Pre GE2025 Wananchi wa Kilimanjaro wachangishana kurekebisha barabara mbovu yenye urefu wa kilomita 72

Pre GE2025 Wananchi wa Kilimanjaro wachangishana kurekebisha barabara mbovu yenye urefu wa kilomita 72

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Huu ni ujumbe kuwa Dr. Kimei anapelea hapo Jimboni.
Kati ya jimbo ambalo halina mbunge ni jimbo la Vunjo.
Alitokea mfadhili mmoja kutaka kurekebisha barabara ya Mamba Kiria, Kimei kwa woga alienda kumshtaki bungeni kwamba ana ingiliwa kwenye jimbo lake. Bahati nzuri mfadhili alisha weka kifusi hadi nyumbani kwake na mchezo uka ishia hapo.
Kimei ni bomu hatuna mbunge.
 
Mimi nilidhani moshi yote ni lami hadi chooni. Sasa km 72 zimetoka wap?
Pamoja na kuchanga lakin ibane serikali iwajengee Barabara mnalipa kodi kubwa kupitia luku nk halafu pesa zinapeleka wasanii korea?
Na mimi nilikua najua hivyo zamani mpaka pale nilipompeleka binti yangu shule. Kuna sehemu moshi barabara ni mbaya sana. Kipindi cha kiangazi vumbi kama lote, kipindi cha masika tope kama lote. Tabu tupu
 
Hongera sana wananchi na kanisa la KKKT. Barabara inayotengenezwa sio straight line road Moja ni muunganiko wa feeder road way za mitaa mingi ambazo wanaishi watu huko vijijini na kuunganisha na barabara kuu.
Ni SAWA tunatoa pongezi ila km 72 parefu sana hata ingekuwa mitaa 20
 
Inashindwa vipi kutimiza on time? Mbona Barabarani kumejaa Magari Bland mpya za Serikali?Huu ujinga haupaswi kuendelea kuwepo.
maybe right but gov ina priorities, the truth hizi hawawez kubrovide everything everywhere. Ni ukweli ambao hawataki kuusema, na hapa ndipo uchawa unapoanzia

back to wananchi wamefanya the right thing, hawawez kaa wanaisubiri serikal wakati wana uwezo huo, na wao ndio wenye shida
 
Shout out to the people in Kiruweni.

You're really setting an example on how to organize and use resources to develop your communities.

I wish we could do the same here in Arusha. It would be great if we could come together as regular citizens raise funds and fix the awful condition of our streets.

Take Njiro Nalopa for instance, the road leading to Elerai is in terrible shape despite being in an area with many wealthy people and government officials. It's really disappointing
The Geneva of Africa?! We’ve failed to put in place infrastructure to attract investment for the many multinationals who are disappointed at their arrival in Arusha only to find a tiny shoddy town. When would the government care for rural infrastructure which they don’t even think exist.
 
barabarapic.jpg

Shughuli ya kupanua moja ya barabara zilizoko Kijiji cha Kiruweni Wilaya ya Moshi, ambazo zinajengwa kwa nguvu za wananchi wa eneo hilo ikiendelea ili waweze kuondokana na adha ya kusafirisha mazao kichwani.

Changamoto ya ubovu wa miundombinu ya barabara katika eneo la Kiruweni, Kata ya Mwika Kusini, Wilaya ya Moshi, imewalazimu wananchi wa eneo hilo waishio maeneo mbalimbali nchini kuchangishana fedha na kuanza ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 72 kwa kiwango cha changarawe.

Eneo hilo ambalo wananchi wake wanajishughulisha na uzalishaji wa ndizi na kilimo cha mazao mbalimbali, limekuwa na changamoto kubwa ya miundombinu ya barabara.
Hali hii imewalazimisha kusafirisha mizigo kwa kichwa hadi sokoni, hivyo kushindwa kufikia ndoto zao za kujikwamua kiuchumi.

Chimbuko la wazo la ujenzi wa barabara lilianzia katika Usharika wa Kiruweni wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), baada ya mvua kubwa zilizonyesha mwishoni mwa Machi na Aprili, 2024.​

barabara2.jpg

Mtambo wa kushindilia barabara ukiendelea na kazi ya kushindilia moja ya barabara katika kijiji cha Kiruweni, Wilaya ya Moshi,mkoani Kilimanjaro, ambazo zinajengwa kwa nguvu za wananchi.

