Wana JF narudia tena, haribu kabisa tiketi au karatasi yenye taarifa zako kamili

Wana JF narudia tena, haribu kabisa tiketi au karatasi yenye taarifa zako kamili

Mleta mada kuna uwezekano rafiki yako kahusika moja kwa moja kwenye tukio.

Yeye kukataa wito wa polisi na kuzima simu ni viashiria tosha kwamba jamaa kahusika directly ama indirectly

Anyways, Muda utaongea na ukweli utajulikana
Kwakweli
 
Cha msingi kama hajatenda kosa awe huru na ajiamin tu. Aeleze ukweli japo itachukua muda kueleweka kwan had wafanye uchunguzi ni kupotezeana muda... Ila mkifosi sana mtapoteza hela na muda wenu.
 
Ushauri wangu kwa mtu anayeitwa mahali popote na mtu/watu asiowajua ajitahidi kwenda na watu wengine,atoe taarifa kwa ndugu zake,marafiki au jamaa zake kwamba nimeitwa mahali fulani kuondoa dhana ya kwamba niliitwa ila nikaogopa kwa kudhani kwamba nimeitwa na watu waovu,kumbe unatenda kosa la kukaidi kuitikia wito halali wa Polisi.

Kuna siku nilikuwa ninakatiza mtaani alfajiri sana,mara nikasikia ninaitwa "Oyaaa simama mahali hapo ulipo,Wapi saa hizi?" Nikimulikwa na tochi machoni,nikasimama nikidhani ni Polisi wako doria!!

Nakuja kushtuka nimezungukwa na watu wana mapanga, nondo halafu wamevaa vikaptula vifupi,vifua wazi wamejipaka oil mwili mzima,kumbe ni Vibaka.

Kilichonisaidia sikuogopa, nilijikuta ninasema ninaenda kazini nimewaacha masela wangu bado wamelala, wakadhani ninafanya kazi kama zao. Maana waliniuliza upo kundi gani,nikataja majina ya marafiki zangu,lakini wakawa wanashangaa, wanaangaliana tu.

Bahati nyingine nilikuwa nimevaa kawaida sana wakanithaminisha wakaona sina cha kupoteza. Wakaniacha.

Kwahiyo rafiki yako anaweza kuwa hahusiki ila hofu ya kuitwa Polisi ndio ilimfanya aogope kuitikia wito,kumbe njia aliyoitumia haikuwa sahihi.

Mungu amsaidie alimalize salama.

Kutunza nyaraka zenye taarifa zetu ni muhimu sana dunia imeshaharibika,mtu anaweza kuchukua tiketi, vocha iliyotumika, kitambulisho akakitupa sehemu lilipotendeka tukio la uhalifu ilimradi tu uitwe kusaidia upepelezi, mpaka ijulikane hukutenda kosa tayari umeshapoteza muda wako ambao ungeutumia kufanya jambo la msingi.
 
Jamani, Jamani

Wapendwa wa humu narudia tena, Chana au haribu kabisa tiketi au karatasi yoyote yenye taarifa zako sahihi kwa usalama wako.

Niko hapa Police Kimara, rafiki yangu wa kiume amekamatwa na kuwekwa ndani baada ya tiketi yake ya ki-electronic ya basi moja kutoka Arusha kuja Dar kukutwa kwenye tukio la uhalifu Kimara Bucha.

Yeye rafiki yangu anasema baada ya kushuka Mbezi Magufuli stendi, aliamua kuikunja na kuitupa tiketi yake karibu na lango la kutokea na baada ya hapo akaendelea na safari ya kuelekea kwake Tegeta.

Anasema zilipita siku 2 akapigiwa simu na police kuwa anahitajika kituoni Kimara.
Anasema hakwenda kwa kuhofia huenda ni watu wasio wema kisha akazima simu.

Anasema kesho yake anashangaa kuona police wako nyumbani kwake na wakamuweka chini ya ulinzi kwa kosa la uhalifu uliotokea maeneo ya Kimara bucha.

Na anasema walihisi walimpata kupitia Facebook, (mutual friend mmoja akatafutwa kisha akawaelekeza kwake).

Rafiki yangu si mtu wa kujichanganya sana na watu. Iwe usiku au mchana, akiwa ndani hujui na wala akienda kibaruani hujui.

Anasema ahusiki na tukio na wala hajafanya uhalifu wala kuwa na rekodi yoyote ya uhalifu.
Hapa tunashindwa cha kufanya.

Hatujui kama kweli kahusika au lah!

Sisi tunajua ahusiki ila binadamu hubadilika.

