Wanaharakati wa Tanzania wanaugua ugonjwa wa ukosefu wa 'logical thinking'; haimaanishi harakati ni mbaya, tuwasaidie

Wanaharakati wa Tanzania wanaugua ugonjwa wa ukosefu wa 'logical thinking'; haimaanishi harakati ni mbaya, tuwasaidie

Mikopo Consultant

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2024
Posts
529
Reaction score
1,150
Harakati Harakatini

Msingi mkubwa wa haki za binadamu ni mapokeo ya Universal Declaration of Human Rights ya mwaka 1948 ambapo humo kuna vipengele 30 vya hizi haki za binadamu. Ni document ya page 8; yeyote anaweza kuisoma na kujionea kilichomo.

Ukipitia hiyo document ya haki za binadamu ambayo inaenda kutimiza miaka 80; kwa haraka haraka nimeona kwamba Tanzania ya sasa bado haiheshimu haki nyingi sana za binadamu na saa nyingine hata serikali yenyewe imejihusisha wazi wazi kwenye vitendo vya kuzivunja hizo haki za binadamu (rejea uchaguzi uchafuzi wa 2019, 2020 na 2024).

Ukitazama hivo vifungu vya haki za binadamu, nyingi ama zote zina umuhimu mkubwa sana, hata hawa watu wanaozivunja hizi haki za binadamu, endapo mzani ukabadilika na ikawa wao ndo wanavunjiwa, hakika wataona ni kiama ama dunia inawaonea. Unawezaje kustahimili kilichomkuta mzee Ali Kibao au wanachokipitia akiana Deus Soka, hata watekaji wenyewe hawawezi kupitia hizo shuruba.

Hivo basi, kuna maana kubwa ya kuwepo kwa harakati za kupigania haki za binadamu, ni kitu chema. Lakini kwa hapa Tanzania, harakati za kupigania haki za binadamu ni kama sasa zimehodhiwa na makundi ya watu ambao kwa maneno yao na matamshi yao, wanaonekana ni watu waliopungukiwa 'logical thinking'.

Logical thinking kwa tafsiri rahisi kabisa ni ule uwezo wa kuhitimisha jambo ukiwa umeshaainisha masuala kadhaa ya kulithibitisha jambo hilo (concluding something based on well grounded premises). Mfano mdogo, kuna tofauti kubwa ya hawa watu wawili

Mtu A
Hili ni tunda la embe
Embe hili lina wadudu
Embe hili halifai kuliwa

Mtu B
Hili ni tunda la embe
Embe hili halifai kuliwa

Tofauti kati ya mtu A na mtu B ni kwamba, mtu A ameenda kwenye hitimisho la 'Embe hili halifai kuliwa' ikiwa tayari ameweka na sababu ya kwanini embe hili halifai kuliwa (Huyu ni logical thinker kwasababu hitimisho lake haliachi maswali yasiyo na majibu). Mtu B yeye amerukia kwenye hitimishi bila kuweka sababu ya ni kwanini 'embe hili halifai kuliwa' (Huyu sio 'logical thinker' kwasababu maneno yake yanakaribisha maswali badala ya kuja na majibu)

Mfano mchache, nimemsoma mwandishi Erick Kabendera kwenye pages chache zile zenye serious allegations kuhusu Magufuli, nikajaribu kuzipima kwenye mizania ya logical thinking process, nikagundua kwamba nyingi zina lack complete premises. Halafu pia kuna masuala mengine kwenye kitabu yanaonekana kama breach of privacy, ambayo ni haki muhimu ya binadamu. (hapo linaibuka swali, as much as tunazipenda kweli haki za binadamu, ila tunakwepaje mtego wa kuzivunja haki hizo hizo za binadamu kwa gia ya kuzipigania haki za binadamu?)

Mfano mngine, kwa mwanadada huyu Tsehai alopata kashikashi ya kutekwa, yap anajaribu kuwa mstari wa mbele kuzipigania hizi haki lakini naye kuna vitu anaongea ambavyo wakati mwingine ni just rhetoric, havina complete premises, ni kama amekuwa mtu wa kuanguka na kukimbilia kwenye conclusion muda wote.

