Wana macho lakini hawaoni, wana masikio lakini hawasikii. CHADEMA wana macho? Je, wawasamehe Wabunge 19 wabarikiwe, au wakomae nao walaaniwe?

Wana macho lakini hawaoni, wana masikio lakini hawasikii. CHADEMA wana macho? Je, wawasamehe Wabunge 19 wabarikiwe, au wakomae nao walaaniwe?

Moja ya hasara ya kitaifa, ni hawa wabunge 19 kulipwa posho/ mshahara kinyume na sheria.

Wote tunajua kwamba chama kilishawavua uwanachama.
Kama Dola haitaki wale COVID 19 wavuliwe ubunge wao, automatically hawewezi vuliwa ubunge huo,may be chadema wanajua ukweli ila wameamu kuwa safe side ili wasionekane wasaliti,Kwa nchi hii politics is our way to the destination of woe...
 
Ukisoma comments za wadau utaona kwamba zaidi ya asilimia 90 wanapinga ulichokiandika. Maana yake ni kwamba hoja zako hazina relevance yoyote, hivyo unatakiwa kubadilika. Watu si wajinga tena wa kulishwa propaganda zako.
Mkuu malantu , hao asilimia 90 wanaonipinga hawaijui katiba kikamilifu katiba ya Chadema!, bahati nzuri sana imetokea tuu mimi pia ni mwanasheria na somo nililopindua utadhani mtihani natunga mimi ni LW. 100, Katiba!.

Hii sii mara ya kwanza mimi kutofautiana na public opinion humu, hata kwenye issue hii Nimesikitishwa, huzunishwa na kufadhaishwa na uongo wa Kamati ya PAC! Escrow sio fedha za umma! tulitofautiana na wengi na nikasema
Wanabodi,

Kwa waliosoma fasihi, kitabu cha "An Enemy of the People" by Henrik Ibsen mnaweza kuniita mimi Paskali kuwa ni "an enemy of the people!", Ibsen anasema, the strongest man on earth is the man who can stand alone!", hivyo na mimi, katika jambo ambalo nina uhakika nalo na ninaamini ni ukweli, nitasimama nalo, hata kama nitabaki peke yangu!.

Fedha za Escrow, Sio Fedha za Umma!, hizo Bilioni 320 zilizokuwa kwenye account ya Escrow, hazijaibiwa!, bali zimetumika kulipia umeme! kwa kumlipa mfua umeme, IPTL, hivyo sio fedha za umma!
Paskali
Hivyo mimi sifuati formula ya wengi wape hata kama ni vilaza!. Nitasimama na ukweli na mwisho wa siku ukweli ndio husimama mpaka mwisho!.
P
 
Si ndivyo nilivyosema au wewe unataka nisemeje? Soma vizuri tangu nilipoanza ku'post' hii post labda hapo utaelewa ninachokisema. In fact, nilitofautiana na Paskali Mayala anayeona Chadema hawakuwatendea haki. Nikamuuliza kama anaona kugushi barua na sahihi kwamba walipendekezwa na kupewa baraka za chama ni sahihi. Hoja imeanzia hapo. Sasa unaniambia nini, mkuu? Soma tangu mwanzo utaona ninasema nini.
Achana na hilo zee njaa akili zipo tumboni.
Mpka umri huo bado anawaza kupata kazi za kuteuliwa kwa kulamba watu makalio.
Ni aibu sana kwa taifa na shule walizo soma kuwa na watu wa namna hii.
 
Achana na hilo zee njaa akili zipo tumboni.
Mpka umri huo bado anawaza kupata kazi za kuteuliwa kwa kulamba watu makalio.
Ni aibu sana kwa taifa na shule walizo soma kuwa na watu wa namna hii.
Hapana hiyo lugha unayotumia siyo ya staha. Hata mimi ni mzee na hata wewe utakuwa mzee. Tunajadiliana na tunaweza kutofautiana na tukitofautiana tusianze kutoleana maneno ya kuudhi. Au wewe hukuwahi kushiriki mijadala/debate shule ya msingi au sekondari - kununua baiskeli ni bora kuliko kununua radio? Kwani watoa mada kwenye hii mijadala wakitofautiana (kama ulikuwa ukishiriki) walikuwa wakitoleana maneno ya kuudhi? Hapana! Mwisho wa debate walikuwa wakishikana mikono. Ndivyo inavyotakiwa kwa watu wanaojadiliana. Tumia lugha nzuri na utaeleweka tu. By the way, hata mimi ni mzee na bado natafuta ajira ili familia ile maana sitaki niwe ombaomba. Kama una mihela ya kusaidia wazee wasitafute ajira nikupe namba yangu unirushie ili nipunguze idadi ya wazee wanaotafuta ajira wanaokukera.
 
