Wananchi wamepoteza imani kwenye taasisi zote za Serikali. Kama Taifa tunafahamu hatari iliyo mbeleni?

Wananchi wamepoteza imani kwenye taasisi zote za Serikali. Kama Taifa tunafahamu hatari iliyo mbeleni?

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2012
Posts
21,113
Reaction score
65,124
Wananchi wanapopoteza imani kwenye taasisi za serikali huwa kuna uwezekano mkubwa kwa nchi husika kuingia kwenye korongo. Haijalishi idadi ya hao wananchi, madhara ni lazima yawepo tu. Ukisoma historia, mifano iko mingi mno. Wananchi wakikata tamaa kuna kitu huzaliwa ambacho wengi kifalsafa hukiita NIHILISM, ambapo watu huamini kwamba hakuna jambo la maana kwenye hii dunia, kila kitu ni bora liende tu.

Watu wakifikia hatua hii, hata likifanyika jambo baya kiasi gani ndani ya nchi hawawezi kustuka sana zaidi ya kuwa na hasira. Pia hata serikali ikifanyika jambo jema kiasi gani watu hawawezi kuwa na bashasha kubwa sana kwasababu wanaamini kila kitu ni moto wa mabua uliolenga kuwahadaa kiakili. Nchi ikifikia hapa, suala zima la OBJECTIVITY hufa bali watu huendeshwa na PASSION & VENGEANCE (Hisia na kisirani). Bahati mbaya sana hata wasomi huingia kwenye huu mtego.

Taifa likifia hatua hii, basi fahamu fika kwamba likitokea janga lolote kubwa kama Vita (War of Industrial Scale), Mlipuko wa magonjwa (Epidemics), Anguko la kiuchumi (Economic Collapse) au Maafa ya kijiografia (Natural Disaster) nchi haiwezi kusimama kwasababu kila mtu atajiangalia yeye na kuchukua chake mapema. Hatua hii ndiyo tunaita A FAILED STATE, na bahati mbaya sana kama hatutaangalia sisi nasi tunaweza kuelekea huko.

Swali ambalo huwa najiuliza sana ni hili lifuatalo:
Hivi yakitokea kama yale ya mwaka 1979 kule Kagera na nchi ikavamiwa kijeshi, Tanzania yetu ya leo inaweza kushikamana na kuwa moja dhidi ya adui. AU ndiyo wananchi wanaweza kukaa pembeni wakitazama na kusema bora tukose wote kwasababu wanaamini kwamba hawana hisa yoyote ile kwenye taifa lao. Au hata wengine wanaweza kumuunga adui mkono na kusaidia nchi ivurugike ili tukose wote ???

MUNGU EPUSHIA MBALI: Lakini, hivi ikitokea vita, mlipuko wa ugonjwa au baa la njaa , serikali ya Tanzania inaamini kabisa kwamba inaweza kuwatuliza watanzania ambao wamepoteza nayo imani, wenye kisirani na wasio na utii (IMBETTERED NIHILISTIC TEENS) kama ilivyo leo hii. Unaweza kudhani kwamba hili nalozungumza halipo, lakini taswira halisi ya hisia za watanzania ilionekana kwa kiwango kidogo uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Wananchi wengi hawakupiga kura kwa Mzee Edward Ngoyai Lowassa kwasababu walikuwa wanataka mabadiliko peke yake, bali kwasababu walikuwa na hasira na Mzee Jakaya Kikwete na CCM kwa ujumla. Huku wengine wakiwa wanapiga kura wakitegemea yatokee madhara ya kulipizana visasi huko mbele dhidi ya baadhi ya wana-CCM endapo upinzani utachukua nchi.

Kama taifa, tuko hatua mbaya sana.
MUNGU ATUSAIDIE SANA NA AEPUSHIE MBALI.
 
Zamani hii hali ilikuwa afadhali sababu walikuwa nayo raia wa vijijini na uneducated citizens tuu... Wale walio kwenye system walikuwa wana uzalendo sababu walitimiziwa needs expectations zao kwa angalau 80%.

Ila kwa sasa, ni all citizens have zero trust na serikali, wamebaki praise team tuu ndiyo wanajifanya wana imani ila hata wao mioyoni wanajua taifa liko stage mbaya sana.

Na wasidhani hii hali inasababishwa na mambo makuubwa sana, ni mambo madogo sana kama vile kuwaongezea watumishi 23,000/= kwenye mishahara, gharama za maisha kuwa juu, kuminya huduma kama za internet, nk.
 
Wananchi wanapopoteza imani kwenye taasisi za serikali huwa kuna uwezekano kubwa kwa nchi husika kuingia kwenye korongo. Haijalishi idadi ya hao wananchi, madhara ni lazima yawepo tu. Ukisoma historia, mifano iko mingi mno. Wananchi wakikata tamaa kuna kitu huzaliwa ambacho wengi kifalsafa hukiita NIHILISM, ambapo watu haumini kwamba hakuna jambo la maana kwenye hii dunia, kila kitu ni bora liende tu.

Watu wakifikia hatua hii, hata likifanyika jambo baya kiasi gani ndani ya nchi hawawezi kustuka sana zaidi ya kuwa na hasira. Pia hata serikali ikifanyika jambo jema kiasi gani watu hawawezi kuwa na bashasha kubwa sana kwasababu wanaamini kila kitu ni moto wa mabua uliolenga kuwahadaa kiakili. Nchi ikifikia hapa, suala zima la OBJECTIVITY hufa bali watu huendeshwa na PASSION & VENGEANCE (Hisia na kisirani). Bahati mbaya sana hata wasomi huingia kwenye huu mtego.

