#COVID19 Wanaouhubiri chanjo kumbe hawajachanjwa

Nachosema ni kwamba ninyi mnahusisha vifo vya watu na covid pasina kuwa na ushahidi wowote ilimradi tu Kwa sababu kuna covid basi mnaamua tu kuhusisha vifo vya watu na huo ugonjwa kwa
Nani kahusisha?? Wizara ya Afya ama?? Maana wao ndio wamepinga kuwa issue sio chanjo ssa kwanini una generalise? Mimi nimemsingizia nani humu jf? mie niliwahi kukwambia wazazi.... 5 workmates.... Waliponea ICU Na wachungaji wangu 3 walikufa kwa covid kabisa so ukinijibu ni face kwa nachosema sio kwa kutumia random jf comments
 

Uongo mwengine 'JPM na Maalimu walifariki ghafla' Nani alitutangazia hivi?
 
kuna watu mna akili chafu sana...hao freemasons wakuue laeo ili hali hospitalini unakwenda kila siku dawa zote unazotumia wanatengeneza wao. wangetaka kukuua wangekuua tangu hujazaliwa, maana mama yako alipotungwa amimba alipigwa chanjo kibao ili ukue tumboni na uzaliwe ukiwa na fya.

na ulipozaliwa tu ukapigwa chanjo ya dtp-polio, pepo punda, surua etc.....hizo zote zilitengenezwa na nani? acha kuamini videao clips za TicTok!

by the way nani alikwambia kuwa condom ni chanjo na ukimwi?
 
kamuulize mama yako na baba yako ikiwa hukuchanjwa hiyo polio au la?
 
Wewe huna akili ndio sababu hoja za kupinga hizo chanjo unadhan ni hoja za Kitanzania, wengine wanamsingizia Hayati JPM

Kwa kifupi kama huelewi chanjo hizi zinapingwa kwa efficiency yake,

Huko Marekani watu wamegoma kuchanja hadi wanahongwa dola mia mia lakin bado hawataki, hizo chanjo unazozitaja zilipingwa kama hii?

Watu wanechanja, wamepata Corona, wako Hospital kwny machine za upumuaji

Takwimu za UK za mwezi uliopita zilisema 52% ya Admitted patients wa covid ni wale waliokamilisha chanjo, kama una cha kutetea anzia hapo badala ya kujitungia hoja na kujibu

Marekan watu kibao wapo hospital wamelazwa na walishakamilisha chanjo na ndio sababu inayofanya watu kugoma

Kuhusu hiyo hoja yako ya kusema kama kutuua wangetuua zamani kwny chanjo tulizochukua, jibu rahisi ni kuwa akili yako ni ndogo ndio sababu hujiulizi Wimbi la Mabinti wadogo siku hizi kuwa na matatizo ya uzazi hadi kina Dr Mwaka kupata umaarufu, kasi ya kuongezeka matatizo ya figo, liver na kansa zisizo na idadi chanzo chake nini? Au tukisema wanatuua unadhan unaanguka pale pale baada ya kuchanja?
 
mtu aliyechanjwa akipata tatizo mtaanza kujitetea kuwa mara chanjo haihusiani hilo tatizo
Waliochanjwa ni laki 2 kati ya waTanzaia million 60!! Sasa kweli kuna sample ya kutosha ya waliopigwa chanjo hadi kudai kwamba wanaopata shida ni sababu ya chanjo??
 
Kwa hiyo wote ambao hawakuvaa Condom miaka hiyo wakipiga michepuko walikufa kwa Ukimwi?
We unamzodoa mwenzio lakini ww ndio una reasoning ndogo sana.

Hvi unaweza linganisha airborne na ngono?? Yaani mpka umvue binti nguo ndio upate VVU ilihali covid akiwa nayo mmoja tu kwenye kadamnasi anatosha kuwaambukiza kwa salamu tu!!
Hizi ni chanjo za kukupa matumaini tu lakin kama Corona inakubeba kama kawaida na wenywe wamekiri na watu wamelazwa muda huu huko huko zilipoanzia chanjo
Hata dawa za kawaida tu unadhani zinakua na efficacy sawa kwa kila binadamu? Kuna watu wanatumia ARV ila CD 4 zinashuka tu.... je umewahi sikia zinapigwa vita?? Maana its better than nothing!! Hata nkikuuliza hapa una mbadala gani huna jibu?
propaganda za ma Freemasons
Kwahiyo Freemason ndio wameleta pia chanjo ya Polio na Ebola Africa? Kabla ya hapo tulikua tunakufa kma mende eti leo hii wakileta chanjo ya Covid ndio wanakua freemasons??

Typical CCM mindset.... Speculations tu
 
Maelezo meeeengi hujajibu swali,

kuna watu wamemaliza chanjo zote na sasa hivi wapo kwny mitungi ya gesi corona inawamaliza, 52% ya admitted patients kwa takwimu za mwezi uliopita ni wale ambao wapo vaccineted?

