Wanafunzi wawili wafariki kwa kukosa hewa wakitoa maharage kwenye pipa

Wanafunzi wawili wafariki kwa kukosa hewa wakitoa maharage kwenye pipa

Dogo baada ya kusikia kelele za mwenzake aliyekua ndani ya Pipa,akaingia kwenye Pipa ili kumuokoa mwenzake,
Dogo amekufa kishujaa sana,

R.I.P vijana.
 
Wanafunzi wawili wa Shule ya Sekondari Kisomachi, iliyopo Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, wamefariki dunia baada ya kudaiwa kukosa hewa, wakati walipoingia kwenye tenki la kuhifadhia maharage.

Akizungumza Mwenyekiti wa Kijiji cha Kileuwo wilayani hapa, Godfrey Mrema amesema tukio hilo limetokea Mei 12, 2023, wakati wanafunzi hao walipoingia kwenye tenki hilo kwa ajili ya kutoa maharage ya chakula shuleni.

“Wanafunzi hao wote wana umri wa miaka 17, na uongozi wa shule umesema wote walifariki baada ya kuingia kwenye tenki kwa ajili ya kutoa maharage ya kupeleka stoo kwa ajili ya kupika,” amesema.

Ameongeza kuwa “Kwa taarifa tuliyoipata shuleni ni kwamba wanafunzi hao walipanda kwenye pipa hilo kwa kutumia ngazi na kisha kutumbukia ndani kutoa maharage na alianza kuingia mmoja, halafu akaanza kupiga kelele ndipo mwenzake akaingia kwa ajili ya kumuokoa lakini walikosa hewa na hadi kugeuza pipa kutolewa walishafariki,” amesema.

“Hapa inaonekana kuna uzembe, maana kama shule ina mpishi, kwa nini wanafunzi waingie kwenye pipa kwa ajili ya kutoa maharage kupeleka stoo? Alihoji mwenyekiti huyo na kueleza kuwa, tayari vyombo vya usalama pamoja na Mkuu wa Wilaya walifikaa eneo la tukio

Alipotafutwa Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kisare Makori kuzungumzia tukio hilo, amesema atalizungumzia baadaye.

Chanzo: Mwanachi
Uongozi wa shule uchukuliwe hatua
 
Mkuu nilitamani sana kuona Comment kama hii.

Serikali na wadau wengine wa usalama wamejitahidi sana kutoa elimu shuleni juu ya Usalama barabarani ,na kwa kiasi kikubwa mwanga umeonekana.

Lakini ni muda Sasa kutoa elimu zaidi juu ya elimu ya Usalama mahala pa kazi(Safety in the Workplace).

Shule ni eneo lenye Vihatarishi vingi sana ambavyo visivyodhibitiwa vinaweza kuleta madhara makubwa si tu kwa wanafunzi,Bali hata kwa walimu na wafanyakazi wengine wanaozunguka eneo husika.

Natoa pole kwa wazazi na walimu waliopoteza vijana wetu na nguvu kazi kwa taifa.


Hili ni jukumu la Kila mmoja kujielimisha na kuwasaidia wengine.
Uko sahihi The622.

Serikali inatakiwa kuwa na mkakati thabiti na mahsusi wa kuhamasisha Usalama wa Afya na Mazingira kwenye shule zetu, kwani nazo ni mahali pa kazi kama maeneo mengine yoyote ya kazi.

Nadhani taasisi kama OSHA ingejiongeza kwenye hili, kutoa elimu na kuhamasisha.. 'sensitization and awareness' ni muhimu sana.

Uhamasishaji wa elimu ya usalama barabarani unafanyika mashuleni na matokeo kwa kiasi kikubwa ni chanya.

Vivyo hivyo elimu ya Usalama, Afya na Mazingira inahitajika sana mashuleni kwa kuwa huko nako ni mahala pa kazi (work place)
 
Siwaelewi km Mimi Ndo mwenye Mtoto ama zao ,ama zangu aseehh
Shule Ina wapishi,wafanyakazi how comes wamtume mwanafunzi hukooo....
Walimu tuna uzembe mnooo!
Unajifanya mjuaji kishenzi!

Unajua hiyo shule ina wapishi wangapi?

Kwamba mpishi peke yake aende stoo, abebe magunia ya unga, maharage mpaka jikoni (sisi shuleni gunia moja tulikua tunabeba wanafunzi sita na bado tunachemka)

Awashe moto, apike (chakula cha watu 1500+).
 
Back
Top Bottom