Wanasiasa, mna Takwimu hii mpya ili muanze kujipanga kimkakati kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025?

Wanasiasa, mna Takwimu hii mpya ili muanze kujipanga kimkakati kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Takwimu mpya kutoka Mamlaka husika imesema kuwa kwa hivi sasa 77% ya ' Population ' ya Tanzania ni Vijana.

Mnaotaka Kugombea Urais au Kuendelea nao baada ya 2025 Kazi Kwenu sasa katika Kulishawishi, Kulidanganya, Kulirubuni na hata Kulitumia vizuri hili Kundi ili 2025 Ikulu iwe Nyumbani Kwako.

Na nyie (Sisi) Vijana wenye hii 77% hebu tutumie miaka hii Minne (4) iliyobaki kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao wa 2025 Kujitafakari kwamba je, tuendelee Kutumika au Safari hii nasi tuamue kwa Niaba ya Tanzania yetu ya baadae?

Kazi Kwenu Wanasiasa wa Tanzania hii.
 
Hivi nyinyi mnawaza kututawala bila kufikiria hao mnaojipanga kuwatawala nao ni vijana pia?

Kila mwanasiasa wa Tanzania anajiona ni President Material?
 
Tatizo kubwa hatuna chama mbadala chenye Sera na itikadi madhubuti kwa manufaa ya umma. Badala yake tuna vyama vya upinzani vinavyomilikiwa na watu kwa maslahi yao binafsi. Chadema inamilikiwa na Mbowe, ACT inamilikiwa na Zito, CUF inamilikiwa na Lipumba, NCCR inamilikiwa na Mbatia n.k.
Na CCM inamilikiwa na nani
 
Tatizo kubwa hatuna chama mbadala chenye Sera na itikadi madhubuti kwa manufaa ya umma. Badala yake tuna vyama vya upinzani vinavyomilikiwa na watu kwa maslahi yao binafsi. Chadema inamilikiwa na Mbowe, ACT inamilikiwa na Zito, CUF inamilikiwa na Lipumba, NCCR inamilikiwa na Mbatia n.k.
Kwanini usianzishe chako kikamilikiwa n Wanakibamba?
 
Washauri vijana wenzako wadai katiba mpya na tume huru ya uchaguzi mapema kabla ya uchaguzi ili maisha yao na ya vizazi vyao yawe kama walivyotaka wao!

Kinyume na Hilo idadi yao haina maana zaidi ya kutuongezea vibaka mtaani!
 
1623923821193.png
 
Na CCM inamilikiwa na nani
CCM ni chama cha umma hakiendeshwi na mawazo ya mtu mmoja Kama ilivyo Chadema, Mbowe akisema Lowasa ndo mgombea urais basi hakuna wa kupinga. CCM kila baada ya miaka 10 wanabadili mwenyekiti, Mbowe ana miaka zaidi ya 20 amekalia kiti halafu wanajiita chama cha demokrasia.
 
CCM ni chama cha umma hakiendeshwi na mawazo ya mtu mmoja Kama ilivyo Chadema, Mbowe akisema Lowasa ndo mgombea urais basi hakuna wa kupinga. CCM kila baada ya miaka 10 wanabadili mwenyekiti, Mbowe ana miaka zaidi ya 20 amekalia kiti halafu wanajiita chama cha demokrasia.
Jiwe alikipoka chama
 
Tatizo kubwa hatuna chama mbadala chenye Sera na itikadi madhubuti kwa manufaa ya umma. Badala yake tuna vyama vya upinzani vinavyomilikiwa na watu kwa maslahi yao binafsi. Chadema inamilikiwa na Mbowe, ACT inamilikiwa na Zito, CUF inamilikiwa na Lipumba, NCCR inamilikiwa na Mbatia n.k.
Na vijana wao kama wao HAWANA Agenda wala hawajiangalii kama wao.

Wamebaki kuwa Misukule wa Vyama vya siasa, na wasanii, viongozi wa dini.

Hulazimiki kutekeleza mahitaji ya vijana wengi ambao ni wafuasi wa Gwajima wakati ukimpa mtu mmoja tu, Gwajima anachotaka tayari umekamata wafuasi wake wote.

Mfumo huu huu uko kwa wanasiasa, na wasanii.

Vijana wote hawana Agenda wala mahitaji ya pamoja, zaidi ya kuwa misukule ya Agenda binafsi za wanasiasa ambazo mara nyingi hazigusi maslahi ya vijana.

Mfano: Sasa hivi vijana wengi NJAA KALII wanaishi kwa umachinga, lakini kipaumbele cha wanaharakati na wanasiasa mbele ya hii njaa kali ni Tume huru ya uchaguzi na katiba mpya.

Na vijana wanakuwa pushed kuwa nyuma ya Agenda hizi ambazo hazina manufaa kwao ya moja kwa moja.

Wale ambao ni misukule wa Diamond, kazi yao ni kuwa nyuma yake kwa agenda yenye maslahi yake binafsi. Sasa hapo mwanasiasa akishampata yeye ameshapata genge lake lote.
 
katiba mpya.
Hii inaweza kuwa suluhisho zuri la matatizo ya vijana.

Katiba itaweza kuwapa vijana nguvu ya wapi wauze mazao, nani wamchague, nini kifanyike kwa ajili yao na lini kifanyike? Kisipofanyika watakuwa na nguvu ya kumtoa waliempa dhamana ya kuwaongoza.

Katiba ndiyo mwarobaini
 
Hii inaweza kuwa suluhisho zuri la matatizo ya vijana.

Katiba itaweza kuwapa vijana nguvu ya wapi wauze mazao, nani wamchague, nini kifanyike kwa ajili yao na lini kifanyike? Kisipofanyika watakuwa na nguvu ya kumtoa waliempa dhamana ya kuwaongoza.

Katiba ndiyo mwarobaini
Hii ni kwa hisia zako.

Unaweza kuwa na katiba nzuri lakini hakuna anayeuheshimu na usiwe na kitu cha kufanya.

Maadili na kuheshimu matakwa ya watu siyo kitu ambacho unaweza kukipatia suluhisho la moja kwa moja kwa katiba.

Leo tuna katiba hiyo hiyo mbovu lakini haiheshimiwi.

Zanzibar wana katiba nzuri sana ya mwaka 2007 lakini hakuna anayeiheshimu.

Kenya wana katiba nzuri sana lakini matatizo mengi yako vile vile.

Mahakama ina amuru Miguna Miguna ni raia halali wa Kenya arudi Kenya, lakini serikali haiheshimu hiyo amri.

Kama maadili na kuheshimu taratibu hakupo, Mwisho wa siku yule anaekaa na hazina na kuheshimiwa na jeshi ndio ataamua hata mkiwa na katiba kutoka wapi.
 
Back
Top Bottom