Wanajeshi wawili wa Tanzania washikiliwa DRC kupisha uchunguzi wa mauaji ya raia

Wanajeshi wawili wa Tanzania washikiliwa DRC kupisha uchunguzi wa mauaji ya raia

USSR

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2015
Posts
10,904
Reaction score
26,184
Afisa mmoja wa Umoja wa Mataifa amewaambia waandishi wa habari kuwa askari walinda amani wa MONISCO waliokamatwa siku ya jumapili ni kutoka Tanzania, wamekamatwa kupisha uchunguzi wa mauaji ya waandamanaji raia wa Congo.

Tangu kuzuka kwa maandamano ya kupinga walinda amani nchini DRC askari watano wameuwa, waliouwawa ni wahindi wawili, wamoroco wawili na moja aliuwawa peke yako na utaifa wake haukawekwa wazi ambao wote hawajafanya kazi zaidia ya miezi sita.

Maandamanaji wamekuwa wakivamia kambi za askari walinda amani wakishinikiza waondoke kwa kuwa wameshindwa kuleta amani kwa miaka kadhaa huku hali ikizidi kudhorota mashariki mwa Congo.

========

Afisa wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa ameiambia BBC kwamba walinda amani waliokamatwa siku ya Jumapili kwa kuwapiga risasi watu wawili hadi kufa katika mpaka kati ya Congo na Uganda walikuwa wanatoka Tanzania.

Haya ni kwa mujibu wa, Naibu Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa MONUSCO, Khassim Diagne, aliyezungumza na BBC

Umoja wa Mataifa umeshtumu vikali shambulio hilo ambapo watu 15 walijeruhiwa .

Katika kipindi cha juma moja lililopita takriban watu 20 wamefariki katika maandamano ya ghasiadhidi ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanaojulikana kama MONUSCO .

Raia wengi wa DR Congo wamewashtumu walinda amani hao kwa kushindwa kuwalinda raia kutokana na mashambulizi yanayotekelezwa na waasi.

Huku shambulizi hilo la siku ya Jumapili likitarajiwa kuliharibia sifa jeshi hilo la Umoja wa mataifa , wanahabari wanasema vurugu zimejitokeza kutokana na kile wakazi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wanaona kushindwa kwa kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa kusitisha mashambulizi ya makundi yenye silaha katika eneo hilo na kusababisha maandamano makali wiki iliyopita.

Waandamanaji hao walishambulia kambi mbili za Umoja wa Mataifa huko Goma na Butembo, ambapo walinda amani wanne wa Umoja wa Mataifa waliuawa.

Walinda amani wawili kati ya hao walikuwa raia wa Morocco na wengine wawili walikuwa Wahindi, wote walikuwa wamefanya kazi nchini DR Congo kwa Umoja wa Mataifa kwa muda wa chini ya miezi sita - huku mmoja wa waliouawa akiwa amekaa kwa miezi miwili na siku 22 pekee.

Mwezi Juni vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa viliondoka katika jimbo tofauti la mashariki - Tanganyika - baada ya kile walichokieleza kuwa kuimarika kwa hali ya usalama.

Chanzo: BBC
 
DRC, Nigeria, Mozambique nk..kuna nini? Nchi hazina amani na usalama lakini kuna resources adimu na muhimu ambazo zinazohitajika na nchi kubwa na zilizoendelea duniani. Hitimisho langu ni kuwa hayo mataifa makubwa ni chanzo na yanachangia hali tete ya kiusalama katika nchi nyingi duniani kwa ajili ya kutimiza maslahi yao.
 
Mbona umenukuu gazeti Wala ujaandika hbr hyo ya jwtz asbh nitazikioiza bbc
 
Afisa mmoja wa umoja wa mataifa amewaambia waandishi wa habari kuwa askari walinda amani wa MONISCO waliokamatwa siku ya jumapili ni kutoka Tanzania ,wamekamatwa kupisha uchunguzi wa mauaji ya waandamanaji raia wa congo.

Tangu kuzuka kwa maandamano ya kupinga walinda amani nchini DRC askari watano wameuwa ,waliouwawa ni wahindi wawili ,wamoroco wawili na moja aliuwawa peke yako na utaifa wake haukawekwa wazi ambao wote hawajafanya kazi zaidia ya miezi sita .

Maandamanaji wamekuwa wakivamia kambi za askari walinda amani wakishinikiza waondoke kwa kuwa wameshindwa kuleta amani kwa miaka kadhaa huku hali ikizidi kudhorota mashariki mwa Congo

BBC


USSR View attachment 2311558
Uchochezi huu. TCRA mkamateni huyu USSR
 
Hawa wananchi wa DRC wako sahihi.
UN na genge lao waondoke DRC
Imekuwa kama biashara, watu wanaletwa kuchuma mali, lakini kazi wanayofanya haionekani..