Ila maadam iko mikononi mwa jeshi la polisi tutajua tu hatma yake na wahusika halisi

Chana au haribu kabisa karatasi/tiketi ya basi/meli/treni/ndege/CV/copy yako ya NIDA na nyinginezo zenye taarifa zako sahihi ili kuepuka kupata matatizo.
Hakuna kitu kibaya sana kama kumwambia mwanamke au demu wako kwenye simu njoo tuonane alafu ghafla auawe. Nakuambia hutokaa utoke hata ulipe ile sent ya mwisho kama huna connection inayoeleweka
 
Nilidhani wamepajua kwake kupitia some advanced techniques, kumbe wamempata kupitia Facebook. Hahaha. Hiyo ndiyo sababu situmii jina langu kwenye mtandao wowote. Sababu hii nchi ina wajinga wengi madarakani, let alone kwamba internet ni wino usiofutika. Kuwa paranoid ni beneficial sometimes.
 
Ndio, na ndio maana nikasema 'binadamu hubadilika'
Lakini tiketi kweli ni yake na imekutwa eneo la vita...how🤷‍♀️?
HIVI TICKETI HIZI UNAZOENDA NA KUTAJA JINA NA NAMBA YA SIMU BASI NI TICKETI?

NIMEKATIA WATU TICKET,BILA WAO KUJUA,SIKU YA SAFARI NI KUONDOKA TU.
 
Hata kondomu mkuu bora uondoke nayo , inaweza likakutwa janaba lako kwenye tukio la ubakaji sijui utaambia nin watu wakuamini
 
Kikubwa uchunguzi wa Uhakika ndio utabaini kwamba sio muhalifu lakini kwa Bongo utakesha sana mpaka ije kueleweka kwamba sio kweli, wameshakuharibia mambo yako
 
Ndomana ukipoteza kitambulisho au nyaraka yoyote muhimu unaambiwa katoe taarifa police

Ova
 
Ushauri wangu kwa mtu anayeitwa mahali popote na mtu/watu asiowajua ajitahidi kwenda na watu wengine,atoe taarifa kwa ndugu zake,marafiki au jamaa zake kwamba nimeitwa mahali fulani kuondoa dhana ya kwamba niliitwa ila nikaogopa kwa kudhani kwamba nimeitwa na watu waovu,kumbe unatenda kosa la kukaidi kuitikia wito halali wa Polisi.

Kuna siku nilikuwa ninakatiza mtaani alfajiri sana,mara nikasikia ninaitwa "Oyaaa simama mahali hapo ulipo,Wapi saa hizi?" Nikimulikwa na tochi machoni,nikasimama nikidhani ni Polisi wako doria!!

Nakuja kushtuka nimezungukwa na watu wana mapanga, nondo halafu wamevaa vikaptula vifupi,vifua wazi wamejipaka oil mwili mzima,kumbe ni Vibaka.

Kilichonisaidia sikuogopa, nilijikuta ninasema ninaenda kazini nimewaacha masela wangu bado wamelala, wakadhani ninafanya kazi kama zao. Maana waliniuliza upo kundi gani,nikataja majina ya marafiki zangu,lakini wakawa wanashangaa, wanaangaliana tu.

Bahati nyingine nilikuwa nimevaa kawaida sana wakanithaminisha wakaona sina cha kupoteza. Wakaniacha.

Kwahiyo rafiki yako anaweza kuwa hahusiki ila hofu ya kuitwa Polisi ndio ilimfanya aogope kuitikia wito,kumbe njia aliyoitumia haikuwa sahihi.

Mungu amsaidie alimalize salama.

Kutunza nyaraka zenye taarifa zetu ni muhimu sana dunia imeshaharibika,mtu anaweza kuchukua tiketi, vocha iliyotumika, kitambulisho akakitupa sehemu lilipotendeka tukio la uhalifu ilimradi tu uitwe kusaidia upepelezi, mpaka ijulikane hukutenda kosa tayari umeshapoteza muda wako ambao ungeutumia kufanya jambo la msingi.
Umenielewesha vizuri sana
🤝
 
Jamani, Jamani

Wapendwa wa humu narudia tena, Chana au haribu kabisa tiketi au karatasi yoyote yenye taarifa zako sahihi kwa usalama wako.

Niko hapa Police Kimara, rafiki yangu wa kiume amekamatwa na kuwekwa ndani baada ya tiketi yake ya ki-electronic ya basi moja kutoka Arusha kuja Dar kukutwa kwenye tukio la uhalifu Kimara Bucha.

Yeye rafiki yangu anasema baada ya kushuka Mbezi Magufuli stendi, aliamua kuikunja na kuitupa tiketi yake karibu na lango la kutokea na baada ya hapo akaendelea na safari ya kuelekea kwake Tegeta.

Anasema zilipita siku 2 akapigiwa simu na police kuwa anahitajika kituoni Kimara.
Anasema hakwenda kwa kuhofia huenda ni watu wasio wema kisha akazima simu.

