Wanaoishambulia ACT-Wazalendo kujiunga SUK wajiulize kama CHADEMA hawajapokea ruzuku ya Novemba 2020

Wanaoishambulia ACT-Wazalendo kujiunga SUK wajiulize kama CHADEMA hawajapokea ruzuku ya Novemba 2020

Nimeshuhudia humu mitandaoni makamanda wakimshambulia sana Zitto Kabwe kufuatia chama chake kujiunga na SUK huko visiwani Zanzibar.

Kigezo ni kwamba Chadema na ACT wazalendo hawayatambui matokeo ya uchaguzi mkuu na wao wanaita "uchafuzi"

Wanachosahau makamanda wa Chadema ni kuwahoji viongozi wao kama hawajapokea ruzuku ya mwezi November kutoka serikalini.

Ikumbukwe kuwa ruzuku ni zao la kura na idadi ya wabunge na madiwani ambao chama kimepata kwenye uchaguzi mkuu.

Natumai Matola na Salary slip mtauhoji uongozi kwa niaba yetu.

Maendeleo hayana vyama!

Ruzuku sio pesa ya CCM ni pesa ya Serikali! Ni ujinga kugomea pesa ambayo wakikataa itaenda kufanyiwa ufisadi ni bora watumie hiyo pesa kutoa mokopo kwa vijana na kujenga chama. Hii haina maana misamamo imebadilika mfano inawezekana kabisa wakapata njia ya kupeleka wabunge kwa muafaka maalumu bila wenyewe kukubali matokeo ya wizi
 
Bila kuathiri msimamo wangu wa kutoshabikia vyama vya siasa, naomba kukukumbusha kuwa Ruzuku wanayopokea vyama vya siasa sio hisani ya chama tawala, ni takwa la kisheria, lakini kubwa zaidi ruzuku ni kodi ya watanzania sio fedha inayotokana na michango ya chama tawala. PERIOD.
Kwani chadema wamesusia uchaguzi kwa sababu uchaguzi ni hisani ya chama tawala?
 
Nimeshuhudia humu mitandaoni makamanda wakimshambulia sana Zitto Kabwe kufuatia chama chake kujiunga na SUK huko visiwani Zanzibar.

Kigezo ni kwamba Chadema na ACT wazalendo hawayatambui matokeo ya uchaguzi mkuu na wao wanaita "uchafuzi"

Wanachosahau makamanda wa Chadema ni kuwahoji viongozi wao kama hawajapokea ruzuku ya mwezi November kutoka serikalini.

Ikumbukwe kuwa ruzuku ni zao la kura na idadi ya wabunge na madiwani ambao chama kimepata kwenye uchaguzi mkuu.

Natumai Matola na Salary slip mtauhoji uongozi kwa niaba yetu.

Maendeleo hayana vyama!

"Ikumbukwe kuwa ruzuku ni zao la kura na idadi ya wabunge na madiwani ambao chama kimepata kwenye uchaguzi mkuu."
Hiyo ni sheria ya nchi wewe unatakaje?
 
Swadaktaa, hiki ndicho nilichokuwa nataka unijibu hiki.
Okay sasa turudi kwenye mada hapo juu halafu tujibu hoja ya msingi. Chadema wamekataa kutambua matokeo yote na uchaguzi hata kwa Jimbo waliloshinda pamoja na hata viti vya udiwani walivyopata akiwa sambamba na kukataa kuteua wabunge wa viti maalum (mpaka sasa bado ni sintofahamu) huo ndio msimamo wa chadema hadi sasa kwamba uchaguzi huu ni haramu kwao na matokeo yote ni haramu kwao.
Swali ni je uhalali wa wao kuipokea ruzuku inayotokana na uchaguzi walio kataa kuutambua wameupata wapi? Kama msimamo wako ni kuto kutambua uchaguzi na matokeo yake ambayo ndio chanzo Cha hiyo ruzuku kwanini uipokee?
Kuipokea hiyo ruzuku sio dalili ya kukubaliana na hayo matokeo ya uchaguzi?
Ruzuku inatokana na Kodi za wananchi ambao ni chadema na ccm, mambo ya Kodi hayana chama

