Wanaopinga kuungama dhambi kwa Padri, ndio wapinga Kristo wanaohubiriwa na wasabato na ndio wale wanaosoma maandiko kwa kurukaruka.

Sijaona kama una hoja nyingine zaidi ya hii. Kifupi ni kuwa padri wala mchungaji HANA NA HATAKUWA NA UWEZO WA KUMWONDOLEA MTU DHAMBI. Ni Mungu pekee anafanya hilo. Sema binadamu wanahiaji utukufu waweze pata sababu ya kupewa sadaka na kicho. Sijui hata kama unaweza elewa kiswahili hiki chepes hivi.

Usisome Biblia kwa kurukaruka....
 
Sijaona kama una hoja nyingine zaidi ya hii.
Ipi hiyo ..?? Hoja kuu na majibu yote yapo kwenye uzi..

Kifupi ni kuwa padri wala mchungaji HANA NA HATAKUWA NA UWEZO WA KUMWONDOLEA MTU DHAMBI.
Kwanini iwe kifupi...? Kwanini unaifunga akili yako kuizuia kujifunza zaidi na zaidi....

Inamaana unaenda kinnyume na maneno ya Yesu alipowaachia Mitume uwezo huo wa Kuondolea zambi...??

Ni Mungu pekee anafanya hilo.
Ni kweli kabisa.....ila ni kwa kupitia Mapadre....

adamu wanahiaji utukufu waweze pata sababu ya kupewa sadaka na kicho. Sijui hata kama unaweza elewa kiswahili hiki chepes hivi.
Na kuelewa sana....kudhihirisha kuwa nakuelewa jibu maswali niliyokuuliza
 
Msiabishe hizo elimu mlizopata japo kidato cha nne..

Umeshindwa kung'amua lugha mbili za kigiriki na Kilatini
Lugha si hoja, Biblia ninayosoma mimi hakuna sehemu iliyoandikwa Yesu kristu sasa sijui natumia biblia yenye lugha ya kilatini au kigiriki. Umeshawahi kujiuliza kwa nini wakatoliki hawatumii neno kristo wanatumia kristu kama makanisa mengine hata kama neno hilo lina maana moja?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Una uhakika na hiki ulichoandika...??


Ni sawa kabisa....Mungu abasamehe kupitia kwa Padre

Wakati wa agano la kale waisraeli walikua wakikosea wanaenda kwa nabii kumweleza awaombee msamaha kwa Mungu. Elewa sio nabii anayewaondolea dhambi bali alikua anawaombea msamaha lakini pia ukumbuke haikua sheria kwamba ni lazima uje kwa nabii akuombee usamehewe, walikua wanaangalia nani yupo karibu na Mungu ndio waombee msamaha kwa sababu wao walikua wanajiona wakosefu.

Wakati wa agano jipya baada ya ujio wa Yesu toba na kila kitu wanaomba watu wenyewe na Yesu lekee ndiye anayesamehe dhambi. Ili andiko liende kwa udhibitisho onyesha sehemu Yesu alipotoa maagizo kwamba watu waende kuungama dhambi zao kwa mitume ili wasamehewe. Onyesha mfano ni wapi mtume petro au paulo au yoyote yule walisamehe mtu dhambi? Agano jipya mchungaji anakuongoza sala ya toba na unakiri kwa kinywa chako mwenye ila jukumu la kusamehe dhambi sio lake.
 
Umeshawahi kujiuliza kwa nini wakatoliki hawatumii neno kristo wanatumia kristu kama makanisa mengine hata kama neno hilo lina maana moja?
Mimi ni mkatoliki...Na maneno yote hayo yanatumika sana tuu....


Sasa sijui waongelea wakatoliki gani..???

Muwe mnatendea haki elimu zanu...mambo mengine mnavyoandika ni mpaka aibu yani...

Mnatia aibu....
 
Wakati wa agano la kale waisraeli walikua wakikosea wanaenda kwa nabii kumweleza awaombee msamaha kwa Mungu.
Unaweza niambia walikuwa wanaenda kwa nabii gani...,??

Kasome tena kitabu cha Walawi ujue kazi ya Kuhani.....
 
Kwaiyo mkuu unavyosema ata padri akiwa ni mtenda dhambi wewe ukienda kutubu unasamehewa bila kujali matendo ya padri sasa nikuulize swali unaweza kuchota maji masafi kwenye ndoo chafu na ukapata maji masafi kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
padri ndo nani kwenye wokovu wa mwanadamu
Ni kuhani...ndiye aliyepewa mamlaka ya kufundisha neno la Mungu ili watu waupate uzima wa milele...

Pia ndiye aliyepewa mamlaka ya Kusamehe dhambi kupitia kwa Yesu Kristo
 
Mimi sio mkatoliki na hata ningekuwa mkatoliki kamwe nisingekwenda kwa binadamu/Padri mwenye mwili wa nyama kama wangu kuungama dhambi.
 
Umemjibu vema mleta uzi!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kuhani...ndiye aliyepewa mamlaka ya kufundisha neno la Mungu ili watu waupate uzima wa milele...

Pia ndiye aliyepewa mamlaka ya Kusamehe dhambi kupitia kwa Yesu Kristo

acha kukalili nioneshe wapi alipo pewa hayo mamlaka ya kufundisha na kusamehe na uo ukuhani
 
Umeandika nin? Nakushauri soma biblia ndugu uelewe kwa msaada wa Roho Mtakatifu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…