Akizungumza kuhusu ujenzi huo, Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Kiruweni, Joram Mamuya amesema barabara hizo zimefikia hatua mbaya na kufanya wananchi kushindwa kutumia vyombo vya usafiri na hivyo kulazimika kubeba mazao yao kichwani kuyapeleka sokoni, huku wakitembea umbali mrefu.

"Barabara zetu zilikuwa zimefikia hatua mbaya na hazikuwa zinapitika. Mwaka huu mvua zilinyesha nyingi, barabara zimeharibika zaidi kiasi kwamba hata wananchi wanashindwa kupeleka ndizi sokoni," amesema Mchungaji Mamuya na kuongeza:
Aidha, amesema kufuatia hali hiyo walilazimika kuwatangazia waamini na wananchi kwa ujumla kuona ni namna gani kutengeneza barabara hizo, ili kurahisisha shughuli za usafiri na kuchochea ukuaji wa uchumi wa eneo hilo.

"Tunamshukuru Mungu, wananchi wetu wanaoishi nje ya hapa waliokuja kusherekea Sikukuu ya Pasaka, ambao walikuwa ibadani siku hiyo, nao waliona changamoto hiyo na wakaamua kuchangia. Aprili 7, 2024 tulianza kuchangia kanisani na kuhamasisha kazi hiyo.

"Tuliwaomba Tarura wakafika, wakakagua barabara na kutupa ushauri namna bora ya kuzifanyia kazi. Sisi kwa pamoja tukaona tuanzie hapo. Gharama walizotupa zilikuwa kubwa, zaidi ya Sh180 milioni, lakini haikutukatisha tamaa. Tuliungana kwa pamoja kama jamii na kuanza kazi hii,” amesema mchungaji huyo.

barabara3.jpg

Mtambo wa kumwagilia maji barabara ukiendelea na kazi hiyo katika moja ya barabara katika kijiji cha Kiruweni, Wilaya ya Moshi,mkoani Kilimanjaro, ambazo zinajengwa kwa nguvu za wananchi.

Wananchi wafunguka
Wakizungumza baadhi ya wananchi wa kijiji hicho, wamesema ujenzi wa barabara hizo utawawezesha kusafirisha mizigo yao kwa urahisi kutoka nyumbani hadi sokoni na kuchochea ukuaji wa uchumi katika eneo hilo.

John Tarimo, amesema barabara hizo walizoea kuzitengeneza kwa majembe ya mkono kupitia msaragambo wa kijiji, lakini kwa sasa hilo lilishindikana kutokana na mvua ambazo ziliharibu zaidi barabara hizo.

Anasema baadhi zilijifunga na nyingine kuwa na mashimo makubwa ambayo yalifanya zisipitike.

"Barabara zetu tumekuwa tukizitengeneza kwa majembe ya mikono na mbaya zaidi kwa sasa kijijini huku hakuna vijana, ni wazee ambao hawawezi kutoka msaragambo kutengeneza barabara, hali iliyosababisha barabara kuharibika na kutopitika kabisa. Hii imechangiwa zaidi na mvua nyingi zilizonyesha mwaka huu,” amesema.
barabara1.jpg

Moja ya barabara zinazoendelea kutengenezwa katika kijiji cha Kiruweni, Wilaya ya Moshi, mkoani Kilimanjaro. Picha na Omben Daniel

Tarimo amesema Aprili walivyokwenda kijijini huko, barabara zilikuwa hazipitiki. Kupitia uongozi wa kanisa, wananchi wa eneo hili walijichangisha na kuwashirikisha Wana-Kiruweni wanaoishi maeneo mbalimbali nchini. “Tukashirikishana changamoto hiyo na hivyo tukakubaliana kuchangishana, ili kufungua barabara zote za kijiji hiki ambazo mtandao wake ni kilometa 72,” amesema Tarimo.

Amesema asilimia kubwa ya wakazi wa kijiji hicho ni wakulima, wanahitaji mazao yao yasafirishwe kupeleka sokoni, hali iliyowafanya wengi kuyabeba kichwani kufikia soko kutokana na ubovu wa barabara.

Amesema kutokana na Serikali kukabiliwa na mambo mengi, anatoa wito kwa wananchi katika maeneo mbalimbali kuanza kuchukua hatua ya kutatua changamoto zinazowakabili watu waishio vijijini.
“Tusisubiri kila kitu kifanywe na Serikali. Pale wanapoweza kufanya waunganishe nguvu kama jamii na kufanya jambo, wajitokeze na kufanya. Watu wanapotoka vijijini na kwenda mijini, wakifanikiwa wasisahau nyumbani. Warudi nyumbani kuboresha mazingira ya kwao,” amesisitiza Tarimo.

