Wanaowatetea machinga kuondolewa maeneo yasiyo rasmi kwa biashara wana uelewa mdogo

Wanaowatetea machinga kuondolewa maeneo yasiyo rasmi kwa biashara wana uelewa mdogo

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Kila kitu kina mpangilio katika maisha.. Huwezi kufanya kinyume na mpangilio na ukijaribu kufanya hivyo matokeo yake ni zogo na kupaganyika.

Kwenye hili la machinga lilikosa mpangilio..Na likafugwa na wanasiasa kwa maslahi binafsi ya kisiasa.. Sasa kama tumeamua kurudi kwenye mpangilio lawama zinatoka wapi?

Hata majumbani mwetu.. Tuna mipangilio ya kila kitu kitanda kina sehemu yake, choo, vyombo viatu nguo vyakula nknk.. Miili yetu nayo ina mipangilio macho yakae wapi, mikono, miguu nknk havijarundikwa tu sehemu moja.. Mifano ni mingi sana.

Sasa tunapata wapi uthubutu wa kutetea watu wanafanya biashara sehemu zisizo rasmi?
Kwenye njia za waenda kwa miguu
Kwenye mitaro ya maji
Kwenye vituo vya kupumzikia
Kwenye maeneo ya wazi
Kwenye vituo vya magari njiani
Mbele ya maduka ya wengine nknk

Tuna kitu kinaitwa mipango miji... Hii ndio huamua miji iweje
Wapi sehemu za makazi
Wapi sehemu za biashara
Wapi sehemu za michezo
Wapi sehemu za kupumkizia
Wapi sehemu za starehe
Wapi sehemu za ibada
Wapi sehemu za huduma za jamii nknk
Sehemu za zilizotengwa kwa shughuli fulani zibaki hivyo kwa shughuli tazamiwa..ukianza kuchanganya unaharibu na kuleta zogo

Uchafuzi wa mazingira ni pamoja na kuweka vitu mahali pasipopaswa viwepo... Usafi wa miji ni pamoja na kuwa na mpangilio kwenye kila jambo...Je watetezi wa machinga wanajua yote haya?
Tazama picha hizi za jiji bila vibanda vya machinga! Je mji hauvutii!?

IMG-20211020-WA0051.jpg
IMG-20211020-WA0052.jpg
 
Well Said;
Itapendeza *TARURA/TANROAD wanapojenga Barabara, wasiweke service road , wala peavings , WAWEKE MABANDA PEMBEZONI mwa Barabara zote nchini yakae tu hata kama hakuna wahitaji maana wanyonge wanatakiwa wafanye Biashara Humo!

Hawa watu wana familia, WAACHWE WAFANYE LOLOTE so long as wanapata kipato cha kulisha familia

Pia; Serikali iwache wanyonge wote waliochukua MAENEO YA HIFADHI ZA TAIFA, ni ajabu eti Mtu unaishi Morogoro huna ardhi wakati kuna mbuga ya Mikumi imekaa tu.

Kila mtu aachwe atafute maisha yake, hawa matajiri wao wanaishi, Njiro, Shanty-town, Masaki, Kisota na Uzunguni, Gangilonga hawajui adha ya sisi wanyonge!
 
Well Said;
Itapendeza *TARURA/TANROAD wanapojenga Barabara, wasiweke service road , wala peavings , WAWEKE MABANDA PEMBEZONI mwa Barabara zote nchini yakae tu hata kama hakuna wahitaji maana wanyonge wanatakiwa wafanye Biashara Humo!

Hawa watu wana familia, WAACHWE WAFANYE LOLOTE so long as wanapata kipato cha kulisha familia

Pia; Serikali iwache wanyonge wote waliochukua MAENEO YA HIFADHI ZA TAIFA, ni ajabu eti Mtu unaishi Morogoro huna ardhi wakati kuna mbuga ya Mikumi imekaa tu.

