Pre GE2025 Wanaojadili Urais wa 2030 ilihali 2025 Kuna Uchaguzi mkuu, wanatuonaje Watanzania?

Pre GE2025 Wanaojadili Urais wa 2030 ilihali 2025 Kuna Uchaguzi mkuu, wanatuonaje Watanzania?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Rabbon

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2022
Posts
21,625
Reaction score
33,688
Salaam, Shalom!!

Nchini petu Tanzania , mwaka kesho 2025 kutakuwapo na uchaguzi mkuu Kwa ngazi zote, Udiwani, ubunge na nafasi ya Urais.

Limeibuka kundi dogo la watu linaloanza kujadili habari za 2030 kana kwamba 2025 tayari Kuna kiongozi special amekwishawekwa tayari Kwa nafasi ya Urais, kwamba tutaingia Uchaguzi 2025 kuchagua Wabunge na Madiwani pekee, hili Si sawa na kinatakiwa kukemea vikali.

Rais aliyepo, ikifika muda wa mchakato ndani ya vyama,akipita mchujo, itafikia time atakuwa mgombea sawa kabisa na wagombea wengine ikitokea chama chake kikampa ridhaa kupeperusha bendera.

Watanzania 2025 Wana HAKI ya msingi kabisa kumchagua kiongozi wamtakaye katika nafasi zote kuanzia Udiwani,ubunge na Urais.

Soma Pia: Wanasiasa na mbinu ya kuweka TV kwenye mikusanyiko ili kuhadaa wapiga kura

Nchi hii ni ya mfumo wa vyama vingi, wananchi Wana HAKI kabisa kumchagua Rais, Mbunge au Diwani Kutokea chama chochote Cha Siasa na akawa Kiongozi.

ANGALIZO: 2025 Kuna Uchaguzi Mkuu, Wananchi tunajua HAKI zetu na tutamchagua kiongozi tumtakaye utakapowadia muda huo adhimu, na kamwe hatutapangiwa. Na wote wanaojadili Urais wa 2030 kana kwamba 2025 hakuna uchaguzi Kwa nafasi ya Urais "WAPUUZWE".

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Karibuni 🙏
 
Ikitokea wananchi wakaamua wapate kiongozi mpya Kwa nafasi yeyote kati ya hizo tatu za Udiwani, ubunge au Urais, Kutoka chama chochote waipendacho, uamuzi wao uheshimiwe.

HIZI habari za kuuziana mbuzi kwenye gunia zipuuzwe.
 
Na Watanzania tulio nje ya Nchi tupewe HAKI yetu ya msingi ya kupiga kura.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿.
 
CCM tuna utaratibu wetu mgombea wa CCM ana save vipindi viwili hiyo inajulikana kwahiyo hayo mengine ya ni formalities tu.
Huyu aliyepo aligombea Urais Awamu ya kwanza lini?

Na ikiwa aligombea, yupi alikuwa mgombea Urais wake mwenza?
 
Huyu aliyepo aligombea Urais Awamu ya kwanza lini?

Na ikiwa aligombea, yupi alikuwa mgombea Urais wake mwenza?
Kasome katiba ya nchi inasemaje Rais aliyepo madarakani anapofariki au kuumwa na kushindwa kutimiza majukumu yake .
 
Kasome katiba ya nchi inasemaje Rais aliyepo madarakani anapofariki au kuumwa na kushindwa kutimiza majukumu yake .
Kwahiyo Katiba ndio imetamka fomu itolewe Moja?

Jitahidi kujibu sawasawa na ulivyouluzwa.
 
Salaam, Shalom!!

Nchini petu Tanzania , mwaka kesho 2025 kutakuwapo na uchaguzi mkuu Kwa ngazi zote, Udiwani, ubunge na nafasi ya Urais.

Limeibuka kundi dogo la watu linaloanza kujadili habari za 2030 kana kwamba 2025 tayari Kuna kiongozi special amekwishawekwa tayari Kwa nafasi ya Urais, kwamba tutaingia Uchaguzi 2025 kuchagua Wabunge na Madiwani pekee, hili Si sawa na kinatakiwa kukemea vikali.

Rais aliyepo, ikifika muda wa mchakato ndani ya vyama, itafikia time atakuwa mgombea sawa kabisa na wagombea wengine ikitokea chama chake kikampa ridhaa kupeperusha bendera.

Watanzania 2025 Wana HAKI ya msingi kabisa kumchagua kiongozi wamtakaye katika nafasi zote kuanzia Udiwani,ubunge na Urais.

Soma Pia: Wanasiasa na mbinu ya kuweka TV kwenye mikusanyiko ili kuhadaa wapiga kura

Nchi hii ni ya mfumo wa vyama vingi, wananchi Wana HAKI kabisa kumchagua Rais, Mbunge au Diwani Kutokea chama chochote Cha Siasa na akawa Kiongozi.

ANGALIZO: 2025 Kuna Uchaguzi Mkuu, Wananchi tunajua HAKI zetu na tutamchagua kiongozi tumtakaye utakapowadia muda huo adhimu, na kamwe hatutapangiwa. Na wote wanaojadili Urais wa 2030 kana kwamba 2025 hakuna uchaguzi Kwa nafasi ya Urais wapuuzwe.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Karibuni 🙏
jiandae kuchagua nchi ya kuishi 2025

Tutaigawana nchi vipande vipande Bora tukose wote

Sijui hiyo bandari na dp world itaangukia nchi gani na je itabeba mizigo ipi, ni kitendawili
 
Kwahiyo Katiba ndio imetamka fomu itolewe Moja?

Jitahidi kujibu sawasawa na ulivyouluzwa.
Jaribu kuwa specific unataka kujua awamu ya kwanza ni ipi au why ccm itoe fomu moja 2025?
 
Back
Top Bottom