Na huu Ujinga ndo wanaotumia ccm kwamba usipotuchagua hatukuletei maendeleo, mbowe analipa Kodi kwanin asipewe ruzuku au kupelekewa maendeleo

Ruzuku sio hela magufuli anatoa mfukoni kwake
 
Ruzuku inatokana na Kodi za wananchi ambao ni chadema na ccm, mambo ya Kodi hayana chama
Eeh aisee!!
Wewe si ndio umesema ruzuku wanapewa chama kilichopata uwakirishi au sio wewe ulie sema?

Sasa chadema wamekataa huo ushindi walio upata ambao unawapa haki ya kupata ruzuku, sasa kwanini waipokee wakati hawatambui matokeo ya uchaguzi?

Kabla hujajibu soma kwanza ninacho andika ukielewe.
 
Eeh aisee!!
Wewe si ndio umesema ruzuku wanapewa chama kilichopata uwakirishi au sio wewe ulie sema?

Sasa chadema wamekataa huo ushindi walio upata ambao unawapa haki ya kupata ruzuku, sasa kwanini waipokee wakati hawatambui matokeo ya uchaguzi?

Kabla hujajibu soma kwanza ninacho andika ukielewe.Wana mbunge mmoja lazima wapewe ruzuku, kutokutambua matokeo sio kosa la jinai ndo mpaka sasahiv hawajafunguliwa mashtaka ya kuvunja Sheria Sasa kwanin unawahukumu na hawajafanya kosa
Wana mbunge mmoja kwa hiyo ruzuku ni lazima, kutokutambua matokeo sio kosa kisheria, ndo maana hawajafunguliwa mashtaka
 
Wana mbunge mmoja kwa hiyo ruzuku ni lazima, kutokutambua matokeo sio kosa kisheria, ndo maana hawajafunguliwa mashtaka
Haki nimecheka sana.
Ahsante sana aheri wewe umekuwa mkweli mkuu, Kama ni hivi basi hawa chadema ni wanafiki wa kiwango Cha lami hawa jamaa.

Basi na kule Zanzibar ACT hakuna haja ya kuwaandama mana hata wao kule SUK ipo kikatiba sio kosa kisheria!.
 
Haki nimecheka sana.
Ahsante sana aheri wewe umekuwa mkweli mkuu, Kama ni hivi basi hawa chadema ni wanafiki wa kiwango Cha lami hawa jamaa.

Basi na kule Zanzibar ACT hakuna haja ya kuwaandama mana hata wao kule SUK ipo kikatiba sio kosa kisheria!.
Wanafki kwa lipi ruzuku ni haki yao kikatiba, na chadema wapo kikatiba upinzani wao unatumbulika kikatiba, we wapi mtu Aki yake unataka Tena aiombe
 
Zanzimana anahangaika kwelikweli kuzitafuta tilioni mbili za wafadhili , mpaka analazimisha kuwapa watu ubunge wa lazima ? (mabunzi) , analazimisha kuwapa ruzuku wapinga maendeleo Chadema wanaomkwamisha kwenda uchumi wa kati wa Lumumba wa kufikirika .
 
Tatizo lenu wote akili zinafanana, misalaba ya taifa.

Hao wabunge 20 umewatoa wapi?!
Wewe punga kweli kweli hizo ni hesabu namba huwa hazidanganyi nisawa na kwenye daladala kunakuwa na seat za wanafunzi kadhaa hivyo hivyo na bunge limetenga seat kadhaa kutokana na idadi ya tiketi zilivyo nunuliwa
 
Uliza maswali ya maana tafadhali, kasome sheria ujue kwa nini.

Narudia tena, pesa ya ruzuku sio mali ya CCM, ni pesa za wananchi, tafuteni propaganda nyingine.
Kama ni mali ya wananchi kwa nini hamutambui maamuzi ya wananchi? Kwa nini hamtaki kupeleke wanawake bungeni?
 
Back
Top Bottom