Wana JF narudia tena, haribu kabisa tiketi au karatasi yenye taarifa zako kamili

Wana JF narudia tena, haribu kabisa tiketi au karatasi yenye taarifa zako kamili

Unafikiri wale wapelelezi ni wajinga hawakwenda shule? Ukiwa na kesi inayohitaji upelelezi utajua kuwa wanajua wanachofanya.
Polisi wana vitengo,kuna vitengo tofauti.
Nilishuhudia hi kwenye ile kesi ya yule billionaire wa Arusha(jina limenitoka;aliuliwa alipokwenda kuonana na wauza madini).

Sema kibongobongo resources zinatumika kesi kihusisha wakubwa tu tofauti na mbele. Ili mradi umefia kwenye nchi yao lazima wareconstuct tukio na kusaka wahusika
 
Ninaelewa kwamba kila kinachokutwa kwenye crime scene kinaweza tumika kuanzisha mchakato wa upepelezi...

Sasa kwenye tukio la uvamizi na ujambazi kama ilivyoelezwa na mleta mada, kitu pekee kinachomuunganisha jamaa na huo uhalifuni ni uwepo tu wa karatasi "inayodhaniwa" kuwa ni tiketi ya basi...

Polisi walipaswa wajue kwanza uhalali wa hiyo tiketi,

1. Je ni halisi au imenakiliwa?

2. Huyu mtu alisafiri, je huko alipokwenda si alikutana na watu, hao watu wanaweza kuthibitisha uwepo wake huko?

3. Kwenye database za makampuni ya telecom, simu huwa zinaacha kumbukumbu ikiwemo periodic locations wakati inapohama mahali hadi mahali, polisi wangeweza kutumia hili pia...

Polisi inapokamata mtu inabaswa iwe na ushahidi wa kutosha usio na shaka, hatua ya ukamataji iwe ni ya mwisho.
Sasa Bongo unapata mtu anakamatwa, halafu unaambiwa upelelezi unaendelea ili mradi tu wamtie mtu lupango wamtese kulazimisha akiri makosa...
Si ndio maana wanaendelea na uchunguzi. Kwani vitu vyote hivyo wanaweza kuvipata siku moja kama unasema watatakiwa pia kuwasiliana na makampuni ya simu, wenye bus husika pia maswala ya DNA kama yanahitajika. Tuwaacha waendelee na upelelezi kwanza. Pia hatuwezi kumsemea sana huyo jamaa anaweza akawa alihusika pia tena kama inasemekana ni mtu mkimya sana na msiri sana, wengi wao huwa ni hatari sana.
 
Kosa la rafiki yako ni kushindwa kutii sheria bila shuruti.

Kwa nini azime simu baada ya kujua kuwa anahitajika kituo cha Polisi.
 
Kuna kitu kinaitwa alibi. Na sio mara zote kisapotiwe na rafiki zako, siku hizi kuna smartphone ambayo inaweza kutumika kujua ulikuwa wapi na wakati gani.

Najua kwasababu sio kada atapata shida, lakini ni jambo dogo sana hilo, kama una alibi mzuri na kuna namna ya kuisupport either physically au digitallly unakwepa hizi mambo.

Mfano alienda nyumbani myda wa tukio alikuwa amewasha smartphone, laptop au smartTV hivi vitu vnaweza kukubebaba. Au bodaboda, mangi,jirani pia wanaweza kuhusika kukubeba hapa.

Mwamba arudi mtaani, mafisadi waingie ndani.
mkuu hizi njia zako mbona haziaminiki sana kwenye kukunasua na msala.kwani hiyo kuwasha Smart tv,laptop au simu unaweza usiwe karibu navyo yaani unaweza kuwasha simu au trakick device yoyote alafu unaiacha geto kwako mfano unaishi mbagala au bagamoyo kisha unaenda kupiga tukio huko mbezi.mpaka hapo ushapiga chenga hii ya kuangalia simu yako ilisoma wapi wakati wa tukio kwa wapelezi smart haiwezi kuwa na nguvu sana japo inafaa..kwa ishu ya jamaa kwa maelezo ya mtoa mada hiyo risiti yake ya basi ya EFD baada ya wezi kuvunja duka na kuiba vitu kisha hiyo risiti ya basi ya EFD wakaweka juu ya meza wakasepa zao ..hapo finger print inaweza saidia kujua nani alishika ticket mara ya mwisho.
 
mkuu hizi njia zako mbona haziaminiki sana kwenye kukunasua na msala.kwani hiyo kuwasha Smart tv,laptop au simu unaweza usiwe karibu navyo yaani unaweza kuwasha simu au trakick device yoyote alafu unaiacha geto kwako mfano unaishi mbagala au bagamoyo kisha unaenda kupiga tukio huko mbezi.mpaka hapo ushapiga chenga hii ya kuangalia simu yako ilisoma wapi wakati wa tukio kwa wapelezi smart haiwezi kuwa na nguvu sana japo inafaa..kwa ishu ya jamaa kwa maelezo ya mtoa mada hiyo risiti yake ya basi ya EFD baada ya wezi kuvunja duka na kuiba vitu kisha hiyo risiti ya basi ya EFD wakaweka juu ya meza wakasepa zao ..hapo finger print inaweza saidia kujua nani alishika ticket mara ya mwisho.
Zinafanya kazi inategemea kwa angle gani umetazama.Screen time, authentication, interaction zako kwenye apps zinafanya kazi nimeona kesi kibao watu wa digital forensic wakitumia.

Inaporeconstruct tukio huwezi tegemea dhan moja pekee, vipi kama aliyepiga tukio alihakikisha ticket haiguswi na mwingine mpaka anapeleke kwenye scene? unadhani ni ngumu?