Shicha Mmbando, mkazi wa kijiji hicho, amesema wameamua kutoa sehemu ya mashamba yao na nguvu kazi, ili kuhakikisha miundombinu ya barabara inapitika kwa urahisi wakati wote wa mvua na kiangazi.

"Barabara zilikuwa ni changamoto. Tunatembea zaidi ya kilometa 10 na mizigo kichwani tukitoa mazao shambani maeneo ya Riata na Holili. Tunapeleka mizigo kichwani kwa sababu magari hayawezi kupita, tunashukuru zikikamilika sasa maisha yatakuwa rahisi," amesema.
Utasikia CCM kwenye kampeni wakijinadi kuwa Mama Samiah amewajengea wanakijiji wa Kiruweni kwa kiwango cha changarawe jambo ambalo wanaume walishindwa.
 
The Geneva of Africa?! We’ve failed to put in place infrastructure to attract investment for the many multinationals who are disappointed at their arrival in Arusha only to find a tiny shoddy town. When would the government care for rural infrastructure which they don’t even think exist.
I agree with you, it's really disappointing how bad the road standards are.

It seems like nobody cares.

Why are we so selfish and careless?

Don't we want better streets?

The roads in Arusha ARE IN TERRIBLE CONDITION .

It's a shame that neither us residents nor the so called government seem interested in improving our city.

I believe corruption and selfishness are to blame. It's ridiculous that so much money is collected but only a few benefit and we just allow it to happen 🤡
 
Hawalipi Kodi? Yaani Kodu walipe zineende kununua wapinzani, kulipa Bongo Muvi kule Korea then Raia wachangishane kijenga Barabara. Wachaga wamenza ufala
Fikiri boss, Nchi nzima tukiweza kufanya hivi nini kitatokea. Maana tunawanyang'anya wagombea na viongozi sababu ya kuwapa kura na kodi. Unakuja unakuta tushatengeneza barabara zetu, tushavuta maji yetu, tuna hospitali zetu. Haya tuambie unataka pesa zetu ukafanyie nini? Unataka kura zetu utupe nini?
 
maybe right but gov ina priorities, the truth hizi hawawez kubrovide everything everywhere. Ni ukweli ambao hawataki kuusema, na hapa ndipo uchawa unapoanzia

back to wananchi wamefanya the right thing, hawawez kaa wanaisubiri serikal wakati wana uwezo huo, na wao ndio wenye shida
Kwa hiyo ni sawa kununua v8 ila sio sahihi kutenga fedha kwa ujenzi wa barabara za vijijini?
 
Na mimi nilikua najua hivyo zamani mpaka pale nilipompeleka binti yangu shule. Kuna sehemu moshi barabara ni mbaya sana. Kipindi cha kiangazi vumbi kama lote, kipindi cha masika tope kama lote. Tabu tupu
Washukuru Mungu zile lami za kuelekea kwenye mageti ya mlima Kilimanjaro ( hizo ndo zinawafanya wajione wameendelea) la sivyo moshi ni sehemu yenye Barabara mbovu kupindukia sio moshi tu. Kasikazini kote ikiwepo hii Barabara kuu ya moshi Arusha ina viraka hatari. Kuna ile ya kuelekea chemka waterspring, kuna ya kahe, mabogini, majengo, kibosho juu kule, uru nk. Kote huko Barabara zinatisha na yale mabonde na milima sasa.
Sijui wachagga huwa kiburi cha kujiona wameendelea kinatoka wap wakati huo mkoa bado sana ( bila kusahau hiace zao chakavu za kuelekea huko vijijini nyingine zina kunguni) na sasa mji wa moshi umevamiwa na bajaji na bodaboda vijana wanatia huruma sio poa.


Sisi Bukoba tushajikubali kuwa na matatizo ndo maana tumetulia. Na kinachopatika kinaijenga Bukoba mdogo mdogo wala hatuna kelele. Bukoba sasa kuna ujenzi wa Barabara ya njia nne km 5.1, stendi mpya mbili, shopping complex, upanuzi wa bandari nk.

Acha takwimu za serikali zizidi kuwadanganya wazubae
 
I believe corruption and selfishness are to blame. It's ridiculous that so much money is collected but only a few benefit and we just allow it to happen 🤡
In addition to these, in Tanzania we have put a gang of dull skunks to lead us, they don’t know the basics for a good town! I believe ignorance rules over the purported leaders of this country and it’s up until we’re tired of these idiots we’re nowhere.
 
