Pre GE2025 Wananchi wa Kilimanjaro wachangishana kurekebisha barabara mbovu yenye urefu wa kilomita 72

Pre GE2025 Wananchi wa Kilimanjaro wachangishana kurekebisha barabara mbovu yenye urefu wa kilomita 72

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Safi sana na wanafuata nyayo za Mwanza, tena Mwanza wanazijenga kwa kiwango cha mae. Barabra wanazojenga wananchi huko zinaubora kuliko za tarura.

Wachaga walikuwa wamelala, ni heri sasa wanaanza kuamka. Utakuta mkuu wa Mkoa huko siyo mchaga, kawazindua.
Wewe binti vp? Yaani unasema mkuu wa mkoa anawazindua wachagga au wao ndio wamzindua mkuu wa mkoa na boss wake yule bibi wa matumizi?
 
Mentality za ujamaa, na hapo sasa hizi ndio habari watawala wanapenda sana kuzisikia make zina wapa nguvu na ari kubwa sana ya kupiga pesa za umma, kwa sababu wanajua fika mwisho wa siku raia watachangishana walete huduma wenyewe.
Pesa zinakusanywa sana nchi hii na zinapigwa sana, then Raia tujihudumie wenyewe. Ujinga ujinga Ujinga
Mtasubiri sana mletewe maendeleo na huyo mama wa matumizi.
 

Changamoto ya ubovu wa miundombinu ya barabara katika eneo la Kiruweni, Kata ya Mwika Kusini, Wilaya ya Moshi, imewalazimu wananchi wa eneo hilo waishio maeneo mbalimbali nchini kuchangishana fedha na kuanza ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 72 kwa kiwango cha changarawe.

Eneo hilo ambalo wananchi wake wanajishughulisha na uzalishaji wa ndizi na kilimo cha mazao mbalimbali, limekuwa na changamoto kubwa ya miundombinu ya barabara.

Hali hii imewalazimisha kusafirisha mizigo kwa kichwa hadi sokoni, hivyo kushindwa kufikia ndoto zao za kujikwamua kiuchumi.

Chimbuko la wazo la ujenzi wa barabara lilianzia katika Usharika wa Kiruweni wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), baada ya mvua kubwa zilizonyesha mwishoni mwa Machi na Aprili, 2024.

Mvua hizo zimesababisha barabara hizo zishindwe kupitika kwa vyombo vya usafiri, zikiwamo pikipiki.

Akizungumza kuhusu ujenzi huo, Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Kiruweni, Joram Mamuya amesema barabara hizo zimefikia hatua mbaya na kufanya wananchi kushindwa kutumia vyombo vya usafiri na hivyo kulazimika kubeba mazao yao kichwani kuyapeleka sokoni, huku wakitembea umbali mrefu.
Mbona Huwa mnatuambua Kilimanjaro Ina lami Hadi kweymigomba,Sasa imekuaje tena? 😁😁😁
 
Hivi ndivyo inavyotakiwa kuwa.

Kadiri wananchi wanavyoachana na kuitegemea serikali ndivyo wanavyozidi kupata nguvu na mwishowe serikali haiwezi kuwa na maamuzi juu yao bila wananchi kusema hivyo.

1. Haya mambo si magumu sana. Tuanze kuongea na majirani zetu hapo mtaani tusiwe wabinafsi sana, inawezekana kabisa kuhalikisha barabara za mtaa zinapitika miezi 12 ya mwaka.

2. Jinsi mitaa/vijiji vyetu inavyopendeza kwa kuwa na barabara nzuri, miti imepandwa vizuri, vibanda vya kuuzia vitu vidogo vidogo vimepangwa vizuri ndivyo spirit yakutaka maendeleo zaidi inakuwa kali.

3. Kuishi kwenye mitaa michafu, barabara mbovu, uhalifu etc inakatisha sana tamaa na inazuia watu kuwaza kwa ukubwa kwasababu hii hali ni kifungo. Ukisikia mikono yako haijafungwa pingu lakini haupo free ndiyo hali hii niliyoelezea.
wakati huo huo report za CAG zinaonyesja upigaji upigaji, mimi concern iko hapo tu.
 
Hivi ndivyo inavyotakiwa kuwa.

Kadiri wananchi wanavyoachana na kuitegemea serikali ndivyo wanavyozidi kupata nguvu na mwishowe serikali haiwezi kuwa na maamuzi juu yao bila wananchi kusema hivyo.

1. Haya mambo si magumu sana. Tuanze kuongea na majirani zetu hapo mtaani tusiwe wabinafsi sana, inawezekana kabisa kuhalikisha barabara za mtaa zinapitika miezi 12 ya mwaka.

