Wana JF narudia tena, haribu kabisa tiketi au karatasi yenye taarifa zako kamili

Wana JF narudia tena, haribu kabisa tiketi au karatasi yenye taarifa zako kamili

Polisi nao huwa hawaeleweki. Wengine nao ni vibaka tu. Na kuna wengine uwezo wa kiakili na kielimu ni duni. Wameajiriwa na div 4-30. na kila kitu wanataka kusolve kinguvu badala ya kufikiria kwa weledi mkubwa. Ifike mahali jeshi liwe linapima uwezo wa mtu kabla ya kumpa jukumu la upelelezi.

Aliyekamatwa kwenye hii story, kazi yake ya uwakala inawezekana pia imemhusisha na tukio fulani la dhuluma na sasa wameamua kumbambika hiyo kesi. Na pia inawezekana naye ni criminal na alihusika kwenye tukio la Kimara. Lolote linawezekana.
 
Jamani, Jamani

Wapendwa wa humu narudia tena, Chana au haribu kabisa tiketi au karatasi yoyote yenye taarifa zako sahihi kwa usalama wako.

Niko hapa Police Kimara, rafiki yangu wa kiume amekamatwa na kuwekwa ndani baada ya tiketi yake ya ki-electronic ya basi moja kutoka Arusha kuja Dar kukutwa kwenye tukio la uhalifu Kimara Bucha.

Yeye rafiki yangu anasema baada ya kushuka Mbezi Magufuli stendi, aliamua kuikunja na kuitupa tiketi yake karibu na lango la kutokea na baada ya hapo akaendelea na safari ya kuelekea kwake Tegeta.

Anasema zilipita siku 2 akapigiwa simu na police kuwa anahitajika kituoni Kimara.
Anasema hakwenda kwa kuhofia huenda ni watu wasio wema kisha akazima simu.

Anasema kesho yake anashangaa kuona police wako nyumbani kwake na wakamuweka chini ya ulinzi kwa kosa la uhalifu uliotokea maeneo ya Kimara bucha.

Na anasema walihisi walimpata kupitia Facebook, (mutual friend mmoja akatafutwa kisha akawaelekeza kwake).

Rafiki yangu si mtu wa kujichanganya sana na watu. Iwe usiku au mchana, akiwa ndani hujui na wala akienda kibaruani hujui.

Anasema ahusiki na tukio na wala hajafanya uhalifu wala kuwa na rekodi yoyote ya uhalifu.
Hapa tunashindwa cha kufanya.

Hatujui kama kweli kahusika au lah!

Sisi tunajua ahusiki ila binadamu hubadilika.

Ila maadam iko mikononi mwa jeshi la polisi tutajua tu hatma yake na wahusika halisi

Chana au haribu kabisa karatasi/tiketi ya basi/meli/treni/ndege/CV/copy yako ya NIDA na nyinginezo zenye taarifa zako sahihi.
Tukio lilitokea lini? Muda gani? Kukuta tiketi yake sio uthibitisho kuwa alikuwa eneo la tukio. Bado polisi wanatakiwa kuthibitisha kuwa alikuwepo eneo la tukio. Tiketi inawezekana iliachwa hapo n mhalifu makusudi ili kuwapoteza polisi.
Mtuhumiwa awaambie alikuwa wapi siku na muda ambao tukio linatokea. Na anaweza kutafuta ALIBI...wapo watu alikuwa nao,alikuwa kazini(miamala aliofanya itaonekana) na simu yake inaweza kutumika kuonesha alikuwa wapi siku hio.
Yeye ni mtuhumiwa tu na polisi inabidi wathibitishe,watansumbua tu ila kama hakupiga tukio itajulikana.
 
Usimtetee sana....

kuna kesi ya dogo mmoja hivi, dem wake alikua anaapa viapo vyote "huyu hawezi kubaka namjua tangu utotoni bla bla anasali ni mpole bla bla blaaa" jamaa nmekaa nae mezani nkaongea nae vizuri tu " kuwa mkweli hili tukio umefanya au haujafanya" kwa kinywa chake akasema kafanya....kabaka.

