Wanaume mnajua mna matatizo

Madam umeanzisha uzi wenye akili, lakini tukiufumua tutakutana na matobo kibao.

Kwa nini huyo mchumba atoe udhuru wa namna hiyo?

Anamueleza nani maneno hayo, anakueleza wewe kwa niaba ya wazazi wake au anakueleza wewe ili ukawaeleze wazazi wako?

Kama anakueleza wewe tu, mmeanza kuelezana nini mpaka afikie kwenye sentensi hiyo?

Maneno hayo anakueleza mkiwa katika jiografia gani ya compound ya nyumba mliyopo, nje uwanjani ama ndani kabisa kitandani?

Nimeuliza maswali yote hayo kutaka kujenga picha ya kuonesha udhaifu wa watoto zetu wa kike ulipo!

Picha inajengeka hiviii:
Huyo anayeongea maneno ya 'kujitafuta kwanza' ni hawara anayekumiliki kwa gia ya uchumba.

Ushamfikisha hadi nyumbani kwenu kwa wazazi na kujitambulisha.

Keshatoa kishika uchumba na katanguliza mahari ama katoa yote!

Mfumo huo ovu wa ukiukwaji wa maadili ya kimila na kiutamaduni wa mTz ndipo kilipo kiini cha tatizo.

Wasichana wa siku hizi mnafanya kwa kujua ama kutokujua, lakini mila huwa hazibadiliki zinasimama kama 'nature'.

Topic kama hizi hunigusa sana mimi kama mzazi wa watoto wa kike na disciplinary officer wa maadili ya kimila.

Ushauri wangu kwako binti yangu: kila jambo liweke katika mkondo wake, uwe na uwezo wa kutafsiri mambo kwa namna yalivyo katika maisha yako.

Neno 'nakupenda' huwahadaa sana wasichana wasielewe kutamaniwa nako hutamkwa 'nakupenda' pia, hakuna mwanaume anaweza kukutamkia kuwa anakutamani, iwe hadharani ama sirini.

Wanawake walio wengi hawawezi kutafsiri mazingira ya kupendwa ama kutamaniwa, ndipo hapo wanaume hunasia ndege wao wajanja kwenye tundu hilo bovu!

Huweza kuhodhi watumwa wa ngono kwa gia ya maneno 'nakupenda'... 'kutoa kishika uchumba/mahari'... 'najijenga ama najitafuta kwanza' nk nk.

Wewe utabaki kumuamini kwa kuhisi huyo jamaa kuwa anakupenda kweli na ana nia ya dhati, maana mpaka katoa na mahari kabisa, kumbe ni mchezo tu wa kisaikolojia huo ili aendelee kukutumia atakavyo!

Nisikuchoshe:
Ni mwiko kumvulia nguo mchumba ama mwanaume anayekuja kwa gia ya uchumba, akupate pindi atakapo kuoa tu.

Ukimvulia nguo, tayari anakuweka katika daftari la orodha ya mahawara zake kama 'Egonga'.

Anaweza akakuoa kweli, lakini hawezi kuwa na 'muhu' wa kuharakisha, atafanya apendavyo kaika kufikia lengo hilo.

Mwanaume anaweza akakutamani mwanzo na baadaye akakupenda ama asikupende, kwa hiyo dawa yake 'mnyime' ili ajiseti fasta!

Akitaka akuoe ama aende, hautabaki na simanzi wala sononi.

Ukimnyima ndipo naye atajinyima ili kufanikisha kukupata ili akipate unachomnyima.
 
😲😲😲
 
Mwanamke Malaya utamjua tu.
 
Nanyie endeleeni kuchakazwa huko chini..nikija kuchungulia nakuta bonge la creta..mimi ninan niendelee kuwa nawe
 
Mseme mwanamme wako, au mwanamme fulani.

Usitujumuishe wanaume kiujumla wengine hatutaki ujinga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…