Anasema kesho yake anashangaa kuona police wako nyumbani kwake na wakamuweka chini ya ulinzi kwa kosa la uhalifu uliotokea maeneo ya Kimara bucha.

Na anasema walihisi walimpata kupitia Facebook, (mutual friend mmoja akatafutwa kisha akawaelekeza kwake).

Rafiki yangu si mtu wa kujichanganya sana na watu. Iwe usiku au mchana, akiwa ndani hujui na wala akienda kibaruani hujui.

Anasema ahusiki na tukio na wala hajafanya uhalifu wala kuwa na rekodi yoyote ya uhalifu.
Hapa tunashindwa cha kufanya.

Hatujui kama kweli kahusika au lah!

Sisi tunajua ahusiki ila binadamu hubadilika.

Ila maadam iko mikononi mwa jeshi la polisi tutajua tu hatma yake na wahusika halisi

Chana au haribu kabisa karatasi/tiketi ya basi/meli/treni/ndege/CV/copy yako ya NIDA na nyinginezo zenye taarifa zako sahihi ili kuepuka kupata matatizo.
Hapa kuna mambo kadhaa ya kutafakari;
1. Kwanza hakuna mhalifu mjinga ambaye atafanya uhalifu wake huko kisha aache ushahidi wa wazi kama huo. Yaani mtu atoe tiketi mfuko wa suruali ama kwenye begi kisha aidondoshe mahali hapo ni ngumu hivo kiupelelezi inaonekana kabisa ni mbinu ya wahalifu kutaka kumwangushia jamaa jumba bovu.

2. Pili, huyo mkazi wa Tegeta kama ni kweli alitoka Arusha basi hakukuwa na ulazima wa kushuka Mbezi. Hii inaonesha kwamba alipanda gari la kupitia Chalinze ambapo njia rahisi kwake ilikuwa ni kupanda magari yapitayo Bagamoyo ili ashuke Tegeta. Kitendo cha yeye kueleza kwamba alishuka Mbezi na kutupa tiketi yake hapo kinaleta ukakasi na kufanya azidi kutiliwa shaka.

3. Kupokea wito wa polisi ni jambo moja, kuitikia wito huo ni jambo jingine. Hapa namaanisha kwamba huyo jamaa kama alipata mashaka ya hao waliompatia wito basi angeenda kituo cha karibu yake aeleze jinsi alivyoitwa huko (Kituo A) kisha awaambie hao jamaa wamsaidie kuthibitisha kupitia njia ambazo wao wanazifahamu kuliko yeye kujiamulia kuzima hadi simu kabisa.

Hitimisho la mchango wangu hapa ni kwamba tuache mamlaka ifanye uchunguzi wake japokuwa itakula muda wa mhusika lakini ndo hivo jumba lishamuangukia. Kama atachomoka Amen na kama akinasa pia hatuna budi kumuombea🙏🙏
Jamani, Jamani

Wapendwa wa humu narudia tena, Chana au haribu kabisa tiketi au karatasi yoyote yenye taarifa zako sahihi kwa usalama wako.

Niko hapa Police Kimara, rafiki yangu wa kiume amekamatwa na kuwekwa ndani baada ya tiketi yake ya ki-electronic ya basi moja kutoka Arusha kuja Dar kukutwa kwenye tukio la uhalifu Kimara Bucha.

Yeye rafiki yangu anasema baada ya kushuka Mbezi Magufuli stendi, aliamua kuikunja na kuitupa tiketi yake karibu na lango la kutokea na baada ya hapo akaendelea na safari ya kuelekea kwake Tegeta.

Anasema zilipita siku 2 akapigiwa simu na police kuwa anahitajika kituoni Kimara.
Anasema hakwenda kwa kuhofia huenda ni watu wasio wema kisha akazima simu.

Anasema kesho yake anashangaa kuona police wako nyumbani kwake na wakamuweka chini ya ulinzi kwa kosa la uhalifu uliotokea maeneo ya Kimara bucha.

Na anasema walihisi walimpata kupitia Facebook, (mutual friend mmoja akatafutwa kisha akawaelekeza kwake).

Rafiki yangu si mtu wa kujichanganya sana na watu. Iwe usiku au mchana, akiwa ndani hujui na wala akienda kibaruani hujui.

Anasema ahusiki na tukio na wala hajafanya uhalifu wala kuwa na rekodi yoyote ya uhalifu.
Hapa tunashindwa cha kufanya.

Hatujui kama kweli kahusika au lah!

Sisi tunajua ahusiki ila binadamu hubadilika.

Ila maadam iko mikononi mwa jeshi la polisi tutajua tu hatma yake na wahusika halisi

Chana au haribu kabisa karatasi/tiketi ya basi/meli/treni/ndege/CV/copy yako ya NIDA na nyinginezo zenye taarifa zako sahihi ili kuepuka kupata matatizo.
 
Back
Top Bottom