Wanabodi

Kama kawa kila nipatapo fursa, huja na makala zangu elimishi za kwa maslahi ya taifa, Chadema ni chama cha Kitaifa hivyo haya yanayoendelea ndani ya Chadema katika huu mgogoro wake na wabunge wake 19 wa viti maalum, una athari za Kitaifa zenye maslahi kwa taifa. Hoja yangu ya leo ni hii ,"kuna watu wana macho lakini hawaoni!, na wana masikio lakini hawasikii!". Swali ni je Chadema wana macho na yanaona?. Je wana masikio na yanasikia?. Kwenye hili la Wabunge 19, je Chadema wawasamehe wabarikiwe, au waendelee kukomaa nao mpaka kieleweke hata kama ni kulaaniwa?.

Naomba kukiri kupandisha bandiko hili, kwa inspirational kutoka andiko la Kaka yangu/mdogo wangu na bosi wangu kule TEF, Deodatus Balile.

Balile ameandika bandiko hili akiwa safarini jijini New Delhi nchni India.
C&P ya Balile

Mwisho wa kunukuu

Chief @⁨Balile⁩ , nikiwa New Delhi nilijifunza imani ya Hinduism kuhusu kitu kinachoitwa karma, hivyo ushauri wako kwa Chadema, utawaepushia Chadema karma ya mambo
mabaya waliowatenda hawa wadada 19 ambao mimi nawaita ni mashujaa, hivyo huu ni ushauri mzuri, wa hekima na busara sana kwa Chadema wenye maslahi kwa Chadema na maslahi kwa taifa only if Chadema wana macho ya kuona na wanaona, na wana masikio ya kusikia na wanasikia, kwasababu kuna watu wana macho lakini hawaoni, na wana masikio lakini hawasikii.

Wakati Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe anakabiliwa na kesi ya ugaidi, nilipandisha makala mfufulizo za Kilio cha Haki, nikiangazia haki jinai.
Kwenye sala yetu ya Baba Yetu, kuna mstari "Utusamehe makosa yetu kama tunavyowasamehe waliotukosea" hivyo tulimpongeza rais Samia kwa kauli hii baada ya Freeman Mbowe kuombewa msamaha
Watanzania tumshukuru Mungu kupata mtu mwenye moyo wa kusamehe. Je, tumuombe asamehe tu bila kuombwa msamaha au akomae naye?

Baada tuu ya bandiko hili, haukupita muda hatimaye Freeman Mbowe alisamehewa na kesi ya Mbowe ilifutwa!,

Sisi wa kupongeza tukapongeza
Asante sana Rais Samia kwa kuliponya Taifa. Umeonesha kwa kauli na matendo; tunajenga nyumba moja, hakuna sababu ya kugombea fito!

Sasa kuna ugumu gani Chadema kuwasamehe hawa wabunge wake 19?.

Hili sakata la wabunge hawa toka lilipoanza, mimi nimekuwa very open, objective and very transparent
Na nikashauri Chadema



Katika Salaam zangu kwa mwaka mpya, Mahali ni pazuri ndugu wanapokaa, wakipata vema na kupendana. Tulikotoka ni kugumu, tunakokwenda ni kurahisi, kuzuri! Heri ya Mwaka Mpya wahusika wote

Japo kwa jicho la juu juu, hao 19, wanaonekana kama wameshinda kesi yao mahakamani but in reality ni wameshindwa na hili nililisema The Voices From Within: "Mahakamani Watashindwa Tena!" Sababu ni Mawakili! Jee Tanzania Tuna Mawakili wa Calibre ya Murtaza Lakha?Jitokezeni Kusaidia! kwasababu katiba ya Chadema ina kipengele kilicho kinyume cha katiba, mwanachama wa Chadema akifungua shauri lolote mahakani, akishindwa kesi ni amejifukuzisha, hivyo Mahakama tayari imeishabariki kufukuzwa kwao, salama yao ni kusamehewa tuu!.

Kwa vile mimi namfahamu Freeman Mbowe kuliko Chadema wengi, Mbowe ni muungwana, Mbowe ni mtu wa shukrani, na baada ya kikao cha CC kuwatimua, Freeman Mbowe aliingia huruma na kufukuzwa kwao, akawasamehe, akawaita Nairobi, akawasamehe, akawashauri waombe msamaha, ili wayamalize, wakamgomea!.

