Wanaobahatika kuwa Marais wa nchi hii wanapoteza fursa ya kuingia katika historia ya kudumu kwa kushindwa tu kuwapa Watanzania Katiba Mpya

Wanaobahatika kuwa Marais wa nchi hii wanapoteza fursa ya kuingia katika historia ya kudumu kwa kushindwa tu kuwapa Watanzania Katiba Mpya

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Huu ndio ukweli mchungu kwa wote waliowahi kuwa Maraisi wa nchi hii baada ya Mwalimu Nyerere kuondoka madarakani.Raisi Mstaafu Kikwete alikaribia sana kupata nafasi hii ya kihistoria ila inawezekana alipotoshwa na wenzake ndani ya chama na huenda hili ni jambo analolijutia katika maisha yake na si ajabu siku moja anaweza kuja kukiri/kusema hadharani.

Watawala watambue hakuna kitu wanachoweza ku-achieve na kitachowapa heshima ya kudumu kama kuipatia nchi hii katiba Mpya, Katiba itayokubaliwa na makundi karibu yote ya watanzania kuanzia wanasiasa, wakulima,wafanyakazi,viongozi wa dini, watanganyika, wazanzibari, n.k.

Unaweza kujenga barabara na ma-flyover nchi nzima, kusimamisha majengo makubwa nchi nzima, kuinua uchumi wa watu na Taifa kwa ujumla, n,k, lakini baada ya muda yote haya yatazoeleka na kuonekana ni ya kawaida tu lakini kamwe sio Katiba Mpya inayoweza kuweka msingi bora wa ku-achieve zaidi ya hayo katika Taifa letu.

Raisi Samia, wewe ndio Raisi uliepo madarakani leo hii, hivyo uzi huu unakulenga wewe moja kwa moja na ukiifunyia kazi utakuja kukumbuka maneno yangu haya siku zote za maisha yako.

Mama kazi kwako, kwani fursa sasa iko kwako, hivyo usiache mwingine akaja kuitumia ukaishia kujilaumu.

Unapokuwa Raisi, si ajabu ukazungukwa na watu wanaotamani kuipata fursa hiyo, hivyo wanaweza kukupotosha ili wao au watu wao waje waipate hiyo fursa(sio rahisi kuliona hili au kuliamini, ila ni jambo linalowezekana kabisa kwa wenye kuona mbali).

Nelson Mandela aliepigani uhuru na usawa wa watu weusi nchini mwake, anaheshimika nchini mwake na duniani kuliko makaburu walioijenga Afrika Kusini tena akiwa amekaa madarakani kwa muhula mmoja wa miaka mitano tu.
 
Katiba ya nini sisi? Tunataka mishahara, unapanda, posho zinapanda,lami inajengwa, reli inajengwa, vituo vya afya bwelele, kilimo tumepewa ruzuku, usalama wa kutosha nchini, mashule tele, Hilo li kitabu mnaliita katiba linaliwa na Mboga gani?
 
Katiba mpya wanaiogopa kwa sababu itagusa muungano. Kitu ambacho Nyerere aliwaonya CCM wasikiguse maana kuna vidonda vitatonyeshwa.
 
Katiba mpya wanaiogopa kwa sababu itagusa muungano. Kitu ambacho Nyerere aliwaonya CCM wasikiguse maana kuna vidonda vitatonyeshwa.
Katiba mpya haitaleta mana kama za enzi ya Mussa, mambo ni yale yale, marekani katiba yao Ina miaka 200, hawajaibadili, na bado waafrika wanalia "I can't breath", bado watu wanalala vibarazani, ubaguzi wa hali ya juu, hakuna usawa.
 