Kama mtu unafuatilia hiyo ishu ya fingerprint mbona inakwepa sana. Watu wanaingia ndani wanaua, wanachomoka polisi wanainvestigate scene hawapati ushahidi wowote.

Ndiyo maana unaona polisi mbele wanaanza na alibi ya mtu kabla ya kitu kingine chochote na nani au kwa namna gani inaweza kuthibitishwa.
 
mkuu hizi njia zako mbona haziaminiki sana kwenye kukunasua na msala.kwani hiyo kuwasha Smart tv,laptop au simu unaweza usiwe karibu navyo yaani unaweza kuwasha simu au trakick device yoyote alafu unaiacha geto kwako mfano unaishi mbagala au bagamoyo kisha unaenda kupiga tukio huko mbezi.mpaka hapo ushapiga chenga hii ya kuangalia simu yako ilisoma wapi wakati wa tukio kwa wapelezi smart haiwezi kuwa na nguvu sana japo inafaa..kwa ishu ya jamaa kwa maelezo ya mtoa mada hiyo risiti yake ya basi ya EFD baada ya wezi kuvunja duka na kuiba vitu kisha hiyo risiti ya basi ya EFD wakaweka juu ya meza wakasepa zao ..hapo finger print inaweza saidia kujua nani alishika ticket mara ya mwisho.
Umenifurahisha, unawaza kwamba hawa jamaa wanapeleleza kiutalaam kama kule majuu?
Labda kama mwathirika wa wizi (mwenye mali) awe kigogo mkubwa, ndio watafanya hayo yote ya fingerprints, sijui DNA etc. Kama tukio limetokea dukani tu kwa Massawe au Mpemba wa kawaida, kanatumwa kapolisi fulani ambako kanataka pesa kutoka kwa aliyeibiwa na kutoka kwa mtuhumiwa.

Nimewahi kuibiwa kwa kwa kubomolewa milango na madirisha, na wakaondoka na vitu. Matukio mawili yalikuwa ya usiku na moja la mchana.
Katika matukio yote hayo nilikuwa nafikiri polisi watakuja na full gear na kufanya kama nionavyo kwenye CSI tv series lakini wapi bwana.
Wanafika wanakuuliza unamshuku nani? una hela ya maji? Wanazunguka zunguka tu na kusema faili sijui limefunguliwa kituoni. Kila ukienda kuulizia, mara gari halina mafuta, eti uweke mafuta kwenye defender halafu wakafanye upelelezi. Hii nchi ukiwa mdogo kiuchumi na kimadaraka, ni mateso sana.

Katika matukio hayo, tukio mmoja nilifanikiwa kumkamata mwizi mmoja kwa ushirikiano wa wananchi wenzangu na kutumia polisi wakituo kingine (kishikaji) ambapo tulianzia kwa aliyekutwa na mali iliyoibwa.
 
Huu ushauri ni mzuri lakini inategemea na mazingira unachana tiketi ukiwa umekamilisha mambo yako yote , mfano imetokea nimekamatwa usikia na ndo nimetoka safari nikionyrsha ticket itakuwa ni isalama wangu, usichane tiketi kabla ya kufika sehemu kisudiwa na kumaliza mambo yako kisha geuka
Sahihi kbsa
 
Hata vocha ya karatasi , chana vipande vipande tupa.
Hili ni tangazo lilitolewa kabisa ukiitumia chana, natumia vocha mara chache sana, jamaa walifanya uhalifu/mauaji wakaacha vocha kwenye tukio, kilichomkuta mtumiaji wa ile vocha anakijua mwenyewe, kuanzia hapo nikutumia nachana vipande hata 20 maana vinne vitano wataungaunisha
 
Ni kwamba police hawana akili; sio issue ya kuchana na kutupa! Maisha yamejawa na Mazingira ambayo yanaweza kumuingiza mtu kwenye shida nyingi, ni busara za hao Police zinatakiwa!

Imagine umekutana na Mdada kwenye Bus, mrembo, ukamtongoza, ukaomba namba ya simu, ukamtext jioni hiyo fresh mkachat usiku.

Usiku huo huo akauwawa, unajua kwa akili za Police wa Tanzania unaweza kukaa magereza miaka 3 kama mtuhumiwa wa mauaji? Lakini sio USA, kum arrest mtu sio jambo rahisi!
Kwa polisi wetu wa Tanzania Mtu wa Mwisho kuwasiliana au kuonana na marehemu ndo mtuumiwa mkuu hakuna cha upelelezi ni kubashiri tu
 
Mleta mada kuna uwezekano rafiki yako kahusika moja kwa moja kwenye tukio.

Yeye kukataa wito wa polisi na kuzima simu ni viashiria tosha kwamba jamaa kahusika directly ama indirectly

Anyways, Muda utaongea na ukweli utajulikana
 
Pole yake sana.
Hayo maujinga yanatumiwa sana na wahalifu, lengo likiwa ni kuchelewesha ufuatiliaji wa Polisi.

Mkuu siyo tiketi na document zingine muhimu tu, hata hizi vocha za kukwangua ni mbaya sana kutupa tupa ovyo.

Ikiokotwa na hao jamaa kisha kutupwa kwenye tukio, wakifuatilia vocha ilijazwa kwenye simu gani, utakwenda na maji.

Kuja kujulikana hauhusiki, pamepitwa!
Huu ni uzembe na uvivu wa wapelelezi na polisi, Ni simple tu kabla ya kukamata mtu waangalie vocha ilijazwa mda gani na tarehe ngapi, walinganishe na mda wa tukio la uhalifu, na siyo kukurupuka kukamata mtu kwakua tu umekuta vocha kwenye eneo la tukio
 
Back
Top Bottom