Wanaume mnaocheza vikoba mnatia aibu

Wanaume mnaocheza vikoba mnatia aibu

Moja...Wake zetu na mademu zetu wakikutana kwenye vicoba wanaliwa sana na wakopeshaji , wasiwasi ni kwamba je, na wanaume wanaliwa au wanafanyaje huko?


Pili...Vicoba vinapandikiza umbea sana kwa wanaume ndiyo maana sasa hivi huwezi tofautisha wanaume wa kwenye vicoba na wanawake wa vibarazani.


MWANAUME KUCHEZA VICOBA NI TABIA ZA KIKE
 
Nawaza Hapa,

1. Hivi mwanaume unapata wapi ujasili kucheza kikoba Kama wanawake? Lengo lako Ni Nini hasa? Unajiskiaje kwa mfano.

2. Tena wengine utashangaa kabisa, anakuaga hadharani mwanaume mwenzie kua Anaenda kwenye kikoba! Unabaki unamwangalia Mara mbili mbili humpatii picha.

3. Hivi wanaume wanaocheza vikoba, nao upitia Changamoto kama hizi wanazopitia dada zetu na mama zetu ktk kusaka pesa za marejesho ya vikoba kila baada ya siku kadhaa za wiki au mwezi?

Mimi nacheza VIKOBA kwani kuna shida gani. Tunajifanya jeuri tu za kipumbavu. Yaani Kwa sababu za ajabu niache VIKOBA nakopa Kwa asilimia tano, niende benki nikakope kwa asilimia kumi na tano. Tuheshimu ushirika ni muhimu sana.
 
Sijawahi kufikiri kama ndugu Deep Pond nawe una fikra kama hizi. Village Community Bank (VICOBA) ina tatizo gani? Au ulimaanisha upatu? Vicoba viko karibu nchi zote za SADC & EAC na imeonyesha mafanikio makubwa. Tatizo kwa hapa nchini utakuta havijasajiliwa na havina utaratibu unaoeleweka. Arusha Club SACCOS ilianziaga chini sana kwa marafiki tu kuanzisha umoja wao ila kwa sasa ipo level nyingine ikijumuisha matajiri wengi wa Arusha. Bado serikali inatakiwa itoe elimu kuhusu mambo ya fedha kwa wananchi. Itawasaidia kina Oscar Oscar na Deep Pond kutambua kuwa VICOBA havina jinsia. Umaskini hautaisha au kupungua kwa fikra kama hizi za Oscar Oscar na Deep Pond.
Uko vizuri mkuu watu wana mitazamo hasi tu ya VIKOBA. Mimi na watumishi wenzangu tisa tulikaa tukawaza tukaona hatutoboi na mikopo ya benki, mtu unakopa 20mil unalipa 30mil. Tukaona hapana, tukajiunga tukaweka, tukasajili kikundi ustawi wa jamii na tukaweka lengo la kukusanya 12 mil Kwa mwaka wa kwanza. Hivi ninavyoongea mwaka wa tano tunaelekea 100 mil. Hakuna kwenda benki tena.
 
Niliwahi kuwafundisha Sacco's moja Njombe wale jamaa sasa hivi wanatisha, wana pesa ya kufa mtu na wana mmiliki asset mbalimbali.

Lakini Vicoba Endelevu ndio vizuri zaidi kuliko vya kuvunja ambalo mnapovunja mwenyewe hisa nyingi za uwekezaji ndio anaondoka na bahasha nzito.

Tofauti na Vicoba Endelevu asset zote mtakazoinvest ni za wanachama.
JF nzima wew ni mmoja kati ya Watu ambao huwa Anamjibu Mtu/kumuelekeza kwa Facts,

Nakuheshimu sana Bro Kazi nzuri Dr Matola PhD
 
Upatu ndio vikoba au ina tofauti mbona hamtueleweshi vizuri
Sisi tuko watu 10 na kila mmoja anatoa 6m kwa mwezii na baada ya miezi kumi kila mmoja anakuwa amechukua zake x 10
Sasa kama ni aibu basi na iwe tu [emoji1]
Kama vikoba ina tofauti tuelimishane
Naomba kujua mkuu.. hii ina tofauti gani na kufungua fixed akaunti alafu uwe unaweka hela wewe mwenyewe tu then unaenda kuwithdraw baada ya muda uliopanga?
 
Naomba kujua mkuu.. hii ina tofauti gani na kufungua fixed akaunti alafu uwe unaweka hela wewe mwenyewe tu then unaenda kuwithdraw baada ya muda uliopanga?

Naomba kujua mkuu.. hii ina tofauti gani na kufungua fixed akaunti alafu uwe unaweka hela wewe mwenyewe tu then unaenda kuwithdraw baada ya muda uliopanga?
Haina tofauti kubwa ila fixed unawekeza kwa mkataba tuseme miaka 2 au 3 na unapata faida kidogo
Sasa mimi hiyo faida ndio siitaki na credit cards ninazo ila kwa mfano nikilipia huduma ya gari kama petrol au shopping zangu kabla ya riba tu yaani mwisho wa mwezi nalipa haraka

Natumia credit card kwa sababu ina guaranteed kama nikilipia kwa matapeli
Hii ninayotumia kwa kuchanganya na wenzangu ni wakati nahitaji hela ndefu kwa mara moja ambapo naweza kupewa mtu wa pili au wa 3 na kufanya jambo haraka

Riba ndio naikimbia hapo sio kingine ingawa kuna Bank hapa zinafuata sharia
 
Nitakuelewesha vizuri utaelewa achana na mleta mada hajui umuhimu wa vicoba

Kwenye vicoba akiba yako ndio inakubeba kwa mfano umekwama labda una akiba ya mill 3 unaweza kukopa mill 9 kwenye kicoba chetu unakopeshwa mara 3 ya akiba yako

Na wanaume wengi wanakopewa na wake zao
Ngoja nitarejea vizuri nikae darasan.. halafu kumbe ni tofauti na upatu
 
Uko vizuri mkuu watu wana mitazamo hasi tu ya VIKOBA. Mimi na watumishi wenzangu tisa tulikaa tukawaza tukaona hatutoboi na mikopo ya benki, mtu unakopa 20mil unalipa 30mil. Tukaona hapana, tukajiunga tukaweka, tukasajili kikundi ustawi wa jamii na tukaweka lengo la kukusanya 12 mil Kwa mwaka wa kwanza. Hivi ninavyoongea mwaka wa tano tunaelekea 100 mil. Hakuna kwenda benki tena.
Hongereni sana wakuu. Watu wanachanganya tu mambo kwa uelewa wao mdogo. Hivi vikundi vya upatu ni shida. Mikopo ya benki na hizi Microfinance ni sumu ya maendeleo. Mimi nilikopeshwa na Microfinance 15m kwa riba 20% kwa muda wa miezi 6 karibia nikimbie nchi. Biashara iliyumba kidogo mambo yakawa magumu kuanzia rejesho la 4. Dada yangu ndo aliniokoa kwa kunipa mchongo wa Vicoba. Ilinisaidia sana kumalizana na majamaa.
 
Nitakuelewesha vizuri utaelewa achana na mleta mada hajui umuhimu wa vicoba

Kwenye vicoba akiba yako ndio inakubeba kwa mfano umekwama labda una akiba ya mill 3 unaweza kukopa mill 9 kwenye kicoba chetu unakopeshwa mara 3 ya akiba yako

Na wanaume wengi wanakopewa na wake zao
Hapo kwenye bold🤣🤣
 
Back
Top Bottom