Madhara ya kukosekana 'logical thinking' kwa wanaharakati ni kwamba endapo watatokea 'logical thinkers' kwa upande wa oppressors, kuna hatari ya harakati za wanaharakati kupoteza ushawishi kwasababu mwisho wa siku, ili hizi haki zisimame imara wanaharakati watatakiwa kuzigonganisha hoja zao na zile za upande wa pili (oppressors), ila ikiwa wanaharakati wametawaliwa na poor reasoning, kuna hatari ya wao kushindwa hii vita na wengi wao hata wakaishia magerezani. Mfano mdogo tu, as much as hata mimi siupendi utawala wa Samia kwenye kusimamia haki za binadamu, mwanaharakati anayetoa statement ya 'Rais fulani ni muuaji na mla rushwa' unadhani mtu huyu akienda kwenye chujio la sheria anatokaje salama bila kufungwa? obvious hawezi kuja na proof kuhusu hiyo statement, sasa who is the loser?

Maana yake ni kwamba, wanaharakati wajitahidi kuwekeza kwenye utafiti na kupangilia hoja zao, hii itawafanya kutoonekana watu wa hovyo na kukurupuka, na itawapa pia uhalali na ushindi pindi mnapoingia kwenye dialogue dhidi ya oppressors; mimi naamini endapo kama 'logical thinking' iki prevail kwa wanaharakati wetu, in the long run matunda ya harakati tutayaona Tanzania, ila kama tukiendelea na aina hii ya harakati zilizo na basis ya poor logical thinking, naona itatuchukua muda sana kwa harakati kuzaa matunda.
 
Harakati Harakatini

Msingi mkubwa wa haki za binadamu ni mapokeo ya Universal Declaration of Human Rights ya mwaka 1948 ambapo humo kuna vipengele 30 vya hizi haki za binadamu. Ni document ya page 8; yeyote anaweza kuisoma na kujionea kilichomo.

Ukipitia hiyo document ya haki za binadamu ambayo inaenda kutimiza miaka 80; kwa haraka haraka nimeona kwamba Tanzania ya sasa bado haiheshimu haki nyingi sana za binadamu na saa nyingine hata serikali yenyewe imejihusisha wazi wazi kwenye vitendo vya kuzivunja hizo haki za binadamu (rejea uchaguzi uchafuzi wa 2019, 2020 na 2024).

Ukitazama hivo vifungu vya haki za binadamu, nyingi ama zote zina umuhimu mkubwa sana, hata hawa watu wanaozivunja hizi haki za binadamu, endapo mzani ukabadilika na ikawa wao ndo wanavunjiwa, hakika wataona ni kiama ama dunia inawaonea. Unawezaje kustahimili kilichomkuta mzee Ali Kibao au wanachokipitia akiana Deus Soka, hata watekaji wenyewe hawawezi kupitia hizo shuruba.

Hivo basi, kuna maana kubwa ya kuwepo kwa harakati za kupigania haki za binadamu, ni kitu chema. Lakini kwa hapa Tanzania, harakati za kupigania haki za binadamu ni kama sasa zimehodhiwa na makundi ya watu ambao kwa maneno yao na matamshi yao, wanaonekana ni watu waliopungukiwa 'logical thinking'.

Logical thinking kwa tafsiri rahisi kabisa ni ule uwezo wa kuhitimisha jambo ukiwa umeshaainisha masuala kadhaa ya kulithibitisha jambo hilo (concluding something based on well grounded premises). Mfano mdogo, kuna tofauti kubwa ya hawa watu wawili