Katiba mpya wanaiogopa kwa sababu itagusa muungano. Kitu ambacho Nyerere aliwaonya CCM wasikiguse maana kuna vidonda vitatonyeshwa.
Matokeo ya alichofanya Nyerere ni kuleta Muungano uliojengengwa katika msingi mbovu na ndio maana mpaka leo hii inatumika nguvu na mabavu kulazimisha aina ya muungano tulionao.
 
tatizo ni kua
bado kuna kundi kubwa ambalo linaona bado linanufaika na hii mbovu iliopo
wengi ni wapigaji na waoga kushtakiwa
na hao ndio wanatushawishi tusiwe na katiba mpya kwa sasa
na wengi wao eidha bado hawajaridhika na walichoiba hivyo wanaona ngoja waendelee kuiba na wale chawa wanaotamani kushika nafasi ili waibe kama watangulizi wao

kama unabisha soma hizo koment hapo juu ndio utaelewa
 
Mtu anayepigania katiba nakuacha kupigania masuala ya msingi yanayomgusa mtu mmojammoja ni kama kichaa tu anayeikota makopo jalalani
 
katiba bila maoni ya wananchi ambao ndio msingi wenyewe itakuwa ni batili... maoni ya mchakato ni kuanza kupiga kura ili wananchi waamue kama kuna uhitaji wa katiba au la... na maoni yao yaheshimiwe

na sio vyama vya siasa kujipa jukumu la kudai katiba... tumeona nguvu ya umma katika nchi mbali mbali wakidai katiba bila sauti ya vyama...

mfano tunisia kama sijakosea, wananchi wame andamana kudai katiba...

hii katiba tunao idai ni katiba ya wanasiasa bila kujali vyama vyao, na ndio maana tuna peana na majina ya mchakato wenyewe, kama katiba ya warioba na sio ya wananchi ambao katiba ya sasa imeeleza wazi kuwa wananchi ndio msingi wenyewe.

NB
kila siku narejea huru, ujinga wa wananchi ndio mtaji wa wanasiasa...
 
Katiba mpya wanaiogopa kwa sababu itagusa muungano. Kitu ambacho Nyerere aliwaonya CCM wasikiguse maana kuna vidonda vitatonyeshwa.
huna unacho kijua kuhusu muungano... kama wa kuuvunja wangekuwa viongozi waliopo sasa...
 
Bwashee huku kwetu makonde plateau tuna matatizo ya maji, shule, barabara, masoko ya uhakika ya mazao yetu, huduma bora za afya, nk. Tushughurikieni hayo kwanza maana ni basic needs za kuishi, katiba itafuata baadae.
 
huna unacho kijua kuhusu muungano... kama wa kuuvunja wangekuwa viongozi waliopo sasa...
Hakuna kiongozi atakayesubutu. Nyerere alikubali vyama vingi lakini muungano alisema usiguswe.
 
Huu ndio ukweli mchungu kwa wote waliowahi kuwa Maraisi wa nchi hii baada ya Mwalimu Nyerere kuondoka madarakani.Raisi Mstaafu Kikwete alikaribia sana kupata nafasi hii ya kihistoria ila inawezekana alipotoshwa na wenzake ndani ya chama na huenda hili ni jambo analolijutia katika maisha yake na si ajabu siku moja anaweza kuja kukiri/kusema hadharani.

Watawala watambue hakuna kitu wanachoweza ku-achieve na kitachowapa heshima ya kudumu kama kuipatia nchi hii katiba Mpya, Katiba itayokubaliwa na makundi karibu yote ya watanzania kuanzia wanasiasa, wakulima,wafanyakazi,viongozi wa dini, watanganyika, wazanzibari, n.k.

Unaweza kujenga barabara na ma-flyover nchi nzima, kusimamisha majengo makubwa nchi nzima, kuinua uchumi wa watu na Taifa kwa ujumla, n,k, lakini baada ya muda yote haya yatazoeleka na kuonekana ni ya kawaida tu lakini kamwe sio Katiba Mpya inayoweza kuweka msingi bora wa ku-achieve zaidi ya hayo katika Taifa letu.