Umoja wa mataifa hapa ni mfano mbaya kabisa wa kuigwa.

Wawawwezeshe waCongo wenyewe walinde nchi yao, siyo kupeleka watu toka nchi zingine.

Pole yao hawa wajeshi wetu. Pengine maisha yao yalikuwa hatarini, huwezi juwa.
 
DRC, Nigeria, Mozambique nk..kuna nini? Nchi hazina amani na usalama lakini kuna resources adimu na muhimu ambazo zinazohitajika na nchi kubwa na zilizoendelea duniani. Hitimisho langu ni kuwa hayo mataifa makubwa ni chanzo na yanachangia hali tete ya kiusalama katika nchi nyingi duniani kwa ajili ya kutimiza maslahi yao.
Watawala wao sasa, wakishahakikishiwa kushinda uchaguzi they can offer anythng
 
Hao walinda amani huko DRC ambao wanaambiwa waondoke, si watoke warudi Makwao, kwan shida nn? Wenye nchi yao hawataki kwan lazima?

Naungana na wananchi wa DRC, walinda amani husika watoke huko warudi makwao.
 
DRC, Nigeria, Mozambique nk..kuna nini? Nchi hazina amani na usalama lakini kuna resources adimu na muhimu ambazo zinazohitajika na nchi kubwa na zilizoendelea duniani. Hitimisho langu ni kuwa hayo mataifa makubwa ni chanzo na yanachangia hali tete ya kiusalama katika nchi nyingi duniani kwa ajili ya kutimiza maslahi yao.
Na hakutowai pata amani kamwe kama wataendelea kushikilia demokrasia ya kipumbavu ya kuwakumbatia viongoz waizi na hili la kuendekeza majumuiya ya kishenzi kama hayo ya umoja wa kimataifa usio na misingi zaid ya kufuata matakwa ya wazungu.

Tz bahati yetu watangulizi walifanya mema kuyatimua mabeberu or otherwise tungekuwa sawa na south afrika kwa kubaguliwa ama kuporwa ardhi nzuri pia migogoro kama ys kongo ingekuwa sehem ya maisha yetu.

Hili jambo hawapendi kulisikia wale washenzi wanaojiita watetezi wa haki pia wale wapumbavu mapuppets wa wahuni wa kimagharibi.

Afrika ili migogoro ikwishe ilitakiwa kufumuliwa upya uongozi.

Huwezi kusuruhishwa migogoro kwa bunduki wakati wasababishaji wa migogoro na ugaidi ni sehem ya viongoz na wanasiasa, so kila jambo lifanyikalo kuzuia machafuko wanalijua wahun ambao ni miongoni mwa viongoz wanaokesha kwenye majukwaa ya kuleta amani kumbe nyuma ya pazia ndio hao hao waharibifu.

Nchi za Africa kama zitatulia na migogoro kuisha nawahakikishia uchumi wa nchi mnazoziita zinanguvu basi zitashuka na kupotea within the short time.

Ni vile waafrika hatujielewi kwa kupumbazwa na propaganda za kipumbavu, ikiwepo siasa&elimu ya kishenzi.

Itafika muda watu wakiamka haya yatakwisha tu
 
Afisa mmoja wa Umoja wa Mataifa amewaambia waandishi wa habari kuwa askari walinda amani wa MONISCO waliokamatwa siku ya jumapili ni kutoka Tanzania, wamekamatwa kupisha uchunguzi wa mauaji ya waandamanaji raia wa Congo.

Tangu kuzuka kwa maandamano ya kupinga walinda amani nchini DRC askari watano wameuwa, waliouwawa ni wahindi wawili, wamoroco wawili na moja aliuwawa peke yako na utaifa wake haukawekwa wazi ambao wote hawajafanya kazi zaidia ya miezi sita.

Maandamanaji wamekuwa wakivamia kambi za askari walinda amani wakishinikiza waondoke kwa kuwa wameshindwa kuleta amani kwa miaka kadhaa huku hali ikizidi kudhorota mashariki mwa Congo.

========

Afisa wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa ameiambia BBC kwamba walinda amani waliokamatwa siku ya Jumapili kwa kuwapiga risasi watu wawili hadi kufa katika mpaka kati ya Congo na Uganda walikuwa wanatoka Tanzania.

Haya ni kwa mujibu wa, Naibu Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa MONUSCO, Khassim Diagne, aliyezungumza na BBC

Umoja wa Mataifa umeshtumu vikali shambulio hilo ambapo watu 15 walijeruhiwa .