Mtu A
Hili ni tunda la embe
Embe hili lina wadudu
Embe hili halifai kuliwa

Mtu B
Hili ni tunda la embe
Embe hili halifai kuliwa

Tofauti kati ya mtu A na mtu B ni kwamba, mtu A ameenda kwenye hitimisho la 'Embe hili halifai kuliwa' ikiwa tayari ameweka na sababu ya kwanini embe hili halifai kuliwa (Huyu ni logical thinker kwasababu hitimisho lake haliachi maswali yasiyo na majibu). Mtu B yeye amerukia kwenye hitimishi bila kuweka sababu ya ni kwanini 'embe hili halifai kuliwa' (Huyu sio 'logical thinker' kwasababu maneno yake yanakaribisha maswali badala ya kuja na majibu)

Mfano mchache, nimemsoma mwandishi Erick Kabendera kwenye pages chache zile zenye serious allegations kuhusu Magufuli, nikajaribu kuzipima kwenye mizania ya logical thinking process, nikagundua kwamba nyingi zina lack complete premises. Halafu pia kuna masuala mengine kwenye kitabu yanaonekana kama breach of privacy, ambayo ni haki muhimu ya binadamu. (hapo linaibuka swali, as much as tunazipenda kweli haki za binadamu, ila tunakwepaje mtego wa kuzivunja haki hizo hizo za binadamu kwa gia ya kuzipigania haki za binadamu?)

Mfano mngine, kwa mwanadada huyu Tsehai alopata kashikashi ya kutekwa, yap anajaribu kuwa mstari wa mbele kuzipigania hizi haki lakini naye kuna vitu anaongea ambavyo wakati mwingine ni just rhetoric, havina complete premises, ni kama amekuwa mtu wa kuanguka na kukimbilia kwenye conclusion muda wote.

Madhara ya kukosekana 'logical thinking' kwa wanaharakati ni kwamba endapo watatokea 'logical thinkers' kwa upande wa oppressors, kuna hatari ya harakati za wanaharakati kupoteza ushawishi kwasababu mwisho wa siku, ili hizi haki zisimame imara wanaharakati watatakiwa kuzigonganisha hoja zao na zile za upande wa pili (oppressors), ila ikiwa wanaharakati wametawaliwa na poor reasoning, kuna hatari ya wao kushindwa hii vita na wengi wao hata wakaishia magerezani. Mfano mdogo tu, as much as hata mimi siupendi utawala wa Samia kwenye kusimamia haki za binadamu, mwanaharakati anayetoa statement ya 'Rais fulani ni muuaji na mla rushwa' unadhani mtu huyu akienda kwenye chujio la sheria anatokaje salama bila kufungwa? obvious hawezi kuja na proof kuhusu hiyo statement, sasa who is the loser?

Maana yake ni kwamba, wanaharakati wajitahidi kuwekeza kwenye utafiti na kupangilia hoja zao, hii itawafanya kutoonekana watu wa hovyo na kukurupuka, na itawapa pia uhalali na ushindi pindi mnapoingia kwenye dialogue dhidi ya oppressors; mimi naamini endapo kama 'logical thinking' iki prevail kwa wanaharakati wetu, in the long run matunda ya harakati tutayaona Tanzania, ila kama tukiendelea na aina hii ya harakati zilizo na basis ya poor logical thinking, naona itatuchukua muda sana kwa harakati kuzaa matunda.
Mkuu,
Rahisi Sana kuandika Lakini kutenda ni kitu kigumu mno.
Unataka wanaharajati wa TZ wawe hivyo kwenye mazingira ya TZ? Ni kuwaonea bure.
Kitabu cha Kabendera mimi naendelea kukisoma. Unataka ushahidi gani? Vitabu vya uchunguzi sio mahakamani na havihitaji ushahidi kama wa mahakamani. Taarifa inatakiwa tu iwe collaborated. Kwa mfano watu watatu wasiojuana wakasema Ben Saanane aliuawa Ikulu. Na ukachunguza na kugundua source ya info sio moja. Hiyo inatosha kuandika kwenye kitabu. Lakini haitoshi kumfunga mtu mahakamani.

