Wanasema Hayati Magufuli Alikuwa Anakubalika sana: Kwanini basi aliiba Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu 2020?

Wanasema Hayati Magufuli Alikuwa Anakubalika sana: Kwanini basi aliiba Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu 2020?

Hao unaowahita wapinzani hawakuonesha ni watu wanaoweka maslahi ya Taifa mbele kwenye kipindi chake Cha uongozi walikuwa wanapinga hadi mambo mazuri yaliyokuwa yanafanyika watakuwaje wanakuwa wa maana? Wanawatetea mafisadi kama Manji,hanspope Serikali inapochukua hatua za kifisadi dhidi yao.Wanapinga miradi iliyoanzishwa bila hata hoja za msingi ilimradi tu waonekane wanapinga, wanapinga hatua zilizokuwa zinachukuliwa na Serikali kuhusu mali zetu za asili ikiwemo madini kwa lengo la kulinda our resources utawaitaje hao jamaa wanafaida? Kitu ambacho nadhani umesahau wapinzani ndio walioanzisha vita na Magu walianza na kampeni ya kusema hawamtambui kuwa ni raisi na awakuishia hapo walimzomea kipindi Cha ufunguzi wa bunge na wakawa wanatoa lugha chafu dhidi yake ilipofika hatua ndio Magu akaanza kuwachukia na akapiga marufuku siasa za majukwaani kwasababu aliona wanatumia vibaya uhuru wao
Kwa hiyo unasemaje, Magufuli alikuwa sahihi kuuzima upinzani?

Binafsi sikumwelewa wala sikuunga mkono uamuzi wake maana aliamua kwa jazba na alikuwa na jazba haswa.

Wezi na mafisadi ni CCM damu damu hivyo alipaswa kupambana nao ndani ya chama, na alipaswa aanze na yule rais mstaafu, hapo angeudhihirisha uzalendo wake.

Kumbuka viwanja vyote vya mchezo vinavyomilikiwa na CCM vimejengwa kwa nguvu ya wananchi, Magufuli angekuwa mzalendo wa ukweli angerudisha viwanja hivyo vya umma kwa wananchi, lkn mzee baba akakomaa na upinzani mwisho akakata pumzi akiwaacha mafisadi (wana ccm wenzake) wakikenua meno.

Alichemsha sana mzee baba.
 
Watetezi wa legacy ya Magufuli wanasema kuwa Jiwe Alikuwa anakubalika sana na "Wanyonge" kuliko Rais Samia aliyekumbatia matajiri.

Swali; Kama alikuwa anakubalika kwa nini aliiba Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Vitongoji wa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa 2020?

Kama alikuwa anakubalika kwannini alifanya biashara ya kununua wabunge wa CDM na CUF akina Silinde, Gekul, Katambi, Mtulia na Mollel.

You can be foolish but you can't fool us!!
Mbona mnahangaika sana na Magufuli? Msifieni Royal Tour wenu inatosha na 2025 mshinde Urais na Wabunge wengi kupitia CHADEMA
 
Mbona mnahangaika sana na Magufuli? Msifieni Royal Tour wenu inatosha na 2025 mshinde Urais na Wabunge wengi kupitia CHADEMA
Tusipangiane majukumu, kila mmoja ashinde mechi zake. Wewe kwa nini unawashwa matako kwa Magufuli kusemwa?
 
Kila mtu ana haki ya kutoa mawazo yake bro, naheshimu pia mawazo yako kama ambavyo n wewe unapaswa kuheshimu ya kwangu. Kupishana mitazamo wala sio tatizo
Matumizi mabaya ya uhuru wa maoni, poleni Sukuma Gang kwa kufiwa na mungu wenu. Ila tambueni hatorudi tena hayawani kama Magufuli kutawala nchi yetu
 
Kila mtu ana haki ya kutoa mawazo yake bro, naheshimu pia mawazo yako kama ambavyo n wewe unapaswa kuheshimu ya kwangu. Kupishana mitazamo wala sio tatizo
katika uhuru wa kutoa mawazo mmefikia hatua mnasema kuua na kuteka ni mapungufu madogo madogo ya kinadamu. kweliiiii?!!!
 
Watetezi wa legacy ya Magufuli wanasema kuwa Jiwe Alikuwa anakubalika sana na "Wanyonge" kuliko Rais Samia aliyekumbatia matajiri.

Swali; Kama alikuwa anakubalika kwa nini aliiba Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Vitongoji wa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa 2020?

Kama alikuwa anakubalika kwannini alifanya biashara ya kununua wabunge wa CDM na CUF akina Silinde, Gekul, Katambi, Mtulia na Mollel.

