Wanasheria wa nchi hii mko wapi? Simameni muwaambie akina Mwigulu Nchemba ukweli kuhusu haki katika sheria zetu

Wanasheria wa nchi hii mko wapi? Simameni muwaambie akina Mwigulu Nchemba ukweli kuhusu haki katika sheria zetu

Status
Not open for further replies.

Fumadilu Kalimanzila

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2016
Posts
1,770
Reaction score
5,423
Law is an art, na sisi kama Taifa katika Sheria tumerithi doctrines mbalimbali kutoka common law na hivyo suala la kujua Kiingereza (English) haliepukiki!

Tanzania tunajenga utamaduni wa ajabu sana kwamba kama mtu fulani au kikundi fulani hakijui jambo fulani badala ya kuwekeza katika kujifunza jambo hilo basi kunajengwa mazingira ya kubadili jambo hilo kutoa nafuu kwa wasiojua jambo hilo.

Hili la kubadili sheria zetu zilizoandikwa kwa Kiingereza kwenda kuandikwa kwa Kiswahili ni mojawapo.

Ukifuatilia kwa makini miaka ya hivi karibuni hapa nchini mwetu kumekuwa na kasumba ya ajabu sana kwamba kujua Kiswahili ndio uzalendo na kutumia au kujua Kiingereza (English) siyo uzalendo!

Ukichunguza vizuri wanaopigania dhana hiyo hata Kiswahili fasaha pia hawajui.

Mimi naamini muda wote kuwa suala la kutokuwepo au kukosekana haki katika sheria zetu haliko katika lugha iliyotumika katika uandishi wa sheria zetu bali ni katika contents (maudhui) ya sheria zetu!

Mfano, sheria zetu zinapinga matokeo ya kura za Rais kupingwa Mahakamani, hivi ukiandika sheria hiyo leo kwa Kiswahili basi itabadilika na kutoa haki hiyo ya msingi inayonyimwa kwa Watanzania?

PhD za akina Mwigulu Nchemba zitumike kuleta hoja zilizofanyiwa Tafiti za kina kwenye public domain na waache kufanya kazi kwa mihemuko au kumfurahisha mtu fulani!

Tatizo kubwa tulilo nalo kwa sasa ni Watanzania wengi na hasa Viongozi kutojua kiingereza (English) kwa ufasaha!

Tutafute ufumbuzi wa tatizo hilo badala ya "kuhamisha magoli" ili kujipa ushindi wa bure!

Dunia inakwenda kwa kasi sana na wala haiwezi kutusubiri sisi Tanzania na mawazo yetu ya ajabu ajabu!

Kina Mwigulu Nchemba wanawadanganya "wanyonge" kuwa wanawapenda na wanapigania haki zao ikiwemo ili la kubadili sheria zetu kuwa kwa Kiswahili wakati wao wanasomesha watoto wao FEZA SCHOOLS (English medium) ambako wanalipa ada ya Primary School ya Tshs. 5 milioni hadi 7 milioni kwa mwaka!

(Akili za kuambiwa changanya na za kwako: by Mhe. Jakaya M. Kikwete).

Mambo mengi tumeanza kushindwa kuwasiliana na Dunia kwa sababu ya kutojua lugha kwa ufasaha.

Huwezi kusema kila jambo utabeba Wakalimani, kuna mambo mengine ni "top secrets" unahitaji kuwasiliana "one to one"!

Chukulia hata chaguzi zetu kunatokea makando kando mengi lakini wananchi, wanahabari hata baadhi ya wanasheria hawawezi ku- communicate na Dunia ili kueleza tatizo lilipo!

Ukiangalia vyombo vikubwa vya habari Duniani kama vile CNN, BBC, Aljazeera n.k vinawahoji sana watu wa Africa kutoka katika mataifa ya Nigeria, Ghana, Kenya, Uganda n.k. they are eloquent and can talk to the World!

Hapa kwetu mwananchi,mwanahabari au hata kiongozi mkubwa akihojiwa utasikia, " Zeeee,Zeeee, Zeeee, Zisi , Zisi, To meeee, To meeee, Onole (only)! Upuuzi mtupu!

