Kasiano Muyenzi
JF-Expert Member
- Feb 3, 2018
- 13,858
- 22,729
Kwa hiyo unasemaje, Magufuli alikuwa sahihi kuuzima upinzani?Hao unaowahita wapinzani hawakuonesha ni watu wanaoweka maslahi ya Taifa mbele kwenye kipindi chake Cha uongozi walikuwa wanapinga hadi mambo mazuri yaliyokuwa yanafanyika watakuwaje wanakuwa wa maana? Wanawatetea mafisadi kama Manji,hanspope Serikali inapochukua hatua za kifisadi dhidi yao.Wanapinga miradi iliyoanzishwa bila hata hoja za msingi ilimradi tu waonekane wanapinga, wanapinga hatua zilizokuwa zinachukuliwa na Serikali kuhusu mali zetu za asili ikiwemo madini kwa lengo la kulinda our resources utawaitaje hao jamaa wanafaida? Kitu ambacho nadhani umesahau wapinzani ndio walioanzisha vita na Magu walianza na kampeni ya kusema hawamtambui kuwa ni raisi na awakuishia hapo walimzomea kipindi Cha ufunguzi wa bunge na wakawa wanatoa lugha chafu dhidi yake ilipofika hatua ndio Magu akaanza kuwachukia na akapiga marufuku siasa za majukwaani kwasababu aliona wanatumia vibaya uhuru wao
Binafsi sikumwelewa wala sikuunga mkono uamuzi wake maana aliamua kwa jazba na alikuwa na jazba haswa.
Wezi na mafisadi ni CCM damu damu hivyo alipaswa kupambana nao ndani ya chama, na alipaswa aanze na yule rais mstaafu, hapo angeudhihirisha uzalendo wake.
Kumbuka viwanja vyote vya mchezo vinavyomilikiwa na CCM vimejengwa kwa nguvu ya wananchi, Magufuli angekuwa mzalendo wa ukweli angerudisha viwanja hivyo vya umma kwa wananchi, lkn mzee baba akakomaa na upinzani mwisho akakata pumzi akiwaacha mafisadi (wana ccm wenzake) wakikenua meno.
Alichemsha sana mzee baba.