Wanaotangaza vifo vya watu mashuhuri kila kukicha kwenye mitandao ya kijamii wajumuishwe kwenye uhujimu uchumi, hawana nia njema na Taifa letu

Wanaotangaza vifo vya watu mashuhuri kila kukicha kwenye mitandao ya kijamii wajumuishwe kwenye uhujimu uchumi, hawana nia njema na Taifa letu

Mimi nilisoma Political Science achana na Civics,ila hakuna uhuru usio na mipaka.Aliyekuambia kuna 100% freedom of speech kakudanya.Hata hao waliokudanganya kwamba kuna kitu kinaitwa freedom of speech kwao hakuna.
Halafu msiwe mnapenda kutuchanganya. Mbona baadhi ya hizo taarifa huwa mnazitoa wenyewe? Kwa nini mna akili kama za kenge?

Kifo cha Katibu mkuu kiongozi kilitolewa taarifa na nani? Yule Mbunge wa Mhambwe ni nani aliyetoa taarifa? Yule mbunge wenu wa viti maalum Martha Umbura kifo chake kilitangazwa na nani?

Na kwa nini wakitangaza wengine mnapagawa? Mbona mnajiona mna haki ya kila kitu nyinyi viumbe mnaokera kupitiliza? Unafahamu maana halisi ya neno Uhujumu uchumi wewe kweli?
 
Kifo hakitangazwi,kinajitangaza.
Kwa njia ya Infra-red au electromagnetic waves ?

Fahamu kwamba nyakati zimebadilika mitandao ya kijamii ndio imekuwa communication medium ambayo enzi hizo habari zingepatikana through redio, simu na word of mouth (sasa hivi ni information at your fingertips)
 
Shetani kazi yake ni kuharibu,kuua na kuiba,ndivyo Biblia inavyosema.Kwa hiyo kila mahali utakapo shuhudia uharibifu,vifo na wizi,ni lazima mkono wa Shetani upo.Si ajabu kwa hiyo kwamba Shetani hufurahia matukio hayo na hufanya kila mbinu chafu ili watu waibiwe,wafe na kuwe na uharibifu.

Kumezuka siku za hivi karibuni tabia ambayo si ya kawaida na kiungwana kabisa,kwa binadamu,ambayo sina shaka yeyote kwamba ina mkono wa Shetani.Tabia hii ni tabia ya kutangaza na kushabikia vifo vya watu mbali mbali,hasa wenye mamlaka au ukwasi,katika hali inayo-ashiria kwamba matangazo hayo yanafurahia vifo hivyo.Kiukweli ni Shetani tu anayeweza kufurahia kifo cha binadamu yeyote.

Ukitafakari kwa kina matangazo hayo, utagundua pasi shaka yeyote kwamba ushabiki huu wa watu kufa una misingi ya kishetani.Najua wapo watu wenye nia mbaya na taifa letu,hii ni pamoja na kuona kwamba Taifa letu linapata majanga ya kila aina,ili lisifanikiwe kwa njia yeyote ile. Makundi yenye nia hii ovu ni ya watu ambao waliigeuza Tanzania kuwa shamba la bibi na hata kulifanya kuwa soko la madawa ya kulevya.

Ni vigumu hasa kuona watu hawa wanapata faida gani kwa hararaka haraka kwa kuitangazia dunia kwamba Tanzania watu wanakufa sana.Hata hivyo ukitafakari kwa kina utagundua sababu ya kushabikia vifo hivyo!

Sababu ya msingi ni Ili Tanzania ionekane kwamba ina ugonjwa wa Corona na hivyo kuharibu uchumi wa nchi yetu.Haishangazi kwa hiyo kwamba Ubalozi wa Marekani umetangaza kwamba Tanzania sio salama kutembelea,eti kwa kuwa kuna Corona,wakati Marekani kwenyewe tatizo lipo,tena kubwa sana hata kuliko Tanzania.Haishangazi pia kwamba Marekani imetangaza eti nia yake ya kuisaidia Tanzania ishinde Corona,wakati kwao wameshindwa!Nia ya matangazo yote haya ni ile ile,kuifanya dunia iamini kwamba Tanzania kuna Corona na hivyo kuharibu tashwira yake kimataifa na uchumi wake.

Tupo kwenye vita ya kiuchumi ambapo tumediriki hata kuanzisha mahakama za mafisadi.Hawa wanaotangaza vifo vya watu mashuhuri kwenye mitandao ya kijamii na forums zingine,hawana tofauti yeyote na wahuju uchumi,wawe rounded up na wafikishwe kwenye vyombo vya sheria.Tukiwachekea tutakula mabua.
Wewe fala kwani wao ndio wanawaua hao watu mashuhuri?
Wengine ni akili zenu mnawaachiaga kina nani wawatunzie?
Dili na kinachowauwa hawa wanaotangaza wataacha tu. Pumbavu
 
Sio ubinadamu kushabikia kifo,ni Shetani tu anayefurahi binadamu wakifa,tena dhambini.
Ukiongelea Shetani basi hapo unaongelea Imani..., kwa logic yako kifo kingekuwa ni kibaya hakitakiwi na shetani pekee ndio mnufaika si Mungu angekizuia ?
Au?
 
