Wanaharakati wa Haki za Wanawake Afrika Kusini wataka shoo ya Chris Brown ifutwe

Wanaharakati wa Haki za Wanawake Afrika Kusini wataka shoo ya Chris Brown ifutwe

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wanaharakati wa kutetea haki za wanawake nchini Afrika Kusini kutoka Taasisi ya Women for Change wameanzisha kampeni ya kutaka kusitishwa kwa shoo ya staa wa RnB duniani, Chris Brown maarufu Breezy pnchini humo linalotarajiwa kufanika kwa siku mbili, Desemba 14 na 15, 2024.
IMG_0170.jpeg

Wanaharakati hao wamedai kuwa Breezy ana historia mbaya ya unyanyasaji wa kijinsia kwa tukio lake la kumpiga aliyekuwa mpenzi wake, Rihanna na kwamba tarehe ya shoo hizo itaangukia katika Maadhimisho ya Wiki ya Kupinga Ukatili na kwamba hatakiwi kufanya shoo nchini humo kwani itakuwa ni sawa na kuhalalisha ukatili wanaofanyiwa wanawake.
IMG_0171.jpeg

Licha ya tiketi za shoo yake kumalizika ndani ya saa mbili tu tangu zilipoanza kuuzwa Oktoba 3 na kuwalazimu waandaaji kuongeza siku nyingine kutokana na uhitaji, bado kuna kigugumizi katika kupitisha tamasha hilo, ambapo wanaharakati hao wamekusanya saini 20,000 mpaka sasa, huku mawakili wakiitaka Idara ya Mambo ya Ndani kumfutia viza yake.

Soma:

=>
Tamasha la Chris Brown Johannesburg: Tiketi zote zimeuzwa, zikiwa na bei kuanzia Tsh. 94,000 hadi 800,000
=> Afrika Kusini ndio nchi yenye Kiwango kikubwa cha Mauaji ya Wanawake barani Afrika na mara 5 ya Wastani wa Dunia
 
Hao wanaharakati ni wapumbavu, chriss na Riri walishayamaliza siku nyingi na wako poa kbs, wao wanaibukia Afrika huku na upumbavu wao! unyanyasi wa kijinsia ni kosa kubwa sana nchini Marekani kiasi kwamba ingethibitika chriss ana makosa basi angekuwa lupango kama P Diddy.
 
Hawo wanaharakati vipi,kuna mauaji ya kutisha hapo hapo SA yanaripotiwa kila siku,mbona wasilazimishe serikali yao kukokesha hayo matukio?
 
Wanaharakati wa kutetea haki za wanawake nchini Afrika Kusini kutoka Taasisi ya Women for Change wameanzisha kampeni ya kutaka kusitishwa kwa shoo ya staa wa RnB duniani, Chris Brown maarufu Breezy pnchini humo linalotarajiwa kufanika kwa siku mbili, Desemba 14 na 15, 2024.
View attachment 3123414
Wanaharakati hao wamedai kuwa Breezy ana historia mbaya ya unyanyasaji wa kijinsia kwa tukio lake la kumpiga aliyekuwa mpenzi wake, Rihanna na kwamba tarehe ya shoo hizo itaangukia katika Maadhimisho ya Wiki ya Kupinga Ukatili na kwamba hatakiwi kufanya shoo nchini humo kwani itakuwa ni sawa na kuhalalisha ukatili wanaofanyiwa wanawake.
View attachment 3123415
Licha ya tiketi za shoo yake kumalizika ndani ya saa mbili tu tangu zilipoanza kuuzwa Oktoba 3 na kuwalazimu waandaaji kuongeza siku nyingine kutokana na uhitaji, bado kuna kigugumizi katika kupitisha tamasha hilo, ambapo wanaharakati hao wamekusanya saini 20,000 mpaka sasa, huku mawakili wakiitaka Idara ya Mambo ya Ndani kumfutia viza yake.

Soma:

=>
Tamasha la Chris Brown Johannesburg: Tiketi zote zimeuzwa, zikiwa na bei kuanzia Tsh. 94,000 hadi 800,000
=> Afrika Kusini ndio nchi yenye Kiwango kikubwa cha Mauaji ya Wanawake barani Afrika na mara 5 ya Wastani wa Dunia
Ina athari gani kwenye uboreshwaji wa daftari la wapiga kura?
 
Hao wapumbavu hawaoni na kupinga matatizo yote yaliyopo Afrka kama vile rushwa,mauaji hususani Afrika kusini,ubakaji nk ila wanaona manyanyaso ya yanayofanyika mamia ya maili toka walipo.
Wana baraka ya upumbavu.
 
Hao wanaharakati ni wapumbavu, chriss na Riri walishayamaliza siku nyingi na wako poa kbs, wao wanaibukia Afrika huku na upumbavu wao! unyanyasi wa kijinsia ni kosa kubwa sana nchini Marekani kiasi kwamba ingethibitika chriss ana makosa basi angekuwa lupango kama P Diddy.
Wanataka sifa tu za kijinga
 
Back
Top Bottom