Wana JF narudia tena, haribu kabisa tiketi au karatasi yenye taarifa zako kamili

Wana JF narudia tena, haribu kabisa tiketi au karatasi yenye taarifa zako kamili

Kabisa, Mimi Hakuna namna nitaitwa Police nisiende, tena wakisema niende kesho wala sitalala, I want to get over issues haraka, na wala sina mtu wa kuniteka!

Kuna dogo Mmoja niliambiwa ameiba Milioni Tatu. Sasa Kwa jinsi Mimi ninavyomjua Yule dogo nikawa namtetea. Yule boss akaniambia "Robert wewe hujui. Mimi mtu mzima nimeona wezi wa aina nyingi. Huyu dogo sio wakwanza"
Dogo hataki kwenda kwa Boss, tumemuitia Polisi katoroka kwao.

Hapo ndio nikaanza kuwa na mashaka, wazazi wake Wanamtetea kuwa hakukimbia kwa sababu ya wizi Bali Sababu ya hofu ya Polisi.

Polisi wakaishia kucheka tuu. Siku mbili zilizofuata, dogo Akiwa na Wazazi wake wakaleta Milioni mbili na Laki Moja na nusu wakasema hizo zingine wataleta kidogokidogo. Kwani dogo amezitumia.

Yaani yule dogo alinifundisha Jambo Moja, usimpime mtu Kwa kumwangalia
 
Katika nchi zenye tawala Bora na za kisheria sambamba na kuwa na Jeshi la Polisi lenye uadilifu, suala hili lingeweza kuwa rahisi sana. Lakini kwa kuwa Jeshi la Polisi lililopo halina sifa hizo za Uadilifu, basi huyo mtu anatakiwa ajipange sawa sawa, he should expect the worse to come. Namuonea huruma sana huyo mtu, tayari ameshaingia kwenye mtego mbaya wa hawa jamaa, huyo Sasa amegeuzwa kuwa fursa na hao Polisi waliomkamata.
Enzi hizo kama 20yrs ago niko nchi za watu nilinunua simu ya dili. Nina rafiki yangu alikuwa mwingi kidogo. Alikuwa na rafiki zake Wapakistan. Wale walikuwa wanaiba simu kutoka warehouse inayohifadhi handset za kampuni fulani wa simu. Moja ya hio simu,very latest and expensive nikauziwa mimi.
Siku moja nikapokea simu mtu akajitambulisha ni polisi kutoka investigation unit blah blah. Akanitaja kwa majina,akataja simu ninayotumia na akaniuliza umeipata wapi. Nikamwambia nimenunua lkwa mtu ambae nilikuwa introduced na rafiki yangu. Akasema sawa,hio simu ni ya wizi na ni sehemu ya uchunguzi wa uhalifu mkubwa. Kwasababu umetoa ushirikiano endelea kutumia. Akakata simu. Alipokata tu simu nikaachana na ile simu na hawakujitafuta tena. Baadae nilisikia wale vijana Wapakistan walikula miaka 7 jela.
Sasa hapa unaona polisi wanaojua kazi yao. Ingekuwa hapa Tz sijui ingekuwaje.
 
Tuseme hivi, kujiunga na jeshi la polisi kiwango cha chini kabisa ni degree kutoka chuo kinachotambuliwa.
Unafikiri wale wapelelezi ni wajinga hawakwenda shule? Ukiwa na kesi inayohitaji upelelezi utajua kuwa wanajua wanachofanya.
Polisi wana vitengo,kuna vitengo tofauti.
 
Jamani, Jamani

Wapendwa wa humu narudia tena, Chana au haribu kabisa tiketi au karatasi yoyote yenye taarifa zako sahihi kwa usalama wako.

Niko hapa Police Kimara, rafiki yangu wa kiume amekamatwa na kuwekwa ndani baada ya tiketi yake ya ki-electronic ya basi moja kutoka Arusha kuja Dar kukutwa kwenye tukio la uhalifu Kimara Bucha.

Yeye rafiki yangu anasema baada ya kushuka Mbezi Magufuli stendi, aliamua kuikunja na kuitupa tiketi yake karibu na lango la kutokea na baada ya hapo akaendelea na safari ya kuelekea kwake Tegeta.

Anasema zilipita siku 2 akapigiwa simu na police kuwa anahitajika kituoni Kimara.
Anasema hakwenda kwa kuhofia huenda ni watu wasio wema kisha akazima simu.

Anasema kesho yake anashangaa kuona police wako nyumbani kwake na wakamuweka chini ya ulinzi kwa kosa la uhalifu uliotokea maeneo ya Kimara bucha.

Na anasema walihisi walimpata kupitia Facebook, (mutual friend mmoja akatafutwa kisha akawaelekeza kwake).

Rafiki yangu si mtu wa kujichanganya sana na watu. Iwe usiku au mchana, akiwa ndani hujui na wala akienda kibaruani hujui.

Anasema ahusiki na tukio na wala hajafanya uhalifu wala kuwa na rekodi yoyote ya uhalifu.
Hapa tunashindwa cha kufanya.

Hatujui kama kweli kahusika au lah!