You can be foolish but you can't fool us!!
yule alijikubali mwenyewe na ubabe wake hakuna aliemkubali ila daima tutamkumbuka alikua na nia njema na alibeba maono ya taifa
 
katika uhuru wa kutoa mawazo mmefikia hatua mnasema kuua na kuteka ni mapungufu madogo madogo ya kinadamu. kweliiiii?!!!
Pengine huyo Idimi hakuna ndugu yake aliyeathirika kwa maamuzi ya DIKTETA Magufuli kuanzia kwa waliiouliwa, waliobomolewa Kibamba, wauza korosho Mtwara, waliotumbuliwa kazi na walionyang'anywa fedha na TRA
 
yule alijikubali mwenyewe na ubabe wake hakuna aliemkubali ila daima tutamkumbuka alikua na nia njema na alibeba maono ya taifa
Unaweza kubeba maono yakawa ya HOVYO, bado yatakuwa ya Taifa? Labda ya Taifa la Wasukuma. Kiongozi mwenye maono anashirikisha waenzie, ndiyo leadership. Huyu alikuwa ni kichaa tu, hustahili kuwa Rais wa nchi kubwa ya wastaarabu kama Tanzania
 
Pengine huyo Idimi hakuna ndugu yake aliyeathirika kwa maamuzi ya DIKTETA Magufuli kuanzia kwa waliiouliwa, waliobomolewa Kibamba, wauza korosho Mtwara, waliotumbuliwa kazi na walionyang'anywa fedha na TRA
Mie ni mwathirika pia wa awamu ya mwendazake mkuu, ila ninachokataa ni hawa wanaodai kwamba kila alichokifanya mwendazake ni kibaya. Kuna mazuri pia alifanya, including kurudisha nidhamu kwa watumishi wa umma. Shilingi ina pande mbili.
 
katika uhuru wa kutoa mawazo mmefikia hatua mnasema kuua na kuteka ni mapungufu madogo madogo ya kinadamu. kweliiiii?!!!
In case nimeeleweka vibaya, siungi mkono matendo maovu ya awamu iliyopita kwa sababu yamenigusa pia kwa namna moja ama nyingine. Napingana na wale ambao hawaoni zuri lolote la Mwendazake, ikiwemo kurudisha nidhamu ya utumishi wa umma. Tumhukumu kwa mabaya, lakini penye credit pia tumpatia credit zake.
 
Matumizi mabaya ya uhuru wa maoni, poleni Sukuma Gang kwa kufiwa na mungu wenu. Ila tambueni hatorudi tena hayawani kama Magufuli kutawala nchi yetu
Nasikitika sana kusoma comment mbovu ya senior member. Binafsi sio Msukuma wala sitokei kanda ya ziwa. Soma comment yangu ya mwanzo kabisa bro, utaelewa nilikuwa naongelea nini! Siungi mkono matendo maovu ya awamu yoyote ile, including ya mwendazake.
 
JuL
yule alijikubali mwenyewe na ubabe wake hakuna aliemkubali ila daima tutamkumbuka alikua na nia njema na alibeba maono ya taifa
Litekaj na Iiuaji nan alikumbuke?!!! Utalikumbuka wew na hawara yako mnywa gongo lakin hata mkeo halali wa ndoa hawazi likumbuka liuaji.
 
Mbali na mapungufu yake kama binadamu, jamaa alikuwa mtu wa maamuzi... RIP JPM
Angefanya maamuzi kulingana na katiba kina sabaya na makonda wasingepelekwa mahakamani. Wale watu waliokufa na kujeruhiwa nao walikuwa hawana sababu za kuishi Kama yeye? Wapambe wake mzigo mnao mtujibu.

Hii laaana inawezekana huko alipo amepangiwa kitengo Cha kushinda na Moto usiku na mchana.

Mnanikumbusha kilio Cha yule tajiri akiwa kwenye Moto na Lazaro akiwa kifuani mwa Abraham. Kama namwona mwendazake na kina Ben.

Au ndiyo salamu zimewafikia wanaomwombea msamaha?

Baba nakuomba umtume Lazaro akawaambie ndugu zangu maisha ya dunia wayaache baada ya Happ kuna mbingu na Moto.
 
Nasikitika sana kusoma comment mbovu ya senior member. Binafsi sio Msukuma wala sitokei kanda ya ziwa. Soma comment yangu ya mwanzo kabisa bro, utaelewa nilikuwa naongelea nini! Siungi mkono matendo maovu ya awamu yoyote ile, including ya mwendazake.
Hapo sasa kwenye nidhamu ya watumishi wa Serikali unayoisifia ndiyo kafanya makosa makubwa. Sijui uleo wa elimu yako ukoje. Nikukumbushe alivyosema Obama mwaka 2009 pale Ghana alipoalikwa kuhutubia bunge; "Africa needs strong institutions and not strong men".

Maana yake kama ni nidhamu ya wafanyakazi ilikuwa vile kwa kuwa Magufuli ni mkali, basi ni nidhamu ya woga. Akiondoka wanarudi palepale walipokuwa kabla. Angalia nidhamu ya private sector kama una ndugu ameajiriwa huko muulize kama ana Magufuli anayemuogopa!!
 
If wishes were horses
Unasema upinzani haujafa?
Acha hizo, jiwe alipiga kila kona ktk upinzani kuhakikisha kwamba wapinzani hawapo TZ, na hao watakaobaki kuwa wapinzani ni wale wa kupewa bilioni 6 wanatulia.

Ni kweli yeye ndiye alikufa, ila upinzani wa sasa haupo hot, lbd waje wapinzani wapya wa kizazi Kipya ila sio hao kina Mbowe, Kabwela mzito, na wote wenye akili za kudanganywa kizembe kisha wakapoa kama maji ya mtungini.
if wishes were horses....
 

Attachments

  • Screenshot_20230814-162422.png
    Screenshot_20230814-162422.png
    21.1 KB · Views: 1
  • Screenshot_20230814-162502.png
    Screenshot_20230814-162502.png
    77.6 KB · Views: 1
Back
Top Bottom