Wakati fulani huko nyuma Mwl. Julius Nyerere alialikwa na akina Prof. Mugyabuso Mulokozi wa TUKI pale UDSM na ajenda zao za kutumia Kiswahili kufundishia elimu ya juu na wakazungumza Kiswahili kigumu kuliko hata Kiingereza. Kwa mshangao wao Mwl. Nyerere aliwaambia Kiingereza ndio Kiswahili cha Dunia hii.

Hivyo mimi pia nawambia akina Mwigulu Nchemba na the like tusidanganyane! ni kweli tunapaswa kujifunza Kiswahili chetu na kukienzi lakini hatupaswi ku- undermine role ya kiingereza (English) katika Dunia tuliyonayo sasa!

After all ni aibu pia kuwa na Waziri wa Sheria asiyejua chochote katika sheria. Hii inawezekana na kuonekana kawaida tu kwa Nchi kama yetu hii ambayo fundi mchomelea vyuma (Welder) anaweza pia kuwa Daktari (Tabibu) hata kama hajasomea taaluma hiyo!
 
Hapa umempa makavu jaji mkuu ambaye ameacha kutekeleza majukumu yake ya kikatiba amebaki kujipendekeza kwa wanasiasa vihiyo!
Mkuu usisahau na TLS imekuwa kimya kama mwana mkiwa anaye ngojea wasamaria wema wampiganie
 
Wanasheria wa nchi hii wamewekwa mfukoni mwa Jiwe!
 
Nimekusoma mwanzo mpaka mwisho nimeelewa lengo lako ni kwamba " kubadili katiba yetu kutoka kingereza kwenda kwenye kiswahili sio sababu ya wananchi kupata haki yao" lakini umeshauri itazamwe vipi namna ili kila mmoja apate kujua lugha ya dunia ? Sasa je hili linawezakana ??

Kwangu mimi nilivyoelewa licha ya kua kingereza ni lugha ya dunia na ndio inatumika katika katiba yetu, lakini kuna kundi la wazawa ambao ni waswahili, vilevile kwa sababu kiswahili ni lugha yetu sio kosa kukawa na katiba iliyo katika kiswahili.
Nilichokiona kwako ni kuwa umedhani katiba ikitafsiriwa basi kingereza kitatelekezwa kitu ambacho sio kweli ila jambo ambalo wanataka ni kua yule alie ishia la nne, la saba , kidato cha pili , kidato cha nne , kidato cha sita mpaka chuo au anajua kusoma na kuandika asome kwa kiswahili na aelewe haki yake kwa lugha mama ili ajue uzito wa jambo lenyewe na vilevile hao ambao wameweza kusoma na kuandika watawasomea na kuwaeleza wale ambao hawajui kusoma.

"Kwa mfano sio wote tunaweza kusoma kingereza cha sheria ( law) " hata kama umesoma kiingereza na umefika chuo ila kuna misamiati inaleta uzito kupata mantiki kamili ya haki yako katika masuala mbalimbali yanayotusibu .
Isipokuwa ndungu mwandishi umelenga sana uwanja wa siasa ila katiba yetu ikiwa kwa kiswahili hata lile kundi kubwa linalo bebwa na mfumo kwa sababu halina elimu tutaweza kulishawishi kwa kutumia lugha mama.
Kuna mambo ya kifamilia kama ndoa, urithi wa mali, matumizi ya aridhi, mamlaka ya mwananchi juu ya viongozi wake n.k

Hivyo katiba ikiwa katika kiswahili itapunguza kubagua kundi la ambao hawakusoma lakini wanahitaji katiba kukabili changamoto zao za kisiasa mfano (wabunge ambao hawajasoma, madiwani, wenyeviti wa mitaa n.k), Kijamii kama haki ya kupata huduma( afya, shule , kusali n.k), kiuchumi ( kufungua biashara, kulipa kodi , kukabidili dhuluma dhidi ya mamlaka) hata kama anajua kuandika na kusoma hii itawasaidia kusimamia haki dhidi ya mamlaka au wenye kujichukulia mamlaka.

Mwisho nawasilisha.
 
Simon2016;
Shida kubwa siyo kuwafuta hao walioishia darasa la saba au la nne. Je umeshajiuliza kwanini katiba yetu iliandikwa kwa kiingereza kwa nyakati ambayo walioishia darasa la saba au nne au hambao hawakupata elimu kabisa walikua wengi zaidi ya sasa?