It's high time Mwenyekiti wa Chadema, Mhe. Freeman Aikael Mbowe, kuitumia kofia yake ya Uenyekiti wa Chadema kwa kuitekeleza kwa vitendo sala ya Baba Yetu, kwa mtindo wa reciprocity kama yeye alivyosamehewa bila kuomba msamaha, sasa ni zamu ya na yeye kusamehe tuu bila kuombwa msamaha?., au Chadema iendelee kukomaa nao ili kuwaonyesha, kuwakomoa na kuwanyorosha?.

Tena na mimi kwa vile ubavu wangu ni pande za Kaskazi, na mimi nimeunga tela hija za migombani.

Merry Christmas

Paskali.
PASCAL, PASCHAL, PASKALI ni jina la Kikristo. Sikuwahi kuona andiko katika vitabu vitakatifu linalosema watu wote watakwenda mbinguni bila masharti maana Mungu alishawasmehe Kwa kifo cha Yesu Msalabani.
Kwa hiyo wewe unapoleta andiko la kuwataka CHADEMA kuitisha kikao Peke yao, kuwasamehe Covid 19 bila wao kukiri kosa wlilotenda sijui unalitoa katika andiko gani au unàlitoa katika desturi gani? Wapi huko uliwahi kuona msamaha unatangazwa kabla ya mkosaji kukiri na kuomba kusamehewa?
Mt 18:15-17
15-Nduguyo akikukosea muonye mkiwa wawili Peke yenu, akikubali (AKIKIRI) umempata nduguyo.
16-Asipokubali chukua pamoja na mashahidi wawili au watatu......
17-Asipowasikiliza lijukishe Kanisa na asipowasikia na wao na awe kwako kama MTU WA MATAIFA na MTOZA USHURU.

1.Wameambiwa Peke yao hawakusikia.
2.Wakaitwa mashahidi wachache (Kamati Kuu) hawakushuka wala kukiri kosa.
3.Likaambiwa Kanisa(Wanachama wote) wakakaidi na kwenda mahakamani.

Sasa wamefanywa kama watu Baki, unawalàumu CHADEMA Kwa nini wasiwasamehe?
 
Figure of speech in quotation marks. Some kind of reward au mere gratification of the soul.
Thanks ila kwa ruhusa yako naomba kuitumia post yako hii kama mbegu ya kuoteshea bandiko langu fulani.
Nimesoma mada zako nyingi kuhusu CHADEMA na sijashawishika kuwa zinaandikwa na mtu mwenye nia njema kuhusu hicho chama na upinzani kwa ujumla. Ni kama mtu anaye-celebrate ubabe wa chama dola kwa wapinzani na wananchi kwa ujumla.
Mkuu Drifter, honestly nimefarijika sana na comments zako, kwasababu kiukweli kabisa humu JF ni wachache sana wanaonisoma na kunielewa most of times naishia kutukanwa, kubezwa na kusimangwa, wenzangu wengi wa calibre yangu wenye ngozi laini, ama wameachana na JF, ama wapo wapo tuu kama hawapo, mimi naendelea kuwepo kwasababu naandika from my heart and I love it, 2024 nitakuwa naandikia magazeti 6!, na kipindi changu hiki,
View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=BsKLwZgJL2nHPPqF
kinarushwa kwenye vituo 5 vya TV, najihesabu very honest, truthfully, bonafide na genuine, kujua na wewe unanisoma, ni furaha yangu.
Ushauri wangu kwa Chadema ni very truthful na wenye nia njema ya kweli!. Mimi ni mmoja wa wana CCM ambao hata CCM ikiboronga, tunaibalasa, rais akiboronga tunambananisha.
Angalia mabandiko yangu haya kwa viongozi wa CCM - Elections 2015 - Kama Hii ni Kweli, Then, Serikali Yetu ni Serikali Dhalimu?, Haramu?. Hukumu ya Karma ii Juu Yake!
Na hata sasa Mama nae anakula spana za kutosha tuu, ila kwa vile ni Mwanamke, respect na humility is applied as well wakati spana za JPM zilikuwa ni spana za makavu live!. Kumuenzi Magufuli: Tujikumbushe 'spana' za JF zilivyomsaidia Hayati Magufuli na Taifa. Je, Samia pia tumsaidie kwa 'spana' au tumkune tu tusimpare?

