Wanachama Yanga wachana na kuchoma magazeti ya Reginald Mengi!

Tatizo kubwa sana ni elimu.

Hata common sense hawana.
 
Ni
Huu ushamb sijui utaisha lini??
Vema hata Mwandishi angesema tu " baadhi ya wanachama wa Yanga" ndio wamefanya hilo tukio badala ya kuandika kama vile wanachama walio wengi ndio wamefanya hivyo.
 
Hivi wanachama wote wa Yanga kama wangeenda Jangwani hali ingekuaje?
 

Wanachama wa Yanga wamecharuka na kufanya kitendo kinachoonyesha ni hasira kutokana na kuchana na kuchoma moto magazeti.
Wanachama hao wa Yanga, leo wamechoma moto magazeti ya Nipashena The Guardian katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye makao makuu ya klabu hiyo mtaa wa Jangwani na Twiga, Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Wanachama hao wamefanya hivyo wakipinga Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji kusakamwa kw amakusudi na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi.
“Hii sasa imetosha, huyu Mengi na magazeti yake anamsakama Manji kila anapoona Yanga inafanya vizuri. Mara tu baada ya Yanga kutinga robo fainali hatua ya Kombe la Shirikisho, basi vyombo vyake vimeanza kuandika kwamba anatakiwa sijui kuondolewa Coco Beach.
“Hakuna asiyejua Manji amestaafu Quality Group, sasa anamtaja wa nini. Au anataka ashindwe kufanya kazi za Yanga kwa utulivu.

“Watuache, kweli tutatangaza watu wa Yanga waachane na kununua bidhaa zake,” alisema Abuu Chehekaheka.
Pamoja naye, wanachama wengine kama Edward Matiku, Clement Michael na Hashimu Mtanza nao walimuunga mkono pamoja na wengine waliokuwa pale kabla ya kuanza kuchoma moto magazeti hayo wakionyesha kuwa na jazba.

Hata walipoulizwa sababu kuu za kuchoma magazeti hayo yanayomilikiwa na Mengi, hakuna aliyetaka kujibu huku wakionyesha kuwa na jazba.

 
wana ubavu wa kugomea bidhaa zote za Mengi?
 
Mambo mengine aibu sana hata kuyasimulia. Hawa ndio baadhi ya 'wadau' ambao mimi huwa nalia nao sana.

Wananunua ugomvi usiowahusu kwa karanga za kuonjeshwa.
 
Nilidhani wamewavamia wauza magazeti na kuyachoma,kumbe wameyanunua!!Hili zoezi likiwa endelevu tena nchi nzima,Mengi atatengeneza pesa sana.

Mimi nawasihi wana Yanga wote kila siku asubuhi wanunue kila mmoja nakala mojamoja za NIPASHE na Guardian halafu wazichome moto. Lazima huyu Mengi akione cha moto mwaka huu.....NB naomba manji atenge fungu maalumu kwa zoezi hili....
 
Mkuu wala usipoteze muda na hao wavamizi na waharibifu wa makazi ya vyura pale Jangwani.
 
Uko sahihi mkuu..ila ukweli Manji keshawaweza mapoyoyo wengi pale Yanga..ila kuna siku atawaliza..trust me ipo hiyo siku.
 
Mashabiki wa Yanga Luninga kwa kweli ni mamburula... Tatukuru wakija pita hapo sijui watamficha Manji hapo... kwenye MAFURIKO...

Na viwanja vya hapo walipo wanatakiwa wavunje hilo Jengo sehemu hatarishi....

Hapo Udini na kupewa pewa pesa za kulinda mfuko wanaona Manji mtu wa Maana..

Ila Mengi ana kimavi na Mirangi ya Kijani na Njano hajui tu na sijui anaipenda kwa nini ana damu ya kunguni tuseme... CCM walijiapiza kutotizama ITV kwenye uchaguzi ilipendelea sana upinzani... japo kwa kumsingizia wakati habari zake zilikuwa zinabalance ujinga wa baadhi ya wanachama hawataki upinzani uoneshwe... ila Mengi aendelee na msimamo wake wa kutoagua story Kampuni yake ibaki kuwa Super Brand.. Ndio Maana haichuji... walizokuwa wanazipenda ndio zimekosa radha... huu Ubaguzi ubaguzi sio siasa zetu Haki sawa kwa Wote ndio Msingi wetu tuendelee....

Unachoma Gazeti kila limemtaja Mwizi aliyemo ndani mwako... so Anaiba ili wewe ule... Mbabu pu zenu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…