Katika kipindi cha juma moja lililopita takriban watu 20 wamefariki katika maandamano ya ghasiadhidi ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanaojulikana kama MONUSCO .

Raia wengi wa DR Congo wamewashtumu walinda amani hao kwa kushindwa kuwalinda raia kutokana na mashambulizi yanayotekelezwa na waasi.

Huku shambulizi hilo la siku ya Jumapili likitarajiwa kuliharibia sifa jeshi hilo la Umoja wa mataifa , wanahabari wanasema vurugu zimejitokeza kutokana na kile wakazi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wanaona kushindwa kwa kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa kusitisha mashambulizi ya makundi yenye silaha katika eneo hilo na kusababisha maandamano makali wiki iliyopita.

Waandamanaji hao walishambulia kambi mbili za Umoja wa Mataifa huko Goma na Butembo, ambapo walinda amani wanne wa Umoja wa Mataifa waliuawa.

Walinda amani wawili kati ya hao walikuwa raia wa Morocco na wengine wawili walikuwa Wahindi, wote walikuwa wamefanya kazi nchini DR Congo kwa Umoja wa Mataifa kwa muda wa chini ya miezi sita - huku mmoja wa waliouawa akiwa amekaa kwa miezi miwili na siku 22 pekee.

Mwezi Juni vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa viliondoka katika jimbo tofauti la mashariki - Tanganyika - baada ya kile walichokieleza kuwa kuimarika kwa hali ya usalama.

Chanzo: BBC
Wamezoea huku kwao ni kupiga risasi waandamanaji kisha wanasifiwa.
 
Wamezoea huku kwao ni kupiga risasi waandamanaji kisha wanasifiwa.
Huna unalolijua. Ingetokea hao waandamanaji kuwauwa hao Askari wetu bado mngesema Askari wetu wamekaa kindezi tu. Maandamano yanayoendelea huko unaambiwa yamesababisha walinda amani kadhaa kupigwa risasi na kufa. Mimi siamini hao askari wetu wamekurupuka tu
 
Wiki iliyopita GENTAMYCINE nilianzisha Uzi wa 'Kufumba' hapa JamiiForums (nashukuru Werevu baadhi walinielewa nilichokuwa nakilenga) na kuitaka nchi Moja ikatoe Askari. Wake wa Kulinda Amani wanaounda Kikosi cha MONUSCO huko Congo DR ila nikaambulia Dhihaka nyingi na Kuonekana nina Chuki na hiyo nchi pamoja na Rais wake.

Taarifa ikufikie kuwa Umoja wa Mataifa kupitia Katibu Mkuu wake Umesikitishwa na Kitendo cha Wanajeshi wa Tanzania (JWTZ) wanaounda sehemu ya Jeshi la Kulinda Amani la MONUSCO kwa Makusudi Kuua Raia Wawili wa Congo DR ( mpaka wa Congo DR na Uganda ) katika Maandamano ya kutowataka Wao (MONUSCO) kuendelea kuwepo huko.

Kwa mujibu wa Afisa kutoka UN ni kwamba tayari Wanajeshi hao kutoka Tanzania wa JWTZ wanaounda Kikosi cha MONUSCO walioua Wameshakamatwa na taratibu zingine za Kinidhamu zinaendelea.

Haya tunaomba pia Serikali ya Tanzania, Balozi wa Tanzania nchini Congo DR na hata JWTZ litoe Tamko na Wote hawa Wasione Aibu Kukiri na Kuwaomba Radhi Wakongo na hata Watanzania kwani tayari Tukio hili limeshaichafua Tanzania.

Taarifa hii (ya hili Tukio) GENTAMYCINE nimeitoa (nimeisikia) kutoka Amka na BBC Asubuhi hii ya Leo tarehe 2 August, 2022.

Nimalizie tu kwa kutoa Pongezi zangu za dhati kwa Majeshi ya Kenya, Uganda na Rwanda ambayo nayo yana Wanajeshi wao huko MONUSCO kwa kuwa na Nidhamu na Maadili ya Kijeshi kiasi cha Kutolalamikiwa na Raia wa Congo DR au hata kutakiwa Kuondoka huko kama wanavyotakiwa Kuondoka Askari (Wanajeshi) wa MONUSCO wanaotokea nchini Tanzania.

Haya kawaondoeni upesi Askari wenu huko Congo DR kwani Raia wa Congo DR hawawataki na hawawapendi kutokana na tabia yao ya Kuua Raia hovyo badala ya Kuua Waasi ambao Wamejaa huko na kila Siku Wanatesa Watu.
 
Back
Top Bottom