Taifa likifia hatua hii, basi fahamu fika kwamba likitokea janga lolote kubwa kama Vita (War of Industrial Scale), Mlipuko wa magonjwa (Epidemics), Anguko la kiuchumi (Economic Collapse) au Maafa ya kijiografia (Natural Disaster) nchi haiwezi kusimama kwasababu kila mtu atajiangalia yeye na kuchukua chake mapema. Hatua hii ndiyo tunaita A FAILED STATE, na bahati mbaya sana kama hatutaangalia sisi nasi tunaweza kuelekea huko.

Swali ambalo huwa najiuliza sana ni hili lifuatayo:
Hivi yakitokea kama yale ya mwaka 1979 kule Kagera na nchi ikavamiwa kijeshi, Tanzania yetu ya leo inaweza kushikamana na kuwa moja dhidi ya adui. AU ndiyo wananchi wanaweza kukaa pembeni wakitazama na kusema bora tukose wote kwasababu wanaamini kwamba hawana hisa yoyote ile kwenye taifa lao. Au hata wengine wanaweza kumuunga adui mkono na kusaidia nchi ivurugike ili tukose wote ???

MUNGU EPUSHIA MBALI: Lakini, hivi ikitokea vita, mlipuko wa ugonjwa au baa la njaa , serikali ya Tanzania inaamini kabisa kwamba inaweza kuwatuliza watanzania ambao wamepoteza nayo imani, wenye kisirani na wasio na utii (IMBETTERED NIHILISTIC TEENS) kama ilivyo leo hii. Unaweza kudhani kwamba hili nalozungumza halipo, lakini taswira halisi ya hisia za watanzania ilionekana kwa kiwango kidogo uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Wananchi wengi hawakupiga kura kwa Mzee Edward Ngoyai Lowassa kwasababu walikuwa wanataka mabadiliko peke yake, bali kwasababu walikuwa na hasira na Mzee Jakaya Kikwete na CCM kwa ujumla. Huku wengine wakiwa wanapiga kura wakitegemea yatokee madhara ya kulipizana visasi huko mbele dhidi ya baadhi ya wana-CCM endapo upinzani utachukua nchi.

Kama taifa, tuko hatua mbaya sana.
MUNGU ATUSAIDIE SANA NA AEPUSHIE MBALI.
Kijana mbona kama unakuja Kuja?. Haya njoo Lumumba kesho tukufanyie mpango wa jimbo na wewe
 
Zamani hii hali ilikuwa afadhali sababu walikuwa nayo raia wa vijijini na uneducated citizens tuu... Wale walio kwenye system walikuwa wana uzalendo sababu walitimiziwa needs expectations zao kwa angalau 80%.

Ila kwa sasa, ni all citizens have zero trust na serikali, wamebaki praise team tuu ndiyo wanajifanya wana imani ila hata wao mioyoni wanajua taifa liko stage mbaya sana.

Na wasidhani hii hali inasababishwa na mambo makuubwa sana, ni mambo madogo sana kama vile kuwaongezea watumishi 23,000/= kwenye mishahara, gharama za maisha kuwa juu, kuminya huduma kama za internet, nk.
Ila sikio la kufa huwa halisikii dawa......
Sijui kwanini hata hawastuki juu ya hiki kinachoendelea......
 
TENA OGOPENI SANA HAWA WANAO SEMA, MAMA KAFANYA HIVI, MAMA KAFANYA VILE.HATA AKIITWA NI MAMA WA YESU, WATU HAWANA IMANI NAYE. NDIO MAANA SIFA ZA KUMTUKUZA NI KWENYE KILA HOTUBA, KILA SHEREHE ANA PEWA MIALIKO NA KUUDHURIA. IMANI HUJA KWA MATENDO... SIO HOTUBA NA MAAGIZO.
 
**Swali ambalo huwa najiuliza sana ni hili lifuatayo:
Hivi yakitokea kama yale ya mwaka 1979 kule Kagera na nchi ikavamiwa kijeshi, Tanzania yetu ya leo inaweza kushikamana na kuwa moja dhidi ya adui. AU ndiyo wananchi wanaweza kukaa pembeni wakitazama na kusema bora tukose wote kwasababu wanaamini kwamba hawana hisa yoyote ile kwenye taifa lao. Au hata wengine wanaweza kumuunga adui mkono na kusaidia nchi ivurugike ili tukose wote ???**



Viongozi wetu waliozungukwa na wapambe sidhani kama wanajiuliza maswali kama haya....

Taifa letu linahitaji ukombozi wa haraka .
 
TENA OGOPENI SANA HAWA WANAO SEMA, MAMA KAFANYA HIVI, MAMA KAFANYA VILE.HATA AKIITWA NI MAMA WA YESU, WATU HAWANA IMANI NAYE. NDIO MAANA SIFA ZA KUMTUKUZA NI KWENYE KILA HOTUBA, KILA SHEREHE ANA PEWA MIALIKO NA KUUDHURIA. IMANI HUJA KWA MATENDO... SIO HOTUBA NA MAAGIZO.
M2WAWA2

...tuwape muda hao wanaojiita "chawa wa mama ukimvaa mama,tunakuvaa" atakayekuja naye watamsifu kwa mapambio. Ina maana mama amekubali hizi sifa zote ? Lakini mama ameshindwa kusoma alama za nyakati kwa mtangulizi wake ? Leo viongozi wanasifia kila kitu na kusahau kazi waliyopewa na watawaliwa.
 
Back
Top Bottom