2. Jinsi mitaa/vijiji vyetu inavyopendeza kwa kuwa na barabara nzuri, miti imepandwa vizuri, vibanda vya kuuzia vitu vidogo vidogo vimepangwa vizuri ndivyo spirit yakutaka maendeleo zaidi inakuwa kali.

3. Kuishi kwenye mitaa michafu, barabara mbovu, uhalifu etc inakatisha sana tamaa na inazuia watu kuwaza kwa ukubwa kwasababu hii hali ni kifungo. Ukisikia mikono yako haijafungwa pingu lakini haupo free ndiyo hali hii niliyoelezea.
Kabisa. Tukiambukizana hii spirit ni suala la muda tu.
 
Unakosea.

Hii si kuhusu sisi Wachaga wale Wahaya.

Wananchi wa Kilimanjaro walio wengi wala hawana habari yakujisifia eti mkoa umeendelea kuliko mikoa mingine.

Hapa jambo la msingi ni kuboresha hali zetu iwe unaishi Nachingwea au Njiro Arusha.

Watu wote wanastahili maisha mazuri yasiyo na stress.
Sisi tuliokaa humu toka miaka ya 2016 tunaongea tuchokijua kupitia nyuzi zinazoanzishwa humu kuhusu Moshi na vijiji vyake.
Labda ndo vinafanya serikali ipotezee moshi kwa sababu ya majigambo kuwa wameendelea. Tanzania nzima hii wengi wanaamini Kilimanjaro na huko kasikazini kumeendelea lami kila sehemu, maji safi, makazi bora nk. Jambo ambalo sio kweli hata kidogo. Tanzania kama nchi bado sana
 
Hiiiiiiii jamani!!
Bado sijachanga kwakweli. Watu watumbue pesa huko, mie nichangie!!!
 
Na mimi nilikua najua hivyo zamani mpaka pale nilipompeleka binti yangu shule. Kuna sehemu moshi barabara ni mbaya sana. Kipindi cha kiangazi vumbi kama lote, kipindi cha masika tope kama lote. Tabu tupu
Nyie badala ya kuwaunga mkono hawa watu kwamba wanajitahidi kujenga barabara za kuunganisha mtaa na mtaa huko vijijini badala yake mnawacheka?!! Kweli nchi ina watu!
 
Sisi tuliokaa humu toka miaka ya 2016 tunaongea tuchokijua kupitia nyuzi zinazoanzishwa humu kuhusu Moshi na vijiji vyake.
Labda ndo vinafanya serikali ipotezee moshi kwa sababu ya majigambo kuwa wameendelea. Tanzania nzima hii wengi wanaamini Kilimanjaro na huko kasikazini kumeendelea lami kila sehemu, maji safi, makazi bora nk. Jambo ambalo sio kweli hata kidogo. Tanzania kama nchi bado sana
Sasa ukitoa hisia zako kuhusu Kilimanjaro kwasababu ya nyuzi 10, 50 au 100 hapa JF basi you are making a blunder.

Tanzania ni ya kwetu wote.

Nini kuhusu Kilimanjaro, Kagera au Arusha au Mbeya?

Pia tazama namna ulivyoelezea kuhusu serikali haipeleki miradi ya barabara Moshi kwasababu wakazi wa Moshi wanajisifia.

Are you serious man?

Hiyo si namna bora yakufikiria jambo.

Critical thinking ni muhimu. Kwasababu itakusaidia kuwaza kwa usahihi.

Uwe na siku njema.
 
Mbona Huwa mnatuambua Kilimanjaro Ina lami Hadi kweymigomba,Sasa imekuaje tena? 😁😁😁
Ngoja ufike utacheka , sehemu nyingi ni maungio ya kwenda mlima kilimanjaro ndio kuna lami , Na hizo sehemu hawakujenga walipelekewa na serikali kipindi viongozi walikuwa wachaga .

Angalia hata youtube msiba wa Gadner , watu kibao huko kwao hamna lami kawaida sana labda sehemu kama Machame na Rombo kwa mbali .
 
Sasa ukitoa hisia zako kuhusu Kilimanjaro kwasababu ya nyuzi 10, 50 au 100 hapa JF basi you are making a blunder.

Tanzania ni ya kwetu wote.

Nini kuhusu Kilimanjaro, Kagera au Arusha au Mbeya?

Pia tazama namna ulivyoelezea kuhusu serikali haipeleki miradi ya barabara Moshi kwasababu wakazi wa Moshi wanajisifia.

Are you serious man?

Hiyo si namna bora yakufikiria jambo.

Critical thinking ni muhimu. Kwasababu itakusaidia kuwaza kwa usahihi.

