Hapana. Hii ya kufundisha namna ya kujibu maswali badala ya topic nzima ipo kwenye shule za serikali hasa advanced level.
Hizo shule za kanisa kama St.Francis na seminary huwa wanafundishwa topics zote za silabasi nzima kwa uelewa mpana. Halafu wanafunzi huwa wanalala mapema tu,hawakeshi wanasoma kama Ilboru au Kibaha .
Baadhi ya walimu wanaomfundisha mwanafunzi wa form one seminary kama mapadri unakuta wana elimu yenye level ya kumfundisha mwanafunzi wa chuo kikuu. Mapadri wanapofundisha wanafunzi unakuta wanaichimba topic mpaka kwenye extra ordinary level . Automatically mwanafunzi anayepata bahati ya kufundishwa na ma-philosopher kama hawa lazima atakuwa na I.Q kubwa.
Halafu seminarini au hizi shule za kanisa huwa hawadekezi wanafunzi. Mbali na kusoma , mwanafunzi ana fundishwa kuheshimu muda na kufanya kazi haswa. Mimi kwa uzoefu wangu seminarini muda kujisomea binafsi ulikuwa ni limited na ni mchache sana lakini tulifaulu vizuri.