Wanaume acheni huu uchafu

Wanaume acheni huu uchafu

Naona hapa kuna kutwanga maji kwenye kinu..ukirudi kwenye uhalisia ni ngumu mwanaume kwenda na maji wakati wa kukojoa tu. ..ni ngumu (mbishe,mkubali) wao wanajua kwenda kutoa dushelele zao wakojoe wasepe, maji atabeba kama anaenda kupuu au kuoga.

Tukirudi kwa nyie mnaotaja taja UTI,inaonesha na nyie kiwango cha usafi wenu hakijavuka 90+% na pia hamnywi maji ya kutosha.
Mwanadamu ukinywa maji ya kutosha na ukiwa perfect enough kwenye suala la usafi UTI utaisikia kwenye bomba tu.
Huo ni ubinafsi, kwa sababu mtu hachuchumai basi atuachie mikojo yake? Lakini wapo wanaume wanaomwaga maji
 
Yaani kuambiwa habari ya usafi unasema unapangiwa masharti? We wa wapi ndugu yangu?
Nimemshanga Sana huyu jamaa, kuwa mwanaume hakutufanyi tuwe wachafu, jali mazingira yako kwa usalama wako na wengine!!

House girl(dada wa kazi) Ni binadamu aheshimiwe, apumzike, apewe Uhuru wa kuabudu pia
 
Huku kwetu kuna changamoto sana kaka
 
Huku kwetu kuna changamoto sana kaka
Daaah, afu mtu mzima kabisa anakataa ushauri mzuri kabisa, Hawa si wanaume Bali wavulana

House girl(dada wa kazi) Ni binadamu aheshimiwe, apumzike, apewe Uhuru wa kuabudu pia
 
Una point lakini umefanya jumuishi mno.
Nadhani ungesema kwa wale wanaoishi kwenye nyumba ambazo hazina maji vyooni wabebe maji. Na siyo wanaume tu, tunashudia wanawake wengine wakitinga bila maji. Ukiona wanabeba ujue wako ktk "nyakati". Ila wahusika ujumbe umewafikia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa hilo nalo ni la kusema mkuu mbona unataka kunifanya niwe mwalimh wa chekechea au wanaume akili zenu ndio zipo hivyo? Hivi inawezekana kukawa na mfumo wa maji chooni na mtu akabeba maji kutoka nje?
 
Japokuwa mtoa mada unaweza kuwa upo sahihi , ila nyumba mnayokaa nayo usataarabu umepita kushoto, iliitakiwa yoo vyenu viwe na access ya maji huko huko ndani, ili.mtu akijisaidia ayatumie akiwa huko.

Wakati nakaa nyumba za kushare vyoo, tulikuwa na utaratibu wa mwenye zamu ya usafi ni lazima ahakikihshe anajaza maji kwenye Jaba la chooni. Hilo lingefanyika naamini usingekuja na uzi huu hapa.

Wekeni utaratibu huo , naamini hutajisiskia vizuri siku mkweo akija kukutembalea halafu akalazimika kukuomba maji ili aende msalani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Japokuwa mtoa mada unaweza kuwa upo sahihi , ila nyumba mnayokaa nayo usataarabu umepita kushoto, iliitakiwa yoo vyenu viwe na access ya maji huko huko ndani, ili.mtu akijisaidia ayatumie akiwa huko.

Wakati nakaa nyumba za kushare vyoo, tulikuwa na utaratibu wa mwenye zamu ya usafi ni lazima ahakikihshe anajaza maji kwenye Jaba la chooni. Hilo lingefanyika naamini usingekuja na uzi huu hapa.

Wekeni utaratibu huo , naamini hutajisiskia vizuri siku mkweo akija kukutembalea halafu akalazimika kukuomba maji ili aende msalani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahaha mkuu ni kweli na huu ndio ustaarabu ila kwa huku uswahilini jambo hili ni gumu kidogo. Kwanza choo chenyewe unaingia upande upande hiyo nafasi ya kuweka jaba itatoka wapi? Pili watu sio wastaarabu mtu anaenda huko msalani akikuta maji yamejaa kwenye ndoo full kujiachia anaoga huko huko. Mimi binafsi siwezi kutumia maji yanayokaa huko huko chooni kwa sababu ustaarabu ni sifuri, mtu anachukua kopo lile la kuchotea maji analiweka chini sakafuni anaenda zake halafu akija mwingine kopo lilelile alilochukua chini anatumbukiza kwenye ndoo ya maji halafu maji hayo ndio nije nitumie kujiswafi? Hapana kwa kweli
 
Back
Top Bottom