DOKEZO Wanafunzi wanaagizwa kupeleka matofali ikiwa kama adhabu wanapofanya makosa shuleni

DOKEZO Wanafunzi wanaagizwa kupeleka matofali ikiwa kama adhabu wanapofanya makosa shuleni

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kukimbia tatizo si kulimaliza, hapa ni mwazo wa kufikisha ujumbe kwa mamlaka husika, haiwezekani mwanafunzi ashindwe kuandika kazi au akose swali mzazi ukanunue matofali, kuna adhabu za kufyeka nyasi, kuchimba mashimo, kudeki madarasa na vyoo, hill la mtoto kutozwa pesa haikubaliki
Braza nimekueleza humu wengi ni walimu tegemea kupata upinzani. Huyo unayemjibu ni Mwalimu wa shule ya msingi.

Mimi nachokueleza ni hivi mpigie simu huyo mwalimu au mfuate, mwambie hiko kitu hakipo utaona jinsi atavyokua mpole. Wanawafanyia hivyo wakijua hamuwezi kuuliza, Ila ukianza kuuliza watajua huyu ni mjanja kashtuka.
 
Soma uelewe,sijasema kupiga tofali, mwalimu anamwambia mwanafunzi akanunue tofali hela anapata wapi? Ulishawahi kumpa mtoto tsh 10000 aweke ili alichelewa kumaliza kazi za darasani alipe kama adhabu?
Hii ni sawa na kulipia adhabu kwa pesa badala ya kazi na viboko, hakuna mwongozo wa elimu unaoruhusu mwanafunzi kulipia makosa yao ya kishule kama kutokusaya daftari, kupiga kelele na kuchelewa kwa pesa
Kaa nae kwako mtoto wako umfungulie shule yako
 
Ndio mwongozo unavyosema mwanafunzi atoe pesa akifanya kosa? Tena kosa la kutokusanya daftari?
Bei ya tofali unaijua? Huyo mtoto anapata wapi 5000 tshs za kwenda kununua tofali na kuzileta shuleni? Au mmekula hela za ujenzi mnatafuta pa kuijazia?
Mchukue kaa nae kwako
 
Yaani tofali tatu tu unakuja kuanzisha thread?

Mie shule moja nimepata nafasi ya mwanangu kuamia hapo baada ya kupeleka tofali 70.

Makosa mengine ya utovu wa nidhamu yanatozwa tofali kuanzia tofali 20 na kuendelea.

Mambo ya bure bure aliondoka nayo Mwendazake.!
duh mbona chuki zitaliua bara la afrika , hatuez pembua akili vzr ,na hawa watoto wakiwa viongoz na wao wanaweka tozo bila kujali maoni ya wengine kisa hata yeye alipitia msoto
 
Kukimbia tatizo si kulimaliza, hapa ni mwazo wa kufikisha ujumbe kwa mamlaka husika, haiwezekani mwanafunzi ashindwe kuandika kazi au akose swali mzazi ukanunue matofali, kuna adhabu za kufyeka nyasi, kuchimba mashimo, kudeki madarasa na vyoo, hill la mtoto kutozwa pesa haikubaliki
Mchukue mpeleke kwenye shule yenu ya ukoo
 
Huo ni ujuha wa walimu.
Walimu wengi ni wapumbavu
Nikiwa nasoma O -level mwalimu wetu wa mathematics alikuwa Mmarekani, ukifanya mistake adhabu zake ni very simple sema tu utaona aibu kesho lazima ujitahidi.
Jamaa mara nyingi wale waliopata below au kutokufanya zoezi anawatoa nje mnakimbia mchakamchaka pamoja naye dk 15.
Bongo yaani mwalimu anaamuru wanafunzi wawazomee watatu walioshika mkia bila kuangalia reasons behind.
Hii kada bongo imeshikiliwa na vilaza
 
Jamaa anachekesha Sana.
Wengine tofali tushapigaga Sana kama 200 alafu Sisi wengine Bora adhabu kulipo kuchapwa[emoji4][emoji4]
duh unaandikq ujinga ila hujui kuwa ni ujinga nq mkitoka hapo mnasema viongoz wenu wabovu kumbe wamezoea maisha ya kukandamizana tangu utotoni , shule ni pa kujifunzia mazur na sio kujifunza umwiny
 
