Wana JF narudia tena, haribu kabisa tiketi au karatasi yenye taarifa zako kamili

Wana JF narudia tena, haribu kabisa tiketi au karatasi yenye taarifa zako kamili

Tukio lilitokea lini? Muda gani? Kukuta tiketi yake sio uthibitisho kuwa alikuwa eneo la tukio. Bado polisi wanatakiwa kuthibitisha kuwa alikuwepo eneo la tukio. Tiketi inawezekana iliachwa hapo n mhalifu makusudi ili kuwapoteza polisi.
Mtuhumiwa awaambie alikuwa wapi siku na muda ambao tukio linatokea. Na anaweza kutafuta ALIBI...wapo watu alikuwa nao,alikuwa kazini(miamala aliofanya itaonekana) na simu yake inaweza kutumika kuonesha alikuwa wapi siku hio.
Yeye ni mtuhumiwa tu na polisi inabidi wathibitishe,watansumbua tu ila kama hakupiga tukio itajulikana.
Hapo kitakachomuokoa labda simu imuoneshe alikuwa wapi wakati huo.
Manaa tukio limetokea saa 9 alfajiri, keshatoka kwenye kazi zake za uwakala. Na anasema baada ya kufunga alijifungia ndani mpaka kesho yake alipofungua tena kibanda chake.
Mimi na wewe hatujui, tuwaachie polisi
 
Nj

Hizi Huwa ni njia dhaifu na za kivivu kwa askari vipi kama vocha imewekwa siku mbili nyuma alafu tukio likatoke siku mbili MBELE?
Kuna jamaa alihusishwa na mauaji kisa yeye ndiye alikuwa wa mwisho kuongea na marehemu, kuna watoto walifungwa baada ya kuokota simu zilizotupwa na jambazi aliyetekeleza mauaji maala flani.
 
Pole yake sana.
Hayo maujinga yanatumiwa sana na wahalifu, lengo likiwa ni kuchelewesha ufuatiliaji wa Polisi.

Mkuu siyo tiketi na document zingine muhimu tu, hata hizi vocha za kukwangua ni mbaya sana kutupa tupa ovyo.

Ikiokotwa na hao jamaa kisha kutupwa kwenye tukio, wakifuatilia vocha ilijazwa kwenye simu gani, utakwenda na maji.

Kuja kujulikana hauhusiki, pamepitwa!
Hao police nao itakua ni wendawazimu tu kwamba wahalifu waache kufanya uhalifu wao uliowapelek hayo maeneo waanze kuhangaika na kutia vocha kwenye simu au sio ? 😄
 
Hao police nao itakua ni wendawazimu tu kwamba wahalifu waache kufanya uhalifu wao uliowapelek hayo maeneo waanze kuhangaika na kutia vocha kwenye simu au sio ? 😄
Hapana, hajamaanisha hivo.
Kamaanisha kuwa jambazi anaweza okota vocha yako iliyotumika akaja kuiacha sehemu alikofanyia uhalifu ili msala ukuangukie wewe na si wao kuweka vocha.
 
Hamna kesi hapo na hajazingiziwa.kapiga deal katambaa na watu wakamtafuta.
Hizo tkt huwezi kuforge nk qr code na pin ambazo ni wewe utamiliki.
Kutupa ni kupoteza ushahidi pia.
 
Rafiki yangu si mtu wa kujichanganya sana na watu. Iwe usiku au mchana, akiwa ndani hujui na wala akienda kibaruani hujui.

Hatujui kama kweli kahusika au lah!

Sisi tunajua ahusiki ila binadamu hubadilika.

Ila maadam iko mikononi mwa jeshi la polisi tutajua tu hatma yake na wahusika halisi.
 
Usimtetee sana....

kuna kesi ya dogo mmoja hivi, dem wake alikua anaapa viapo vyote "huyu hawezi kubaka namjua tangu utotoni bla bla anasali ni mpole bla bla blaaa" jamaa nmekaa nae mezani nkaongea nae vizuri tu " kuwa mkweli hili tukio umefanya au haujafanya" kwa kinywa chake akasema kafanya....kabaka.

Baadae kidem kinakuja vipi amesemaje, namie nkakipoza tu hajafanya.

Huyo jamaa yeye mwenyewe ndio anaujua ukweli
Oya mwanangu usiniambie ulimuacha bila hata vibao huyo nyang'au
 
Hapana, hajamaanisha hivo.
Kamaanisha kuwa jambazi anaweza okota vocha yako iliyotumika akaja kuiacha sehemu alikofanyia uhalifu ili msala ukuangukie wewe na si wao kuweka vocha.
Nimemuelewa vyema tu ila iyo vocha haitoshelezi kuwa ni kithibitisho cha ushahidi kuwa kweli mwenye vocha ndio amehusika na uwo uhalifu,

Kwa akili ya kawaida tu mhalifu hana uwo muda wa kuhangaika na kutia vocha kwenye cm yake tena sehemu ambayo amefanyia uhalifu.

