Iyerdoy
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,755
- 1,939
Niwe mkweli. Sijui jinsi kiwanda cha MO kinavyomwaga maji machafu. Mm naishi huku Mkoani. Kero zetu huku ni migogoro baina ya Wafugaji na Wakulima.Naona wafanyakazi wa kiwanda cha MO umekuja ,
Unajua kiwanda cha MO kinavyo mwaga maji machafu kwenye kiwanda chake cha textile.
Mo alitakiwa Aya treat maji humo humo kiwandani kwake , yatoke yakiwa meupe, Kuna kipindi cha jk Kuna waziri alifika kiwandani hapo na akakiri uharifu wa mazingira unao fanywa na kiwanda cha MO na kuamriasha kiwanda hicho kufuata Sheria .lakini jamaa ni MTU anayependa kitonga, ku treat maji anaona ni gharama zinaongezeka ,kwake ni bora TU ayatiririshe mtoni ,(rangirangi na harafu Kali za kemikali)
Lakini hoja yangu ni kwamba jambo hilo linafanywa na watu wenye akili na utashi. Kwa nini wafanye hivyo kana kwamba hakuna Sheria zinazozuia hilo? Je, wao wanaomwaga hizo sumu kweli wanajua ila wanafanya makusudi. Je, wale watu wanaohusika Upande wa Afya na upande wa Mazingira hawapo? Je, Wale wanaotakiwa kuhakikisha Kwamba kunatakiwa kuwepo na Utii wa Sheria bila shuruti hawapo au hilo haliwahusu? n.k.
Aidha tusisahau kwamba waathirika wamewekewa mabango ya Tahadhari lakini pia nao hawataki Kuzingatia hiyo Tahadhari. Sasa tutakwenda kwa mtindo na mwondoko huo mpaka lini?