Baadae kidem kinakuja vipi amesemaje, namie nkakipoza tu hajafanya.

Huyo jamaa yeye mwenyewe ndio anaujua ukweli
Kumbe mjeda😂
 
Tiketi ya basi inahusiana vipi na uhalifu hata kama imekutwa eneo la uhalifu??

Anyway, tiketi za electronics huwa zinaacha footprint kwenye database husika iliyotumika kukata tiketi, mtandao wa simu nao hubaki na kumbukumbu...

Simu yake kama alisafiri inaacha alama za mahali alipotembelea kwenye database za mitandao ya simu...

Hakuna kesi hapo unless hii iwe togwa mixer alkasusu...
Katika mambo ya investigation kitu chochote kinachokuwa eneo la tukio.lazima kifanyiwe kazi,iwe,leso kipande cha chupa hata kipisi cha sigara,humo zitapatikana alama za vidole,au chochote kile iwe nywele,mate nakadhalika

Kuna tukio moja la mauji nadhan mwanza kuna mwanadada maarufu sana aliuwawa,bahati mbaya muuaji aliacha chupa ya soda eneo la tukio,basi ikapimwa DNA ikasoma,ikasaidia uchunguzi
 
Tatizo ni kwamba you're not a logical thinker kama hao polisi tu, naona umeshindwa kuelewa comment yangu kwamba polisi hawajawaza nje ya boksi wametumia shortcut kama kawaida yao...
Haya, wewe na u-logical thinker wako utanisaidia nini kwenye hii ishu bhana?
Acheni kujifanya mnajua kila kitu katika maisha ya watu wengine.
Halafu sikukuita wala kukuambia ni lazima uchangie post yangu.
Majukwaa yako mengi bro na unaweza kwenda jukwaa lolote mkuu.
 
Tukio lilitokea lini? Muda gani? Kukuta tiketi yake sio uthibitisho kuwa alikuwa eneo la tukio. Bado polisi wanatakiwa kuthibitisha kuwa alikuwepo eneo la tukio. Tiketi inawezekana iliachwa hapo n mhalifu makusudi ili kuwapoteza polisi.
Mtuhumiwa awaambie alikuwa wapi siku na muda ambao tukio linatokea. Na anaweza kutafuta ALIBI...wapo watu alikuwa nao,alikuwa kazini(miamala aliofanya itaonekana) na simu yake inaweza kutumika kuonesha alikuwa wapi siku hio.
Yeye ni mtuhumiwa tu na polisi inabidi wathibitishe,watansumbua tu ila kama hakupiga tukio itajulikana.
Yes, na ndio manaa leo tunasubiri kukuche vizuri ili tukajue kinachoendelea.
 
Katika mambo ya investigation kitu chochote kinachokuwa eneo la tukio.lazima kifanyiwe kazi,iwe,leso kipande cha chupa hata kipisi cha sigara,humo zitapatikana alama za vidole,au chochote kile iwe nywele,mate nakadhalika

Kuna tukio moja la mauji nadhan mwanza kuna mwanadada maarufu sana aliuwawa,bahati mbaya muuaji aliacha chupa ya soda eneo la tukio,basi ikapimwa DNA ikasoma,ikasaidia uchunguzi
Yaani mkuu, kuna watu humu ndani sijui wanajikutaga wao nani.
Yaani ni pointless kabisa.
Kasoma mada kuu bila kuichambua kaja kukimbilia ku-comment bila kufikiri.
Yote tuwaachie jeshi la police wa dili na mtu wao.
Wanaleta sana ujuaji wakati kichwani ni sifuri.
 
Tatizo kubwa vyombo vyetu vya usalama vinafanya kazi kwa ramli, mazoea na kwa kuwanyanyasa watu wa Hali ya chini.....kwa kuwa hakuna Askari aliyewahi kuwajibishwa kwa uonevu wao dhidi ya wanyonge wenyewe wanaona kawaida.......