Kama wewe ni msomi mzuri na mfuatiliaji wa lugha ya kiswahili ni kua kinachofundishwa kwa ajili ya matumizi ya kila siku katika jamii yetu ni 30% tu ya maneno ya kiswahili. Kubabi au kataa maneno ya lugha ya kiswahili ni magumu na hayana maana yoyote yenye kuelewesha mtu katika dunia hii ya sayansi na teknolojia.

Tunaendekeza ujinga kwasababu ya mtu mmoja kusema kua sheria zetu ziwe kwa kiswahili. Kama neno softcopy yenyewe ni wachache sana wanakijua kua ni TETE kwa kiswahili.
 
"ofukozi pipo yuzidi tu dai in ze reki" [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
"ofukozi pipo yuzidi tu dai in ze reki" [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Wamelala fofofo............
 
Ukiwafikiria watawala wa nchi hii, utapata sonona bure
Nchi ya Watawala wapuuzi!!
Tatizo la nji hii ni CCM kwa asilimia 100(100%). Watawala wa CCM wana jiona kama wana hati miliki ya kuitawala Tanzania hii milele! CCM wanatumia udhaifu wa Watz wa kuwapa elimu duni tokea Awali,Msingi, Upili hadi Chuo kikuu!!!

Haiwezekani Graduate wa kiwango cha Daktari au Profesa awe hawezi kujieleza kwa Kiingereza iwe cha kuongea au cha kuandika. Rais Magufuli ni Daktari lakini ukija kwene Ung'eng'e ni jamaa ana zero yenye maskio!!!

Mtu anajiuliza huyu mtu alipataje udaktari wake??Aliandikaje papers zake wakti wa presentation na desertation desertation? Je, alikuwa ana-hire watu wamwandikie au alifanya ile kitu tunaita " copy & paste"?

SHERIA: Bila shaka hakuna taaluma yenye kutakiwa mtu kujua SHERIA NA KUITAFSIRI TENA KWA LUGHA FASAHA IWE NI KISWAHILI AU KIINGIREZA.
Sheria zote za Tanzania zinafundishwa kwa Vitabu vilivo andikwa kwa Kiingereza. Yumkini ndo maana Wana sheria wetu wanajifunza kwa kukariri siyo kuelewa.....!!!!
 
Nchi ya Watawala wapuuzi!!
Tatizo la nji hii ni CCM kwa asilimia 100(100%). Watawala wa CCM wana jiona kama wana hati miliki ya kuitawala Tanzania hii milele! CCM wanatumia udhaifu wa Watz wa kuwapa elimu duni tokea Awali,Msingi, Upili hadi Chuo kikuu!!!

Haiwezekani Graduate wa kiwango cha Daktari au Profesa awe hawezi kujieleza kwa Kiingereza iwe cha kuongea au cha kuandika. Rais Magufuli ni Daktari lakini ukija kwene Ung'eng'e ni jamaa ana zero yenye maskio!!!

Mtu anajiuliza huyu mtu alipataje udaktari wake??Aliandikaje papers zake wakti wa presentation na desertation desertation? Je, alikuwa ana-hire watu wamwandikie au alifanya ile kitu tunaita " copy & paste"?
Mimi nikishaacha kushangaa mtu kutojua chochote.

Tatizo kubwa sana la Magufuli kama hajui kitu analazimisha na kuhalalisha watu wote wawe kama yeye.

Yaani kwa kuwa yeye hajui Kiingereza basi anapambana kwa kila namna kudiscourage matumizi yake huku akijifanya mzalendo wa Kiswahili wakati Kiswahili chenyewe hajui.
 
Mimi nikishaacha kushangaa mtu kutojua chochote.

Tatizo kubwa sana la Magufuli kama hajui kitu analazimisha na kuhalalisha watu wote wawe kama yeye.

Yaani kwa kuwa yeye hajui Kiingereza basi anapambana kwa kila namna kudiscourage matumizi yake huku akijifanya mzalendo wa Kiswahili wakati Kiswahili chenyewe hajui.
Msikilize Rais wa Tanzania akitema yai .......!!!
 