Sisi tunajua ahusiki ila binadamu hubadilika.

Ila maadam iko mikononi mwa jeshi la polisi tutajua tu hatma yake na wahusika halisi

Chana au haribu kabisa karatasi/tiketi ya basi/meli/treni/ndege/CV/copy yako ya NIDA na nyinginezo zenye taarifa zako sahihi ili kuepuka kupata matatizo.
Hata vocha oliyotumika
 
Katika mambo ya investigation kitu chochote kinachokuwa eneo la tukio.lazima kifanyiwe kazi,iwe,leso kipande cha chupa hata kipisi cha sigara,humo zitapatikana alama za vidole,au chochote kile iwe nywele,mate nakadhalika

Kuna tukio moja la mauji nadhan mwanza kuna mwanadada maarufu sana aliuwawa,bahati mbaya muuaji aliacha chupa ya soda eneo la tukio,basi ikapimwa DNA ikasoma,ikasaidia uchunguzi

Ninaelewa kwamba kila kinachokutwa kwenye crime scene kinaweza tumika kuanzisha mchakato wa upepelezi...

Sasa kwenye tukio la uvamizi na ujambazi kama ilivyoelezwa na mleta mada, kitu pekee kinachomuunganisha jamaa na huo uhalifuni ni uwepo tu wa karatasi "inayodhaniwa" kuwa ni tiketi ya basi...

Polisi walipaswa wajue kwanza uhalali wa hiyo tiketi,

1. Je ni halisi au imenakiliwa?

2. Huyu mtu alisafiri, je huko alipokwenda si alikutana na watu, hao watu wanaweza kuthibitisha uwepo wake huko?

3. Kwenye database za makampuni ya telecom, simu huwa zinaacha kumbukumbu ikiwemo periodic locations wakati inapohama mahali hadi mahali, polisi wangeweza kutumia hili pia...

Polisi inapokamata mtu inabaswa iwe na ushahidi wa kutosha usio na shaka, hatua ya ukamataji iwe ni ya mwisho.
Sasa Bongo unapata mtu anakamatwa, halafu unaambiwa upelelezi unaendelea ili mradi tu wamtie mtu lupango wamtese kulazimisha akiri makosa...
 
Polisi wanaingia kwenye mfumo wa mawasiliano na kuangalia namba hiyo inafanya manunuzi gani, mfano, kulipa bill za maji au manunuzi ya LUKU, halafu wanatafuta mamlaka sahihi labda TANESCO nk wanapata exact location ya ilipo LUKU ndio unakuta hao wametimba kwako hata kama ni chaka kiasi gani.
Ohh, kumbe.
Basi sisi tukajua hawa mutual wametumika kumlengesha
Kuna njia mbalimbali za kiuchunguzi za kuweza ku-trace na ku-track Watu au Wahalifu. Zipo njia nyingi sana,
 
Haya, wewe na u-logical thinker wako utanisaidia nini kwenye hii ishu bhana?
Acheni kujifanya mnajua kila kitu katika maisha ya watu wengine.
Halafu sikukuita wala kukuambia ni lazima uchangie post yangu.
Majukwaa yako mengi bro na unaweza kwenda jukwaa lolote mkuu.

Eboh! mbona una panic na kupangia watu vitu vya kuandika...

Wewe si ndiye uliyeleta kisa cha maisha ya mtu mwingine hapa tujadili tukio lake 😂
 
Kuna kitu kinaitwa alibi. Na sio mara zote kisapotiwe na rafiki zako, siku hizi kuna smartphone ambayo inaweza kutumika kujua ulikuwa wapi na wakati gani.

Najua kwasababu sio kada atapata shida, lakini ni jambo dogo sana hilo, kama una alibi mzuri na kuna namna ya kuisupport either physically au digitallly unakwepa hizi mambo.

Mfano alienda nyumbani myda wa tukio alikuwa amewasha smartphone, laptop au smartTV hivi vitu vnaweza kukubebaba. Au bodaboda, mangi,jirani pia wanaweza kuhusika kukubeba hapa.

Mwamba arudi mtaani, mafisadi waingie ndani.
 
Kuna dogo Mmoja niliambiwa ameiba Milioni Tatu. Sasa Kwa jinsi Mimi ninavyomjua Yule dogo nikawa namtetea. Yule boss akaniambia "Robert wewe hujui. Mimi mtu mzima nimeona wezi wa aina nyingi. Huyu dogo sio wakwanza"
Dogo hataki kwenda kwa Boss, tumemuitia Polisi katoroka kwao.

Hapo ndio nikaanza kuwa na mashaka, wazazi wake Wanamtetea kuwa hakukimbia kwa sababu ya wizi Bali Sababu ya hofu ya Polisi.

Polisi wakaishia kucheka tuu. Siku mbili zilizofuata, dogo Akiwa na Wazazi wake wakaleta Milioni mbili na Laki Moja na nusu wakasema hizo zingine wataleta kidogokidogo. Kwani dogo amezitumia.

Yaani yule dogo alinifundisha Jambo Moja, usimpime mtu Kwa kumwangalia

Kabisa, ni sahihi!
 
Back
Top Bottom