Sema kwa nchi zetu za africa izi polisi wetu wapo nyuma san kweny mambo ya upelelezi lolote linawezekana kwa wao 🤣🤣
 
Umewahi kuchunguza karatasi zinazotumika kama mifuko kufungia vitafunio au kwenye maduka ya Mangi?
 
Nimemuelewa vyema tu ila iyo vocha haitoshelezi kuwa ni kithibitisho cha ushahidi kuwa kweli mwenye vocha ndio amehusika na uwo uhalifu,

Kwa akili ya kawaida yu mhalifu hana uwo muda wa kuhangaika na kutia vocha kwenye cm yake tena sehemu ambayo amefanyia uhalifu.

Sema kwa nchi zetu za africa izi polisi wetu wapo nyuma san kweny mambo ya upelelezi lolote linawezekana kwa wao 🤣🤣
Kabisa, na hapo mpaka kujinasua ujue muda ushaenda sana tu
 
Katika mambo ya investigation kitu chochote kinachokuwa eneo la tukio.lazima kifanyiwe kazi,iwe,leso kipande cha chupa hata kipisi cha sigara,humo zitapatikana alama za vidole,au chochote kile iwe nywele,mate nakadhalika

Kuna tukio moja la mauji nadhan mwanza kuna mwanadada maarufu sana aliuwawa,bahati mbaya muuaji aliacha chupa ya soda eneo la tukio,basi ikapimwa DNA ikasoma,ikasaidia uchunguzi
Kweli kabisa, kwenye nchi zilizoendelea kwa sayansi na teknolojia kwenye Matumizi ya kazi za kijeshi, jambo kubwa la Kwanza kabisa kulitekeleza ingekuwa ni Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kisayansi wa kupima DNA kuhusiana na hiyo ticket iliyookotwa ili kutambua ni Watu gani hasa waliohusika katika kuishika hiyo tiketi iliyookotwa katika eneo la tukio (scene of crime)? Majibu yangepatikana ndani ya muda mfupi kabisa usiozidi saa moja.
Lakini kwa kuwa Jeshi la Polisi la nchi hii bado linafanya kazi zake kwa mtindo wa Ujima Kama vile bado tupo kwenye zama za mawe za kale, Basi matokeo ya uchunguzi wao utakuwa Kama ni matokeo ya kutoka kwa mganga wa kienyeji katika zoezi la kupiga 'ramli chonganishi.'
 
Umewahi kuchunguza karatasi zinazotumika kama mifuko kufungia vitafunio au kwenye maduka ya Mangi?
Yaani zina full details za watu.
hizi bahasha nyeupe za karatasi kariakoo kwenye maduka ya vipodozi yaani ni hatari
 
Kweli kabisa, kwenye nchi zilizoendelea kwa sayansi na teknolojia kwenye Matumizi ya kazi za kijeshi, jambo kubwa la Kwanza kabisa kulitekeleza ingekuwa ni Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kisayansi wa kupima DNA kuhusiana na hiyo ticket iliyookotwa ili kutambua ni Watu gani hasa waliohusika katika kuishika hiyo tiketi iliyookotwa katika eneo la tukio (scene of crime)? Majibu yangepatikana ndani ya muda mfupi kabisa usiozidi saa moja.
Lakini kwa kuwa Jeshi la Polisi la nchi hii bado linafanya kazi zake kwa mtindo wa Ujima Kama vile bado tupo kwenye zama za mawe za kale, Basi matokeo ya uchunguzi wao utakuwa Kama ni matokeo ya kutoka kwa mganga wa kienyeji katika zoezi la kupiga 'ramli chonganishi.'
Kabisa, yaani hapo pona pona yake sijui itakuwaje
Wenzetu kesi ingekuwa imeisha chap!!!
 
Na anasema walihisi walimpata kupitia Facebook, (mutual friend mmoja akatafutwa kisha akawaelekeza kwake).
Polisi wanaingia kwenye mfumo wa mawasiliano na kuangalia namba hiyo inafanya manunuzi gani, mfano, kulipa bill za maji au manunuzi ya LUKU, halafu wanatafuta mamlaka sahihi labda TANESCO nk wanapata exact location ya ilipo LUKU ndio unakuta hao wametimba kwako hata kama ni chaka kiasi gani.
 
Jamani, Jamani

Wapendwa wa humu narudia tena, Chana au haribu kabisa tiketi au karatasi yoyote yenye taarifa zako sahihi kwa usalama wako.

Niko hapa Police Kimara, rafiki yangu wa kiume amekamatwa na kuwekwa ndani baada ya tiketi yake ya ki-electronic ya basi moja kutoka Arusha kuja Dar kukutwa kwenye tukio la uhalifu Kimara Bucha.

