Wanafunzi Dar na Dharau kwa Wakubwa Wao

Wanafunzi Dar na Dharau kwa Wakubwa Wao

Halafu wakifeli walimu wanawajibishwa..kwa staili hii walimu nawahurumia mtapata tabu sanaa
Ndio hapo sasa. Sababu mtoto kama hana adabu kiasi hicho sidhani kama anaweza muheshimu mwalimu wake na kutokumuheshimu ndio mwanzo wa kufanya vibaya darasani sababu hakuna kitakachoingia.

Sababu katika kusoma nidhamu nayo ni muhimu.
 
Nadhani chanzo hapo ni sisi wazazi tunaowalea. Sababu angelelewa vyema na Mzazi au Mlezi nyumbani basi hadi hapo angekuwa na heshima.

Hili ni somo kwa wazazi na walezi kwamba tulee watoto katika mstari ulionyooka kuanzia chini.

Japo kanikera sana huyo mtoto.
Zamani mtoto alikuwa mali ya wote akikosea mtu yeyote anamkanya na mzazi anafurahi tu lkn kwasasa mtoto akikosea mzazi ndiyo kwanza anambembeleza.

Wazazi wasasa tunajiona tunajua uchungu bure kabisa
 
Ndio hapo sasa. Sababu mtoto kama hana adabu kiasi hicho sidhani kama anaweza muheshimu mwalimu wake na kutokumuheshimu ndio mwanzo wa kufanya vibaya darasani sababu hakuna kitakachoingia.

Sababu katika kusoma nidhamu nayo ni muhimu.
uko sawa kabisa Hajar nidhamu ni muhimu sehemu yoyote iwe kazini au biashara au kwa wanamichezo
 
Asilimia kubwa ya tabia za watoto hujengwa na wazazi/walezi, japo kuna suala la mazingira, na asili.
Wazazi/walezi tukibadili aina ya malezi natumaini na watoto wetu watabadilika.
Mithali 22 : 6 "Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha hata atakapokua Mzee"

Pole kwa kugadhabika.
 
Mkuu kinachozungumziwa ni yale majibu machafu.

Kwani angeamua kulaza kichwa kwenye siti ya mbele yake kama wanavyofanyaga au kukaa kimya na kutokujibu huu uzi ungekuwepo?

Nimekupata mkuu ila kwa mwonekano tu wa haraka mwanafunzi alitaka kuonesha kuwa nae yumo so kuonewa tu kwa kuwa ni mwanafunzi
 
Zamani mtoto alikuwa mali ya wote akikosea mtu yeyote anamkanya na mzazi anafurahi tu lkn kwasasa mtoto akikosea mzazi ndiyo kwanza anambembeleza.

Wazazi wasasa tunajiona tunajua uchungu bure kabisa
Kweli kabisa na tena akija kumwambia mzazi alichokufanyia basi jiandae kuongezewa fimbo ili usirudie tena.

Na hii ndio shida tuliyo nayo sasa. Yatupasa tubadilike katika malezi la sivyo huko mbele itakuwa mtihani.
 
Mkiwalumu wazazi mtakosea hata ninyi mnastahili pia kwa kulaumia kwa kusababisha tabia mbaya kwa hao vijana. Unalaumu hapa vijana hawana adabu, baadae tunakukuta katka jukwa la siasa unawatukana babu zako. Na hao wanafunzi wapo humu wanajifunza nini kutoka kwetu, ndio matokeo hayo. Kuharibika kwa maadili ya vijana sote tunachangia katik jamii, wazazi, marafiki, mitandao, michezo, burudani, nk ambazo humo zi wazazi tu peke yao wanaohusika na sisi pia tupo.
 
Yani we acha tu dunia inazidi kuruka singeli siku zinavyozidi kwenda
Umeonaeeee. Ndio maana wanasema siku hizi malezi magumu yapo kwa mtoto wa kike kwani ukimchekea tu basi huko mbeleni jiandae na ndio kama huyo mtoto wa kwenye hiace.

Nawaza kwa hali hiyo sidhani kama huko nyumbani anamuheshimu mzazi au mlezi wake?
 
Wadau.

Wakati nikiwa mwanafunzi wa kidato cha tatu niliwahi kuhudhuria semina ya wiki ya nenda kwa usalama.

Hakuna sheria inayotaka mwanafunzi asimame.

Hakuna sheria inayozuia idadi ya wanafunzi kuzidi.

Sheria inataka basi kua levo siti kwakua ajali ikitokea bima itakava levo siti tu.

Tiketi ni lazima kwa kila abiria kwakua mwenye tiketi ana nafasi kubwa ya kuhudumiwa na bima.

Watu wazima waTanzania mmelemazwa mno na huu utaratibu wa chini ya mwamvuli wa maadili. Utakuta kasista du kamepanda gari kanataka kapishwe na mwanafunzi.

Halafu akiingia mama mjamzito au mzee hako hako kasista du hakasimami hapo maadili tena tupa kule.

Mnapandikiza chuki mbaya sana kwa wanafunzi. Mwanafunzi anasoma Mbweni halafu anaishi Magereza, kakaa kuanzia Mwenge mtu anapanda Tabata anataka apishwe na huyu mwanafunzi.

Hayo majibu machafu ya huyo mtoto yametokana na hii tabia shit. Mwanafunzi akizuiwa kupanda gari hakuna anayeongea mnajifanya mpo kimya hamuoni leo abiria mwenzenu kagewa za uso ndiyo mmeona tatizo?

Ila sishangilii alichofanya ila pia sioni kosa.
 
Nimekupata mkuu ila kwa mwonekano tu wa haraka mwanafunzi alitaka kuonesha kuwa nae yumo so kuonewa tu kwa kuwa ni mwanafunzi
Kabisaaaa. Na ukute kulikuwa na wanafunzi wenzie hapo ndio akataka kabisa wamjue kwamba yeye ni Mwajuma Ndala Ndefu. [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] lol
 
Back
Top Bottom