Wanaharakati wa Jamhuri ya Twitter

Wanaharakati wa Jamhuri ya Twitter

Jamani nisaidieni....

Hivi yule zwazwa KIGOGO 2014 ni binadamu ama JINI?!!

Kama ni binadamu...je ni mtu was namna gani na amefanya kazi sehemu zipi?!!

Nisaidieni kujua jamani kwani ni mtu gani yule hata akisomewa ALBADIRI haimkumbi na inadunda tu?!!!

Maendeleo hayana vyama
Anakula Sana kiti moto Yule mtu na anatembea na mifupa ya kitimoto kwenye pochi lake

😂😂😂😂
 
Hakuna kitu kibaya kwa mwanadamu kama akiandamana ndani ya moyo wake ni hatari sana, ndiyo maana kwamwenye hekima akimkosea mtu inafaa akamwombe msamaha ili roho yake ipate amani. laana huanzia hasa kwenye mtu kusononeka nadhani ndiyo maana afrika haiendelei kwasababu imejaa laana za watu wake.
 
Anakula Sana kiti moto Yule mtu na anatembea na mifupa ya kitimoto kwenye pochi lake

😂😂😂😂
🤣🤣🤣🤣

Hakika itakuwa NDIVYO...

Kwani binafsi nilimweleza SHEIKH wangu amsomee ALBADIRI....Sheikh akaangalia RAMLI na kudai JAMAA GOGO kweli...na kamwe HAROGEKI...😂😂

Mshana Jr naye anamshindwa?!!!

Je yule Mndengereko KITOABU mzee wa kuroga kule MOCIMBOA DA PRAIA Msumbiji kwa yule babu naye pia atamshindwa?!!!
 
Pia ni mtandao unaotolewa macho na mfalme gharama walizotumia kupambana kuzisuspend account za activists kipindi kile ni jibu tosha kuna ujumbe wanaupata mengineyo muda utatuambia ...
 
🤣🤣🤣🤣

Hakika itakuwa NDIVYO...

Kwani binafsi nilimweleza SHEIKH wangu amsomee ALBADIRI....Sheikh akaangalia RAMLI na kudai JAMAA GOGO kweli...na kamwe HAROGEKI...😂😂

Mshana Jr naye anamshindwa?!!!

Je yule Mndengereko KITOABU mzee wa kuroga kule MOCIMBOA DA PRAIA Msumbiji kwa yule babu naye pia atamshindwa?!!!
Mashana si atakuwa ni ndugu yake Yule!!😂
 
Miaka minne ilopita nilitoa maoni kuwa, endapo wale jamaa wa UKUTA wangenywea na kutokufanya maandamano yao waliyokuwa wameyapania, basi huo ungekuwa ni ushindi mkubwa kwa Rais Magufuli. Si tu ushindi uonekanao kwa macho, bali ushindi wa kisaikolojia pia.

Niliandika hapa:


Maandamano hayo hayakufanyika. Rais Magufuli aliwaambia hao walokuwa wamepanga hayo maandamano kuwa yeye ‘hajaribiwi’.

Nadhani walimwelewa alichokisema.

Miaka 2 baadaye kukapangwa tena kuwe na maandamano makubwa ambayo yangefanyika siku ya muungano. Haya hayakuitishwa na chama chochote cha kisiasa. Yaliitishwa na dada’ake na Salary Slip 🤣.

Hakuna aliyethubutu kuingia barabarani.

Mwaka huu tena vyama vya ACT-Wazalendo na CHADEMA baada ya kushindwa uchaguzi mkuu na kudai kuwa vimefanyiwa hujuma, viongozi wake wakaitisha maandamano ya amani nchi nzima, yasiyo na kikomo, ya kupinga matokeo.

Hakuna hata mtu mmoja aliyeingia barabarani na kuthubutu kuandamana.

Huwa naona sana humu wale akina dada wa Twitter, wale wanaharakati wa Jamhuri ya Twitter, Shangazi na yule mwezake Binti Maria wakisifiwa sana wanapo longalonga huko kwenye hiyo jamhuri yao. Halafu kuna huyu raia mpya aitwaye Amsterdam. Naye naona anapenda sana kulonga huko kwenye hiyo jamhuri.

Kwamba eti ni majasiri sana. Hawamwogopi mtu, blah blah blah.

Sasa, kama kweli hawamwogopi mtu na hawaogopi kitu, kwa nini sasa huwa wanaishia kupiga mayowe kwenye hiyo jamhuri yao? Kwa nini wasitende kwa vitendo hayo maneno yao kwa kuingia barabarani na mabango yao na vipaza sauti kumpinga huyo wasiyempenda?

