Wanaharakati wa Jamhuri ya Twitter

Wanaharakati wa Jamhuri ya Twitter

Kazi ya Mambosasa ni kushika bunduki mkuu. Unataka aje barabarani na maua?
Umenichekesha sana aisee. Kimsingi wafuasi wa Mbowe na genge lake kwa sasa wanapitia kipindi kigumu sana. Wana msongo mkubwa sana wa mawazo.

Huwezi amini wengi wao wanakesha mitandaoni wakiombea eti nchi iwekewe vikwazo utadhani wao watakuwa immune. Wapuuzi kweli hawa empty heads.
 
Jamani nisaidieni....

Hivi yule zwazwa KIGOGO 2014 ni binadamu ama JINI?!!

Kama ni binadamu...je ni mtu was namna gani na amefanya kazi sehemu zipi?!!

Nisaidieni kujua jamani kwani ni mtu gani yule hata akisomewa ALBADIRI haimkumbi na inadunda tu?!!!

Maendeleo hayana vyama
Muulize Kangi Lugola alisema siku zake zinahesabika Mwaka Jana..
 
Ni kutokuwa serious kwa waitisha maandamano. Laiti wote na famili + koo zao wangeingia barabarani tayari unazungumzia watu 100+. Wakakaa mstari wa mbele wananchi tungejitokeza.
Halafu mkiitwa keyboard warriors mnamaindi. Yaani unatamani maandamano ila waanze wengine! Bure kabisa. Upinzani wa kweli ulikuwa kabla ya 2015, sasa hivi mmebaki akina ...
2607682_Screenshot_20201101-2117262.jpg
 
Umenichekesha sana aisee. Kimsingi wafuasi wa Mbowe na genge lake kwa sasa wanapitia kipindi kigumu sana. Wana msongo mkubwa sana wa mawazo.

Huwezi amini wengi wao wanakesha mitandaoni wakiombea eti nchi iwekewe vikwazo utadhani wao watakuwa immune. Wapuuzi kweli hawa empty heads.
Wanadhani wao hawatahusika na hivyo vikwazo
 
Ingia barabarani kamanda.
Ndio maana unajiiata nyani. wewe mwenyewe upo uhamishoni, hata chadema unawaogopa, halafu unajifanya kushauri. wewe endelea na vibarua vya kulea wazee utunnze familia yako. hayo mengine tuachie/ kwa hiyo kwa akili yako ulitaka watu wainngie barabarani kupambana na vichaa kama msukuma mwenzako Magu and Mambosasa? Jiongeze mzee
 
Unafurahia kuona vyombo vya dola vinapotumika kukandamiza wapinzani wasio na silaha?

No way mtu anafurahia kukandamizwa kwa haki. Ila kuna wakati mtu anakudanganya unamshitukia na kukataa. Upinzani unakosea sana kufikiri mafanikio yao yatakuja na mashua au meli kama lugha ya kiingereza
 
Miaka minne ilopita nilitoa maoni kuwa, endapo wale jamaa wa UKUTA wangenywea na kutokufanya maandamano yao waliyokuwa wameyapania, basi huo ungekuwa ni ushindi mkubwa kwa Rais Magufuli. Si tu ushindi uonekanao kwa macho, bali ushindi wa kisaikolojia pia.

Niliandika hapa:


Maandamano hayo hayakufanyika. Rais Magufuli aliwaambia hao walokuwa wamepanga hayo maandamano kuwa yeye ‘hajaribiwi’.

Nadhani walimwelewa alichokisema.

Miaka 2 baadaye kukapangwa tena kuwe na maandamano makubwa ambayo yangefanyika siku ya muungano. Haya hayakuitishwa na chama chochote cha kisiasa. Yaliitishwa na dada’ake na Salary Slip 🤣.

Hakuna aliyethubutu kuingia barabarani.

Mwaka huu tena vyama vya ACT-Wazalendo na CHADEMA baada ya kushindwa uchaguzi mkuu na kudai kuwa vimefanyiwa hujuma, viongozi wake wakaitisha maandamano ya amani nchi nzima, yasiyo na kikomo, ya kupinga matokeo.

