DOKEZO Wanafunzi wanaagizwa kupeleka matofali ikiwa kama adhabu wanapofanya makosa shuleni

DOKEZO Wanafunzi wanaagizwa kupeleka matofali ikiwa kama adhabu wanapofanya makosa shuleni

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

fikirakali

Member
Joined
Sep 15, 2014
Posts
15
Reaction score
18
Je, huu ni ubunifu au kuwakomoa wazazi? Kinachoendelea katika shule ya Sekondari Mbande ni kitu cha kutizamwa kwa Jicho la kipekee kwa kuwa kina madhara yake na kisipozungumzwa na kutolewa maamuzi na mamlaka kitaleta shida.

Kumeibuka mtindo wa kuwatoza wanafunzi matofali matatu na kuendelea kulingana na makosa ya kiuanafunzi kama vile kuchelewa, kutokusanya kazi au kutokumaliza kazi za darasani. Wakati naambiwa jambo hili na mtoto wangu anaesoma katika shule hiyo nilichukulia kuwa utani. Nilikuja kuamini baada ya kujionea mwenyewe nilipofika shuleni hapo mmoja wa waalimu akimwambia mwanafunzi alete tofali tatu kwa kutokumaliza kazi ya darasani.

Swali langu kwa wanajamii anaetozwa tafali ni mwanafunzi au mzazi? Mwanafunzi atapata wapi pesa kununua tofali?

Mamlaka husika wanalijua hili? Je, wazazi tumeridhia haya?
Je kuna meongozo unaoruhusu adhabu za kishule kwa wanafunzi kulipwa kwa pesa?
 
Yaani tofali tatu tu unakuja kuanzisha thread?

Mie shule moja nimepata nafasi ya mwanangu kuamia hapo baada ya kupeleka tofali 70.

Makosa mengine ya utovu wa nidhamu yanatozwa tofali kuanzia tofali 20 na kuendelea.

Mambo ya bure bure aliondoka nayo Mwendazake.!
 
Mbona Maeneo mengi Kilimanjaro ndio yapo hivyo.

Mimi nilishapigaga tofali 200 Enzi hizo Kwa Utovu wa nidhamu shuleni.
Tofali hizohizo ndizo zinatumika kujenga shule. Aidha ni mabweni au madarasa au majengo mengine.

Alafu wengine tunapenda adhabu za nje Kwa sababu hatupendi waalimu wakiingia darasani 😀😀
 
Yaani tofali tatu tu unakuja kuanzisha thread?

Mie shule moja nimepata nafasi ya mwanangu kuamia hapo baada ya kupeleka tofali 70.

Makosa mengine ya utovu wa nidhamu yanatozwa tofali kuanzia tofali 20 na kuendelea.

Mambo ya bure bure aliondoka nayo Mwendazake.!

Jamaa anachekesha Sana.
Wengine tofali tushapigaga Sana kama 200 alafu Sisi wengine Bora adhabu kulipo kuchapwa😊😊
 
Je, huu ni ubunifu au kuwakomoa wazazi? Kinachoendelea katika shule ya Sekondari Mbande ni kitu cha kutizamwa kwa Jicho la kipekee kwa kuwa kina madhara yake na kisipozungumzwa na kutolewa maamuzi na mamlaka kitaleta shida.

Kumeibuka mtindo wa kuwatoza wanafunzi matofali matatu na kuendelea kulingana na makosa ya kiuanafunzi kama vile kuchelewa, kutokusanya kazi au kutokumaliza kazi za darasani. Wakati naambiwa jambo hili na mtoto wangu anaesoma katika shule hiyo nilichukulia kuwa utani. Nilikuja kuamini baada ya kujionea mwenyewe nilipofika shuleni hapo mmoja wa waalimu akimwambia mwanafunzi alete tofali tatu kwa kutokumaliza kazi ya darasani.

Swali langu kwa wanajamii anaetozwa tafali ni mwanafunzi au mzazi? Mwanafunzi atapata wapi pesa kununua tofali?

Mamlaka husika wanalijua hili? Je, wazazi tumeridhia haya?
Sawa tuu sisi tulikuwa tunalima na kufyatua tofari kabisa.
 
Je, huu ni ubunifu au kuwakomoa wazazi? Kinachoendelea katika shule ya Sekondari Mbande ni kitu cha kutizamwa kwa Jicho la kipekee kwa kuwa kina madhara yake na kisipozungumzwa na kutolewa maamuzi na mamlaka kitaleta shida.

Kumeibuka mtindo wa kuwatoza wanafunzi matofali matatu na kuendelea kulingana na makosa ya kiuanafunzi kama vile kuchelewa, kutokusanya kazi au kutokumaliza kazi za darasani. Wakati naambiwa jambo hili na mtoto wangu anaesoma katika shule hiyo nilichukulia kuwa utani. Nilikuja kuamini baada ya kujionea mwenyewe nilipofika shuleni hapo mmoja wa waalimu akimwambia mwanafunzi alete tofali tatu kwa kutokumaliza kazi ya darasani.