Fikiri boss, Nchi nzima tukiweza kufanya hivi nini kitatokea. Maana tunawanyang'anya wagombea na viongozi sababu ya kuwapa kura na kodi. Unakuja unakuta tushatengeneza barabara zetu, tushavuta maji yetu, tuna hospitali zetu. Haya tuambie unataka pesa zetu ukafanyie nini? Unataka kura zetu utupe nini?
Hivi ndivyo inavyotakiwa kuwa.

Kadiri wananchi wanavyoachana na kuitegemea serikali ndivyo wanavyozidi kupata nguvu na mwishowe serikali haiwezi kuwa na maamuzi juu yao bila wananchi kusema hivyo.

1. Haya mambo si magumu sana. Tuanze kuongea na majirani zetu hapo mtaani tusiwe wabinafsi sana, inawezekana kabisa kuhalikisha barabara za mtaa zinapitika miezi 12 ya mwaka.

2. Jinsi mitaa/vijiji vyetu inavyopendeza kwa kuwa na barabara nzuri, miti imepandwa vizuri, vibanda vya kuuzia vitu vidogo vidogo vimepangwa vizuri ndivyo spirit yakutaka maendeleo zaidi inakuwa kali.

3. Kuishi kwenye mitaa michafu, barabara mbovu, uhalifu etc inakatisha sana tamaa na inazuia watu kuwaza kwa ukubwa kwasababu hii hali ni kifungo. Ukisikia mikono yako haijafungwa pingu lakini haupo free ndiyo hali hii niliyoelezea.
 
Washukuru Mungu zile lami za kuelekea kwenye mageti ya mlima Kilimanjaro ( hizo ndo zinawafanya wajione wameendelea) la sivyo moshi ni sehemu yenye Barabara mbovu kupindukia sio moshi tu. Kasikazini kote ikiwepo hii Barabara kuu ya moshi Arusha ina viraka hatari. Kuna ile ya kuelekea chemka waterspring, kuna ya kahe, mabogini, majengo, kibosho juu kule, uru nk. Kote huko Barabara zinatisha na yale mabonde na milima sasa.
Sijui wachagga huwa kiburi cha kujiona wameendelea kinatoka wap wakati huo mkoa bado sana ( bila kusahau hiace zao chakavu za kuelekea huko vijijini nyingine zina kunguni) na sasa mji wa moshi umevamiwa na bajaji na bodaboda vijana wanatia huruma sio poa.


Sisi Bukoba tushajikubali kuwa na matatizo ndo maana tumetulia. Na kinachopatika kinaijenga Bukoba mdogo mdogo wala hatuna kelele. Bukoba sasa kuna ujenzi wa Barabara ya njia nne km 5.1, stendi mpya mbili, shopping complex, upanuzi wa bandari nk.

Acha takwimu za serikali zizidi kuwadanganya wazubae

Unakosea.

Hii si kuhusu sisi Wachaga wale Wahaya.

Wananchi wa Kilimanjaro walio wengi wala hawana habari yakujisifia eti mkoa umeendelea kuliko mikoa mingine.

Hapa jambo la msingi ni kuboresha hali zetu iwe unaishi Nachingwea au Njiro Arusha.

Watu wote wanastahili maisha mazuri yasiyo na stress.
 
Unakosea.

Hii si kuhusu sisi Wachaga wale Wahaya.

Wananchi wa Kilimanjaro walio wengi wala hawana habari yakujisifia eti mkoa umeendelea kuliko mikoa mingine.

Hapa jambo la msingi ni kuboresha hali zetu iwe unaishi Nachingwea au Njiro Arusha.

Watu wote wanastahili maisha mazuri yasiyo na stress.
Hizo Greda zipo halmashauri mnachangia mafuta na posho tu ndio mnaita tena kwa kushirikiana na mwenyekiti wa mtaa , ni mchango tu kwa nyumba hadi nyumba maana zile Greda zinakula mafuta .

Watoto mbona wanachangia wanasafishiwa uwanja wa mpira , ukisema barabara ni ile iko full lami ndio barabara kwa sehemu nyingi ni uongo kusema hamna , ila ukipitisha bila ya lami na huo udongo kipind vcha mvua ndio yale yale tope la kufa mtu .

Kama wanajenga lami ni jambo la pongezi kubwa kwa sababu sio suala la kitoto ila kama wanasafisha ni kawaida sana .
 
Back
Top Bottom