Sisi wengine tumeenda mbali zaidi kwa kuingia kwenye mijadala kule Clubhouse ya interested parts za kitabu hicho. Wadau mbalimbali wakiwemo wahusika wakuu wa awamu ya tano wanakubali mambo mengi kwamba ni kweli. Hata alipokosea Kabendera wengine wanasema hili ni sawa ila hili sio sawa. Kumbuka huo ni uchunguzi. Mfano Zitto, mzee Diallo na wengine wanathibitisha mambo mengi.
Vitabu vya uchunguzi ni fictions za ukweli. Vinatoa mwanga ndani ya giza. Havitoi ushahidi wa mahakamani.

Mimi sijamaliza kukisoma ila jamaa kafanya utafiti mkubwa sana. Sio kitabu cha kukidharau. Kuna mambo mazito ya nchi yetu ambayo Watanzania wengi hawayajui.

Nakushauri soma kitabu chote au shirika humo clubhouse ambako wanasoma chapter kisha kuijadili. Utagundua mambo mengi yametokea hata kama sio kwa usahihi wa asilimia 100 wa Kabendera.

Hivi unafikiri Kwanini serikali wameshindwa kuongea kitu? Ni kwasababu wao wenyewe wanajua ukweli huo ba sehemu zingine wao wenyewe Ndio source.

Hiki kitabu kitusaidie kupata tume huru kuchunguza vifo vya watu.

Kwa Mfano kusema JPM alifariki tarehe 12/03 ni kitu watu wengi wanathibitisha.

Kwamba alikufa kwa covid hivi unahitaji hata collaborators? Angalia tu waliomzunguka walivyopukutika wakati huo. Makamu akaponea chupuchupu.
 
Mkuu,
Rahisi Sana kuandika Lakini kutenda ni kitu kigumu mno.
Unataka wanaharajati wa TZ wawe hivyo kwenye mazingira ya TZ? Ni kuwaonea bure.
Kitabu cha Kabendera mimi naendelea kukisoma. Unataka ushahidi gani? Vitabu vya uchunguzi sio mahakamani na havihitaji ushahidi kama wa mahakamani. Taarifa inatakiwa tu iwe collaborated. Kwa mfano watu watatu wasiojuana wakasema Ben Saanane aliuawa Ikulu. Na ukachunguza na kugundua source ya info sio moja. Hiyo inatosha kuandika kwenye kitabu. Lakini haitoshi kumfunga mtu mahakamani.

Sisi wengine tumeenda mbali zaidi kwa kuingia kwenye mijadala kule Clubhouse ya interested parts za kitabu hicho. Wadau mbalimbali wakiwemo wahusika wakuu wa awamu ya tano wanakubali mambo mengi kwamba ni kweli. Hata alipokosea Kabendera wengine wanasema hili ni sawa ila hili sio sawa. Kumbuka huo ni uchunguzi. Mfano Zitto, mzee Diallo na wengine wanathibitisha mambo mengi.
Vitabu vya uchunguzi ni fictions za ukweli. Vinatoa mwanga ndani ya giza. Havitoi ushahidi wa mahakamani.

Mimi sijamaliza kukisoma ila jamaa kafanya utafiti mkubwa sana. Sio kitabu cha kukidharau. Kuna mambo mazito ya nchi yetu ambayo Watanzania wengi hawayajui.

Nakushauri soma kitabu chote au shirika humo clubhouse ambako wanasoma chapter kisha kuijadili. Utagundua mambo mengi yametokea hata kama sio kwa usahihi wa asilimia 100 wa Kabendera.

Hivi unafikiri Kwanini serikali wameshindwa kuongea kitu? Ni kwasababu wao wenyewe wanajua ukweli huo ba sehemu zingine wao wenyewe Ndio source.

Hiki kitabu kitusaidie kupata tume huru kuchunguza vifo vya watu.

Kwa Mfano kusema JPM alifariki tarehe 12/03 ni kitu watu wengi wanathibitisha.

Kwamba alikufa kwa covid hivi unahitaji hata collaborators? Angalia tu waliomzunguka walivyopukutika wakati huo. Makamu akaponea chupuchupu.
Thinking logically haihitaji kuangalia mazingira, ni habit tu ambayo mtu ukiishi nayo maana yake ni kwamba hautakuwa unatoa statement zenye mkanganyiko.

