Wanaowatetea machinga kuondolewa maeneo yasiyo rasmi kwa biashara wana uelewa mdogo

Wanaowatetea machinga kuondolewa maeneo yasiyo rasmi kwa biashara wana uelewa mdogo

Palikua na agenda gani ya kuwaacha Vijana wenye nguvu wa Kimatumbi wakimbilie DSM na kuacha ardhi yao yenye utajiri mkubwa namna hiyo? Ardhi ya Lindi na Mtwara inakimbiliwa na wafugaji toka kanda ya ziwa na Manyara na Arusha.[emoji848][emoji848][emoji2827][emoji2827]
Ulimsikia Mbunge na kada wa CCM toka kanda ya Ziwa ,mh.Musukuma kipambana ili Wamatumbi wanaoitwa Wamachinga wasipatiwe maeneo rasmi ya biashara ? Anapambana na kuwatetea ili wajenge vibanda vya biashara kwenye mitaro ya barabarani ?
Jiulize Mbenge kutoka kwa wafugaji wasio na ardhi ,Mbunge mfanyabiashara ya madini ,Mbunge ambaye wanapiga kura wake kuna wakati walikua wanahamasishana kufyatua watoto na kuongeza wake wengi!!
Hivi ni kweli Huyo Mbunge anauchungu na Wamatumbi toka mchinga palipojaa Jipsam na Korosho?
Tujiulize Wakati wamachinga walipoanza Kurudi Vijijini kulima korosho ,mbona hakuwatetea wasiporwe pesa zao za Korosho ? Serikali ilipokwapua pesa za Korosho na Musukuma na Polepole walikaa kimya na kusababisha zao lao LA Korosho liporomoke na kukosa soko mpaka Leo na kusabisha wamachinga warudi Kwenye hifadhi za barabara kuuza midoli toka China na pipi toka China huku wakizidi kukuza uchumi wa China kwa kukwepa kodi rasmi na kusababisha Wafanyabiashara toka Kongo na Sudani kusini kukimbilia Kampala baada ya kuziba kila mahali na kufanya jiji kuwa kama eneo la vibaka na wababaishaji.

Wakati huo huo awamu ya NNE ilipoanzisha miradi mikubwa ya Gesi, viwanda ,vikubwa vya Saruji walilenga kuwavutia vijana wa kimatumbi maarufu kama wamachinga warudi kwao kuendeleza ardhi yao yenye utajiri mkubwa sana Afrika na duniani. Ardhi ambayo inapaswa kuwa kivutio kikubwa cha watalii kwani ndilo eneo lililothibitika mpaka sasa kuwa waliishi Mijusi wakubwa sana Karene nyingi zilizopita. Na moja ya mabaki ya mijusi hao ipo mpaka Leo kule Ujeruman. Badala ya serikali kupambana ili mabaki hayo yarejeshwe Tanzania wao wanapambana na watu wanaovaa tisheti za Katiba mpya na kuwatelekeza kwa kudhibiti zao la Korosho lisije likawanufaisha Wakulima na kuvuruga Uwekezaji kwenye Gesi na Viwanda vya Sariji. Matokeo yake Wamatumbi wamekimbilia kuishi na kufanya biashara mitaroni DSM . Wakati huo wafugaji wanaotoka kwenye jimbo la Musukuma na wafanyabishara wa madini wanakimbilia kwa kasi kubwa sana Lindi na Mtwara ambapo kuna ardhi nzuri na kubwa.
Tchaaaah!




Sent from my TECNO L8 Lite using JamiiForums mobile app
 
Hili swala ni very complex kwa kweli. Unatamani mji uwe msafi na kuwe na mpangilio mzuri, lakini unapita njiani unaona the way watu wanavyobomoa and they don't know where to go, some have got mikopo, vikoba, wanasomesha na kulisha watoto...it's very complicated kwa kweli.

Kama kuna namna serikali ikafanya, mazingira wezeshi na maeneo walau yenye tija kwa wafanyabiashara za kupanga (manake wengi wetu tunafanya biashara ndogondogo hata kama tumepanga frem).

Nimeona hapo Mbezi mwisho people are demolishing mabanda kwa mikono yao, sad sad yani. Ila msumeno wa sheria ni mkali, mkali hasa kwa walio chini. Basi hata hizi tozo ziende kusaidia kuwekeza katika eneo hili pia ili hii tunaiita keki ya taifa igawiwe kwao pia. I just don't know how this will end, Ila naona kundi kubwa la kipatoless, kundi kubwa la watu waliojikatia tamaa..sad sana!!
 