Hakuna hata mtu mmoja aliyeingia barabarani na kuthubutu kuandamana.

Huwa naona sana humu wale akina dada wa Twitter, wale wanaharakati wa Jamhuri ya Twitter, Shangazi na yule mwezake Binti Maria wakisifiwa sana wanapo longalonga huko kwenye hiyo jamhuri yao. Halafu kuna huyu raia mpya aitwaye Amsterdam. Naye naona anapenda sana kulonga huko kwenye hiyo jamhuri.

Kwamba eti ni majasiri sana. Hawamwogopi mtu, blah blah blah.

Sasa, kama kweli hawamwogopi mtu na hawaogopi kitu, kwa nini sasa huwa wanaishia kupiga mayowe kwenye hiyo jamhuri yao? Kwa nini wasitende kwa vitendo hayo maneno yao kwa kuingia barabarani na mabango yao na vipaza sauti kumpinga huyo wasiyempenda?

Jibu ni moja tu: na wao wanajua kuwa huyo Ngosha hajaribiwi. Akisema kitu akiwa amekasirika huwa anamaanisha. Aliposema hajaribiwi, naamini wote walioisikia hiyo kauli, waliielewa.

Kelele zipigwazo jamhuri ya Twitter haziwezi kubadili chochote kilichopo huku uraiani.

Kauli ya Ngosha na virungu vya kamanda Mambosasa, vimewapa watu uhamisho toka Tanzania kwenda Jamhuri ya watu wa Twitter.
Sawa aendelee kujimwambafai na sisi tumegundua maandamano ya amani hayawezekani tanzania kwa sababu wanaopaswa kutulinda ili tuwe na maandamano ya amani nao ni washiriki wa uovu kifuatacho ni kwamba kaa mkao wa kula na familia yako watanzania si wajinga!!!!!
 
Twitter japo mnaiponda lakini inawakera, mnatamani isiwepo kabisa.

Hilo nimethibitisha leo kwenye hotuba ya jamaa aliposema "haki huendana na wajibu", tena akarudia mara mbili na kusisitiza nadhani nimeeleweka, hapo alikuwa anawajibu wale wasumbufu kule twitter.

Sauti ya mtu huwezi kuidharau, hata mkiwepo mia moja na kati yenu akawepo mmoja anaewapinga mtamsikia tu, na atawakera pamoja na nguvu zenu, matokeo yake hamtapata usingizi mzuri mkilala usiku na ndicho kinachokupata Ngabu.
Hiyo ndio dhumuni la tweeter ni kufanya watu wakereke na sio ajenda maalumu ya kupata haki?
 
Miaka minne ilopita nilitoa maoni kuwa, endapo wale jamaa wa UKUTA wangenywea na kutokufanya maandamano yao waliyokuwa wameyapania, basi huo ungekuwa ni ushindi mkubwa kwa Rais Magufuli. Si tu ushindi uonekanao kwa macho, bali ushindi wa kisaikolojia pia.

Niliandika hapa:


Maandamano hayo hayakufanyika. Rais Magufuli aliwaambia hao walokuwa wamepanga hayo maandamano kuwa yeye ‘hajaribiwi’.

Nadhani walimwelewa alichokisema.

Miaka 2 baadaye kukapangwa tena kuwe na maandamano makubwa ambayo yangefanyika siku ya muungano. Haya hayakuitishwa na chama chochote cha kisiasa. Yaliitishwa na dada’ake na Salary Slip 🤣.

Hakuna aliyethubutu kuingia barabarani.

Mwaka huu tena vyama vya ACT-Wazalendo na CHADEMA baada ya kushindwa uchaguzi mkuu na kudai kuwa vimefanyiwa hujuma, viongozi wake wakaitisha maandamano ya amani nchi nzima, yasiyo na kikomo, ya kupinga matokeo.

Hakuna hata mtu mmoja aliyeingia barabarani na kuthubutu kuandamana.