Hizi taarifa ndio zinasababisha watu wakatae chanjo Dunia nzima hadi Marekan wameanza kutoa rushwa ya dola mia baada ya hoja kushindwa kushawishi Umma, toa ufafanuzi wa wasiwas huu usikimbilie kwny kichaka cha kuitaja Ccm haihusiki hapa
 
Wewe unadhani wanaohimiza kuvaa condom unadhani wao wanazitumia ? lkn je ukimwi si upo na unaua? kwahiyo maamuzi ni yako, kwenda pekupeku au kutumia, mwingine anainunua lkn akifika kwenye tukia ile shape ikimchanganya condom anatupilia mbali.
 
Wewe ni mmoja kati ya wanaodai kuwa Magufuli alikufa kwa corona pasina kuwa na ushahidi na ndio maana nikakuweka kwenye hilo kundi kama watu ambao mnahusisha vifo vya watu na corona pasina ushahidi.
 
Yaan chakushangaza ni kuwa watu wanatumia nguvu kubwa kupinga chanjo ukiuliza sababu kubwa hakuna ni ilimradi tu kasikia[emoji848] kwani huyo mzungu anayetaka kutuua anashindwa kuweka hiyo sumu kwenye panado? Au hata kwenye bia tu
Sio kila anayepinga chanjo anatumia hoja ya sijui wazungu wanataka kutuuwa inaonesha wewe umeishia kumsikiliza Gwajima tu hujui kama kuna hadi madaktari Maprofesa wenye kupinga chanjo kwa kutumia hoja za kisayansi.
 
Waliochanjwa ni laki 2 kati ya waTanzaia million 60!! Sasa kweli kuna sample ya kutosha ya waliopigwa chanjo hadi kudai kwamba wanaopata shida ni sababu ya chanjo??
Haya mkuu, kwanza hata hivyo hata ukipata madhara yenyewe huwezi kushtaki popote hivyo sio muhimu hayo malalamiko.
 
Je hawa wanaotuminisha chanjo ni salama na wakadiriki kucheza futuhi kumchoma mama ili watu tuamini ni salama
Halafu cha ajabu wao wenyewe hawajachanja?
Mkuu usiige kunya kwa tembo, jifikirie wewe mwenyewe kwanza.
Ukiona chanjo itakusaidi, kachanje, kama unaona fiksi we sare tu.
Wengine tumeona ni heri kuchanja ili kuwa salama.
 
Bahati nzuri COVID-19🦠 haiui kila mtu kwa watu wataendelea kupinga lakini hawatakufa
 
Hyo ni variant tofauti usidai kwamba chanjo haifanyi kazi useme hapa kwamba chanjo haikua 100% compatible for variant ya delta ambayo ilikuja Zaidi ya mwaka toka chanjo igundulike ndio maana pfizer et al wameanza tengeneza zilizo more efficient kwa variant mpya.

Kingine unasema tu waliofika hospitali 52% ndio wagonjwa ila hausemi data kabla ya chanjo kulikua na vifo mpka elfu 3 kwa siku huko US.... Ila wengi waliochanjwa vifo na wagonjwa wamepungua, niliweka hapa JF Data za Israel kuwa toka chanjo wapate zaidi ya 70% vifo na symptomatic cases zimeshuka kwa zaidi ya 80%. Kwanini hizo takwimu hamsemi mnakimbilia walioenda hospitali tu....

Ukitaka kupima efficacy chukua namba ya General population sio waliolazwa tu. Utakua unapotosha maana hau factor in waliopaswa kuumwa lakini hawaoni dalili sababu ya chanjo kuwalinda
 
Wewe ni mmoja kati ya wanaodai kuwa Magufuli alikufa kwa corona pasina kuwa na ushahidi na ndio maana nikakuweka kwenye hilo kundi kama watu ambao mnahusisha vifo vya watu na corona pasina ushahidi.
Mkuu mimi nina uhakika 100% naomba uende kwa cardiologist yeyote pale JKCI ukiambiwa jibu tofauti na hili ntafuta akaunti yangu hapa JF.

Nimeconfirm from two very credible sources kuwa JPM aliondoka kwa Covid 19. Na sina aibu kusema hili wala sio speculation, whether alitupiwa ili kukomolewa hiyo ni topic nyingine but nilicho na uhakika nacho ni hiko. Nmekupa homework ndogo tu, ssa usibishe wakati hujaenda kuuliza.

Ni sawa na wale wanaodai eti corona ikwapi mbona mtaani sijaona mazishi? Ila ukimuuliza ameenda mloganzila,KCMC,MNH,JKCI n.k au pale Aga Khan kupata data za vifo utakuta hana, ila anabisha tu kisa yye hana taarifa sahihi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…