Nikweli mkuu, kuna jamaa ana duka la spare za magari lkn yeye uvusha kidokidogo kutoka nchi jurani kwa baiskeli na wala hauwezi kumdhania.
Uko sahihi, maana wasiolipa hawana uchungu na ufisadi.
Sijaelewa ni kwa nini unasema kila mtu huwa analipa Kodi.Mkuu logic ni moja tu kwamba kila mtu analipa kodi sio kusema kwamba eti watu wanaolipa kodi ni watu wachache tu !
we jamaa sijakuita bwege kwa sababu u wa home! Nadhani andiko lako ungeiambia serikali iache anasa kwenye kodi tunazolipa! Mchukulie abiria analipa nauli ambayo tra amechukua kodi, latra amechukua za route, ewura amekata za mafuta,tanroad kakusanyiwa zake na tra, mwenye basi pia kalipa kodi, tbs nae kachukuamo! Halaf unakuja na fact eti hatulipi kodi mpare wa wapi usiejua abc za uchumi? Au nunua vocha weka kwenye simu halafu soma ule mchanganuo! Serikalini humo kumejaa wezi na wanyonyajiWafanyabisha wao wanaelewa utitiri huo wa kodi upo wapi.
Kama swali hilo litakuwa hujalielewa.
Unafikiri ni kwa nini vijana wanaona ni akheri kuajiriwa kuliko kujiajiri na kuanzisha biashara?
Huwezi nielewawe jamaa sijakuita bwege kwa sababu u wa home! Nadhani andiko lako ungeiambia serikali iache anasa kwenye kodi tunazolipa! Mchukulie abiria analipa nauli ambayo tra amechukua kodi, latra amechukua za route, ewura amekata za mafuta,tanroad kakusanyiwa zake na tra, mwenye basi pia kalipa kodi, tbs nae kachukuamo! Halaf unakuja na fact eti hatulipi kodi mpare wa wapi usiejua abc za uchumi? Au nunua vocha weka kwenye simu halafu soma ule mchanganuo! Serikalini humo kumejaa wezi na wanyonyaji
Anayepika maandazi amelipia kodi aliponunua unga, sukari na mafuta.Njoo hapa mtaani kwetu kuna sehemu wanatengeneza viatu vya ngozi, sendo, makobazi na hawana kibali wala hawalipi kodi md vinaenda sokoni kuuzwa.
Nguo nazo halikadhalika.
Wapika maandazi, chapati na vitumbua hizo zote ni bidhaa.
Na Watu wananunua ingawaje mpikaji au mtengenezaji halipi kodi.
Sasa turudi kwa wakubwa.
Hujawahi sikia Watu wanapitisha mizigo bandarini bure bila kulipa kodi yoyote? Hujawahi kusikia bidhaa zinazopitishwa kimagendo huko mipakani?
Kama uliwahi kusikia, je vipi kama hizo nguo au kiatu unachokivaa kimepitia katika mchakato huo mpaka kukufikia wewe?
Kipi kinakufanya uamini kuwa kimelipiwa kodi ilhali wewe shughuli au huduma zako au bidhaa zako hulipi kodi?
Kama mtu kiwango cha biashara yake hakijafikia kulipa kodi unataka afanyaje?? Sio upambane na serikali ikawabane hao wanaoingiza mizigo huko bandarini. Yani mtu ananua pair tatu za viatu za kutembeza mtaani unataka aanze kumkagua muuzaji kama alilipia kodi bandarini!Sasa turudi kwa wakubwa.
Hujawahi sikia Watu wanapitisha mizigo bandarini bure bila kulipa kodi yoyote? Hujawahi kusikia bidhaa zinazopitishwa kimagendo huko mipakani?
Kama uliwahi kusikia, je vipi kama hizo nguo au kiatu unachokivaa kimepitia katika mchakato huo mpaka kukufikia wewe?
Kipi kinakufanya uamini kuwa kimelipiwa kodi ilhali wewe shughuli au huduma zako au bidhaa zako hulipi kodi?