Jibu ni moja tu: na wao wanajua kuwa huyo Ngosha hajaribiwi. Akisema kitu akiwa amekasirika huwa anamaanisha. Aliposema hajaribiwi, naamini wote walioisikia hiyo kauli, waliielewa.

Kelele zipigwazo jamhuri ya Twitter haziwezi kubadili chochote kilichopo huku uraiani.

Kauli ya Ngosha na virungu vya kamanda Mambosasa, vimewapa watu uhamisho toka Tanzania kwenda Jamhuri ya watu wa Twitter.

Lissu alikuja kuomba urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wafuasi wake wako Jamhuri ya Twitter; ni afdahalai angegombea huko
 
Twitter japo mnaiponda lakini inawakera, mnatamani isiwepo kabisa.

Hilo nimethibitisha leo kwenye hotuba ya jamaa aliposema "haki huendana na wajibu", tena akarudia mara mbili na kusisitiza nadhani nimeeleweka, hapo alikuwa anawajibu wale wasumbufu kule twitter.

Sauti ya mtu huwezi kuidharau, hata mkiwepo mia moja na kati yenu akawepo mmoja anaewapinga mtamsikia tu, na atawakera pamoja na nguvu zenu, matokeo yake hamtapata usingizi mzuri mkilala usiku na ndicho kinachokupata Ngabu.
Sauti zenu za Twitter tu haziwezi kuizuia CCM kutawala Tanzania. Nitakukumbusha hili 2030.
 
Lissu alikuja kuomba urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wafuasi wake wako Jamhuri ya Twitter; ni afdahalai angegombea huko
Huko na humu JF angeshinda kwa kishindo! Hata akihamasisha maandamano humu yatafanikiwa kwa asilimia mia! Ahahahahahah!!
 
Nyani Ngabu,

..kwanini unadhani wapinzani wa Tz ambao hawana silaha, wanaweza kukabiliana na chama tawala ambacho kina silaha?

..au kwanini unadhani Ngosha ana ubavu wakati anachofanya ni kutuma wenye silaha kupiga wasio na silaha?
Mbaya zaidi hata hizo silaha za Polisi ambazo analingia nazo Ngosha na anazowanyanyasa nao wapinzani, zimenunuliwa kwa pesa zetu walipa kodi Wa nchi hii, wanaccm na wana Chadema
 
..na wanasiasa na wanaharakati kazi yao siyo kushika bunduki.

..sasa kwanini unataka asiyeshika bunduki apambane na anayeshika bunduki?
Wanamshikia bunduki yoyote anayeandamana bila kibali.
 
Sio ishirini tu ni kwamba hakuna aliyekuwa tayari. Hata waitishaji wenyewe. Kilichofanyika ni waitishaji kusubiri tulio tayari tuanzishe. Bahati mbaya kumbe hata sisi hatukuwa tayari.
Si maandamano bila kikomo?
Hata sasa wanawaeza/tunaweza kuanza kuandamana.
Yupo maza mmoja anaitwa Ananilea Nkya. Anatoka zake nyumbani anaenda mjini mitaa ya posta na kabango kake kadogo anapiga picha amekashikilia anarudi zake nyumbani, baadae anapost tuone ameandamana au vipi bado sijamuelewa hadi sasa. [emoji3]
 
Miaka minne ilopita nilitoa maoni kuwa, endapo wale jamaa wa UKUTA wangenywea na kutokufanya maandamano yao waliyokuwa wameyapania, basi huo ungekuwa ni ushindi mkubwa kwa Rais Magufuli. Si tu ushindi uonekanao kwa macho, bali ushindi wa kisaikolojia pia.

Niliandika hapa:


Maandamano hayo hayakufanyika. Rais Magufuli aliwaambia hao walokuwa wamepanga hayo maandamano kuwa yeye ‘hajaribiwi’.

Nadhani walimwelewa alichokisema.

Miaka 2 baadaye kukapangwa tena kuwe na maandamano makubwa ambayo yangefanyika siku ya muungano. Haya hayakuitishwa na chama chochote cha kisiasa. Yaliitishwa na dada’ake na Salary Slip 🤣.

Hakuna aliyethubutu kuingia barabarani.

Mwaka huu tena vyama vya ACT-Wazalendo na CHADEMA baada ya kushindwa uchaguzi mkuu na kudai kuwa vimefanyiwa hujuma, viongozi wake wakaitisha maandamano ya amani nchi nzima, yasiyo na kikomo, ya kupinga matokeo.

Hakuna hata mtu mmoja aliyeingia barabarani na kuthubutu kuandamana.

