyaga Hilo jiji hebu tukutane hapa na kufarijiana maana wanadarisalama wanatudharau Sana.

Jambo moja kubwa ambalo naamini kwa asilimia Mia moja ni kwamba sisi wanaume wa vijijini tunawazidi nguvu wanaume wa Dar.

Kwani dar kuna nini cha ajabu,,,,wenyewe wakienda Dubai wanashangaa magorofa, magari, zile barabara za kupishana, fly over, mandege n.k 😁 kwaiyo ucdhani wakutoka kijijini tu washamba mzehe.
 
Mko lainilain maisha yenu hayana suruba ngozi zenu hata hazionekani kwasababu ya ulainilain wenu.
Hii sio kweli, sisi ni watu wa kazi, hata sura zetu zinatisha.
Pamoja na umri nilionao shughuli yangu sio ya kitoto.
 
Imagine unaitwa "mwanaume wa dar"...
Hii ndo sababu pekee inayonifarij mimi wa mkoan
 
Back
Top Bottom