Hiyo issue ingemhusisha mtoto au ndugu wa kigogo wa serikali asingemkamata kama kuku hivyo na pengine angemuomba kumkamata......

Imagine unakamatwa ndio uchunguzi unafanyika ukionekana huna hatia unaachiliwa kama kuku......
 
Yaani mkuu, kuna watu humu ndani sijui wanajikutaga wao nani.
Yaani ni pointless kabisa.
Kasoma mada kuu bila kuichambua kaja kukimbilia ku-comment bila kufikiri.
Yote tuwaachie jeshi la police wa dili na mtu wao.
Wanaleta sana ujuaji wakati kichwani ni sifuri.
Penye wengi pana mengi my dear,tuwavumilie tu wasije wakakuharibia siku yako

Stay strong
 
Jamani, Jamani

Wapendwa wa humu narudia tena, Chana au haribu kabisa tiketi au karatasi yoyote yenye taarifa zako sahihi kwa usalama wako.

Niko hapa Police Kimara, rafiki yangu wa kiume amekamatwa na kuwekwa ndani baada ya tiketi yake ya ki-electronic ya basi moja kutoka Arusha kuja Dar kukutwa kwenye tukio la uhalifu Kimara Bucha.

Yeye rafiki yangu anasema baada ya kushuka Mbezi Magufuli stendi, aliamua kuikunja na kuitupa tiketi yake karibu na lango la kutokea na baada ya hapo akaendelea na safari ya kuelekea kwake Tegeta.

Anasema zilipita siku 2 akapigiwa simu na police kuwa anahitajika kituoni Kimara.
Anasema hakwenda kwa kuhofia huenda ni watu wasio wema kisha akazima simu.

Anasema kesho yake anashangaa kuona police wako nyumbani kwake na wakamuweka chini ya ulinzi kwa kosa la uhalifu uliotokea maeneo ya Kimara bucha.

Na anasema walihisi walimpata kupitia Facebook, (mutual friend mmoja akatafutwa kisha akawaelekeza kwake).

Rafiki yangu si mtu wa kujichanganya sana na watu. Iwe usiku au mchana, akiwa ndani hujui na wala akienda kibaruani hujui.

Anasema ahusiki na tukio na wala hajafanya uhalifu wala kuwa na rekodi yoyote ya uhalifu.
Hapa tunashindwa cha kufanya.

Hatujui kama kweli kahusika au lah!

Sisi tunajua ahusiki ila binadamu hubadilika.

Ila maadam iko mikononi mwa jeshi la polisi tutajua tu hatma yake na wahusika halisi

Chana au haribu kabisa karatasi/tiketi ya basi/meli/treni/ndege/CV/copy yako ya NIDA na nyinginezo zenye taarifa zako sahihi.
Katika nchi zenye tawala Bora na za kisheria sambamba na kuwa na Jeshi la Polisi lenye uadilifu, suala hili lingeweza kuwa rahisi sana. Lakini kwa kuwa Jeshi la Polisi lililopo halina sifa hizo za Uadilifu, basi huyo mtu anatakiwa ajipange sawa sawa, he should expect the worse to come. Namuonea huruma sana huyo mtu, tayari ameshaingia kwenye mtego mbaya wa hawa jamaa, huyo Sasa amegeuzwa kuwa fursa na hao Polisi waliomkamata.
 
Shida ipo Kwa hao polisi hapo pia, unaokotaje tu kikaratasi kinachoweza kusafiri hata na upepo ukaanza kufanya ndio ushahidi wa kumuweka mtu ndani?
Tiketi isafiri na upepo kutoka Mbezi hadi ndani ya duka ulikotokea uhalifu?
Ndio maana nasema tuwaachie jeshi la police lifanye yao.
Ukweli utajulikana tu mkuu
Ndio maana nikasema pale 'binadamu hubadilika' huenda kahusika au hajahusika.
Ushahidi utajionesha
 
Back
Top Bottom