Pre GE2025 Wananchi wa Kilimanjaro wachangishana kurekebisha barabara mbovu yenye urefu wa kilomita 72

Pre GE2025 Wananchi wa Kilimanjaro wachangishana kurekebisha barabara mbovu yenye urefu wa kilomita 72

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hujui historia ya Kilimanjaro miaka ya 1950 watu walishajenga barabara na madaraja vijijini kwenda kwenye mashamba ya kahawa chini ya chama cha wenyeji KNCU. Miaka hiyo watu wa Mwanza walikuwa hawajitambui kwamba wao ndio ng’ombe au ng’ombe ni akina nani!
Kama walijenga sasa wanafanya nini? Wanabomoa?

Ungenambia kuiba ningekuelewa.
 
Nyie badala ya kuwaunga mkono hawa watu kwamba wanajitahidi kujenga barabara za kuunganisha mtaa na mtaa huko vijijini badala yake mnawacheka?!! Kweli nchi ina watu!
Nioneshe kicheko changu
 
Mbunge kazi yake sio Kujenga Barabara ni kuisimami Serikali,
Kazi ya Bunge ni kuisimamia Serikali. Hata hivyo, mbunge anapaswa kuwasilisha changamoto za eneo lake kwa Serikali ili zipate utatuzi. Hata hivyo,.kwa miradi midogo inaweza kutekelezwa kupitia fedha za Mfuko wa Maendeleo wa Jimbo. Fedha hizi ziko chini ya mbunge. Hivyo, hakuna utetezi kwa mbunge ikiwa Jimbo lake litakosa huduma muhimu.
 
Unakosea.

Hii si kuhusu sisi Wachaga wale Wahaya.

Wananchi wa Kilimanjaro walio wengi wala hawana habari yakujisifia eti mkoa umeendelea kuliko mikoa mingine.

Hapa jambo la msingi ni kuboresha hali zetu iwe unaishi Nachingwea au Njiro Arusha.

Watu wote wanastahili maisha mazuri yasiyo na stress.

..Watz wengi wameaminishwa kwamba Kilimanjaro "imependelewa" kwa miundombinu ya kila aina. Hata ukisoma mijadala mbalimbali hapa JF utakutana na hoja za namna hiyo.
 
Sisi tuliokaa humu toka miaka ya 2016 tunaongea tuchokijua kupitia nyuzi zinazoanzishwa humu kuhusu Moshi na vijiji vyake.
Labda ndo vinafanya serikali ipotezee moshi kwa sababu ya majigambo kuwa wameendelea. Tanzania nzima hii wengi wanaamini Kilimanjaro na huko kasikazini kumeendelea lami kila sehemu, maji safi, makazi bora nk. Jambo ambalo sio kweli hata kidogo. Tanzania kama nchi bado sana
🙄
 
Ngoja ufike utacheka , sehemu nyingi ni maungio ya kwenda mlima kilimanjaro ndio kuna lami , Na hizo sehemu hawakujenga walipelekewa na serikali kipindi viongozi walikuwa wachaga .

Angalia hata youtube msiba wa Gadner , watu kibao huko kwao hamna lami kawaida sana labda sehemu kama Machame na Rombo kwa mbali .
Mimi naona sehemu za vijijini vya kilimanjaro zote zinafikika kwa gari na lami imeunganisha sehemu zote muhimu labda useme lami hazipo kwenye hizo chochoro za kuunganisha kijiji kimoja kwenda kingine ambazo ndio wanaziweka kokoto tu.
 
Mimi naona sehemu za vijijini vya kilimanjaro zote zinafikika kwa gari na lami imeunganisha sehemu zote muhimu labda useme lami hazipo kwenye hizo chochoro za kuunganisha kijiji kimoja kwenda kingine ambazo ndio wanaziweka kokoto tu.
Wilaya zote safi ila ndani hapana sio sehemu zote labda Machame na Rombo
 
Safi sana na wanafuata nyayo za Mwanza, tena Mwanza wanazijenga kwa kiwango cha mae. Barabra wanazojenga wananchi huko zinaubora kuliko za tarura.

Wachaga walikuwa wamelala, ni heri sasa wanaanza kuamka. Utakuta mkuu wa Mkoa huko siyo mchaga, kawazindua.
Nawe acha uongo, wivu na uzushi.
Wewe umeambiwa hicho ni kijiji kimoja huko Kilimanjaro, tena hamasa imeanzia kanisani, na wanafanya ukarabati wa zaidi ya km 72 za barabara.
Sasa ya Mwanza yametokea wapi?
Kuna kijiji gani huko Mwanza wananchi wamefanya hivyo?
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro wapi ametajwa kuhusika?

Jifunze kuwa mkweli na muungwano. Toa hongera kwa wachaga na wakristo wa kijiji cha kiruweni huko Kilimanjaro kwa kuonyesha njia.
 
Wilaya zote safi ila ndani hapana sio sehemu zote labda Machame na Rombo
Kilimanjaro naijua yote vizuri rombo barabara ya mkato ya kenya ikipata lami itakua imezungukwa na lami pande zote , marangu ila lami pande zote mpaka vichochoroni , barabara ya kilema kanisa la katholic ,panda barabara ya hospitality ya marangu njoo barabara ya shule ya Uchira unganisha mpka mwika zungukia himo kote kumewekwa kati na lami .