Raisi Samia, wewe ndio Raisi uliepo madarakani leo hii, hivyo uzi huu unakulenga wewe moja kwa moja na ukiifunyia kazi utakuja kukumbuka maneno yangu haya siku zote za maisha yako.

Mama kazi kwako, kwani fursa sasa iko kwako, hivyo usiache mwingine akaja kuitumia ukaishia kujilaumu.

Unapokuwa Raisi, si ajabu ukazungukwa na watu wanaotamani kuipata fursa hiyo, hivyo wanaweza kukupotosha ili wao au watu wao waje waipate hiyo fursa(sio rahisi kuliona hili au kuliamini, ila ni jambo linalowezekana kabisa kwa wenye kuona mbali).

Nelson Mandela aliepigani uhuru na usawa wa watu weusi nchini mwake, anaheshimika nchini mwake na duniani kuliko makaburu walioijenga Afrika Kusini tena akiwa amekaa madarakani kwa muhula mmoja wa miaka mitano tu.
Ili KINYONGA apate mtoto, lazima TUMBO lipasuke Ili watoto watoke salama, SACRIFCE lazima.

Kuzaliwa Kwa KATIBA iliyopo na CCM, sacrifice ilifanyika, TANU na TAA vilikufa.

Hivyo hivyo Kuzaliwa Kwa KATIBA mpya Kwa njia ya AMANI, lazima CCM ijitoe KAFARA, na Muundo wa Serikali iliyopo ubadilike.

Ni JAMBO gumu sana kulikubali Kwa kiongozi aliyepo, Mungu atasaidia lisowezekana,LIWEZEKANE . Amen.
 
Huu ndio ukweli mchungu kwa wote waliowahi kuwa Maraisi wa nchi hii baada ya Mwalimu Nyerere kuondoka madarakani.Raisi Mstaafu Kikwete alikaribia sana kupata nafasi hii ya kihistoria ila inawezekana alipotoshwa na wenzake ndani ya chama na huenda hili ni jambo analolijutia katika maisha yake na si ajabu siku moja anaweza kuja kukiri/kusema hadharani.

Watawala watambue hakuna kitu wanachoweza ku-achieve na kitachowapa heshima ya kudumu kama kuipatia nchi hii katiba Mpya, Katiba itayokubaliwa na makundi karibu yote ya watanzania kuanzia wanasiasa, wakulima,wafanyakazi,viongozi wa dini, watanganyika, wazanzibari, n.k.

Unaweza kujenga barabara na ma-flyover nchi nzima, kusimamisha majengo makubwa nchi nzima, kuinua uchumi wa watu na Taifa kwa ujumla, n,k, lakini baada ya muda yote haya yatazoeleka na kuonekana ni ya kawaida tu lakini kamwe sio Katiba Mpya inayoweza kuweka msingi bora wa ku-achieve zaidi ya hayo katika Taifa letu.

Raisi Samia, wewe ndio Raisi uliepo madarakani leo hii, hivyo uzi huu unakulenga wewe moja kwa moja na ukiifunyia kazi utakuja kukumbuka maneno yangu haya siku zote za maisha yako.

Mama kazi kwako, kwani fursa sasa iko kwako, hivyo usiache mwingine akaja kuitumia ukaishia kujilaumu.

Unapokuwa Raisi, si ajabu ukazungukwa na watu wanaotamani kuipata fursa hiyo, hivyo wanaweza kukupotosha ili wao au watu wao waje waipate hiyo fursa(sio rahisi kuliona hili au kuliamini, ila ni jambo linalowezekana kabisa kwa wenye kuona mbali).

Nelson Mandela aliepigani uhuru na usawa wa watu weusi nchini mwake, anaheshimika nchini mwake na duniani kuliko makaburu walioijenga Afrika Kusini tena akiwa amekaa madarakani kwa muhula mmoja wa miaka mitano tu.

Katiba ya sasa ina shida gani
 
Back
Top Bottom