Hana elimu ya kodi huyo, Watanzania wengi huwa wanafikiri VAT inalipwa na wafanyabiashara wakati wao wateja ndio wanailipa na wafanyabiashara ni agents/wakusanyaji tu wa hiyo kodi.Hakuna mwananchi asiyelipa kodi sema wafanyabiashara ambao kimsingi ni mawakala tu wa kodi ndiyo wengine wanazila hizo kodi wanazokusanya toka kwa wananchi.
sio mimi tu ambaye siwezi kukuelewa hata ma genius hapa hawatakuelewa! Kwa kifupi kodi inayolipwa kwenye manunuzi makusanyo yake ni makubwa kuliko hyo inayolipwa na makundi/wafanyabiashara! Ndo maana nkakupa mfano wa vocha ya simu! ya elfu moja! Hiv kwa siku wamiliki wa simu wananunua vocha ngap? Kadiria tu halafu uzidishe x 152/= halafu useme hatulipi kodiHuwezi nielewa
Kwani si unapewa risiti za huo mfuko ulionunua? Kama hujapewa linganisha bei ya wanapotoa risiti utajua kama umelipiwa au haujalipwa.Wéwe ndio huelewi hata ninachozungumzia.
Huo mfuko wa cement unaosema unauhakika gani umelipiwa kodi? Hilo ndio swali
" No taxation without representation "Kwema Wakuu!
Taifa ambalo wananchi wanaolipa kodi ni robo tuu ya idadi ya Watu lazima viongozi wawe na nguvu kuliko raia. Zaidi mafisadi huneemeka kwenye nchi za namna hiyo
Kwa sababu watakaolipa kodi ndio watakaokuwa na uchungu na nchi. Watakaokuwa na uchuñgu na kodi wanayoitoa.
Sasa kama robo tuu ndio wanaotoa kodi unafikiri wataweza kupambana na robo tatu iliyobakia. Hawataweza.
Raia ambaye halipi kodi atawezaje kupambana nd viongozi mafisadi?
Mtaani sio ajabu robo tatu ya wafanyabishara hawalipi kodi. Wajasiriamali hawalipi kodi. Bodaboda sijui fundi gereji, fundi nguo, mama nitilie. Hao watakuwaje na uchungu na mafisadi?
Ôooh! Taikon hakuna mtu asiyelipa kodi. Ukinunua kitu au kupata huduma yoyote ukatoa pesa inalipa kodi indirect.
Hiyo najua.
Lakini indirect Tax haiumi kama Direct Tax.
Pesa ya kutoa kwa mkono inauma kuliko pesa hewa ambayo inakatwa juu kwa juu bila kupitia mikononi mwako.
Moja ya njia kukomboa nchi dhidi ya mafisadi ni kuhamasisha Watu walipe kodi kwa wingi angalau nusu au robotatu ya watazania walipe kodi.
Alafu utaona mtiti wake.
Wengi ni wengi tuu.
Serikali za kifisadi kikawaida hazitii ñguvu kubwa kuongeza idadi ya walipa kodi izidi wasiolipa kwa sababu matokeo yake huwa magumu ingawaje yanatija kwa maendeleo ya nchi.
Hivi uliona wapi mtu mzalendo anahitaji mambo ya burebure ilhali nchi ni maskini.
Ukishaona wewe ni maskini alafu serikali yako haitaki uchangie hata kidogo elewa huo ni mkakati wa kukufanya usiwe na nguvu daima.
Mnataka elimu bure wakati nchi ni maskini. Uliona wapi uzalendo unajengwa bila wananchi kugharamia ili wapate maumivu ya kile kizuri wanachohitaji?
Mnataka Afya sijui Dawa bure. Maskini bado utake bure.
Matajiri ndio hupewa vitu bure kwa sababu tayari walishalipia gharama.
Wananchi lazima waambiwe ukweli kuwa kodi na michango yao hata kama ni kidogo ndio itakayowapa huduma.
Watu wajengewe uzalendo kwa kujipigania hata kwa kile kidogo ili viongozi wao wasipate sababu ya kuwatawala kwa njia za dhulma.
Sio ajabu ukasikia kiongozi mmoja mpumbavu akimwambia mtu anayepigania Haki fulani akisema, tumekusomesha bure alafu leo sisi ndio wabaya. Bila sisi kukusomesha bure ungekuwa hapo ulipo? Embu kuwa na shukrani.
Yaani baadaye itakuwa ni lazima ukae kimya ukiona wale waliokupa burebure kama hisani ya kukusomesha.
Ukisema kodi za wananchi ndio zilikusomesha akiwepo mzazi wako. Huyo mzazi wako hana hata leseni yoyote na hajawahi kulipa kodi yoyote Direct.
Ukisema wananunua vitu unauhakika gani hivyo vitu vimelipiwa kodi?
Mangi unayenunua vitu halipi kodi. Pengine sehemu ambayo mangi ananunulia mzigo wake ndiye halipi kodi.
Hujasikia kuna Watu wanapitisha mizigo bandarini bila kulipa kodi.
