Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Waongo hao nimekaa kaskazini hata hao matajiri utosikia tajiri mkubwa ni mwanamke ila wajane kibao wana miliki nyumba na biashara za wanaume zao ila hakuna tajiri wa kutishia mkoa mzima.Yani wanaishia kujiita wanawake wapambanaji
Ndio kwa sababu mnaowakandamiza ni ninyi hivyo jukumu la kuwawezesha ni lenu pia, mwanamke yuko hapo alipo kwa sababu ya kukandamizwa na mwanaume, acheni kuwakandamiza muwawezeshe halafu muwaache bila kuwabugudhi, kuwasimanga, kuwadhalilisha wala kuwatukana muone matokeo yakeEti tukiwezezwa tunaweza!!!! Haya wanayasema wenyewe.
Huko kwa wahindi ndo usiseme kabisa. Wanawake walikuwa wanaua wanaume ili wamiliki mali, hivyo wakaamua kuwa mwanamke atazikwa na mumewe pamoja kama mume akifa. Hii ikasababisha wanawake waache hiyo tabia na wanawahudumia sana waume wao wakiwa wagonjwa ili asife.Mwanaume kuwa na hiari ya kumtumia mwanamke atakavyo haihusiani na mahari hicho ni kichaka tu cha kujifichia ili mahari ionekane mbaya, kuna jamii hazina mambo ya mahari ila bado mwanaume anamtumia mwanamke vile anavyotaka kwa kigezo cha kwamba amemuoa na anamhudumia, kwa wahindi familia ya mwanamke ndio inatoa mahari kwa mwanaume lakini bado mwanaume ndio ana mamlaka kuliko mwanamke