Yeye rafiki yangu anasema baada ya kushuka Mbezi Magufuli stendi, aliamua kuikunja na kuitupa tiketi yake karibu na lango la kutokea na baada ya hapo akaendelea na safari ya kuelekea kwake Tegeta.

Anasema zilipita siku 2 akapigiwa simu na police kuwa anahitajika kituoni Kimara.
Anasema hakwenda kwa kuhofia huenda ni watu wasio wema kisha akazima simu.

Anasema kesho yake anashangaa kuona police wako nyumbani kwake na wakamuweka chini ya ulinzi kwa kosa la uhalifu uliotokea maeneo ya Kimara bucha.

Na anasema walihisi walimpata kupitia Facebook, (mutual friend mmoja akatafutwa kisha akawaelekeza kwake).

Rafiki yangu si mtu wa kujichanganya sana na watu. Iwe usiku au mchana, akiwa ndani hujui na wala akienda kibaruani hujui.

Anasema ahusiki na tukio na wala hajafanya uhalifu wala kuwa na rekodi yoyote ya uhalifu.
Hapa tunashindwa cha kufanya.

Hatujui kama kweli kahusika au lah!

Sisi tunajua ahusiki ila binadamu hubadilika.

Ila maadam iko mikononi mwa jeshi la polisi tutajua tu hatma yake na wahusika halisi

Chana au haribu kabisa karatasi/tiketi ya basi/meli/treni/ndege/CV/copy yako ya NIDA na nyinginezo zenye taarifa zako sahihi ili kuepuka kupata matatizo.
Na hapo unataka police wasikushuku 😂 kama muhusika hadi kuzima simu kwanini yeye asireport police waarifu wanamtafuta hata kituo kingine basi kama si kikara😂
 
Aeleze ukweli wote is all, then akae kimya, wala asisumbuke, ila kama kweli ni Mhalifu basi akomae, tuna wahalifu wengi tu kwenye Jamii zetu humu mtaani!

  • Unaitwaje Police unazima simu?
  • Unakaa kabisa home na Amani?

Dalili za Mhalifu hizo hapo 2, mtu mwema akiwa na wito police hawezi relax!

Mazingira yamamuonyesha Kama mhalifu
 
Jamani, Jamani

Wapendwa wa humu narudia tena, Chana au haribu kabisa tiketi au karatasi yoyote yenye taarifa zako sahihi kwa usalama wako.

Niko hapa Police Kimara, rafiki yangu wa kiume amekamatwa na kuwekwa ndani baada ya tiketi yake ya ki-electronic ya basi moja kutoka Arusha kuja Dar kukutwa kwenye tukio la uhalifu Kimara Bucha.

Yeye rafiki yangu anasema baada ya kushuka Mbezi Magufuli stendi, aliamua kuikunja na kuitupa tiketi yake karibu na lango la kutokea na baada ya hapo akaendelea na safari ya kuelekea kwake Tegeta.

Anasema zilipita siku 2 akapigiwa simu na police kuwa anahitajika kituoni Kimara.
Anasema hakwenda kwa kuhofia huenda ni watu wasio wema kisha akazima simu.

Anasema kesho yake anashangaa kuona police wako nyumbani kwake na wakamuweka chini ya ulinzi kwa kosa la uhalifu uliotokea maeneo ya Kimara bucha.

Na anasema walihisi walimpata kupitia Facebook, (mutual friend mmoja akatafutwa kisha akawaelekeza kwake).

Rafiki yangu si mtu wa kujichanganya sana na watu. Iwe usiku au mchana, akiwa ndani hujui na wala akienda kibaruani hujui.

Anasema ahusiki na tukio na wala hajafanya uhalifu wala kuwa na rekodi yoyote ya uhalifu.
Hapa tunashindwa cha kufanya.

Hatujui kama kweli kahusika au lah!

Sisi tunajua ahusiki ila binadamu hubadilika.

Ila maadam iko mikononi mwa jeshi la polisi tutajua tu hatma yake na wahusika halisi

Chana au haribu kabisa karatasi/tiketi ya basi/meli/treni/ndege/CV/copy yako ya NIDA na nyinginezo zenye taarifa zako sahihi ili kuepuka kupata matatizo.
Sijawahi kuchukua karatasi ya ticket Kwa sababu kwenye simu inatumwa na ikihitajika ofisini Kwa sababu ya refund nina print
 
Polisi wanaingia kwenye mfumo wa mawasiliano na kuangalia namba hiyo inafanya manunuzi gani, mfano, kulipa bill za maji au manunuzi ya LUKU, halafu wanatafuta mamlaka sahihi labda TANESCO nk wanapata exact location ya ilipo LUKU ndio unakuta hao wametimba kwako hata kama ni chaka kiasi gani.
Ohh, kumbe.
Basi sisi tukajua hawa mutual wametumika kumlengesha
 
Back
Top Bottom