Ukiandika kitu ambacho unajua ni half truth ama huna uhakika nalo, unatakiwa utafute namna ya ku li present ili pia wasikilizaji wako wawe na hizo hisia kwamba ni half truth.

Na sio tabia ya ku present kitu kama fact wakati unajua halijakamilika
 
Umepinga swala la mazingira na unacontradict kila ulichokisimamia kwenye andiko lako..twende taratibu kwenye baadi ya hoja ulizoweka

1)Mtu A amesema kwa nini tunda la embe lisiliwe..lakini vipi kama wadudu wanaonekana dhahiri kuna haja gani ya mtu B kusema hilo?hapo mtu B anavuka kizingiti hicho kwasababu anaamini katika common sense kwamba tunaona kuna wadudu kwenye tunda na limeharibika..haibadilishi kwamba ni embe lakini matumizi yanabadilika kwa macho yetu tu bila hata kuhutaji kauli ya mtu kusema kwamba linafaa ama halifai.

2)Mwandishi wa kitabu hana ulazima wa kuthibitisha kwasababu hilo lipo nje ya uwezo wake na ndio maana anatumia maneno kama allegedly..mwandishi hana uwezo wa kuwalinda waliompa fununu hizo ikiwa ataweka ushahidi utakaolead shuhuda kufahamika..ili mwandishi atoe ushahidi wa aina hio ni lazima kuwepo na utayari wa taasisi kusema wazi kua zitawalinda watakaothibitisha matukio hayo kutokea..Ndio maana mwandishi anabakiwa na option moja tu..kurise concerns ili wale wenye uwezo wa kufanya investigation huru bila kua na wasiwasi wa ulinzi juu ya maisha ya mashuhuda wachukue hatua za kuclear hizo allegations!

3)Umejaribu kulinganisha ikiwa watatokea wenye ‘logical thinking’ upande wa watesi..ni rahisi zaidi kuonekana unawaza mawazo yenye ushahidi ikiwa upo upande wenye usalama na every resource at your disposal! System inakupa kila unachokihitaji ilikufanikisha lengo lako la kutetea uovu..media outlets zinakua upande wako.. intelligence agencies zinakua upande wako na unaweza hata kuandaa mazingira ya jambo unalotaka kulifanya hata miaka kadhaa kabla ya kulifanya hivyo ni rahisi zaidi kuonekana una hoja..
Mfano unaweza ukatengeneza tatizo kisha ukalitatua baada ya kuona impact uliyoilenga imekwishapatikana.

Ingawa nakubaliana na wewe juu ya uliyoyasema lakini hili sio swala la ‘black or white’ ni swala lenye mambo mengi hapo katikati.

Mataifa makubwa zaidi duniani wanaeneza propaganda kwasababu wana-resource zote upande wao hivyo wanaweza wakabadili nyeusi kua ‘’yenye giza’’ na kulinda narratives zao dhidi ya mataifa yasiyo na nguvu hivyo hivyo kwa watu binafsi.

Fikiria vizuri hata kwa waandishi wa habari ambao wanajaribu kuhiji logically juu ya mambo ambayo watawala hawataki yawe kwenye spotlight nini hua kinawakuta..wanaorisk zaidi huishia kuziachia familia zao majonzi ya milele ambao wanadumu kidogo ni hawa wanaotuacha na maswali kidogo kuliko kuweka kila kitu wazi haijalishi wanajua ukweli wote au nao wanajua kidogo tu.
 
Harakati Harakatini

Msingi mkubwa wa haki za binadamu ni mapokeo ya Universal Declaration of Human Rights ya mwaka 1948 ambapo humo kuna vipengele 30 vya hizi haki za binadamu. Ni document ya page 8; yeyote anaweza kuisoma na kujionea kilichomo.