"ofukozi pipo yuzidi tu dai in ze reki" [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Nimekusoma mwanzo mpaka mwisho nimeelewa lengo lako ni kwamba " kubadili katiba yetu kutoka kingereza kwenda kwenye kiswahili sio sababu ya wananchi kupata haki yao" lakini umeshauri itazamwe vipi namna ili kila mmoja apate kujua lugha ya dunia ? Sasa je hili linawezakana ??

Kwangu mimi nilivyoelewa licha ya kua kingereza ni lugha ya dunia na ndio inatumika katika katiba yetu, lakini kuna kundi la wazawa ambao ni waswahili, vilevile kwa sababu kiswahili ni lugha yetu sio kosa kukawa na katiba iliyo katika kiswahili.
Nilichokiona kwako ni kuwa umedhani katiba ikitafsiriwa basi kingereza kitatelekezwa kitu ambacho sio kweli ila jambo ambalo wanataka ni kua yule alie ishia la nne, la saba , kidato cha pili , kidato cha nne , kidato cha sita mpaka chuo au anajua kusoma na kuandika asome kwa kiswahili na aelewe haki yake kwa lugha mama ili ajue uzito wa jambo lenyewe na vilevile hao ambao wameweza kusoma na kuandika watawasomea na kuwaeleza wale ambao hawajui kusoma.

"Kwa mfano sio wote tunaweza kusoma kingereza cha sheria ( law) " hata kama umesoma kiingereza na umefika chuo ila kuna misamiati inaleta uzito kupata mantiki kamili ya haki yako katika masuala mbalimbali yanayotusibu .
Isipokuwa ndungu mwandishi umelenga sana uwanja wa siasa ila katiba yetu ikiwa kwa kiswahili hata lile kundi kubwa linalo bebwa na mfumo kwa sababu halina elimu tutaweza kulishawishi kwa kutumia lugha mama.
Kuna mambo ya kifamilia kama ndoa, urithi wa mali, matumizi ya aridhi, mamlaka ya mwananchi juu ya viongozi wake n.k

Hivyo katiba ikiwa katika kiswahili itapunguza kubagua kundi la ambao hawakusoma lakini wanahitaji katiba kukabili changamoto zao za kisiasa mfano (wabunge ambao hawajasoma, madiwani, wenyeviti wa mitaa n.k), Kijamii kama haki ya kupata huduma( afya, shule , kusali n.k), kiuchumi ( kufungua biashara, kulipa kodi , kukabidili dhuluma dhidi ya mamlaka) hata kama anajua kuandika na kusoma hii itawasaidia kusimamia haki dhidi ya mamlaka au wenye kujichukulia mamlaka.

Mwisho nawasilisha.
Nakazia
 
Nchi ya Watawala wapuuzi!!
Tatizo la nji hii ni CCM kwa asilimia 100(100%). Watawala wa CCM wana jiona kama wana hati miliki ya kuitawala Tanzania hii milele! CCM wanatumia udhaifu wa Watz wa kuwapa elimu duni tokea Awali,Msingi, Upili hadi Chuo kikuu!!!

Haiwezekani Graduate wa kiwango cha Daktari au Profesa awe hawezi kujieleza kwa Kiingereza iwe cha kuongea au cha kuandika. Rais Magufuli ni Daktari lakini ukija kwene Ung'eng'e ni jamaa ana zero yenye maskio!!!

Mtu anajiuliza huyu mtu alipataje udaktari wake??Aliandikaje papers zake wakti wa presentation na desertation desertation? Je, alikuwa ana-hire watu wamwandikie au alifanya ile kitu tunaita " copy & paste"?

SHERIA: Bila shaka hakuna taaluma yenye kutakiwa mtu kujua SHERIA NA KUITAFSIRI TENA KWA LUGHA FASAHA IWE NI KISWAHILI AU KIINGIREZA.
Sheria zote za Tanzania zinafundishwa kwa Vitabu vilivo andikwa kwa Kiingereza. Yumkini ndo maana Wana sheria wetu wanajifunza kwa kukariri siyo kuelewa.....!!!!
Waliosoma kiswahili watakubali kuwa walisoma vitabu vya kiingereza.
Huwezi soma sarufi ya kiswahi bila kusoma sarufi ya kiingereza
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom