LGE2024 Wana JF mmejiandikisha? hizi ni faida za kujiandikisha kupiga kura

LGE2024 Wana JF mmejiandikisha? hizi ni faida za kujiandikisha kupiga kura

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Usiseme hivyo mkuu

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
Niseme nini sasa mkuu,ccm ni watu wenye uchu wa madaraka uliyopitiliza kiasi ambacho wapo tayari kufanya chochote ili mradi tu wapate hayo madaraka lakini ipo siku watalipia wanachowafanyia wananchi wala wasifikiri kwamba wao ni wajanja sana kuliko watu wengine wote katika ulimwengu huu.
 
Faida ya Mtanzania kujiandikisha kupiga kura katika uchaguzi wa viongozi wa Serikali ya kitongoji, mtaa, na kijiji ni pamoja na:

1. Kuchagua viongozi bora: Inatoa nafasi ya kuchagua viongozi wenye uwezo wa kuleta maendeleo na kushughulikia maslahi ya jamii.

2. Kuhakikisha uwakilishi wa wananchi: Kupitia kura, wananchi wanapata viongozi wanaowawakilisha kwenye maamuzi yanayogusa maisha yao moja kwa moja.

3. Kuimarisha demokrasia: Kushiriki kwenye uchaguzi ni sehemu ya kutekeleza haki yako ya kikatiba na kuimarisha demokrasia nchini.

Ndugu zangu, wakati wa kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ni huu. Hii ni nafasi yetu ya kuhakikisha tunapata viongozi bora watakaosimamia maendeleo ya jamii zetu. Fanya uamuzi sahihi, jiandikishe leo ili ushiriki kikamilifu kwenye uchaguzi ujao

Mnasubiri nini???
Usitufokee
 
Hizo faida za porojo sizitaki, na kuhusu kupiga kura siwezi kupiga kura kwa namna yeyote ile bila kuona walau laki 5 kwenye Account yangu ya Mpesa kutoka serikalini.
 
Vijana wa hovyo, kesho usianze kulalamika serikali iliyopo madarani inafanya mambo yasiyofaa.
Hata usipoichagua itaunda serikali, alishasema yule ajuza akiwa nchini Mexico City. Sasa unajihangaisha kwa ajili ya nani
 
Back
Top Bottom