Soma uelewe,sijasema kupiga tofali, mwalimu anamwambia mwanafunzi akanunue tofali hela anapata wapi? Ulishawahi kumpa mtoto tsh 10000 aweke ili alichelewa kumaliza kazi za darasani alipe kama adhabu?
Hii ni sawa na kulipia adhabu kwa pesa badala ya kazi na viboko, hakuna mwongozo wa elimu unaoruhusu mwanafunzi kulipia makosa yao ya kishule kama kutokusaya daftari, kupiga kelele na kuchelewa kwa pesa

Na wewe soma comment uelewe legeza fuvu
 
Huo ni ujuha wa walimu.
Walimu wengi ni wapumbavu
Nikiwa nasoma O -level mwalimu wetu wa mathematics alikuwa Mmarekani, ukifanya mistake adhabu zake ni very simple sema tu utaona aibu kesho lazima ujitahidi.
Jamaa mara nyingi wale waliopata below au kutokufanya zoezi anawatoa nje mnakimbia mchakamchaka pamoja naye dk 15.
Bongo yaani mwalimu anaamuru wanafunzi wawazomee watatu walioshika mkia bila kuangalia reasons behind.
Hii kada bongo imeshikiliwa na vilaza
Nenda kaishi huko Marekani
 
Je, huu ni ubunifu au kuwakomoa wazazi? Kinachoendelea katika shule ya Sekondari Mbande ni kitu cha kutizamwa kwa Jicho la kipekee kwa kuwa kina madhara yake na kisipozungumzwa na kutolewa maamuzi na mamlaka kitaleta shida.

Kumeibuka mtindo wa kuwatoza wanafunzi matofali matatu na kuendelea kulingana na makosa ya kiuanafunzi kama vile kuchelewa, kutokusanya kazi au kutokumaliza kazi za darasani. Wakati naambiwa jambo hili na mtoto wangu anaesoma katika shule hiyo nilichukulia kuwa utani. Nilikuja kuamini baada ya kujionea mwenyewe nilipofika shuleni hapo mmoja wa waalimu akimwambia mwanafunzi alete tofali tatu kwa kutokumaliza kazi ya darasani.

Swali langu kwa wanajamii anaetozwa tafali ni mwanafunzi au mzazi? Mwanafunzi atapata wapi pesa kununua tofali?

Mamlaka husika wanalijua hili? Je, wazazi tumeridhia haya?
Je kuna meongozo unaoruhusu adhabu za kishule kwa wanafunzi kulipwa kwa pesa?
Kama tofali zitatumika kuendeleza miundo mbinu ya shule. Naunga hoja
 
duh unaandikq ujinga ila hujui kuwa ni ujinga nq mkitoka hapo mnasema viongoz wenu wabovu kumbe wamezoea maisha ya kukandamizana tangu utotoni , shule ni pa kujifunzia mazur na sio kujifunza umwiny
Yes.
Eti mtu anajisifia kutendewa ujinga.
 
Kukimbia tatizo si kulimaliza, hapa ni mwazo wa kufikisha ujumbe kwa mamlaka husika, haiwezekani mwanafunzi ashindwe kuandika kazi au akose swali mzazi ukanunue matofali, kuna adhabu za kufyeka nyasi, kuchimba mashimo, kudeki madarasa na vyoo, hill la mtoto kutozwa pesa haikubaliki
Toa pesa wewe ili uzio wa shule ukamilike, na mtoto wako asome katika mazingira salama. Elfu 3 tu ya matofali, unalalamika!!

Unategemea hii serikali yako ya tozo itakufanyia kila kitu, bila ya kujiongeza! Ingekuwa hizo hela zinaliwa na hao walimu, sawa! Ila kama huo utaratibu ulipitishwa na bodi ya shule! Basi utaishia tu kuugulia maumivu.

Toa hela ya tofali aisee!! Na hili jambo nitalisimamia mpaka nahakikisha umelipa hiyo hela. Kwa taarifa yako, Mimi ndiye mwenyekiti wa bodi ya hiyo shule anayosomakijana wako mtukutu.
 
Back
Top Bottom