KERO Wanafunzi wa Chuo cha Takwimu Mashariki Mwa Afrika (EASTC) hatujapata malipo ya Fedha za Kujikimu wiki ya tatu sasa

KERO Wanafunzi wa Chuo cha Takwimu Mashariki Mwa Afrika (EASTC) hatujapata malipo ya Fedha za Kujikimu wiki ya tatu sasa

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

NBica

Member
Joined
Sep 13, 2010
Posts
39
Reaction score
36
WhatsApp Image 2024-12-30 at 11.43.50.jpeg

Mimi ni mmoja wa Wanafunzi wa Chuo cha Takwimu Mashariki Mwa Afrika (EASTC), tumepokea Disbursement ya Boom na Tuition Fee tangu Desemba 6, 2024.

Mpaka hivi sasa (leo Desemba 30, 2024) tumepewa cheque No ya Tuition Fee imepita wiki mbili (02) lakini hadi hivi sasa hatujawekewa Cheque No ya Boom (fedha ya kujikimu).

Wanafunzi hatuna fedha za Kujikimu, zimepita siku 24 ambazo ni wiki 3 na siku 1 bila Cheque No, hali ni ngumu, tunasoma tukiwa katika mazingira magumu.

Malipo ya Tuition fee na Boom la pili yaliwekwa (disbursement) siku moja (06.12.2024) lakini Tuition fee cheque no wamesha weka na tumesha saini wiki ya pili sasa . Lakini fedha ya kujikimu (Boom) hatujawekewa Cheque no mpaka hivi sasa.

Pia soma
~
Baadhi ya wanafunzi waliopata Samia scholarship UDSM wakumbana hali ngumu kufuatia kutopata fedha za kujikimu na ada ya masomo

~ Bodi ya Mikopo yatoa ufafanuzi kuhusu Wanafunzi ambao hawajapata Fedha za Kujikimu "Boom"
 
KUELEKEA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO: KWA NINI CHANGAMOTO ZA WANUFAIKA WA SAMIA SCHOLARSHIP KUPOTEZA VIGEZO, WENYE SIFA KUKOSA MIKOPO, NA UCHELEWESHAJI WA FEDHA ZA KUJIKIMU BADO HAZIJATATULIWA?
wanafuika wa Samia Scholarship waliokosa sifa (ambao hawajafikisha GPA ya 3.8) mpaka sasa hawajajua hatima yao
 
Hata Mimi pia huku chuo kikuu Cha Rucu iringa tuliwekewa disbursement Toka tarh 4 Dec ila Cha ajabu tunamaliza mwaka saivi hakuna cheque number na wao wanasema ety mbka siku 70 zipite,,,, kwa kweli maisha yanakua magumu na pia kama chuo chetu inapo fika tarehe flani wanaopiga penalty ko ki ukweli hili suala la kuchelewesha boom tunauumia sisi tunaotegemea boom kulipa ada
 
Kheri ya Kumbukizi ya kuzaliwa Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. SAMIA SULUHU HASSAN
----------------------X-----------------
Ndg:Michael Musa Ollomi Katibu seneti umejielkeza vibaya na Unatuondolea hadhi wasomi juu ya ujumbe huu Aya za mwishoni kwa sababu zifuatazo

1. Umekikua Katiba ya TAHLISO ibara ya 4(a) kwani hii Taasisi ni (a) " students’ non profitable, non religious and nonpartisan organization" kwa maana hiyo hatujihusishi kabsa na maswala ya Kivyama ambayo yanaweza kupelekea kuwagawa Wanafunzi
2. Sisi Wanafunzi wa Elimu ya Juu kupitia katiba yetu ya TAHLISO ibara ya [5] &[6]~malengo na Kazi za Taasisi hakuna Eneo linalosema "tunajukumu la kumtafutia Mgombea yeyote wa chama chochote cha siasa Kura za Ushindi", na kusema hivyo ni kuvunja utawala wa katiba na sheria ndani ya Taasisi pamoja na kukiuka misingi ya uanzishwaji wa Taaisisi

Mwisho: Tuombeni radhi wanafunzi wote wa Elimu ya Juu kwa makosa ya wazi, Makusudi pamoja na kutuongoza kwa Mepenzi ya wachache mbele ya wengi (Personal interest)

TAHLISO NI YETU SOTE
 
Back
Top Bottom