Wanafunzi Dar na Dharau kwa Wakubwa Wao

Wanafunzi Dar na Dharau kwa Wakubwa Wao

Maskini sijui huyo mama alijisikiaje. Sio kwa Dar pekee, watoto wengi wamekua na maadili mabaya.

Halafu nidhamu inaanzia nyumbani, kila mzazi ni lazima amjenge mwanae kitabia na kiimani ili ajue kuishi na jamii inayomzunguka.
 
Nadhani chanzo hapo ni sisi wazazi tunaowalea. Sababu angelelewa vyema na Mzazi au Mlezi nyumbani basi hadi hapo angekuwa na heshima.

Hili ni somo kwa wazazi na walezi kwamba tulee watoto katika mstari ulionyooka kuanzia chini.

Japo kanikera sana huyo mtoto.
Anamwambia mtu mzima kama mama yake etia anatafuta kik. Mpaka yule mama kaacha kuongea mwamafunzi anachamba tu
 
Ndo dar ilivyo, mtoto wa mwenzio mkubwa mwenzio,ingekua mkoani uyo mtoto ungekuta kashacharazwa bakora za kutosha
Alivyoshuka ndo mama mwingine akaanza kumsema ila alivyokuepo wote tulipiga kimya maana kama aliweza mjibu yule mama sisi ni kina nani angetujibu tu
 
Mtoto sio wa jamii tena bali ni wa baba na mama yake tu

Watatuvua sana nguo tujiandae kisaikolojia
Ingekua kijijini angekula fimbo. Sema yule anaonekana hata kwao anawasumbua. Unapata wapi ujasiri wa kumsema vibaya mama mtu mzima tena bila woga kwenye daladala ilojaa jamani.
 
Leo kwenye daladala kuna mama alimwambia mwanafunzi ampishe mzee akae. Yule mwanafunzi badala ya kujibu kistaarabu labda mama nimechoka au nnitalipa nauli ya mtu mzima ila alichokifanya ni kujibishana na yule mama. Akaanza kumwambia simpishi mtu angetaka angewahi. Mama kujibiwa vile akapata moto. Akamwambia nyie watoto wa siku hizi hamna adabu mzee kasimama wewe umekaa halafu unajibu vibaya. Mwanafunzi akamwambia mama "usitafutie kik kwangu kama una stress mshahara hujatoka achana na mimi." "Kwanza nakushangaa unavyoniambia nimpishe si ungempisha wewe". Mama akamwambia "we mtoto nina mtoto kama wewe nyumbani usinijibu vibaya". Mwanafunzi akamjibu "mama kama mtoto yuko kwako ungekua na mtoto kama mimi ungemleta kwenye garia saa hizi mbona hayupo kwanza achana na mimi na stress zako za kutolipwa mshahara".

Haki nilijisikia vibaya yule binti kumjibu vile mama wa watu. Sawa sio jambo zuri kumsimamisha mwanafunzi ili mtu mzima akae lakini yule binti ana mdomo mchafu sanaa. Kwa style hii hawa wanafunzi wa Dar wataendelea kufeli kwa sababu hawana adabu kwa mkubwa wala mdogo. Nimewazia walimu wake atakua anawajibu dharau kiasi gani wakiwa wanamgombeza.


Inasikitisha sana.

Nadhani mtazamo wa kuwa mwanafunzi anasimama kwa sababu analipa nauli kamili nao unachangia kuleta tatizo hili. Wanafunzi/watoto wanachukulia kuwa wanasimama kwa sababu wanalipa nauli kidogo na sio kwamba ili kuwapisha wakubwa wakae. Siku akilipa nauli kamili hatambui kuwa bado anastahili kuwapisha waliomzidi umri!

Kuwarudisha kwenye mstari kunaanza kwako na mimi... ingawa tuna kazi ya ziada, Mungu aingilie kati.
 
Ndio hapo sasa. Sababu mtoto kama hana adabu kiasi hicho sidhani kama anaweza muheshimu mwalimu wake na kutokumuheshimu ndio mwanzo wa kufanya vibaya darasani sababu hakuna kitakachoingia.

Sababu katika kusoma nidhamu nayo ni muhimu.
Mungu anisamehe ila yule anaonekana anaenda shule kusindikiza wenzie tu. Form four yake naona zero kabisa
 
Anamwambia mtu mzima kama mama yake etia anatafuta kik. Mpaka yule mama kaacha kuongea mwamafunzi anachamba tu
Ila ndugu yangu nimecheka kama mazuri ujue.

Naona watu wanamtetea huyo mtoto ila wanasahau kwamba huyo mtoto angeweza kukaa kimya ni jibu pia. Huwezi kusema eti kisa mtoto anakaa mbali na anakwenda mbali basi ndio awe na majibu machafu.

Mie naona angenyamaza ingetosha sababu sidhani kama wangeweza kumyanyua kwa lazima.
 
Zamani mtoto alikuwa mali ya wote akikosea mtu yeyote anamkanya na mzazi anafurahi tu lkn kwasasa mtoto akikosea mzazi ndiyo kwanza anambembeleza.

Wazazi wasasa tunajiona tunajua uchungu bure kabisa
Bure kabisa
 
Sasa mwanafunzi kama huyo unaweza kukuta kashalala na wazee wakubwa sana.

Heshima kwa wakubwa lazima ipotee.

Usiangalie tabia yake tu.

Angalia jamii nzima inavyopitia mmomonyoko wa maadili na hilo linavyosababisha tabia hizi.

Wababa wanaowatongoza na kuwalala hawa wanafunzi wanachangia wanafunzi hawa kukosa heshima kwa wakubwa.

Na wao wanafunzi wanajiona wakubwa tayari.
 
Mkuu kinachozungumziwa ni yale majibu machafu.

Kwani angeamua kulaza kichwa kwenye siti ya mbele yake kama wanavyofanyaga au kukaa kimya na kutokujibu huu uzi ungekuwepo?
Angemdanganya hata najisikia vibaya naumwa. Ni bora kudangaanya kuliko yale majibu aisee
 
Huyo mama naye kataka kujibiwa hovyo huwezi kumwambia mtu akupishe yeye mwenyewe anatakiwa ajue wajibu wake na tabia ya kutopisha siti wagonjwa au wazee mnayo sana wanawake unaweza kukuta mama mjamzito kasimama pembeni ya mwanamke mwenzie lakini hampishi
 
Back
Top Bottom