P
 
Andiko nzuri my Adv.Mayala, ila HAKUNA mgogoro ndani ya CHADEMA, huo mgogoro unaouna wewe kama mwandishi,
Mkuu Nkanini, kuna kitu kinachoitwa reality vs visibility, yaani muonekano, in reality Chadema ina mgogoro na hao 19, ila ni kweli kwa myopic visibility ya Chadema kwa ndani, wao ni hakuna mgogoro wowote, kwasababu kwao baada ya CC kuwatimua kwao hiyo issue imekwisha its final and conclusive. Hili jambo ukiliangalia from point of view of uchama Chadema, then you are right, hakuna mgogoro hili jambo limekwisha!, lakini ukiliangalia kwa jicho la haki bin haki, jee CC ya Chadema imewatendea haki?, jee wamefukuzwa kwa haki?, jee taratibu za kufukuza kwa mujibu wa katiba ya Chadema, zilifuatwa?. Halima Mdee ni Mwenyekiti wa Bawacha, Mamlaka yake ya nidhamu ni Baraza Kuu, CC ya Chadema ilipata wapi mamlaka kusikiliza shauri lake na kumtimua?. Hoja yangu hapa kwenye hii issue, hakuna mkamilifu, Chadema sio wakamilifu kwasababu hawakuwaatimua kwa haki kwa mujibu wa katiba ya Chadema, hivyo the best option kwa muda uliobakia ni kuwasamehe, vinginevyo Chadema waitishe tena Baraza Kuu, wamalizane nao, na wakimalizana, wanarudi mahakamani, kufumba kufumbua ni 2025 hiyo!.
P.
 
issue hii CHADEMA walishatoa uamuzi wake na uamuzi ule ulikua kuwafukuza uanachama wale watuhumiwa,
Mkuu Nkanini, naamini katiba ya Chadema unaijua na umeisoma, imeweka utaratibu gani wa kuwafuta uanachama wanachama wake!, kwanini utaratibu huo haufuatwi?.
kwa shinikizo la chama dola wakaenda mahakamani
Nashauri kwenye hili lets deals with facts on hand, haki ya kutafuta haki mahakamani ni takwa la katiba ya JMT, hivyo hao 19 wanayo haki hiyo bila shinikizo kutoka popote au kwa yeyote, unless kama una ushahidi na uthibitisho wa hilo shinikizo!.
P
 
na hukumu imetoka, case hii imefungwa,
It's true hukumu imetoka case closed. Jee hukumu hii ni ya haki?. Imewatendea haki hawa 19?.

Jee wajua haki ya mtu huwa haipotei?.
Hoja kuu ya bandiko hili sio kuwaombea watu msamaha bali kuwafungua macho watu wenye macho lakini hawaoni!, na wana masikio, wanaambiwa lakini hawasikii!.

Chadema did the same kwa Juliana Shonza, Zitto Kabwe, Prof. Kitila Mkumbo, angalia mahali walipo sasa and compared kama wangekuwa Chadema?.

Pia kuna yule mlinzi wa Dr. Wilbroad Slaa, aitwae Khalid Kagenzi, kuna kitu alifanyiwa Chadema, kuna Mwigamba, kuna kitu alifanyiwa Arusha!.

Chadema fungueni macho muangalie nini kilikuja kuwatokea viongozi wa Chadema walioongoza operations hizo?. Can't you connect the dots kuwa it might be karna?.

Kama wale ni wachache tuu, hawakutendewa haki, karma zake ndio hizo, can you imagine what about hawa 19?.

Kama hawa 19 ni wakosaji, kwa kufoji na kujiteua, kwanini Chadema isithibitishe kwanza kosa, kisha ikawatimua kwa haki?.

Kama katiba ya Chadema imeweka utaratibu wake wa kuyashughulikia masuala ya nidhamu ndani ya chama, kuna ugumu gani kwa Chadema, kuufuata?.

