Wanaopinga kuungama dhambi kwa Padri, ndio wapinga Kristo wanaohubiriwa na wasabato na ndio wale wanaosoma maandiko kwa kurukaruka.

Kubatiza watu wazima wanaojitambua, mtoto hana uchaguzi bado. Yesu alibatizwa akiwa anajitambua.
 
Kweli mkuu
Kweli mkuu maandiko yako wazi ni uvivu wetu kuyasoma na kumtafakari Mungu, ukisoma mathayo 7inafafanua Sana tu

1. Hakuna taasisi hapa duniani aliye champion wa masuala ya kitaaluma kama Kanisa Katoliki. Kanisa Katoliki lina wasomi magwiji katika fani zote za kitaaluma unazozijua wewe. Hata katika anga za mbali,Kanisa lina wasomi wabobezi hatari.Sidhani kama kuna watu wengi,ikiwemo waprotestanti kama wasabato wanafahamu kama Baba wa Genetics Gregory Mendel,alikuwa ni Padri wa Kanisa Katoliki.

2. Ninataka kusema nini hapa? Ni hivi,hakuna dhehebu linaloweza kushindana na Kanisa Katoliki katika masuala ya Teolojia kwa sababu huko ndio liko kongwe kabisa.Kwa hiyo,hiyo habari ya kusema kwamba munayafahamu maandiko matakatifu mintarafu suala hilo la uwezo wa mapadri kuondoa kujidanganya tu. Wasabato mumekuja mwaka 1863, mumelikuta Kanisa lina miaka zaidi ya 1500 linafundisha Teolojia.Kwa hiyo, mnapojigamba kwa lolote kaeni mjitafakari. Ellen White alifundisha kwamba Mungu sio nafsi tatu na hadi leo baadhi ya wasabato mungali mnaamini hivyo.Wakati ninyi mnahangaika na suala hilo,Kanisa Katoliki lilisha-conclude mambo hayo siku nyingi sana.Kwa hiyo,msilione Kanisa liko kimya mnapodanganyana mkafikiri kwamba halina majibu dhidi ya upotoshaji wenu.
 
Jibu rahisi tu. Padiri ni binadamu hasemehi dhambi. Anaesamehe ni MUNGU.Padiri ,mchungaji,Askofu,Shehe n.k wengine hata wametuzidi kwa dhambi. Wewe Mwombe MUNGU akusamehe achana na Padiri. Japo ni kweli kutubu nzuri na yenye msamaha ni ile ya mbepe za watu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu yangu nakuonea huruma sana! Kama Wewe ni msomaji mzuri wa biblia usingesema hivyo ! Ila Roho wa Mungu akupe akufunguliwe ufahamu wa kuelewa neno lake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana Mungu akurehemu ndugu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siyo biblia tuu.....No Catholicism no Christianity......Ukristo ndio Ukatoliki wenyewe kama ulikuwa hujui..
Na yale makanisa saba Yesu aliyomwambia Yohana kwenye kitabu cha ufunuo yametoka wapi? Je mbona Jina Katoliki halimo humo kama ndilo kabisa la kwanza unavyojidai? Umekurupuka ndugu yangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…