Huwa naona sana humu wale akina dada wa Twitter, wale wanaharakati wa Jamhuri ya Twitter, Shangazi na yule mwezake Binti Maria wakisifiwa sana wanapo longalonga huko kwenye hiyo jamhuri yao. Halafu kuna huyu raia mpya aitwaye Amsterdam. Naye naona anapenda sana kulonga huko kwenye hiyo jamhuri.

Kwamba eti ni majasiri sana. Hawamwogopi mtu, blah blah blah.

Sasa, kama kweli hawamwogopi mtu na hawaogopi kitu, kwa nini sasa huwa wanaishia kupiga mayowe kwenye hiyo jamhuri yao? Kwa nini wasitende kwa vitendo hayo maneno yao kwa kuingia barabarani na mabango yao na vipaza sauti kumpinga huyo wasiyempenda?

Jibu ni moja tu: na wao wanajua kuwa huyo Ngosha hajaribiwi. Akisema kitu akiwa amekasirika huwa anamaanisha. Aliposema hajaribiwi, naamini wote walioisikia hiyo kauli, waliielewa.

Kelele zipigwazo jamhuri ya Twitter haziwezi kubadili chochote kilichopo huku uraiani.

Kauli ya Ngosha na virungu vya kamanda Mambosasa, vimewapa watu uhamisho toka Tanzania kwenda Jamhuri ya watu wa Twitter.
Kelele za Twitter zina nguvu sana kuliko hata kutembea mtaani physically na kuandamanà.

Hata wewe Nyani Ngabu unajuwa na ndiyo maana unaingia na unasoma. Pengine kama Twitter Ingekuwa haina nguvu basi TCRA wasinge bana Mtandao. Hilo Magufuri mwenyewe analijuwa .

Usiwaponde hawa mnaowaita Key Board Warriors ukadhani hawana nguvu. Hao ndiyo waliopunguza hata harakati za WASIOJULIKANA ziluzokuwa zinaratibiwa na Makonda.

Ingekuwa Magufuli hatumii Polisi kuua watu, basi ungetuona mtaani.
 
Miaka minne ilopita nilitoa maoni kuwa, endapo wale jamaa wa UKUTA wangenywea na kutokufanya maandamano yao waliyokuwa wameyapania, basi huo ungekuwa ni ushindi mkubwa kwa Rais Magufuli. Si tu ushindi uonekanao kwa macho, bali ushindi wa kisaikolojia pia.

Niliandika hapa:


Maandamano hayo hayakufanyika. Rais Magufuli aliwaambia hao walokuwa wamepanga hayo maandamano kuwa yeye ‘hajaribiwi’.

Nadhani walimwelewa alichokisema.

Miaka 2 baadaye kukapangwa tena kuwe na maandamano makubwa ambayo yangefanyika siku ya muungano. Haya hayakuitishwa na chama chochote cha kisiasa. Yaliitishwa na dada’ake na Salary Slip 🤣.

Hakuna aliyethubutu kuingia barabarani.

Mwaka huu tena vyama vya ACT-Wazalendo na CHADEMA baada ya kushindwa uchaguzi mkuu na kudai kuwa vimefanyiwa hujuma, viongozi wake wakaitisha maandamano ya amani nchi nzima, yasiyo na kikomo, ya kupinga matokeo.

Hakuna hata mtu mmoja aliyeingia barabarani na kuthubutu kuandamana.

Huwa naona sana humu wale akina dada wa Twitter, wale wanaharakati wa Jamhuri ya Twitter, Shangazi na yule mwezake Binti Maria wakisifiwa sana wanapo longalonga huko kwenye hiyo jamhuri yao. Halafu kuna huyu raia mpya aitwaye Amsterdam. Naye naona anapenda sana kulonga huko kwenye hiyo jamhuri.

Kwamba eti ni majasiri sana. Hawamwogopi mtu, blah blah blah.

Sasa, kama kweli hawamwogopi mtu na hawaogopi kitu, kwa nini sasa huwa wanaishia kupiga mayowe kwenye hiyo jamhuri yao? Kwa nini wasitende kwa vitendo hayo maneno yao kwa kuingia barabarani na mabango yao na vipaza sauti kumpinga huyo wasiyempenda?

Jibu ni moja tu: na wao wanajua kuwa huyo Ngosha hajaribiwi. Akisema kitu akiwa amekasirika huwa anamaanisha. Aliposema hajaribiwi, naamini wote walioisikia hiyo kauli, waliielewa.

Kelele zipigwazo jamhuri ya Twitter haziwezi kubadili chochote kilichopo huku uraiani.

Kauli ya Ngosha na virungu vya kamanda Mambosasa, vimewapa watu uhamisho toka Tanzania kwenda Jamhuri ya watu wa Twitter.
Nakala kwa Salary Slip na raia wote wa Jamhuri ya Twitter. Wanajifahamu🤣
 
Back
Top Bottom