Ukipitia hiyo document ya haki za binadamu ambayo inaenda kutimiza miaka 80; kwa haraka haraka nimeona kwamba Tanzania ya sasa bado haiheshimu haki nyingi sana za binadamu na saa nyingine hata serikali yenyewe imejihusisha wazi wazi kwenye vitendo vya kuzivunja hizo haki za binadamu (rejea uchaguzi uchafuzi wa 2019, 2020 na 2024).

Ukitazama hivo vifungu vya haki za binadamu, nyingi ama zote zina umuhimu mkubwa sana, hata hawa watu wanaozivunja hizi haki za binadamu, endapo mzani ukabadilika na ikawa wao ndo wanavunjiwa, hakika wataona ni kiama ama dunia inawaonea. Unawezaje kustahimili kilichomkuta mzee Ali Kibao au wanachokipitia akiana Deus Soka, hata watekaji wenyewe hawawezi kupitia hizo shuruba.

Hivo basi, kuna maana kubwa ya kuwepo kwa harakati za kupigania haki za binadamu, ni kitu chema. Lakini kwa hapa Tanzania, harakati za kupigania haki za binadamu ni kama sasa zimehodhiwa na makundi ya watu ambao kwa maneno yao na matamshi yao, wanaonekana ni watu waliopungukiwa 'logical thinking'.

Logical thinking kwa tafsiri rahisi kabisa ni ule uwezo wa kuhitimisha jambo ukiwa umeshaainisha masuala kadhaa ya kulithibitisha jambo hilo (concluding something based on well grounded premises). Mfano mdogo, kuna tofauti kubwa ya hawa watu wawili

Mtu A
Hili ni tunda la embe
Embe hili lina wadudu
Embe hili halifai kuliwa

Mtu B
Hili ni tunda la embe
Embe hili halifai kuliwa

Tofauti kati ya mtu A na mtu B ni kwamba, mtu A ameenda kwenye hitimisho la 'Embe hili halifai kuliwa' ikiwa tayari ameweka na sababu ya kwanini embe hili halifai kuliwa (Huyu ni logical thinker kwasababu hitimisho lake haliachi maswali yasiyo na majibu). Mtu B yeye amerukia kwenye hitimishi bila kuweka sababu ya ni kwanini 'embe hili halifai kuliwa' (Huyu sio 'logical thinker' kwasababu maneno yake yanakaribisha maswali badala ya kuja na majibu)

Mfano mchache, nimemsoma mwandishi Erick Kabendera kwenye pages chache zile zenye serious allegations kuhusu Magufuli, nikajaribu kuzipima kwenye mizania ya logical thinking process, nikagundua kwamba nyingi zina lack complete premises. Halafu pia kuna masuala mengine kwenye kitabu yanaonekana kama breach of privacy, ambayo ni haki muhimu ya binadamu. (hapo linaibuka swali, as much as tunazipenda kweli haki za binadamu, ila tunakwepaje mtego wa kuzivunja haki hizo hizo za binadamu kwa gia ya kuzipigania haki za binadamu?)

Mfano mngine, kwa mwanadada huyu Tsehai alopata kashikashi ya kutekwa, yap anajaribu kuwa mstari wa mbele kuzipigania hizi haki lakini naye kuna vitu anaongea ambavyo wakati mwingine ni just rhetoric, havina complete premises, ni kama amekuwa mtu wa kuanguka na kukimbilia kwenye conclusion muda wote.

Madhara ya kukosekana 'logical thinking' kwa wanaharakati ni kwamba endapo watatokea 'logical thinkers' kwa upande wa oppressors, kuna hatari ya harakati za wanaharakati kupoteza ushawishi kwasababu mwisho wa siku, ili hizi haki zisimame imara wanaharakati watatakiwa kuzigonganisha hoja zao na zile za upande wa pili (oppressors), ila ikiwa wanaharakati wametawaliwa na poor reasoning, kuna hatari ya wao kushindwa hii vita na wengi wao hata wakaishia magerezani. Mfano mdogo tu, as much as hata mimi siupendi utawala wa Samia kwenye kusimamia haki za binadamu, mwanaharakati anayetoa statement ya 'Rais fulani ni muuaji na mla rushwa' unadhani mtu huyu akienda kwenye chujio la sheria anatokaje salama bila kufungwa? obvious hawezi kuja na proof kuhusu hiyo statement, sasa who is the loser?