Uwe na siku njema.
Mnatakiwa kuwa hivi kitu kimoja ipo siku mtafika , japo malumbano ni lazima
 
Washukuru Mungu zile lami za kuelekea kwenye mageti ya mlima Kilimanjaro ( hizo ndo zinawafanya wajione wameendelea) la sivyo moshi ni sehemu yenye Barabara mbovu kupindukia sio moshi tu. Kasikazini kote ikiwepo hii Barabara kuu ya moshi Arusha ina viraka hatari. Kuna ile ya kuelekea chemka waterspring, kuna ya kahe, mabogini, majengo, kibosho juu kule, uru nk. Kote huko Barabara zinatisha na yale mabonde na milima sasa.
Sijui wachagga huwa kiburi cha kujiona wameendelea kinatoka wap wakati huo mkoa bado sana ( bila kusahau hiace zao chakavu za kuelekea huko vijijini nyingine zina kunguni) na sasa mji wa moshi umevamiwa na bajaji na bodaboda vijana wanatia huruma sio poa.


Sisi Bukoba tushajikubali kuwa na matatizo ndo maana tumetulia. Na kinachopatika kinaijenga Bukoba mdogo mdogo wala hatuna kelele. Bukoba sasa kuna ujenzi wa Barabara ya njia nne km 5.1, stendi mpya mbili, shopping complex, upanuzi wa bandari nk.

Acha takwimu za serikali zizidi kuwadanganya wazubae
Tofauti ya watu wa Bukoba na watu wa Moshi ni kwamba watu wa Bukoba wanajengewa wakati watu wa Moshi wanajijengea miundombinu kwa fedha zao za michango.
 
Wewe binti vp? Yaani unasema mkuu wa mkoa anawazindua wachagga au wao ndio wamzindua mkuu wa mkoa na boss wake yule bibi wa matumizi?
Mlikuwa wapi miaka yote, wenzenu mwanza wameanza zamani sana kujenga barabara zao wenyewe, tena kwa kiwango cha mawe, ambazo ni nzuri kuliko za lami.

Mkuu wenu wa mkoa katokea Mwanza nini?
 
Kwa hiyo ni sawa kununua v8 ila sio sahihi kutenga fedha kwa ujenzi wa barabara za vijijini?
I never said ni sawa, but hii nchi ni kubwa mno and kila mkoa kijiji wiliaya mtaa kuna mahitaji? Is a question of priority, hawawez kufanya yote at once
Siwatetei but hili gov hawataki kulisema but ndio hali halisi

Now back to wananchi, wao ndio wenye uhitaji when gov seems slow wakichukua hatua ni jambo jema zaidi and i support them
 
Mlikuwa wapi miaka yote, wenzenu mwanza wameanza zamani sana kujenga barabara zao wenyewe, tena kwa kiwango cha mawe, ambazo ni nzuri kuliko za lami.

Mkuu wenu wa mkoa katokea Mwanza nini?
Hujui historia ya Kilimanjaro miaka ya 1950 watu walishajenga barabara na madaraja vijijini kwenda kwenye mashamba ya kahawa chini ya chama cha wenyeji KNCU. Miaka hiyo watu wa Mwanza walikuwa hawajitambui kwamba wao ndio ng’ombe au ng’ombe ni akina nani!
 
I never said ni sawa, but hii nchi ni kubwa mno and kila mkoa kijiji wiliaya mtaa kuna mahitaji? Is a question of priority, hawawez kufanya yote at once
Siwatetei but hili gov hawataki kulisema but ndio hali halisi

Now back to wananchi, wao ndio wenye uhitaji when gov seems slow wakichukua hatua ni jambo jema zaidi and i support them
Nani kasema hawawezi kufanya yote? Mnaaminishwa hivyo kwa sababu fedha nyingi zinapelekwa kwenda kushibisha matumbo yao na nyie kwa sababu hamfikirii vizuri mnakubali tu!

Kuna fedha nyingi sana zinatumika ndivyo sivyo hapa nchini na nyingi zinaenda kushibisha kundi la watu wachache.

Endapo zikepelekwa zinapotakiwa kwenda nchi hii ingekuwa mbali sana kimaendeleo
 
Sasa ukitoa hisia zako kuhusu Kilimanjaro kwasababu ya nyuzi 10, 50 au 100 hapa JF basi you are making a blunder.

Tanzania ni ya kwetu wote.

Nini kuhusu Kilimanjaro, Kagera au Arusha au Mbeya?

Pia tazama namna ulivyoelezea kuhusu serikali haipeleki miradi ya barabara Moshi kwasababu wakazi wa Moshi wanajisifia.

Are you serious man?

Hiyo si namna bora yakufikiria jambo.

Critical thinking ni muhimu. Kwasababu itakusaidia kuwaza kwa usahihi.

Uwe na siku njema.
Soma reply yangu vzr na hoja imeanzia wap.
Vinginevyo umekurupuka kunijibu.
Uwe na siku njema
 
Back
Top Bottom