Halafu msiwe mnapenda kutuchanganya. Mbona baadhi ya hizo taarifa huwa mnazitoa wenyewe? Kwa nini mna akili kama za kenge?

Kifo cha Katibu mkuu kiongozi kilitolewa taarifa na nani? Yule Mbunge wa Mhambwe ni nani aliyetoa taarifa? Yule mbunge wenu wa viti maalum Martha Umbura kifo chake kilitangazwa na nani?

Na kwa nini wakitangaza wengine mnapagawa? Mbona mnajiona mna haki ya kila kitu nyinyi viumbe mnaokera kupitiliza? Unafahamu maana halisi ya neno Uhujumu uchumi wewe kweli?
Zipo taarifa njema zenye nia njema,na zipo taarifa zenye nia ovu.Si kila mtu ana mamlaka ya kutoa taarifa ya kifo,kwanza kwa nini.Kama ni kiongozi wa juu serikali itatoa taarifa kwa wananchi,otherwise ni fujo yenye nia ya ku-create hofu na taharuki,it is uncalled for.
 
Ukiongelea Shetani / Imani basi hapo unamuongelea Mungu..., kwa logic yako kifo kingekuwa ni kibaya hakitakiwi na shetani pekee ndio mnufaika si Mungu angekizuia ?
Au?
Unahitaji elimu ya kina,next time.
 
Wewe fala kwani wao ndio wanawaua hao watu mashuhuri?
Wengine ni akili zenu mnawaachiaga kina nani wawatunzie?
Dili na kinachowauwa hawa wanaotangaza wataacha tu. Pumbavu
Wote tunakwenda huko kama sio leo ni kesho,kwa hiyo hakuna sababu ya kufurahia mwenzio akifa.
 
Nijiandae nini,kama unategemea nife sifi.Mabwana zenu akina Biden watatangulia wao,si unaona tayari ana Dimentia.
Speaker yangu mbovu. Naichezea shilingi yangu kwenye tundu la choo. Muda utaongea hata kama hamtaki tuseme.
 
Kwahiyo anayepaswa kushitakiwa ni shetani ambaye kazi yake kuu ni kuua, kuiba na kuharibu au wewe usiyejua unachokitaka?
Je, kifo kaleta shetani au Mungu?
Kama kimeletwa na Mungu, je , Mungu ana chembe za ushetani?
Kama kimeletwa na shetani, je, Mungu alikuwa weak mpaka shetani analeta kifo?
 
Kwa njia ya Infra-red au electromagnetic waves ?

Fahamu kwamba nyakati zimebadilika mitandao ya kijamii ndio imekuwa communication medium ambayo enzi hizo habari zingepatikana through redio, simu na word of mouth (sasa hivi ni information at your fingertips)
Information at your fingertips,so tutumie mtandao vibaya,
tu-create fear and mayhem kwenye jamii kwa kuwa mtandao upo.Lakini unatangaza hivyo vifo ili iweje hasa,kama sio kwa nia ovu ni nini.
 
Kikubwa ulichotaka kuwasilisha ni hiki.
Karibu dunia nzima inapambana na huu ugonjwa. Sasa "taswira ya nchi" inaharibika vipi kujulikana kwamba kuna corona na watu wanakufa? Kila mahali wanakufa.

Hata wasipotangaza vifo haihalalishi kwamba huo ugonjwa haupo. Tusifiche matatizo tujitahidi kuyatatua sio hadi vifo "vituumbue".
Ameeen
 
Information at your fingertips,so tutumie mtandao vibaya to create fear and mayhem kwa kuwa mtandao upo.Unatangaza ili iweje hasa,kama sio kwa nia ovu.
Unasoma ili iweje? Nadhani una choice ? Kupangia watu cha kufanya ni definition fupi ya Dictatorship...
 
Tupo kwenye vita ya kiuchumi ambapo tumediriki hata kuanzisha mahakama za mafisadi.Hawa wanaotangaza vifo vya watu mashuhuri kwenye mitandao ya kijamii na forums zingine,hawana tofauti yeyote na wahuju uchumi,wawe rounded up na wafikishwe kwenye vyombo vya sheria.Tukiwachekea tutakula mabua
Hivi Tanzania iwe kwenye vita ya Uchumi na Nani kweri? Aachen ufala
 
Wote tunakwenda huko kama sio leo ni kesho,kwa hiyo hakuna sababu ya kufurahia mwenzio akifa.
Huna lolote wewe . Corona ipo na inakula vichwa ipendavyo. Mlipoombwa kudhibiti uingiaji holela wa watu mlikataa, na mkatoa mialiko mingi na matangazo kibao . Matokeo yake Covid imepiga kambi. Acha tuone matunda ya kwenda kinyume na science.

Pili Corona na vifo havijaanzia Tz , hivyo hatuna sababu kuvionea aibu labda ushamba wangu
 
Back
Top Bottom