Uchaguzi 2020 Wana JF, nipeni Pole. Msinicheke wala msinibeze; nimegombea ubunge Kawe kupitia CCM nimeambulia kura 1. Ama kweli CCM ina wenyewe!

Shida yako unatanguliza pesa eti utahawa milioni 10 kila kata,mzee wa kitimoto unazingua umeshindwa kuomba kura ipasavyo
Ni kama vile ulienda kujitangaza tu wakufahamu kwamba na wewe upo CCM,eti mm mzee wa kitimoto nimeunga juhudi, huko ndo kujinadi kweli,ndo Gwajima kawapita kwa mbali sana☺☺☺☺
 
Pole mwenzio yaliwahi nikuta miaka hiyo

Nilikwambia kaka mayalla 2020 haifai kwa siasa tusubiri 2025ila wewe ukaamin moyo wako unaojipinga

Usitegemee mbachao kwa msala upitao

Tengeneza siasa yako na Tz unayoitaka
 
Paschal Usikate tamaa 2025 ipo, tuombe uzima kwa Mwenyez Mungu. Kura moja Ni kura halali pia.
 
Huyu ndiye Mjomba wa Magufuli aliyeshinda Kura za Maoni Kawe. Yupo GCLA(maabara ya Taifa) yeye ndo incharge, pale hamna mtu wa kumpinga akisema hold mzee ni hold hamna wa kukupa release hata uende wapi, anaishi masaki kwa sasa. Hata cheo alichonacho ni figisu-figisu.

#Wasifu:
Jina: Furaha Dominic Jacob
Kazaliwa: Chato Kagera
Shule: Chato Secondary School
Shule: Makongo High school
Chuo : DIT
Reseach: Technician at International Institute of Tropical Agriculture (IITA)

Na Kwa sasa anaishi Dar es Salaam


Mtoto wa dada yake Rais MAGUFULI.

 
Dooh!!!
 
Huyo moja aliyekupa Kura hajitambui kabisa. Huwa nikiangalia unachokiandika humu naona sicho unachokiamini, Unajichanganya wee kumbe unatafuta hisani. We na Ole Mushi hamjielewi kabisa. Mna fikra Pana Ila Njaa Kali na tamaaa.

Aliyekupa Kura huyo moja sijui alimaanisha au nazani hajui Kusoma au alikosea tu kuona.
 
Asante kwa kutupa mwanga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…