Wanafunzi waacha shule na kwenda kufanya kazi za ndani kutokana na michango kuwa mingi mashuleni

Wanafunzi waacha shule na kwenda kufanya kazi za ndani kutokana na michango kuwa mingi mashuleni

Hakuna familia ya baba na mama isiyopenda watoto wao wasome, tatizo ni ugumu wa maisha unaosababishwa na kipato duni cha baadhi ya familia maskini.
 
Baadhi ya wanafunzi wanaosoma Shule za serikali za kata wameshindwa kuendelea na masomo na kuacha shule kutokana na kile kinachodaiwa kuwa ni utitiri wa michango mashuleni,.

Moja ya shule kati ya nyingi zilizopo jijini Arusha ni sekondari ya Lemara iliyopo katika Kata ya Lemara kwenye halmashauri ya jiji la Arusha ambazo wanafunzi wameacha masomo Na kukimbilia miji mingine kama Dar es Salaam kwenda kufanya kazi za ndani na baadhi ya vijana kukimbilia kwenye machimbo ya Madini na kwenye vibarua vya ujenzi.

Michango inayodaiwa katika shule hizo ni pamoja na pesa ya Taaluma (20,000) kwa kila mwanafunzi,
Pesa ya chakula (15,000)kila mwezi
Rim paper mbili kwa mwaka kila. Muhula rim paper moja.
Hela ya Ulinzi.

Hela ya Remidial classes kiasi cha shilingi (500)kila siku jioni na ni lazima kwa kila mwanafunzi baada ya masomo kusoma Masomo ya jioni.
Pesa ya mtihani kila jumamosi kiasi cha shilingi( 1000)na (1500) nk.

Kutokana na utitiri wa michango na uwezo Mdogo wa wazazi wengi hushindwa Kumudu gharama hizo.

Huko wilayani Babati katika mkoa wa Manyara baadhi ya shule za kata zimekuwa zikiwaweka wazazi ndani kwa kile kinachodaiwa kushindwa kulipia watoto wao michango mashuleni.
Baadhi ya shule zinazotuhumiwa Kuwaweka ndani wazazi ni shule ya sekondari Burunge na shule ya sekondari kaiti iliyopo katika Kata ya kaiti.
 

Attachments

  • 33D4F8C8-4041-4691-903A-BDA9A92791E7.jpeg
    33D4F8C8-4041-4691-903A-BDA9A92791E7.jpeg
    34.6 KB · Views: 2
Michango imerudi kwa kasi sana katika shule za msingi na sekondari pia, ikiwemo pesa ya taaluma, ulinzi, masomo ya jioni, mitihani ya jumamosi, rimu n.k.. Sasa ningependa kuuliza elimu bure inakuwaje? kama wanafunzi wanatozwa pesa kubwa tena zaidi ya miaka hiyo ilipokuwepo ada.
USHAURI: KAMA SUALA LA ELIMU BURE LIMESHINDWA KUTEKELEZWA KWA VITENDO, NI BORA ADA YA TSH 20,000/= IKARUDISHWA.
 
Ndugu mwandishi:
Yani mwanafunzi anaacha shule kisa michango? Alafu eti anaenda kufanya kazi za ndani?
Mwanafunzi anawezaje kuamua jambo kubwa namna hii la kuacha shule na kuamua kwenda kufanya kazi?
 
Sipendi malumbano na watu na kuhusu ilo jina umesema wewe mi sikutaja mtu, mi mwenyewe ccm na kadi ninayo ndani, kwani maana yake Nini unaupiga mwingi ?
Mkuu ondoa shaka mimi mwenyewe CCM na kadi ipo tena ya electronic ila kwenye kusifu tunasifu na kukosoa lazima
 
Ndio maana dar Kuna vitoto vidogovidogo ni vi beki tatu Hadi unashangaa unasema huyu Si mtoto kabisa unakuta anaenda sokoni,mara kapeleka mtoto shule ,mara anaosha vyombo duhhh balaa ELIMU Bure bado.changamoto
hakuna cha elimu bure
 
Acheni waje mtaani na sisi wanyonge tupate k zinazo bana
 
Hata usithubutu kuuliza ndugu yangu maana hakuna kitu kilicho hatari duniani kama mtu mpumbavu na imani yake. Mpumbavu akiamini lake hata umwambie nini hawezi kubadilika na cha zaidi huwa wanaishia kutukana.
Mi ilinifikilisha kweli, ukiangalia umri na majibizano ya kukera watu, sio Wala Nini, kitu ni kutumia busara.
 
Hawajali watoto wa watu wengine. Wanatengeneza tabaka la kitumwa bila elimu.
Wakumkimboa masikini ni masikini mwenyewe. Tatizo wakipewa tishert na komoni wanasahau shida acha watu wajipigie wanavyotaka.
 
Back
Top Bottom