Kama wapo kwa nini unasema unalipa kodi indirect Kwa kununua vitu kwa Mangi au dukani.
Huoni upo uwezekano wa kununua bidhaa ambayo haijawahi kulipiwa kodi?
Viongozi wa serikali wanajiamini kwa sababu wanajua robo tatu ya watanzania hawalipi kodi.
Hivyo ulileta fyokofyoko wanaanzia na shughuli unayoifanya ambayo hauna kibali wala huna mpango wa kuwa nacho ili ulipe kodi.
Mhalifu mdogo hawezi mdhibiti mhalifu Mkubwa.
Wenye haki wachache hawawezi kuwashinda wasiohaki waliowengi.
Unafikiri kama Watu wengi wangekuwa wanalipa kodi kungekuwa na hayo mambo ya Kikokotoo.
Lakini walipa kodi wachache lazima wamenyeke vilivyo ili serikali iendeshe mambo yake
Acha nipumzike.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Wapo watu wameajiriwa na wanalipwa mishahara kuhakisha kuna VAT compliance, wanaitwa TRA.Umemtukana lakini yuko sahihi kwa kiwango kikubwa..
Watu wengi wameongelea VAT - lakini kwenye nchi yetu VAT compliance ni chini ya asilimia 8. Wakati huo huo bidhaa nyingi za vyakula zimesamehewa kodi ya VAT. Hivyo, watu wengi hawalipi na wanaolipa hawadai risiti.
Pia, umewahi kujiuliza kwa wale wafanyakazi wanaolipa direct tax na bado wanalipa hizo indirect?? Kwa hiyo ni muhimu kundi la wanaolipa direct tax liongezeke la sivyo kulipa indirect tax sio excuse kwa kweli.
TRA wana njia zaidi ya milioni kupata kodi zao, kwenye daladala wakichukua risiti za mafuta tu za gari wanaweza kujua kodi anayopaswa kulipa mwenye gari bila hata kopi ya risiti za abiria, wakichukua risiti za kuingiza mizigo hapo bandarini za mfanyabiashara kwa mwaka wanaweza kumkadiria kodi vizuri tu. Fahamu tu kwamba TRA hawajawahi kushindwa kumkadiria mfanyabiashara kodi eti kwa kukosa risiti, hizo risiti huwa ni kwa ajili ya kufanya kazi yao tu kuwa rahisi.Kama unanunua bidhaa ambayo haijalipiwa kodi md hujadai risiti unapata wapi ujasiri wa kusema hakuna ambaye halipi kodi kwa siku?
Hivi unajua Watu milioni 15 wakilipa kodi kila mmoja ni sawa na Tsh 1.5Trilioni?
Kama kwa siku unayosema mtanzania akilipa kodi walau 500 kwa mwezi ni Tsh 15k kwa Mwaka 150k
Sasa kodi 150k × wananchi milioni 30. Unajua ni Trilioni ngapi
Dubai raia hawalipi direct tax, VAT ni 5% na wana maendeleo makubwa tu.Ni muhimu watu kulipa kodi kwa wingi, hii itasaidia kuihoji serikali na pia kugharamia maendeleo yetu. Tusidanganyane, hizo nchi zilizoendelea watu wanalipa kodi hadi wanachanganyikiwa.
Si kweli kuwa hawalipi direct tax, Bali hawalipi income tax tu. na rate ya VAT ni 5%. Kodi zingine zinalipwa mfano hotel levy n.kDubai raia hawalipi direct tax, VAT ni 5% na wana maendeleo makubwa tu.
Kuwait, Saudi Arabia na Qatar hakuna direct tax.
Kuna direct tax gani nyingine muhimu zaidi ya income tax hapa duniani??Si kweli kuwa hawalipi direct tax, Bali hawalipi income tax tu. na rate ya VAT ni 5%. Kodi zingine zinalipwa mfano hotel levy n.k
Wapo watu wameajiriwa na wanalipwa mishahara kuhakisha kuna VAT compliance, wanaitwa TRA.
Bidhaa nyingi za vyakula zimesamehewa kodi ya VAT kwa sababu wanunuzi wake wengi ni masikini walalahoi wanaoishi maisha ya kuganga njaa, na hii ni kanuni ya kodi duniani Kate kwamba watu walipishwe kodi kulingana na uwezo
Lengo la kodi sip kukusanya mapato tu kama wendawazimu ndio maana hizo direct tax kama kodi ya kichwa zilifutwa kwa sababu kodi nyingine ni uharibifu kwenye uchumi na stability ya nchi.