Kila kitu kina mpangilio katika maisha.. Huwezi kufanya kinyume na mpangilio na ukijaribu kufanya hivyo matokeo yake ni zogo na kupaganyika.

Kwenye hili la machinga lilikosa mpangilio..Na likafugwa na wanasiasa kwa maslahi binafsi ya kisiasa.. Sasa kama tumeamua kurudi kwenye mpangilio lawama zinatoka wapi?

Hata majumbani mwetu.. Tuna mipangilio ya kila kitu kitanda kina sehemu yake, choo, vyombo viatu nguo vyakula nknk.. Miili yetu nayo ina mipangilio macho yakae wapi, mikono, miguu nknk havijarundikwa tu sehemu moja.. Mifano ni mingi sana.

Sasa tunapata wapi uthubutu wa kutetea watu wanafanya biashara sehemu zisizo rasmi?
Kwenye njia za waenda kwa miguu
Kwenye mitaro ya maji
Kwenye vituo vya kupumzikia
Kwenye maeneo ya wazi
Kwenye vituo vya magari njiani
Mbele ya maduka ya wengine nknk

Tuna kitu kinaitwa mipango miji... Hii ndio huamua miji iweje
Wapi sehemu za makazi
Wapi sehemu za biashara
Wapi sehemu za michezo
Wapi sehemu za kupumkizia
Wapi sehemu za starehe
Wapi sehemu za ibada
Wapi sehemu za huduma za jamii nknk
Sehemu za zilizotengwa kwa shughuli fulani zibaki hivyo kwa shughuli tazamiwa..ukianza kuchanganya unaharibu na kuleta zogo

Uchafuzi wa mazingira ni pamoja na kuweka vitu mahali pasipopaswa viwepo... Usafi wa miji ni pamoja na kuwa na mpangilio kwenye kila jambo...Je watetezi wa machinga wanajua yote haya?
Tazama picha hizi za jiji bila vibanda vya machinga! Je mji hauvutii!?

View attachment 1980673View attachment 1980674

Wamachinga walikuwa wamechafua sana jiji kiasi kwamba Jiji lilikuwa linaonekana lichafu kwasababu wamezagaa kila sehemu mara wauza pweza, mara wachoma mahind yani tafrani
 
sijavunjiwa kibanda mimi.

kumbe wewe unashabikia sababu hu miongoni mwa wavunjiwaji!!!!
Wala sishabkii chochote ila naungana na ile iliyo sahihi tuwe na sehemu za kufanyia biashara,, sikuhizi wala ile misongamano isiyokuwa na maana hamna
 
Hili swala ni very complex kwa kweli. Unatamani mji uwe msafi na kuwe na mpangilio mzuri, lakini unapita njiani unaona the way watu wanavyobomoa and they don't know where to go, some have got mikopo, vikoba, wanasomesha na kulisha watoto...it's very complicated kwa kweli.

Kama kuna namna serikali ikafanya, mazingira wezeshi na maeneo walau yenye tija kwa wafanyabiashara za kupanga (manake wengi wetu tunafanya biashara ndogondogo hata kama tumepanga frem).

Nimeona hapo Mbezi mwisho people are demolishing mabanda kwa mikono yao, sad sad yani. Ila msumeno wa sheria ni mkali, mkali hasa kwa walio chini. Basi hata hizi tozo ziende kusaidia kuwekeza katika eneo hili pia ili hii tunaiita keki ya taifa igawiwe kwao pia. I just don't know how this will end, Ila naona kundi kubwa la kipatoless, kundi kubwa la watu waliojikatia tamaa..sad sana!!
Yaah umeandika kwa uchungu sana mno naungana na wewe.............. Sema pia na wao walijisahau kabisa hawakuwa wanaweza kujipanga vema na kuweka angalao sehemu staarabu... its real bad but ukiwa unatembea na ule uhuru wa waenda kwa miguu unaona bora tuu wajipange. Ilikuwa ni shida maana huna pa kukanyaga kamwe
 
Wala sishabkii chochote ila naungana na ile iliyo sahihi tuwe na sehemu za kufanyia biashara,, sikuhizi wala ile misongamano isiyokuwa na maana hamna

misongamano isiyo na maana,itakuwaje na maana wakati umevimbiwa!!!!


mimi nashauri,tumemaliza la machinga,kifatacho kuvunja nyumba duni manispaa tote ili iwe jiji kweli kweli,au unasemaje ndugu???
 
Back
Top Bottom