Half american
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 38,283
- 97,793
Omba koneksheni na wifi, namimi nimpate wa hivyo nikimpa laki 5 si tunauaga umaskini jumlaSio uchokozi 😄
Serious nimetamani hiyo spirit ya kugeuza laki 1 kuwa milioni. Naitaka 😔
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Omba koneksheni na wifi, namimi nimpate wa hivyo nikimpa laki 5 si tunauaga umaskini jumlaSio uchokozi 😄
Serious nimetamani hiyo spirit ya kugeuza laki 1 kuwa milioni. Naitaka 😔
Hahahaha,hapanaa,kama hujui nikuambie tuu siku ingine usirudie kosa.[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] Mi nimeleta maada hapo tujifunze wewe unaanza mambo ya copy na paste umekuwa computer?@sonnita
Bora umesema maana nilitaka kusema ila watu wanakisukariCopy and paste hii,uwe unaweka na source kabisa ya habari.
Ipo huku huku Jf kwa ID mbili tofauti ka sio tatu.Kwan ww uliikuta wapi mkuu?
Mhh mimi napiga kimyaWatu 🤭
Atakuwa labda ni Finance manager.
Hahahaha [emoji23],usemage tuu mkuu. Humu ndani hakunaga jema ilimradi ushawabwagia ukweli wao,wahangaike nao wenyewe.Bora umesema maana nilitaka kusema ila watu wanakisukari
Itabidi aseee sio mchezoHahahaha [emoji23],usemage tuu mkuu. Humu ndani hakunaga jema ilimradi ushawabwagia ukweli wao,wahangaike nao wenyewe.
Alafu kesho mtu huyo huyo unamkuta anaparamia nyuzi za ajira😂😂😂😂 na anakifuata hadi pm kuuliza connection kama panya aliemeza sumu akitafuta maji😆😆😆Hahahaha [emoji23],usemage tuu mkuu. Humu ndani hakunaga jema ilimradi ushawabwagia ukweli wao,wahangaike nao wenyewe.
Shemeji hana baya, najua atatupa namba za wifi tupatemo ABC za kutajirika hata kwa asilimia 1.Omba koneksheni na wifi, namimi nimpate wa hivyo nikimpa laki 5 si tunauaga umaskini jumla
Story yako inafanana sana na yangu, kawaida napambana sana , ila nilikuwa nina matumizi mengi ya kijinga , until nilipokutana na huyu darasa la saba !!Mke wangu mimi elimu yake ni darasa la saba, mimi nimemaliza chuo kikuu ni mhasibu nafanya kazi benki na nina mshahara mkubwa tu. Nilikutana na mke wangu kipindi kaja kuchukua mkopo wa Biashara yake, wakati huo nilikua afisa mikopo. Alinielezea kuhusu Biashara yake, plan zake na namna alivyoanza Biashara nilimuambia ondoka uje kesho.
Lakini alipokua anaondoka nilimuita dada mmoja rafiki yangu na kumuambia nitamuoa yule dada, yule ndiyo mke wangu. Hakuamini lakini nilimtongoza nikampata na sasa hivi ni mke wangu.
Ana akili sana huyu mwanamke, kabla ya kumuoa nilikua nishafanya kazi miaka tisa, nilikua na Gari tena ya mkopo na kiwanja tu. Nilijua sina akili kama yeye hivyo nilimuongezea mtaji kwenye Biashara yake na kumuacha afanye "miujiza" yake maana mimi naiita miujiza. Sasa hivi ndoa yangu ina miaka sita, tuna nyumba mbili, viwanja vitatu maduka mawili makubwa ambayo tunasimamia wote na vitu vingine vingi. Ingawa majina katika hati ni yetu wote wawili lakini ndani ya nafsi yangu nakiri hakuna chakwangu hapo.
Mwaka jana mke wangu aliniambia kuwa anatamani kuwajengea nyumba wazazi wake, nikaridhia ombi lake. Kwetu kuna nyumba kubwa tu ambayo tulijenga na ndugu zangu na nahudumia kama kawaida. Alipoanza kujenga nikaona ndugu zangu kama nyuki, wanavamia na maneno, kunijaza kuwa nimetekwa sijui na maujinga ujinga mengi. Mama naye alianza kumchukia mke wangu mara aniambie kamuongelesha vibaya, mara aniambie hivi mara vile, mara ghafla kabila eti kisa wachaga ataniua sijui nini alikuja hana kitu huku anapendeza.
Baada ya kelele nyingi niliona hii itakuja kuniletea shida. Siku moja nilienda nyumbani, nikaomba kuongea na Mama, alianza kuniambia maneno mengi nikamsikiliza sana nikamuambia....
“Mama hivi kabla ya kuoa nilikua na nini?” Alinyamaza kisha akaniambia Gari, nikamuuliza na sasa hivi? Akataja vile vichache anavyovijua, nilimtajia na vingine vingi ambavyo havijui akabaki kushangaa. Akaniambia tatizo hushirikishi ndugu zako nikamuambia kwani walishiriki kuzichuma?
“Mama nakupenda sana, ila jua kuwa sina akili kama mke wangu nikimuacha yule mwanamke kesho,keshokutwa nitakua kama fala flani hivi sina kitu na yule mwanamke hata nikimuacha na laki moja tu mwakani yeye atakua milionea.