Maana yake ni kwamba, wanaharakati wajitahidi kuwekeza kwenye utafiti na kupangilia hoja zao, hii itawafanya kutoonekana watu wa hovyo na kukurupuka, na itawapa pia uhalali na ushindi pindi mnapoingia kwenye dialogue dhidi ya oppressors; mimi naamini endapo kama 'logical thinking' iki prevail kwa wanaharakati wetu, in the long run matunda ya harakati tutayaona Tanzania, ila kama tukiendelea na aina hii ya harakati zilizo na basis ya poor logical thinking, naona itatuchukua muda sana kwa harakati kuzaa matunda.
Elimu yako kuhusu somo la LOGIC ni ndogo sana.
Anza upya na kozi hizi:
1. TRUTH TABLES
2. LOGIC GATES.
OTHERWISE
Usitupotezee muda.
 
Harakati Harakatini

Msingi mkubwa wa haki za binadamu ni mapokeo ya Universal Declaration of Human Rights ya mwaka 1948 ambapo humo kuna vipengele 30 vya hizi haki za binadamu. Ni document ya page 8; yeyote anaweza kuisoma na kujionea kilichomo.

Ukipitia hiyo document ya haki za binadamu ambayo inaenda kutimiza miaka 80; kwa haraka haraka nimeona kwamba Tanzania ya sasa bado haiheshimu haki nyingi sana za binadamu na saa nyingine hata serikali yenyewe imejihusisha wazi wazi kwenye vitendo vya kuzivunja hizo haki za binadamu (rejea uchaguzi uchafuzi wa 2019, 2020 na 2024).

Ukitazama hivo vifungu vya haki za binadamu, nyingi ama zote zina umuhimu mkubwa sana, hata hawa watu wanaozivunja hizi haki za binadamu, endapo mzani ukabadilika na ikawa wao ndo wanavunjiwa, hakika wataona ni kiama ama dunia inawaonea. Unawezaje kustahimili kilichomkuta mzee Ali Kibao au wanachokipitia akiana Deus Soka, hata watekaji wenyewe hawawezi kupitia hizo shuruba.

Hivo basi, kuna maana kubwa ya kuwepo kwa harakati za kupigania haki za binadamu, ni kitu chema. Lakini kwa hapa Tanzania, harakati za kupigania haki za binadamu ni kama sasa zimehodhiwa na makundi ya watu ambao kwa maneno yao na matamshi yao, wanaonekana ni watu waliopungukiwa 'logical thinking'.

Logical thinking kwa tafsiri rahisi kabisa ni ule uwezo wa kuhitimisha jambo ukiwa umeshaainisha masuala kadhaa ya kulithibitisha jambo hilo (concluding something based on well grounded premises). Mfano mdogo, kuna tofauti kubwa ya hawa watu wawili

Mtu A
Hili ni tunda la embe
Embe hili lina wadudu
Embe hili halifai kuliwa

Mtu B
Hili ni tunda la embe
Embe hili halifai kuliwa

Tofauti kati ya mtu A na mtu B ni kwamba, mtu A ameenda kwenye hitimisho la 'Embe hili halifai kuliwa' ikiwa tayari ameweka na sababu ya kwanini embe hili halifai kuliwa (Huyu ni logical thinker kwasababu hitimisho lake haliachi maswali yasiyo na majibu). Mtu B yeye amerukia kwenye hitimishi bila kuweka sababu ya ni kwanini 'embe hili halifai kuliwa' (Huyu sio 'logical thinker' kwasababu maneno yake yanakaribisha maswali badala ya kuja na majibu)

Mfano mchache, nimemsoma mwandishi Erick Kabendera kwenye pages chache zile zenye serious allegations kuhusu Magufuli, nikajaribu kuzipima kwenye mizania ya logical thinking process, nikagundua kwamba nyingi zina lack complete premises. Halafu pia kuna masuala mengine kwenye kitabu yanaonekana kama breach of privacy, ambayo ni haki muhimu ya binadamu. (hapo linaibuka swali, as much as tunazipenda kweli haki za binadamu, ila tunakwepaje mtego wa kuzivunja haki hizo hizo za binadamu kwa gia ya kuzipigania haki za binadamu?)