Swali langu kwa wanajamii anaetozwa tafali ni mwanafunzi au mzazi? Mwanafunzi atapata wapi pesa kununua tofali?

Mamlaka husika wanalijua hili? Je, wazazi tumeridhia haya?
Labda ni syndicate ya walimu na muuzaji wa tofari
 
Tumesomba mawe, kuponda kokoto, kufyatua tofali, kuchimba na kusawazisha maeneo kama greda.

Wewe umesomea wapi? Au bas inawezekena ni wa kishua
 
Very good,pongezi kwa walimu ziwafikie;ni ubunifu mzuri sana wamefanya kuweka uwiano mzuri kati ya walimu na wazazi katika kusaidiana malezi ya watoto,wazazi wengi wanajisahau sana katika kufuatilia maendeleo ya watoto wao wakishawapeleka shule

Hii inasaidia mzazi kuwa alerted kila mtoto atakapopewa adhabu hiyo na kivyovyote mzazi atamkanya mwanae asirudie tena makosa
 
Yaani tofali tatu tu unakuja kuanzisha thread?

Mie shule moja nimepata nafasi ya mwanangu kuamia hapo baada ya kupeleka tofali 70.

Makosa mengine ya utovu wa nidhamu yanatozwa tofali kuanzia tofali 20 na kuendelea.

Mambo ya bure bure aliondoka nayo Mwendazake.!
Wewe lazima una mtindio wa ubongo, jamii kustaarabika ni ngumu sana kama mtu unaona hizi adhabu ni sahihi.
 
Swali langu kwa wanajamii anaetozwa tafali ni mwanafunzi au mzazi? Mwanafunzi atapata wapi pesa kununua tofali?
"Mchuma janga hula na wa kwao".
Kama ulifika hapo shuleni ungeuliza ujibiwe huko.

Btw, inaonesha nyie wazazi ni wagumu sana kuchangia maendeleo ya shule ya watoto wenu.
Hongera nyingi zimfikie huyo mwalimu aliyebuni hii adhabu.
 
Huu mfumo upo karibu shule nyingi sasahivi

Iringa pale mawelewele mtoto akishindwa kuja shule zaidi ya siku 3 pasipo maelezo ya kueleweka basi mfuko wa cement au bati lazima vikuhusu.

Au umekutwa na simu.

Mfumo huu ni mzuri umewajenga wanafunzi pamoja na wazazi kuwafuatilia watoto wao kwa ukaribu.
 
Adhabu yenye manufaa kwa shule na maumivu kwa mtoto na mzazi. Hutaki kupeleka tofali fuata taratibu na sheria☺☺☺

Zipo nyingine nyingiiii

Miaka hiyooo shuleni kwetu ilikua ukichelewa kufika ile reporting time 7:30 unarudishwa nyumbani, halafu jumamosi unaenda shule kuilipia hiyo siku uliyoikosa. Na usipoenda shuleni kabisa bila sababu ya msingi unalipia siku2 wakati wa likizo kwa kila siku uliyokosa

Sasa nimekutana na nyingine zama hizi... ukichelewa kumpeleka mtoto kurepprt shule siku ya kufungua unalipa elfu5 kwa kila siku aliyochelewa ili usirudie, japo kwa wazazi wala vichwa vyao vibovu ndio wanatumia hii kuendelea kudekeza watoto nyumbani
 
tofali inafyatuliwa,si hamtaki viboko?
mi huwa nawaambia kama ya hapa yanakushinda kaangalie maisha kwingine.
sa hivi kuhama ni rahisi sana pia
 
Huu utaratibu naona ni shule zote nchini, Songea wanafunzi wanafyatua wenyeweee,

Mwenyewe nilishawahi kufyatua tofali 600. Nlichelewa ku report shule wakati wa kufungua.

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
Duh,sie advance tena msichana ukichelewa kuripot yaani kila siku ulochelewa ni tofali mia moja(100)na walikuwa wanahakikisha unafyatua bibi wanakuandalia vifaa na kuoneshwa ardhi ya kuchimba udongo,sijawahi kuvuta make nilikuwa nikifikiria tofali hizo nachoka yaani uchote maji ukande udongo afu ufyatue
 
duh,sie advance tena msichana ukichelewa kuripot yaani kila siku ulochelewa ni tofali mia moja(100)na walikuwa wanahakikisha unafyatua bibi wanakuandalia vifaa na kuoneshwa ardhi ya kuchimba udongo,sijawahi kuvuta make nilikuwa nikifikiria tofali hizo nachoka yaani uchote maji ukande udongo afu ufyatue
Kuna tofauti ya kupewa vifaa ufyatue na kwenda kununua soma uelewe, hela za kununua tofali watoto wanapata wapi?
 
Back
Top Bottom