Kila mtu aachwe atafute maisha yake, hawa matajiri wao wanaishi, Njiro, Shanty-town, Masaki, Kisota na Uzunguni, Gangilonga hawajui adha ya sisi wanyonge!
IMG-20211020-WA0118.jpg
 
sio kosa la machinga,kosa ni letu kutotambu mipango.

hapa ilikuwa simple tu,wapewe mipaka na sandard za vibanda,ili maisha yaendelee tu.

leo hii tunajifanya kuchukia mabati na bishara kila sehem wakati dsm yote ni uchafu uchafu tu kutokea angani!!!unafiki hautatufikisha popote.
 
Tena sio tu wanauelewa mdogo,ni wanaupeo mdogo na ni washamba sababu hawatembei hata miji mikubwa ya nchi nyingine kuona kama kuna huo ujinga wa kuacha machinga watawale kila kona. Eti Dar inazidiwa hadi na Kigali?
sio kosa la machinga,kosa ni letu kutotambu mipango.

hapa ilikuwa simple tu,wapewe mipaka na sandard za vibanda,ili maisha yaendelee tu.

leo hii tunajifanya kuchukia mabati na bishara kila sehem wakati dsm yote ni uchafu uchafu tu kutokea
Basi Itapendeza TARURA/TANROAD wanapojenga Barabara, wasiweke service road , wala peavings , WAWEKE MABANDA Pembezoni mwa Barabara zote nchini yakae tu hata kama hakuna wahitaji maana wanyonge wanatakiwa wafanye Biashara Humo!
 
Poleni na sekeseke na kuondolewa vibanda vyenu machinga sehemu zilizopo mijini.

Swali nalo jiuliza kuhusu vitambulisho vya wamchinga.

Vilikuwa na muongozo au malengo gani ambayo mwisho wa siku kuwa vurugu na hatima isiyojulikana kwa wimbi la wanaojitafutia kipato
IMG_1647.jpg
 
Basi Itapendeza TARURA/TANROAD wanapojenga Barabara, wasiweke service road , wala peavings , WAWEKE MABANDA Pembezoni mwa Barabara zote nchini yakae tu hata kama hakuna wahitaji maana wanyonge wanatakiwa wafanye Biashara Humo!

Machinga mbali na kuchafua jiji ni hasara ipi ya msingi waliyoifanya!!!!
 
sio kosa la machinga,kosa ni letu kutotambu mipango.

hapa ilikuwa simple tu,wapewe mipaka na sandard za vibanda,ili maisha yaendelee tu.

leo hii tunajifanya kuchukia mabati na bishara kila sehem wakati dsm yote ni uchafu uchafu tu kutokea angani!!!unafiki hautatufikisha popote.
Tuanze na hili la kutambua na kuheshimu mipaka ya kila kitu... Penye biashara ifanyike biashara.. Penye eneo la wazi pabaki wazi...penye njia ya waenda kwa miguu pabaki hivyo
 
Basi Itapendeza TARURA/TANROAD wanapojenga Barabara, wasiweke service road , wala peavings , WAWEKE MABANDA Pembezoni mwa Barabara zote nchini yakae tu hata kama hakuna wahitaji maana wanyonge wanatakiwa wafanye Biashara Humo!
Sio maeneo yao ya biashara ndio maana wanahamishwa,hawafukuzwi bado watafanya biashara ila kwenye maeneo yao waliyotengewa. Service road sio kwa ajili ya biashara
 
machinga mbali na kuchafua jiji ni hasara
machinga mbali na kuchafua jiji ni hasara ipi ya msingi waliyoifanya!!!!
Machinga wasababishe Ajali- Waachwe tu, Machinga wasababishe foleni waachwe tu, machinga wasilipe kodi (wahujumu uchumi) waachwe tu, machinga wasababishe tukanyagane na kutukanana nao kwa sababu wamepanga bidhaa kwenye Njia za waenda kwa miguu waachwe tu haleluyaaaaaaaa
 
Back
Top Bottom