A Best Way Forward
Kwa vile mahakama imeamuru kikao cha Baraza Kuu kifanyike upya kusikiliza rufaa zao,
  1. Chadema ianze moja, itoa tangazo la kufuta maamuzi batili ya CC kuwatimua, na badala yake itoe taarifa polisi ya kufanyika jinai ya forgery ndani ya Chadema katika barua za uteuzi
  2. Jeshi la polisi litawataka Chadema kuwasilisha bona-fide genuine headed paper zake stamped na kufanya uchaguzi wa forensic wa barua za uteuzi zilizowasilishwa NEC.
  3. Mamlaka ya kufanya uchaguzi wa kijinai Tanzania ni PT only. Hivyo Polisi wakijiridhisha kweli barua za uteuzi ni forgery, Chadema wanapewa uthibitisho wa evidence ya forgery.
  4. Wanaiandikia NEC kuripoti forgery hiyo na evidence ya polisi. NEC wanatoa barua za utenguzi wa ubunge wao na kuzipeleka Bungeni.
  5. Bunge linawatengua ubunge wao.
  6. Chadema inawaandalia hati 19 za mashitaka ya kufoji.
  7. Inaitisha kikao cha CC kuwasikikiza kwa kufuata taratibu zote kwa mujibu wa katiba ya Chadema na kisha kuwatimua hao 18 isipokuwa Mdee kwasababu Mamlaka yake ya nidhamu sio CC ya Chadema.
  8. Wakikata rufaa, ndipo Chadema Inaitisha kikao cha Baraza Kuu na agenda mbili. Agenda ya kwanza ni kikao cha Baraza Kuu kama mamlaka ya nidhamu ya Halima Mdee, hiki kinakaa full kikiongozwa na mwenyekiti.
  9. Agenda ya pili ni kikao cha Baraza Kuu Chadema kama mamlaka ya rufaa ya wale Wabunge 18 kama watakata rufaa, hapa sasa ndio takwa la mahakama linafuatwa wajumbe wa CC ya Chadema waliowatimua hao 18, wanatoka nje.
  10. Jambo hili linakuwa limemalizika kwa haki na amani na Chadema inabaki salama.
P
 
na tuelewe kuwa kujiunga na chama cha kisiasa ni hiari ila ni muhimu katiba ya chama hicho kuiheshimu.
Mkuu Nkanini, hapa nakuunga mkono asilimia 100% chini ya 100%.
Tanzania yangu inahitaji kuwa na uchaguzi huru na wa haki.
Pia hapa Mkuu Nkanini, hapa nakuunga mkono asilimia 100% chini ya 100% ndio maana mimi mwenyewe nineisha pandisha mabandiko yanafika hata zaidi ya 100 kuzungumzia hitaji la uchaguzi wa huru na haki, utakao simamiwa na Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi.
P
 
Mbowe alikwisha wasamehe ndio maana huwa hazungumzii hao watu ila walio mzunguuka Mbowe ndio tatizo!
Sintashangaa kama Mbowe atakuwa kinara kutaka hao covid19 wasamehewe kwani yeye na hao wanawake ndio vibaraka wa ccm. As long as Mbowe ni Mwenyekiti wa hicho chama kitaendelea kuwa saccos yake and the opposition will forever be weak!
 
Sintashangaa kama Mbowe atakuwa kinara kutaka hao covid19 wasamehewe kwani yeye na hao wanawake ndio vibaraka wa ccm. As long as Mbowe ni Mwenyekiti wa hicho chama kitaendelea kuwa saccos yake and the opposition will forever be weak!
Wee Mkuu Bulesi , usiseme hivi, wenyewe hawapendi maukweli ya kihivi!, niliwahi kuandika kitu humu, Voices From Within: Unaweza usiamini! Aliyetoa A Go ahead kwa Mdee na Wenzake ni Kigogo wa Chadema!. Alikuwepo Ukumbini na Vikaoni! Je, ni nani?
P
 
Sintashangaa kama Mbowe atakuwa kinara kutaka hao covid19 wasamehewe kwani yeye na hao wanawake ndio vibaraka wa ccm. As long as Mbowe ni Mwenyekiti wa hicho chama kitaendelea kuwa saccos yake and the opposition will forever be weak!
Wafuasi watiifu hawataki kusikia hiii!
 
Wanabodi

Kama kawa kila nipatapo fursa, huja na makala zangu elimishi za kwa maslahi ya taifa, Chadema ni chama cha Kitaifa hivyo haya yanayoendelea ndani ya Chadema katika huu mgogoro wake na wabunge wake 19 wa viti maalum, una athari za Kitaifa zenye maslahi kwa taifa. Hoja yangu ya leo ni hii ,"kuna watu wana macho lakini hawaoni!, na wana masikio lakini hawasikii!". Swali ni je Chadema wana macho na yanaona?. Je wana masikio na yanasikia?. Kwenye hili la Wabunge 19, je Chadema wawasamehe wabarikiwe, au waendelee kukomaa nao mpaka kieleweke hata kama ni kulaaniwa?.