Panda barabara ya kcmc katisha rau mpka mamboleo panda juu barabara zote za v ya kwend uru mnini na uru kishumundu zote zina lami .

Banda barabara zote za kwenda kibosho umbwe , kibosho kirima ,kibosho singachina mpka mweka zote zina lami .


Katisha barabara ya kwenda masama panda juu mpka soko la mula katika kona ya kwenda machame kwa juu barabara ya masama secondary tokea machame msikitini ,panda juu mpaka machame hospital ,shuka chini mpaka nshara kwa mbowe , kata chochoro ya kwnda narumu tokezea barabara ya kibosho umbwe kote kuna lami .
 
Nani kasema hawawezi kufanya yote? Mnaaminishwa hivyo kwa sababu fedha nyingi zinapelekwa kwenda kushibisha matumbo yao na nyie kwa sababu hamfikirii vizuri mnakubali tu!

Kuna fedha nyingi sana zinatumika ndivyo sivyo hapa nchini na nyingi zinaenda kushibisha kundi la watu wachache.

Endapo zikepelekwa zinapotakiwa kwenda nchi hii ingekuwa mbali sana kimaendeleo
Wapi gov wamefanya vitu vingi at once na vikaenda sawa? Suala la kuwa wanatumia pesa vibaya hilo kila mtu anasema but ni kiasi gani has no body knows? Can you prove it ?
 
Watu wenye akili kubwa tumekuja hapa kupongeza hili kwa sababu kuu tatu.
1. Hatua hiyo inawafanya wananchi hao kuwa na nguvu juu ya maamuzi ya maendeleo hao. Hakuna kitu au mtu wakuweza kuwababaisha.

2. Hatua hiyo inalazimisha maendeleo mengine kuwafuata. Kesho na keshokutwa serikali itajikuta kwa lazima inaboresha na mengine. (Penye nia pana njia, mwenye nacho ataongezewa)

3. Wananchi hao wamedhamiria kuwa na maisha bora kwa gharama zote. Lazima watafika mbali zaidi.
 
Watu wenye akili kubwa tumekuja hapa kupongeza hili kwa sababu kuu tatu.
1. Hatua hiyo inawafanya wananchi hao kuwa na nguvu juu ya maamuzi ya maendeleo hao. Hakuna kitu au mtu wakuweza kuwababaisha.

2. Hatua hiyo inalazimisha maendeleo mengine kuwafuata. Kesho na keshokutwa serikali itajikuta kwa lazima inaboresha na mengine. (Penye nia pana njia, mwenye nacho ataongezewa)

3. Wananchi hao wamedhamiria kuwa na maisha bora kwa gharama zote. Lazima watafika mbali zaidi.
Hao wananchi wana nia ya dhati na ni mfano wa kuigwa kabisa.
 
Nawe acha uongo, wivu na uzushi.
Wewe umeambiwa hicho ni kijiji kimoja huko Kilimanjaro, tena hamasa imeanzia kanisani, na wanafanya ukarabati wa zaidi ya km 72 za barabara.
Sasa ya Mwanza yametokea wapi?
Kuna kijiji gani huko Mwanza wananchi wamefanya hivyo?
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro wapi ametajwa kuhusika?

Jifunze kuwa mkweli na muungwano. Toa hongera kwa wachaga na wakristo wa kijiji cha kiruweni huko Kilimanjaro kwa kuonyesha njia.
Uongo wanini? Nimekwambia mmechelewa sana, Mwanza wameanza zamani sana, tena kiwango cha mawe, unabisha hilo nikuwekee ushahidi?
 
Uongo wanini? Nimekwambia mmechelewa sana, Mwanza wameanza zamani sana, tena kiwango cha mawe, unabisha hilo nikuwekee ushahidi?
Mkoa wa kwanza Tanzania kupata lami ni dar es salam unaofuati ni kilimanjaro 1960 na harakati za wanakimanjaro kujipambania zilianza zaman mno kipindi cha KNCU 1933
 

Changamoto ya ubovu wa miundombinu ya barabara katika eneo la Kiruweni, Kata ya Mwika Kusini, Wilaya ya Moshi, imewalazimu wananchi wa eneo hilo waishio maeneo mbalimbali nchini kuchangishana fedha na kuanza ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 72 kwa kiwango cha changarawe.

Eneo hilo ambalo wananchi wake wanajishughulisha na uzalishaji wa ndizi na kilimo cha mazao mbalimbali, limekuwa na changamoto kubwa ya miundombinu ya barabara.

Hali hii imewalazimisha kusafirisha mizigo kwa kichwa hadi sokoni, hivyo kushindwa kufikia ndoto zao za kujikwamua kiuchumi.

Chimbuko la wazo la ujenzi wa barabara lilianzia katika Usharika wa Kiruweni wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), baada ya mvua kubwa zilizonyesha mwishoni mwa Machi na Aprili, 2024.

Mvua hizo zimesababisha barabara hizo zishindwe kupitika kwa vyombo vya usafiri, zikiwamo pikipiki.

Akizungumza kuhusu ujenzi huo, Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Kiruweni, Joram Mamuya amesema barabara hizo zimefikia hatua mbaya na kufanya wananchi kushindwa kutumia vyombo vya usafiri na hivyo kulazimika kubeba mazao yao kichwani kuyapeleka sokoni, huku wakitembea umbali mrefu.
Otanenyi wameeku wa Kiruwenyi na papa Mlisi!
 
Back
Top Bottom