Mfano mngine, kwa mwanadada huyu Tsehai alopata kashikashi ya kutekwa, yap anajaribu kuwa mstari wa mbele kuzipigania hizi haki lakini naye kuna vitu anaongea ambavyo wakati mwingine ni just rhetoric, havina complete premises, ni kama amekuwa mtu wa kuanguka na kukimbilia kwenye conclusion muda wote.

Madhara ya kukosekana 'logical thinking' kwa wanaharakati ni kwamba endapo watatokea 'logical thinkers' kwa upande wa oppressors, kuna hatari ya harakati za wanaharakati kupoteza ushawishi kwasababu mwisho wa siku, ili hizi haki zisimame imara wanaharakati watatakiwa kuzigonganisha hoja zao na zile za upande wa pili (oppressors), ila ikiwa wanaharakati wametawaliwa na poor reasoning, kuna hatari ya wao kushindwa hii vita na wengi wao hata wakaishia magerezani. Mfano mdogo tu, as much as hata mimi siupendi utawala wa Samia kwenye kusimamia haki za binadamu, mwanaharakati anayetoa statement ya 'Rais fulani ni muuaji na mla rushwa' unadhani mtu huyu akienda kwenye chujio la sheria anatokaje salama bila kufungwa? obvious hawezi kuja na proof kuhusu hiyo statement, sasa who is the loser?

Maana yake ni kwamba, wanaharakati wajitahidi kuwekeza kwenye utafiti na kupangilia hoja zao, hii itawafanya kutoonekana watu wa hovyo na kukurupuka, na itawapa pia uhalali na ushindi pindi mnapoingia kwenye dialogue dhidi ya oppressors; mimi naamini endapo kama 'logical thinking' iki prevail kwa wanaharakati wetu, in the long run matunda ya harakati tutayaona Tanzania, ila kama tukiendelea na aina hii ya harakati zilizo na basis ya poor logical thinking, naona itatuchukua muda sana kwa harakati kuzaa matunda.
Nikuulize Swali, naomba utoe mifano ya haki za binaadamu ambazo wanaharakati wameshindwa kuzitetea vizuri Kwa kuwa na hoja nzuri na jinsi ya kutatua changamoto hizo
 
Elimu yako kuhusu somo la LOGIC ni ndogo sana.
Anza upya na kozi hizi:
1. TRUTH TABLES
2. LOGIC GATES.
OTHERWISE
Usitupotezee muda.
Mimi sikuwa na maana kwamba elimu yangu ya logic ni kubwa, hayo madai yako sijui umeyatoa wapi.

Kwa kusema kwemba elimu yangu ni ndogo sana, ukilinganisha na elimu ya nani?

Unavyonipa hayo mapendekezo una maana gani? Hivi unadhani source of knowledge inaweza kupatikana kwenye jambo moja tu? Unaweza usimsome Plato ila ukamsoma Aurelius na ukapata knowledge ile ile kuhusu philosophy.

Unaonekana ni mtu uliokengeuka
 
Nikuulize Swali, naomba utoe mifano ya haki za binaadamu ambazo wanaharakati wameshindwa kuzitetea vizuri Kwa kuwa na hoja nzuri na jinsi ya kutatua changamoto hizo
Mimi sijasema kwamba wanashindwa kupigania haki, ila hoja yangu imejikita zaidi kwamba kuna matendo ya wanaharakati matamshi na maandiko yao ambayo yanakosa kufuata kanuni za 'logical thinking'. Maana yake saa nyingine hupelekea kuonekana kwamba madai yao ni ya uongo kitu ambacho kinaweka ukakasi hata kwenye suala zima la kupigania haki za binadamu. Hilo tu
 
Back
Top Bottom