Naomba kukiri kupandisha bandiko hili, kwa inspirational kutoka andiko la Kaka yangu/mdogo wangu na bosi wangu kule TEF, Deodatus Balile.

Balile ameandika bandiko hili akiwa safarini jijini New Delhi nchni India.
C&P ya Balile

Mwisho wa kunukuu

Chief @⁨Balile⁩ , nikiwa New Delhi nilijifunza imani ya Hinduism kuhusu kitu kinachoitwa karma, hivyo ushauri wako kwa Chadema, utawaepushia Chadema karma ya mambo
mabaya waliowatenda hawa wadada 19 ambao mimi nawaita ni mashujaa, hivyo huu ni ushauri mzuri, wa hekima na busara sana kwa Chadema wenye maslahi kwa Chadema na maslahi kwa taifa only if Chadema wana macho ya kuona na wanaona, na wana masikio ya kusikia na wanasikia, kwasababu kuna watu wana macho lakini hawaoni, na wana masikio lakini hawasikii.

Wakati Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe anakabiliwa na kesi ya ugaidi, nilipandisha makala mfufulizo za Kilio cha Haki, nikiangazia haki jinai.
Kwenye sala yetu ya Baba Yetu, kuna mstari "Utusamehe makosa yetu kama tunavyowasamehe waliotukosea" hivyo tulimpongeza rais Samia kwa kauli hii baada ya Freeman Mbowe kuombewa msamaha
Watanzania tumshukuru Mungu kupata mtu mwenye moyo wa kusamehe. Je, tumuombe asamehe tu bila kuombwa msamaha au akomae naye?

Baada tuu ya bandiko hili, haukupita muda hatimaye Freeman Mbowe alisamehewa na kesi ya Mbowe ilifutwa!,

Sisi wa kupongeza tukapongeza
Asante sana Rais Samia kwa kuliponya Taifa. Umeonesha kwa kauli na matendo; tunajenga nyumba moja, hakuna sababu ya kugombea fito!

Sasa kuna ugumu gani Chadema kuwasamehe hawa wabunge wake 19?.

Hili sakata la wabunge hawa toka lilipoanza, mimi nimekuwa very open, objective and very transparent
Na nikashauri Chadema



Katika Salaam zangu kwa mwaka mpya, Mahali ni pazuri ndugu wanapokaa, wakipata vema na kupendana. Tulikotoka ni kugumu, tunakokwenda ni kurahisi, kuzuri! Heri ya Mwaka Mpya wahusika wote

Japo kwa jicho la juu juu, hao 19, wanaonekana kama wameshinda kesi yao mahakamani but in reality ni wameshindwa na hili nililisema The Voices From Within: "Mahakamani Watashindwa Tena!" Sababu ni Mawakili! Jee Tanzania Tuna Mawakili wa Calibre ya Murtaza Lakha?Jitokezeni Kusaidia! kwasababu katiba ya Chadema ina kipengele kilicho kinyume cha katiba, mwanachama wa Chadema akifungua shauri lolote mahakani, akishindwa kesi ni amejifukuzisha, hivyo Mahakama tayari imeishabariki kufukuzwa kwao, salama yao ni kusamehewa tuu!.

Kwa vile mimi namfahamu Freeman Mbowe kuliko Chadema wengi, Mbowe ni muungwana, Mbowe ni mtu wa shukrani, na baada ya kikao cha CC kuwatimua, Freeman Mbowe aliingia huruma na kufukuzwa kwao, akawasamehe, akawaita Nairobi, akawasamehe, akawashauri waombe msamaha, ili wayamalize, wakamgomea!.

It's high time Mwenyekiti wa Chadema, Mhe. Freeman Aikael Mbowe, kuitumia kofia yake ya Uenyekiti wa Chadema kwa kuitekeleza kwa vitendo sala ya Baba Yetu, kwa mtindo wa reciprocity kama yeye alivyosamehewa bila kuomba msamaha, sasa ni zamu ya na yeye kusamehe tuu bila kuombwa msamaha?., au Chadema iendelee kukomaa nao ili kuwaonyesha, kuwakomoa na kuwanyorosha?.

Tena na mimi kwa vile ubavu wangu ni pande za Kaskazi, na mimi nimeunga tela hija za migombani.

Merry Christmas

Paskali.
Paskal hawataweza kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao
 
Back
Top Bottom