Nauchukuia sana umasikini hivyo kawaambie wanao kuwa wakiendelea kumsumbua mke wangu basi hata kwangu hawatakanyaga.Kujifanya wananiheshimu halafu wanamdharau mke wangu ni unafiki.Mke wangu simuachi, kwao haachi kujenga kama unataka nyumba Mama nilishakujengea hao ndugu watafute vya kwao na wenza wao!”
Mama aliongea sana akilalamika kuwa nimetekwa akili nikamuambia wewe ni Mama yangu hata ukinitukana siwezi kuacha kukuhudumia kwani ni kazi yangu lakini siwezi kumuacha mke wangu, ila waambie wanao kuwa wakimsumbua mke wangu nitasahau kuwa tumezaliwa tumbo moja. Mama aliongea, akaongea lakini niliondoka. Walijua kama natania wakidhani kama nimelishwa limbwata, ile nafika nyumbani mke wangu nakuta hajachangamka, nilimuuliza tatizo ni nini hakuniambia alisema yuko sawa.
Nilihisi kitu nikachukua simu yake, nikaangalia meseji mdogo wangu wa kike alikua akimtukana mke wangu kuwa amenilisha limbwata mpaka imefikia hatua namtukana Mama yangu, mara ataondoka tu laana itamshika na mambo kibao. Nilichukua simu ya mke wangu na kumpigia, alipokea hata kabla ya salamu alianza kutukana na vitisho kibao. Nilimuambia kuwa “Inaelekea Mama hakukupa ujumbe wangu vizuri ukauelewa, nilisema atakayeendelea kumsumbua mke wangu nitasahau kama ni ndugu yangu, basi wewe kuanzia sasa nimekwisha kusahau!”
Nilikata simu na sikumtafuta, ilikua mwaka jana, yeye yuko chuo nilikua namlipia mimi kila kitu nikakata kabisa, nikamuambia sitatoa. Mama akapiga simu akalia lakini nikakataa, mke wangu alinibembeleza sana kumsamehe lakini wapi nilimuambia sitaki. Nilifanya makusudi ili wajue kuwa namaanisha kuhusu msimamo wangu.
Mwaka huu wote ada ya chuo ya mdogo wangu aliyelipa ni mke wangu, hawakuniambia lakini najua kwani Mama ndiyo alikua anapiga anamuomba na pia sasa hivi akitaka matumizi anaomba kupitia mgongo wa Mama ili Mama aniombe nimpe.Najua zinaenda wapi nabaki nacheka tu moyoni.
Mdogo wangu nimemsamehe ila natamani ajue kuwa mke wangu ni jembe,ana akili ya Biashara ambayo mimi sina, akili yangu ni ya darasani tu ila kwa Biashara huyu mwanamke hapana.
Wakati mimi nikiiangalia Tsh 100,000 naona raundi kadhaa za bia Baa,yeye anaiona kama mtaji wa Biashara itakayozalisha mamilioni.
Nimuambie tu mdogo wangu najua bado yeye na Mama wanaamini nimelogwa, Si kweli,mimi sitaki tu umasikini nikimuacha huyu mke wangu ataondoka na mali zake.Biashara tunazomiliki sasa sitaweza kuziendeleza na hata nikiwapa ndugu zangu hawataweza kuziendeleza!
Funzo : Wanaume wengi wanafanikiwa kupitia migongo ya Wanawake
Kiukweli wanawake mnaupiga mwingi kongole kwenu, mmeushikilia utajiriShemeji hana baya, najua atatupa namba za wifi tupatemo ABC za kutajirika hata kwa asilimia 1.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]acha kabisa,ndo walimwengu sie tulivyo.Alafu kesho mtu huyo huyo unamkuta anaparamia nyuzi za ajira[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] na anakifuata hadi pm kuuliza connection kama panya aliemeza sumu akitafuta maji[emoji38][emoji38][emoji38]
Poa usijaliHahahaha,hapanaa,kama hujui nikuambie tuu siku ingine usirudie kosa.
Content unayoweka publicly especially kwa maandishi kama sio kazi yako ni vizuri kum-acknowledge owner(ulipoitoa).
Usifanye kavile wewe ndo mhusika mkuu. Ni hayo tuu.
Hii ipo sana kwenye familia zetu masikini, kijana akiendelea kidogo ndugu wote wanajipa hakimiliki ya mali zake.Umasikini ni mbaya sana,mambo ya kufikiria mali ambazo hujazitafuta ni umasikin mbaya sana,hili pepo nilishalifukuza kitambo
Darasa la saba wengi wanaakili natural ambazo hazijachakachuliwa na theories nyingi za kijinga za wazungu na kunyonya nguvu asilia ya Mungu ndani ya mtu!!Story yako inafanana sana na yangu, kawaida napambana sana , ila nilikuwa nina matumizi mengi ya kijinga , until nilipokutana na huyu darasa la saba !!
Maisha yalibadilika the day ameingia ghetto , tukaanza kununua jiko la mchina sufuria na vijiko, baada ya hapo ilifata miujiza mingi sana ya maendeleo , yeye akiwa mama tu wa nyumbani ,sasa hivi anafanya biashara zake kwa usimamizi wake ,naamini nisingeweza bila yeye na mara kadhaa nimempab credit kwa hilo.