Wanaume wa JamiiForums nawajibu kwa nini tunawafungia PM na wengine hatuwajibu

Wanaume wa JamiiForums nawajibu kwa nini tunawafungia PM na wengine hatuwajibu

Kwanza kabisa, namuomba radhi Raynavero
Wakati naandika nilisoma comments za wadada/wahuni ambazo zililenga kuudhi kiasi kwamba nilipoteza kumbukumbu na kumjumuisha Raynavero kama mmoja wao.

Imenibidi nisome tena alichoandika kama kuna sehemu alikusudia kufanya hivyo, sikuona.

Andiko langu lililenga wadada waliokomenti huko kabla yangu, kwa lugha waliyo itumia na kujieleza wanaonesha ni jinsi gani walivyo, hivyo wanacho kipata ni haki yao.

Unakanyaga matope huku unakimbia ukitegemea kutokurukia?

Mimi huwa kawaida sikopeshi, haijalishi itakuuma vipi.
Nimekuelewa kaka.
 
Hey ray,
Kwanza nilitaka kuja huko PM, lkn nilivyokumbuka unapata tabu sana na pm za wanaume imenibidi niandike hapahapa.

Na kwakua nili comment mbele ya hadhara hii, basi ni muhimu pia niandikacho hapa kionekane mbele ya hadhara.

Pili, napenda kuomba radhi kwa comment yangu, nilikujumuisha pasipo kukusudia nikijua uliyo eleza yanafanana na wahuni walio comments mbeleni.

Katika majibu ya wahuni hao walionesha dharau, matusi na kejeli kwa wanaume wenye tabia ambazo wewe hujapendezwa nazo.

Mimi sioni tatizo la wao kuwadharau, tatizo naliona kwao.

Wewe unampaje mtu mawasiliano yako hujazijua tabia zake? Tabia za mtu humu JF kwa kusoma comments zake tu waweza mjua huyu ni wa aina gani though not 100%.

Kwahiyo kama umepata tatizo na tatizo umelisababisha wewe, ni vema ukakubali wewe ni tatizo kwanza.

Tatu, mimi sina chuki na yeyote humu. Kwasababu siichukulii JF serious sana. Ndio maana naweza tibuana na mtu leo lkn kesho tukabonga freshi tu. Na sijui ni wapi nilionesha chuki kwako, km ilitokea si kwamba ni chuki bali ni sehemu ya mijadala tu. Kujenga chuki na nisiye mfahamu, mtu asiyekuwa na impact kwangu ni kujilundikia stress ambazo zitakuwa tatizo kwangu.

Mimi navyo koment mpk siku tukwaruzane ndo naweza kukukariri,lkn km haijawaahi tokea hivyo ninaweza kujibu au koment kwenye mada ya mtu na nisikumbuke alieileta mada ni nani. Najenga chuki na umasikini sio memba wa JF.

Mwisho namalizia kwamba, hapa JF hata mtu akikutukana na umeudhika kweli, we mpe like afu sepa. Kama huna kifua cha kuvumilia, mweke kwenye ignore list afu uwe una mpotezea. Kama ni muungwana zaidi mtafite pm umweleze kiungwana hujapenda hivyo. Mtakuwa marafiki sana.Do not take JF serious, kuna watu wa kila aina humu

Yote ya yote, niwie radhi!!

(Ila una mkwara? Sijawahi mjibu mtu kwa unyenyekevu hivi)

Kazi njema.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].
 
Back
Top Bottom