Wanafunzi wawili wafariki kwa kukosa hewa wakitoa maharage kwenye pipa

Wanafunzi wawili wafariki kwa kukosa hewa wakitoa maharage kwenye pipa

Na vumbi la maharage huchelewi....ni chap! RIP wanangu
Vumbi la maharage au wamezama kwenye maharage ?? Sijawahi kusimama kwenye maharage, sijui surface stability ya maharage.

Watu wa kale walikuwa wanahifadhi chakula kwenye vibanda vya kienyeji na hawatumbukii kwa juu wakati wanayachukua. Sasa wasomi tumeshindwa teknoloji, mbinu, common sense, na watu wa kienyeji ambao hawakweda shule !
 
Bila picha ya pipa tutajiukliza sana, pipa limeua kwa mda mfupi sana au kulikuwa na kitu zaidi ya kukosa hewa, yaani mmoja ameingia akaanza kupiga kelele mwenzake akaiingia kwenda kumuokoa wote wamepoteza maisha, walikaa mda gani humo ndani ya pipa.
Swali kwa aliyesikia kelele za mwanafunzi wa kwanza.

Kwanini hakuona umuhimu wa kuwaita watu wengine watoe msaada badala yake akaamua kusubiri atoe ushahidi wa vifo?
 
Maskini wanafunzi! Walazwe pema na kwa Amani.

Tukio kama hili lingeweza epukika kama wahusika wangefuata 'taratibu au kanuni ya kuingia kwenye nafasi funge' yaani 'Entering confined space safety procedure'.

Elimu kwa wananchi inabidi kutolewa ipasavyo na taasisi husika kuhusiana na vihatarishi vinavyotuzunguka katika sehemu zetu za kazi na kadhalika katika maisha yetu ya kawaida.

Baadhi ya vyanzo vya vifo vitokanavyo na ukosefu wa hewa ya oksijeni ni pamoja na:
-Nafasi funge au 'confined space'
-Mashimo na mitaro funge ya maji taka
-Majiko ya mkaa
-Migodi ya chini ya ardhi au 'underground mines'

Wananchi wakielemishwa vyema hakika vifo vya aina hii vitaepukwa au kupungua kwa kiasi kikubwa.
Mkuu nilitamani sana kuona Comment kama hii.

Serikali na wadau wengine wa usalama wamejitahidi sana kutoa elimu shuleni juu ya Usalama barabarani ,na kwa kiasi kikubwa mwanga umeonekana.

Lakini ni muda Sasa kutoa elimu zaidi juu ya elimu ya Usalama mahala pa kazi(Safety in the Workplace).

Shule ni eneo lenye Vihatarishi vingi sana ambavyo visivyodhibitiwa vinaweza kuleta madhara makubwa si tu kwa wanafunzi,Bali hata kwa walimu na wafanyakazi wengine wanaozunguka eneo husika.

Natoa pole kwa wazazi na walimu waliopoteza vijana wetu na nguvu kazi kwa taifa.


Hili ni jukumu la Kila mmoja kujielimisha na kuwasaidia wengine.
 
Hayo mapipa ya nafaka yameshaua sana watu, ni hatari , hivo hivo 2019 kuna vijana mtaani kwetu walipewa kazi ya kusafisha pipa hilo ndani, walikua watatu, yani pale pale walukufa kwa kukosa hewa
 
Hayo mapipa yametengenezwa kuzuia hewa isiingie ili wadudu wala nafaka wasi survive
 
Wanafunzi wawili wa Shule ya Sekondari Kisomachi, iliyopo Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, wamefariki dunia baada ya kudaiwa kukosa hewa, wakati walipoingia kwenye tenki la kuhifadhia maharage.

Akizungumza Mwenyekiti wa Kijiji cha Kileuwo wilayani hapa, Godfrey Mrema amesema tukio hilo limetokea Mei 12, 2023, wakati wanafunzi hao walipoingia kwenye tenki hilo kwa ajili ya kutoa maharage ya chakula shuleni.

“Wanafunzi hao wote wana umri wa miaka 17, na uongozi wa shule umesema wote walifariki baada ya kuingia kwenye tenki kwa ajili ya kutoa maharage ya kupeleka stoo kwa ajili ya kupika,” amesema.

Ameongeza kuwa “Kwa taarifa tuliyoipata shuleni ni kwamba wanafunzi hao walipanda kwenye pipa hilo kwa kutumia ngazi na kisha kutumbukia ndani kutoa maharage na alianza kuingia mmoja, halafu akaanza kupiga kelele ndipo mwenzake akaingia kwa ajili ya kumuokoa lakini walikosa hewa na hadi kugeuza pipa kutolewa walishafariki,” amesema.

“Hapa inaonekana kuna uzembe, maana kama shule ina mpishi, kwa nini wanafunzi waingie kwenye pipa kwa ajili ya kutoa maharage kupeleka stoo? Alihoji mwenyekiti huyo na kueleza kuwa, tayari vyombo vya usalama pamoja na Mkuu wa Wilaya walifikaa eneo la tukio

Alipotafutwa Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kisare Makori kuzungumzia tukio hilo, amesema atalizungumzia baadaye.

Chanzo: Mwanachi
Wasomi wa nchi hii hawana uwezo wa kufanya kuweka tahadhari ya kuwahami watu mpaka wafe waumie hapo serikali utaisikia heti tunatoa lambi lambi na kusimamia mazishi na kuandaa sehemu salama ya kuhifadhia maharagwe fiweeee
 
Wew ulisoma bweni au day

Na kwa utuuzma wako jambo hilo unaona halikuwafaa wanafunz kufanya



Shule ina wapishi wawali wanafunz 500+ alafu wafanye wao vitu bila man pow sio kweli

Kumbuka hiyo ni kaz ya kawaida labda useme kuna uzembe wa namna fulan kweny kuwasimamia
haya mambo ya kuwashirikisha wanafunzi kwenye mambo ambayo kimsingi hawatakiwi kufanya ni uzembe wa walimu kuruhusu wanafunzi washiriki kazi ambazo tayari kuna mfanyakazi wake.
 
Kukosa elimu ya kujua wapi salama na wapi si salama. Unaingia kwenye ghala la kuhifadhi maharage wakati mule kunachanganywa dawa za wadudu na hakuna hewa inaingia lakini kutojua namna ya kuzibua kama limeziba. Wasimamizi hudhani watoto wanajua mambo yote kumbe wanakuja kuwaumiza tu
 
Mzazi hapo unawaelewaje wahusika?
Siwaelewi km Mimi Ndo mwenye Mtoto ama zao ,ama zangu aseehh
Shule Ina wapishi,wafanyakazi how comes wamtume mwanafunzi hukooo....
Walimu tuna uzembe mnooo!
Kuna janga linakuja hatuombei soon twende tu
Pale shule ya msingi Kifuru Iko very close na lami afu Kuna bonge mtaro,juzi napita nakuta watoto wamebeba maji wanahangaika na ndoo pale barabarani ,nikawaza mnooo Ile scenario nkasema hapa ikitoke minor mistake watoto wanagongwa au wanandokea mtaroni wanapata madhila Kwa Sasa walimu hawalioni hiloo ila SIKU likitokea Ndo watajifanya wanachukua hatua
Hiii nchi Ina mambo ya hovyo Kwa Baadhi ya watendaji mnoo
 
Back
Top Bottom