Huwa naona sana humu wale akina dada wa Twitter, wale wanaharakati wa Jamhuri ya Twitter, Shangazi na yule mwezake Binti Maria wakisifiwa sana wanapo longalonga huko kwenye hiyo jamhuri yao. Halafu kuna huyu raia mpya aitwaye Amsterdam. Naye naona anapenda sana kulonga huko kwenye hiyo jamhuri.

Kwamba eti ni majasiri sana. Hawamwogopi mtu, blah blah blah.

Sasa, kama kweli hawamwogopi mtu na hawaogopi kitu, kwa nini sasa huwa wanaishia kupiga mayowe kwenye hiyo jamhuri yao? Kwa nini wasitende kwa vitendo hayo maneno yao kwa kuingia barabarani na mabango yao na vipaza sauti kumpinga huyo wasiyempenda?

Jibu ni moja tu: na wao wanajua kuwa huyo Ngosha hajaribiwi. Akisema kitu akiwa amekasirika huwa anamaanisha. Aliposema hajaribiwi, naamini wote walioisikia hiyo kauli, waliielewa.

Kelele zipigwazo jamhuri ya Twitter haziwezi kubadili chochote kilichopo huku uraiani.

Kauli ya Ngosha na virungu vya kamanda Mambosasa, vimewapa watu uhamisho toka Tanzania kwenda Jamhuri ya watu wa Twitter.
Waonee huruma wenzako bana. Hawakawii kutukana hawa maana ni jadi yao Khe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
Twitter japo mnaiponda lakini inawakera, mnatamani isiwepo kabisa.

Hilo nimethibitisha leo kwenye hotuba ya jamaa aliposema "haki huendana na wajibu", tena akarudia mara mbili na kusisitiza nadhani nimeeleweka, hapo alikuwa anawajibu wale wasumbufu kule twitter.

Sauti ya mtu huwezi kuidharau, hata mkiwepo mia moja na kati yenu akawepo mmoja anaewapinga mtamsikia tu, na atawakera pamoja na nguvu zenu, matokeo yake hamtapata usingizi mzuri mkilala usiku na ndicho kinachokupata Ngabu.

Hawaipendi Twitter kama walivyo kuwa hawaipendi Zanzibar
 
Sauti ya mtu huwezi kuidharau, hata mkiwepo mia moja na kati yenu akawepo mmoja anaewapinga mtamsikia tu, na atawakera pamoja na nguvu zenu, matokeo yake hamtapata usingizi mzuri mkilala usiku na ndicho kinachokupata Ngabu.
Ubarikiwe kwa upako huo ulio uona ni kweli iliyo wazi
 
Acha uoga mazee.

Huko kwingineko Mbona watu huwa wanazipiga na polisi wenye silaha...


Acha uoga mazee.

Huko kwingineko Mbona watu huwa wanazipiga na polisi wenye silaha...


Huko kwingine polisi wanajua na wanafuata haki za binadamu, huku kwetu hapo ungepigwa risasi ya moto ukafa na hakuna hatua itakayochukuliwa kwa muuaji zaidi ya pongezi na kupandishwa vyeo. Na hata ukijisalimisha utaendelea kupigwa hadi kituoni vitu ambavyo huoni nchi nyingine, huwezi kuona muandamanaji aliyeshika bango anapigwa rungu au risasi, Au rioter aliyerusha jiwe anapigwa risasi. Kama risasi zitatumika ni za mpira na maji yenye pressure, Kila mtu ana haki hata mkosaji, huku kwetu polisi hawajui tofauti ya DEMONSTRATION, PROTEST wala RIOT ili mradi inakosoa CCM basi ni kupiga, kuua,kulezamaza, kujeruhi, kudhalilisha, kukomesha nk nk
 
“Jamhuri ya Twitter” na wenzake bado ni kimbilio sahihi tu kwa nyakati hizi.

Bado watanzania wengi hawajafikia mahali pa kuona hawana cha kupoteza isipokuwa minyororo iliyowafunga lakini wenye kiu ya damu mkiongozeka mtawafikisha huko.
 
Back
Top Bottom